Katiba mpya siyo sera ya chadema ni sera ya watz wote ttzo ni kwamba watz wengi wanaifahamu zaidi simba na yanga kuliko siasa za nchi yao
Katiba Mpya haiwezi kuwa sera ya chama chochote. Ila ilikuwa kipaumbele cha kuvutia hadi siku za karibuni.
Hili la kuwatupia watz ni visingizio tu ndugu. Katika uzi huu:
Bei za vitu kushuka Kenya, sisi tunakwama wapi?
Angalia hoja za huyu
Allen Kilewella kama na majibu aliyopewa. Hapa chini ni moja ya majibu kwake. Katokomea kusikojulikana:
brazaj mfano wako wa maandamano ya Kenya kumhushisha Laila unakosea sana. Ukijikumbusha vita ya Mau Mau utaona kwamba wala si suala la Laila Wakenya kuwa vile.
Lakini pia unajua ushawishi wa Laila Nairobi unatokana na nini. Tafuta kwa karibu habari za Kibera ujielimishe. Mbona siyo Kenya Nzima walioandamana??
Maandamano huratibiwa kwa watu waliotayari kuandamana ila huwezi kuratibu maandamano kwa watu wasio tayari kuandamana. Watanzania ni waoga wa kuandama dhidi ya serikali. Kenya hata bila ya Raila wataandamana tu maslahi yao yanapotishiwa!!
Nimejibu hoja zako mbili zile, nikidhani na ya Liz Truss iko hapa kumbe sivyo. Kwa vile uliileta nitaitembelea pia.
Nitategemea tuwe na forum moja kama ni nia ya majadiliano ya dhati, siyo hii ya kuruka ruka. Hii itafaa kwa flow nzuri na inapobidi inaweza kuwa muhimu kutoa maelezo marefu labda pamoja na references kadha wa kadha. (Ni maoni yangu tu.)
--------
Nikikurejea sasa kwenye post hii ambapo nitalazimika kuzijibu hoja zako kirefu, nikiweka references kadhaa zilizo relevant.
(a) Kwamba watanzania ni waoga:
1. Hoja hii itakuwa ni matusi ya wazi kwa watanzania waliokuwa JKNIA LIssu #1 na hata LIssu Kiluvya alipokuwapo pia Askofu Mwamakula. Wakati huo madarakani akiwapo jiwe kweli kweli pamoja na washirika wake.
Ninaamini kamanda LIssu hawezi kukubaliana na hoja yako hiyo isiyokuwa na afya wala ukweli wowote.
2. Hoja hii ni matusi kwa wazanzibari na wahanga wa risasi za moto kutoka kwa wanaosemekana kuwa askari wa kukodiwa kutokea nchi jirani:
Hiyo ikiwa ni ACT chini ya Maalim Seif (rip).
Ninaamini Maalim Seif akiwa hai angeipinga hoja (mufilisi) yako hiyo.
3. Kumbuka mauaji kwenye maandamano Zanzibar, 27/1/2000, CUF chini ya Maalim Seif.
4. Nani asiyeujua uliokuwa moto wa Chadema chini ya Dkt. Slaa na harakati zilizokuwapo? Nani asiyeujua uliokuwa moto wa wazanzibari chini ya Maalim Seif?
5. Nk nk.
Kuhusiana na hoja yako hiyo, hapa chini ni uzi wenye maelezo ya kina, kama nia yako ni kujadiliana kupata ufumbuzi wa mikwamo yetu yenye kushangaza.
Upinzani - walio waoga (cowards) si Wafuasi
Watanzania walioangaziwa hapo juu ni hawa hawa waliopo leo. Kumbe nini kimebadilika kuwaita wewe leo kuwa ni waoga ndugu?
(b) Kushindwa kutambua umuhimu wa Raila kwenye mapambano haya:
1. Raila hana njaa wala hao viongozi wenziwe. Kwa nini kama Raila si muhimu, maandamano Kenya hayakutokea kabla ya Raila kuyaitisha au hayakuendelea baada ya yeye kuyasitisha ikiwa kumbe kila mmoja alitokea huko kwenye maandamano kivyake vyake (na njaa yake) kama mvua?
2. Hapa zingatia kuwa Zanzibar wameandamana na CUF chini ya Maalim si vingine. Pia wameandamana na ACT chini ya Maalim si vingine. Kenya wanaandamana na Raila, siyo Karua wala Musyoka, na huo ndiyo ulio ukweli. Labda kama unadhani CUF waliandamana na Lipumba au ACT waliandamana na Zitto.
Kujaribu kuukimbia ukweli huo labda kama unataka kujitoa ufahamu tu au kutaka kuacha kujitendea haki wewe mwenyewe.
Harakati za ukombozi kama hizi, ambako maandamano ni silaha pekee hayajaacha kuwa na icons. Wamekuwapokina Mandela, Nyerere, Tutu, Mtikila, Malema nk. Hii kote duniani kama tunavyo wasikia kina Dalai Lama, Aung San Suu Kyi, nk.
Uzi huu hapa hapa chini una maelezo ya kina kuhusiana na hoja yako hii:
Tusilaumiane: Wako wapi kina Nyerere, Maalim Seif, Mtikila, Julius Malema au kina Tutu
(c) Maandamano huratibiwa:
Hakuna mahali popote nilipotumia neno kuratibiwa. Hivyo sijui ni kwa mantiki ipi unalitumia. Hilo ninakiachia mwenyewe.
(d) Kumhusu Liz Truss:
Nimemtumia huyu kuonyesha jinsi demokrasia isivyodanganya. Nikionyesha kuwa tuweke misingi huru, ya haki na demokrasia katika kupata viongozi wetu kulingana na agenda na malengo yetu.
Kwamba mtu anaweza kutokuwa anatufaa, huyo tutamtoa au kudumu naye kwa wakati wowote kulingana na outputs zake.
Kwamba kiongozi ni lazima awe na uungwaji mkono wa kutosha. Ambapo akipoteza huo anatoka au tutamtoa bika kusubiri.
(e) Siyo Kenya yote inayoandamana:
Haikuihitaji Kenya yote kuandamana kumfikisha Ruto na genge lake alipofikishwa. Hayo yako kwenye mada:
"Hakuna mahali popote Kenya (au kwingine) wanakodai kuwa hizi ni harakati za wajaluo au kuwa hata ni za kikabila, isipokuwa Tanzania. Maana kamili ya kuwa mtanzania ni mjuaji mno!"
Bado Raila hana watu wa kufikia 5,000 anaoambatana nao Nairobi, kuitia jamba jamba ya kutosha serikali ya Kenya.
"Inafahamika kuwa hata huko walamba asali, wahuni na hata vijana wa hovyo wapo. Kwamba yaliyoko kwetu na kwao yapo. Hata hivyo ujasiri wa viongozi wao wenye misimamo isiyotetereka ni jambo la kupigiwa mfano sana."
NInasimama na hoja yangu kuwa kuhamasisha na kuongoza maandamano ni wajibu wa viongozi wa harakati za ukombozi.
Kiongozi asiyeliweza hilo ni vyema akang'atuka mwenyewe au akang'atuliwa.
Hatuna upungufu wa watu wenye kuwa na ari, dhamira, kujitoa, nk, kuyafanikisha majukumu yoyote tunayojipangia kidemokrasia katika vyama.