Uchaguzi BAWACHA: Sharifa Suleiman aibuka kidedea Uenyekiti Taifa

Wamecheza vyema kuendana na wakati tulionao na kiongozi wa nchi aliyepo YAKHEE.
 
Mbowe ana hulka fulani ya kuendesha chama kijasiriamali jasiriamali, yaani kifursa fursa.

Mwaka 2015 wakati katili Magu anagombea na Lowassa kulitokea mgawanyiko mkubwa sana. Kura zilipigwa kikanda na kikabila vibaya mno hasa kwa kanda ya kaskazini na Kanda ya Ziwa. Magu alikuwa anatumia hadi kisukuma kwenye majukwaa ya kampeni.

CHADEMA ilikuwa haiwezi kukosa viti vya ubunge mikoa ya Mwanza na Shinyanga, ila 2015 ilikosa kote isipokuwa Ukerewe na Mara.

Vivyo hivyo, CHADEMA ilizoa karibia viti vyote vya ubunge kanda ya kaskazini. Hadi majabali ya kisiasa kanda hiyo walipoteza ubunge.

Sasa ili kurudisha siasa za CHADEMA kanda ya ziwa, Mbowe akaona atafute Katibu Mkuu wa chama Msukuma ili am-neutralize "msukuma" Magu ndio akamuokota huko Mashinji. Ingawa matokeo hayakuwa kama Mbowe alivyotarajia.

Sasa leo kwakuwa Rais ni Mama Mzanzibar mvaa ushungi, kaona njia rahisi ni kumweka mbele Mmama, Mzanzibar.

Hapo hakuna demokrasia ya kura imetumika.

Siasa za Mbowe ni za kipuuzi sana. Ana misiasa ya ajabu sana kama Magufuli, na Sabaya.

Kuna kipindi alikuwa na mgogoro mkubwa sana Zitto kuhusu uenyekiti wa CHADEMA, akatafuta mzee fulani huko huko Kigoma ( anakotokea Zitto ) akamtumia kumchukulia fomu ya kugombea uenyekiti CHADEMA. Hii yote ni kuonesha kuwa licha ya kutofautiana na Zitto watu wa Kigoma wao wanampenda yeye Mbowe na CHADEMA na ndio wanaotaka Mbowe aendelee kuwa mwenyekiti wa chama. Huyo mzee haijulikani sasa hivi yuko wapi ?

Upuuzi gunia 100.
 
..Nawashauri mrudi kwenye KATIBA ya Chadema.

..Katiba yao haielekezi ufanyike uchaguzi mpya kutokana na hiki kilichotokea.

..Mtatoana macho bure kwa jambo ambalo haliko kikatiba.
 
Wamempa Mzanzibar ili apambane na Samia Mzanzibar.

Ni kama walivyowahi kuwapa wasukuma Pambalu na Mashinji ili wapambane na msukuma Magu.

Hakuna rocket science hapo wala kura zilizotumika.
 
Kwani huwajui waliomchagua Mashinji?
 
..mimi nilivyoelewa ni kuwa KATIBA yao ndiyo imewaelekeza hatua za kuchukua baada ya mwenyekiti wa jumuiya ya wanawake kuondolewa.
Wajane hao wahurumie , bado msiba upo kwenye ubongo, wanajiliza liza tu humu ,kupunguza mawazo.
 
Hawana bei kwenye kupigania nchi yao siyo kupigania CHADEMA.

Anyway, kama hujaliona hilo: Wamempa Mzanzibar ili apambane na Samia Mzanzibar.

Ni kama walivyowahi kuwapa wasukuma Pambalu na Mashinji ili wapambane na msukuma Magu.

Hakuna rocket science hapo wala kura zilizotumika.
 
Baada ya kumuona anatoka kwenye nyumba ya kulala wageni ya mbowe, nikajua ametumiza kigezo muhimu lazima ashinde uenyekiti bawacha
 
Mzanzibar alikuwa Seif pekee!

Hao wengine ni penguins tu.
 
Rais wa JMT na Bawacha wapi na wapi bwashee?!
 
Rais wa JMT na Bawacha wapi na wapi bwashee?!
Kwanini sasa hivi BAWACHA ndio wanajibizana na Ndugai kuhusu kina Halima Mdee hasa baada ya Ndugai kujaribu kuonesha kuwa CHADEMA inawaonea wanawake ?

Sasa BAWACHA na Speaker wapi na wapi ?
Hivi unazijua siasa za nchi hii kweli ?
 
Ufanano wa Kabila au utaifa una uhusiano gani na uongozi wa Samia vs Mwenyekiti BAWACHA?! Kwani umeambiwa wanataka kushindana kutambika!
 
Ufanano wa Kabila au utaifa una uhusiano gani na uongozi wa Samia vs Mwenyekiti BAWACHA?! Kwani umeambiwa wanataka kushindana kutambika!
Subiri siku Mbowe akikufu disha mfanano. Maana huna fikra huru.

Una macho lakini huoni.
 
Kwanini sasa hivi BAWACHA ndio wanajibizana na Ndugai kuhusu kina Halima Mdee hasa baada ya Ndugai kujaribu kuonesha kuwa CHADEMA inawaonea wanawake ?

Sasa BAWACHA na Speaker wapi na wapi ?
Hivi unazijua siasa za nchi hii kweli ?
Watu wanasimamia SHERIA wewe unaita kujibizana!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…