Uchaguzi CCM: Marufuku kuchukua fomu kama huna Cheti cha Taaluma

Uchaguzi CCM: Marufuku kuchukua fomu kama huna Cheti cha Taaluma

Status
Not open for further replies.
Siku chache baada ya kuripotiwa sakata la kukatwa ovyo kwa Majina ya wagombea ndani ya CCM bila kufuata utaratibu huko Ilala mapya yaibuka.

Inaelezwa kwamba Makatibu wote wa Mikoa na Wilaya "wamepewa Maagizo" na Katibu Mkuu Chongolo kuhakikisha kila anayegombea anaambatanisha Kopi za Vyeti vyake vya taaluma (form 4, form 6 na Chuo) na Mgombea asiyeambatanisha, fomu yake isipokelewe.

Inaelezwa kwamba mpango huu una lengo la kupunguza "wapiga debe" ndani ya Chama na kuweka Wasomi wenye uwezo wa Kupambanua Mambo.

Pia hii itasaidia Mamlaka za Uteuzi Serikalini kuwateua makada wenye sifa katika nafasi nyeti serikalini.
Kibajaji na Msukuma wana taaluma gani?
 
Mbona huku kwenye Kata na Mitaa uchaguzi umefanyika jumapili ya juzi na wagombea wengi walioshinda hata darasa la saba hawajamaliza?
 
Mbona huku kwenye Kata na Mitaa uchaguzi umefanyika jumapili ya juzi na wagombea wengi walioshinda hata darasa la saba hawajamaliza?
Kata ndio wameanza kuchukua fomu hawajafanya uchaguzi. Chongolo kashtuka hivi sasa baada ya kuona matawini mbumbumbu ni wengi. Kaamua kukaza kamba
 
Wapo ngazi ya kata hivi sasa. Sasa KM wao amekaza Uzi baada ya kuona walioshinda kwenye matawi wengi ni mbumbumbu
Watu wengi waungwana na wasomi wanaona aibu kugombea nafasi za uongozi ccm , sijui wanahofia nini , huku kwenye matawi washindi wengi wamepita bila kupingwa kwa sababu hakukuwa na waliojitokeza kugombea .
 
Kama kweli wamefanya hivyo na wapo na mtazamo huo basi ni jambo jema sana..

Ikiwezekana iwe ni sheria kwenye sheria ya vyama vya siasa na kule kwa msajiri wa vyama....pia lifanye kazi kwa vyama vyote..

Lingine lakuongezea, iwe hivyo kwenye ngazi ya ubunge tena waweke na kipengele cha mtu kuwa amewahi kuajiriwa kwenye position fulani fulani za maamuzi au kumiliki biashara yake mwenyewe yenye mtaji wa kuanzia 100mil...
 
Hivi unafahamu Sugu ni form four lakini anawazidi kwa mbali sana wasomi bingwa kama kina Dr Mwakyembe?

Tanzania hatuhitaji vyeti bali tunahitaji watu wenye akili kichwani vyeti ni nyongeza tu ya maarifa.

Degree na intelligent ni vitu viwili tofauti kabisa.
Mkuu bado nakubaliana na wewe kuhusu drier za saloon Hahaha

Ova
 
Hivi unafahamu Sugu ni form four lakini anawazidi kwa mbali sana wasomi bingwa kama kina Dr Mwakyembe?

Tanzania hatuhitaji vyeti bali tunahitaji watu wenye akili kichwani vyeti ni nyongeza tu ya maarifa.

Degree na intelligent ni vitu viwili tofauti kabisa.
Kama wewe ndo mpima uelewa wa watu basi ni hatari sana. Upinzani umekukaa kichwani mpaka unachuruzika, umetumia vigezo gani kutoa tathmini hyo?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom