Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
..Inahitajika kwanza kuujua uzuri wa vyama vingine ndipo watakapoweza kuuchukia kwa vitendo ubaya wa CCM, fahamu kuwa wengi wenye mashaka na uwezo na umakini wa vyama pinzani wata-opt kuendelea na Zimwi Walijualo, CCM,...
ngome imepigwa nini?
yaaaaaaaaaaah man watanzania wanataka kujua tofauti iko wapi?wakiiona ndio watapata mwamko wa kuitaji kuhama chama na kuchagua chama cha upinzani.mkuu pamoja
<br />Nsiande=bimkora=matola
Hakika unachokisema ndio sahihi kuwa CCM kwa sasa ndio wako kazini kuakikisha wale wote wnaoichukia CCM wageuke kuwa waumini wazuri wa CCM.Na hilo limekuwa hivyo ukizingatia hata humu ndani ya JF watu wamekuwa na chuki ya dhahili juu ya CCM el maalufu humu jamvini kama wanamagamba..
Sipendezwi na siasa za kuona kuwa hakuna watu wazuri ndani ya CCM,na kuwa ni lazima kila jambo sasa liwe ni upinzani tuu,no hiyo siyo sahihi,ili Nchi iende kwenye mstari tunawaitaji wote chama tawala na vyama upinzani,leo hii CCM wakiwa upinzani chadema wakawa chama madaraka CCM wataonekana wa maana kwa mujibu wa mapungufu ambayo CDM watayaonyesha na uhitaji wa matakwa ya umma.
Lakini kinachoendelea sasa haters wamekuwa mbele hata kwa mambo ambayo ni kwa faida ya Taifa na sio ya Chama.Ndio CCM wanamadudu yao lakini sio kuwa sasa kila jambo watu watengeneze chuki isiyo na msingi.Tutashindwa kutofautisha tofauti hiko wapi,itafikia hatua wananchi wataamua ni heri ya zimwi likujualao halikuli likakwishwa.
Yani ili kwa lugha nyepesi ni afadhari ya kubaki na CCM hii ya sasa kuliko kuchagua chama ambacho ujui kesho itakuwaje.Na hili swala itabidi wana JF ambao baadhi wana mapenzi na chama cha CDM, watumie uchaguzi mdogo wa Igunga kubadilika na kuwa na mikakati humu ndani ya kisayansi na sio kuwa na ushabiki wa kupinga kila kitu,vinginevyo tunakokwenda uenda wakatengeneza aina ya usindikizaji.
Ebu tuwe wazi humu ndani wapenzi wa JF ni wangapi uwa wanalusha madongo ya kuwakejeri wanaCDM humu ndani ukiachia FF ambae anajulikana kwa misimamo yake ambayo imeegemea kuchallange zaidi na kujenga mjadala uweze kuleta tofauti ya mawazo lakini hayuko kukejeri kiivyo.
Binafsi nimeshaweka msimamo wangu wazi Tanzania Mbele, kwangu Nchi kwanza vyama baadae,hivyo ni ukiwa mwana CDM kwangu poa,ukiwa CCM mwake,ukiwa CUF kama kawaida,hivyo kila mmoja atizame kuwa kwa zama hizi tuanze kujenga uungwana wa vitendo na maneno kwa kuwa fito wanazopigania CDM,CCM au CUF ni kwa ajili ya ujenzi wa Nchi inayoitwa Tanzania.
Vyama hivi vishiondane kwa HOJA kumjenga MPIGA KURA NA KUKUSANYA WAPENZI NA WANACHAMA WA KUWAUNGA MKONO.Waanze kutoa elimu ya kwa wapenzi na wanachama wao jinsi ya kuwa na muonekano [behave] ambao unabeba sura ya kichama kwa kila mmoja ambao kwa jumuiko lao ndio tunapata taswira ya kundi ambalo ndio chama kwa ujumla wake.
Tukiendelea kuona matusi ya kuwakebehi wana magamba kuliko mikakati ya kuibua mapungufu na changamoto za kuwafungua masikio yao Wananchi kuwa UPINZANI una sababu zote za kuaminika hakika itakuwa ni hadithi na malalamiko yasiyoisha wanaiba kura na maneno kadha wa kadha yasiyo na tija na ufanisi.
Ukiwaangalia CCM uwa wanabolonga kwelikweli,lakini ninachowakubali wakigundua kosa lao hakika CCM uwa ni wepesi sana kujirekebisha kimya kimya tena chini kwa chini ikibidi hata kwa kukopi mbinu ya adui wao lakini wao cha msingi wa win mapenzi yao kwa wananchi wao.Kwa sasa wameeanza kuwa na ustaarabu wa kauri hata kwa viongozi wao,ambao walio wengi walikuwa na busara.CDM viongozi wana ustaarabu wa matumizi ya maneno lakini wapenzi wake na wanachama wamekuwa na lugha za matusi na kejeri kwa wingi sana na kwa mfano mkubwa ni ndani ya JF.
Please tunawategemea CDM,kuleta changamoto kwa CCM na CUF ambao ni vyama tawala,kwa mambo haya tufika kweli mpaka CDM kuwa chama tawala uko tunakokwenda.Kwenye Red ni hakika hesabu mpya zinatakiwa
kweli jeuri ya pesa yaweza fanya jambo, hasa kwa jamii ya ki-kwetu ambayo fedha kwao ni zaidi ya maisha. Hatuna ushahidi wa nani kampanini nani, ila kuna ushahidi wa matukio ambao unahitaji macho tu.. Ukiangalia picha za uzinduzi huu utagundua mambo kama matatu makubwa.
1. Majukwaa
View attachment 36981
jukwaa hili ni gharama sana, kuliunda na kulipack pale lilipo, si chini ya paund 7,218 (kama mil16 zaktz). Nadhani wahandisi wabobezi tunajua hilo. Ama ametoa mtu mmoja au chama kimegharimia, ila tunajua ni fedha toka ardhi ya tanzania, na ni fedha ya wananchi wa tz. Na hii inafanyika tu kwa uchaguzi wa jimbo moja tu kati ya majimbo 348 ya uchguzi nchi nzima. Inatisha. Nadhani chama hiki chawaza kuwa ni cha wafujaji wa mali..
View attachment 36982
jukwaa la hili: Jukwaa la kizalendo, linalo jazia hisia ya uhalisia wa mkutano, wananchi, na matumizi halali ya mali za uma. Sidhani kama viongozi wote wa chama hiki wangechanga nadhani wangeunda jukwaa kubwa sana, but why, kwanini kutumia mali nyingi kwa tukio la siku moja. Mie kwangu nashawishika kufikiri kwamba huo ni moyo wa kizalendo zaidi. Kwa nchi yangu.
2: Mkutanoni.
View attachment 36983
wakazi hawa, maskini ya mungu, mbali na kuvishwa kofia, tshirt, hadi kupewa vuvuzela za njano, ila bado wanaonekana wana tafakari nzito. Wana umakini wa kupima kila jambo na kila neno, hawako kwa kudanganywa. Nadhani wana jua wanachokifanya. Sikubahatika kusikia hotuba iliyotolewa, ila wananchi wanaonekana hawajaridhika na yaliyotamkwa.
View attachment 36984
wananchi wa chama hilki wanaonyesha uhai wa hisia juu ya chama hiki. Kwa hisia moja, tendo moja na hamasiko moja, nadhani chama hiki kinajua kinachofanya kwa watu. Nadhani pia chama hiki kinaelewa nini wananchi wanahitaji ndio mana wako tayari kuonyesha hisia zao kwa chama chao. Sisi tunasema, mwanamke bora ni yule mwenye uwezo wa kuonyesha hisia zake kwa wazi kwa mwanamme ampendaye"..
Mie si mwanasiasa kiivyo sana.. Naangalia tu.. Napitapita
Zitto hawezi kuhudhuria kwasababu ya tofauti zao na Mbowe. Unajua Zitto huwa hapendi kupelekwa pelekwa kama Mkokoteni. Sasa bila yeye sijui mtashinda vipi uchaguzi?
mimi kama mzawa wa kilimanjaro niliyekulia arusha, nawalaani wale vijana waliokua wamebeba bango wakikashifu kua vurugu zao wakafanyie arusha na kilimanjaro,,,, how could someone dare speak something like that to the public???? That is sooo insane,,, walaaniwe na vizazi vyao vyooote milele,, yani nimeshindwa hata kuongea, presha imepanda
Kuwa CCM ufurahie maisha!!
<br />mwita25 ndo atampenda kama mkewe anavyompenda au wameanza mchezo wa kuingiliana kwenye masaburi hawa magamba kwa kauli hiyo sisi watu wa PWANI wallah tungemchalaza bakora m§n¿ yule
Sad to say, but idadi ya mbumbumbu Tanzania haitopungua...!!! :sad:
inaendana sema hujamusosama vizuri. Anamaanisha, ukiwa mweledi huwezi kufika wala kujihusiha na mahali ccm walipo. Kushangalia kwao, kukusanyika kwao, na mbwembwe zao inaonesha ni mbumbumbu, kwa hawajui umaskini na hali duni ya maisha waliyonayo umesababishwa na haohao cmm. Pia hawajui ni kivipi ccm wanaliibia taifa.