Uchaguzi Marekani: Trump amshutumu Biden kuiba kura, Twitter yatoa tahadhari kuhusu chapisho la Trump 'linalopotosha'

Uchaguzi Marekani: Trump amshutumu Biden kuiba kura, Twitter yatoa tahadhari kuhusu chapisho la Trump 'linalopotosha'

Sam Gidori

Senior Member
Joined
Sep 7, 2020
Posts
165
Reaction score
417
Wakati kura zikiendelea kuhesabiwa kufuatia Uchaguzi Mkuu nchini Marekani, mtandao wa Twitter umetoa tahadhari kuhusu chapisho la Rais wa Marekani, Donald Trump alilochapisha katika mtandao wake wa kijamii wa Twitter akiwashutumu wapinzani wake (Joe Biden) kuiba kura.

Trump aliandika: "Tunaongoza kwa kiasi kikubwa, ila wanajaribu kuiba uchaguzi. Hatutawaruhusu wafanye hivyo. Kura haziwezi kupigwa baada ya vituo kufungwa."

Twitter imetoa tahadhari kuwa sehemu au chapisho zima la Trump linaweza kuwa la kupotosha kuhusu zoezi la uchaguzi linaloendelea nchini humo.

Trump amesema kuwa atatoa taarifa zaidi baadaye.


photo_2020-11-04_09-04-25.jpg
 
Twitter wanakataa malalamiko ya Trump lakini nchi zingine ni sawa tu.
 
Kumbe hata Marekani inawezekana, mi nilijua mambo hayo ni Afrika tu.
 
Balozi wa Tanzania atoe tamko huko😂😂😂
Limeshatolewa tayari leo asubuhi kuwa marekani ifanye uchaguzi wa haki na uhuru la sivyo tutasitisha msaada wa maombi ya corona
 
Wiki iliyopita tulimuona Halima Mdee akilia na kudai amekamata karatasi za kupigia kura zilizokuwa zitumike nje ya utaratibu.

RPC Mambosasa wa Dsm akasema hizo karatasi wamekuja nazo wanachama wa Chadema kutoka mikoani ili wazitumie kuiba kura na kuidhulumu CCM.

Binafsi nikashangaa wapinzani wanawezaje kuiba kura?!!

Muda huu kupitia BBC Dira ya Dunia nimemsikia Rais wa Marekani mh Trump akilalamika kuibiwa kura na chama cha upinzani na kwamba hatatambua matokeo kama atashindwa na atakwenda mahakamani.

Kumbe upinzani kuiba kura inawezekana!!!

Maendeleo hayana vyama.
 
Back
Top Bottom