Elections 2010 Uchaguzi mdogo Igunga (UPDATES): Upigaji Kura

Elections 2010 Uchaguzi mdogo Igunga (UPDATES): Upigaji Kura

Status
Not open for further replies.
kuna mdau mmoja keshapiga kura huko igunga anasema kuwa hali ni shwari na cdm ushindi ni LAZIMA. Take my word
 
Kama ni kweli Tundu amsaidie huyo mama kufungua kesi mahakamani
 
Uchaguzi kwa jimbo kwa mjibu wa sheria ni sh 80.0 m, anasema Tendwa. Lakini je, ni kweli hii ndio bajeti
 
Clemmy, shukuru unaishi jirani na mimi meneja Ugavi Tanesco! La si hivyo ungekuwa unalia na wewe!

Hahaha,yawezekana mkuu.
Ila naogopa kusema ni wapi isije kuwa wamesahau.
Me mgao nausikia kwa watu tu saivi kwamba ni mkali.

I hope hauja geuka kuwa week nne nne,nisije kuwa nafurahia kumbe
kuna giza kuu linakuja
 
Mlezi wa vyama vya siasa Mh. Tendwa, hajakerwa na wanasiasa (Mbunge Aden Rage) "kupanda na silaha jukwaani" wakati wa kampeini (maana hakutaja kama hilo lilimkera) bali amekerwa na tukio la Mkuu wa wilaya kufanyiwa fujo, kijana kumwagiwa tindikali, na tukio la kurushiana risasi.

Ameyasema haya wakati akihojiwa na Mtangazaji wa TBC1 kuhusu ni mambo gani yalimkera katika uchaguzi mdogo wa Igunga

source: TBC1 saa saba mchana leo.
CCM imefanya mambo ya kihuni sana kwenye kata zote ambako kulikuwa na kampeni zinaendelea hasa la kuteka watu na kuwa piga na kuwaumiza vibaya sana cha ajabu analiona kukamatwa aliekuwa anabaka demokrasia lakini anasahau matukia ya watu kutekwa na kupatanda majukwaani na silaha, Kumwagiana tindikali wenyewe kwa wenyewe, kuchoma kuchomeana nyumba......
 
Hahaha,yawezekana mkuu.
Ila naogopa kusema ni wapi isije kuwa wamesahau.
Me mgao nausikia kwa watu tu saivi kwamba ni mkali.

I hope hauja geuka kuwa week nne nne,nisije kuwa nafurahia kumbe
kuna giza kuu linakuja
usiombe waukate kuanzia saa 12 jioni.....
 
Tumemkamata mgambo akiwa kwenye foleni ya kupiga kura huku akitoa rushwa ya shs 5,000/= kata ya Swingizi, baada ya kumweka chini ya ulinzi, tukamkuta na shs laki saba, kwa sasa anashikiliwa na polisi, anasema alitumwa na viongozi wa CCM.

Nchemba anapita kila kituo anamwita msimamizi na kumpa hela, kwa sasa amedhibitiwa na vijana wetu
 
Hata mi pia nashauli uwepo umakini mkubwa hao magamba wanambinu nyingi za kuiba kura hasa hiyo ya kubadilisha masanduku ya kura,hivyo mawakala wawe chonjo mtu asiende hata kukojoa akawaacha magamba na washirika wake make chama cha upinzani ni kimoja tu hapa Tanzania,piganieni haki msiogope vitisho vya Vasco Dagama,kila la heli CHADEMA.
 
Huyo mama atakuwa kachanganyikiwa tu. Haiwezekani mtu mzima kama yule aipende CCM. Atakuwa amepewa hela na magwanda ili aichafue CCM
Sasa hivi ni saa nane ngoma bado sana lakini cha kushangaza umechanganyikiwa...Pole sana mkuu nidiyo tatizo la kutetea mzoga kuwa haunuki ili hali wewe unaujua ukweli.......CCM ni mzoga unanuka lakini mnajaribu kuupulizia pafyumu...............
 
Nimekuwa nawasiliana na chanzo changu cha habari kutoka igunga leo na kupata habari kuwa katibu wa ccm-fedha na uchumi bwana mwigulu mchemba anapita kila kituo kuvizia watu wanaokuja kupiga kura na kuwapa pesa ili wawapigie CCM.pia, wamewachukua vijana wao na kuwavalisha magwanda ya kimgambo ambao kazi yao ni kukaa pembeni mwa njia wanazopita wapiga kura jirani na kituo cha kupigia kura na kuwagawia fedha.vijana wa chadema wamewadhibiti mgambo hao kwenye vituo 150 mpaka sasa na mgambo zaidi ya 10 wamepata kipigo cha nguvu kutoka kwa vijana wasimamizi wa CHADEMA katika vituo hivyo..

msimamizi wa CHADEMA anayesimamia vituo karibu 150 vya kupigia kura amemdhibiti mchemba na amemwambia kama anataka amani ivunjike,basi aendelee na mchezo huo...

kwa sasa hali ni shwari na hakuna tafrani yoyote.

TBC1 wametangaza kuwa idadi ya akina mama na wazee ni kubwa kuliko vijana eti nao wanashangaa kwa nini imekuwa hivyo!! ukweli ni kwamba vijana wamejitokeza wengi, akina mama na wazee pia. kutokana na chanzo changu hiki cha uhakika, kimesema kimewahoji wapiga kura 10, na 8 kati yao wamekipigia CHADEMA. ndugu wana jukwaa, habari hizi ni za uhakika sana, na nitaendelea kuzipata mpaka hapo saa 10 jioni vituo vitakapofungwa na matokeo tutakuwa nayo muda mfupi sana baadaye!

Pipoooooz!

--
 
Tumemkamata mgambo akiwa kwenye foleni ya kupiga kura huku akitoa rushwa ya shs 5,000/= kata ya Swingizi, baada ya kumweka chini ya ulinzi, tukamkuta na shs laki saba, kwa sasa anashikiliwa na polisi, anasema alitumwa na viongozi wa CCM.

Nchemba anapita kila kituo anamwita msimamizi na kumpa hela, kwa sasa amedhibitiwa na vijana wetu

Kaazi kweli kweli. Pamoja na gharama zote zile bado wanahonga. Kweli kizuri chajiuza.....
 
kama ni kweli hii mod iweke ktk updates hapo juu. asante wote mnaotupa updates zenu.
 
Abdala Tilata wa StarTV anaongea

Ametembelea vituo 10 hali ni nzuri, usumbufu kidogo.

Askari aliyepotelewa na shahada ya kura aruhusiwa kupiga kura.

Mzee mmoja kaibiwa kadi na mkewe, kafanya kama afande alivofanya hapo juu na karuhusiwa kupiga kura. Mzee kaapa atampa likizo ya unyumba mkewe kwa siku kadhaa kuanzia leo.

Tundu Lissu amekubali hali ni shwari.

Tilata anasifia polisi.
 
saa nane clouds watatoa updates za maendeleo ya upigaji kura igunga. Pale shinyanga vijana wanaogopa polisi.Kamanda wa polisi amewaasa wasiogope waende wakapige kura wanapoogopa wanatia shaka kwa nini wanaogopo.
 
attachment.php


Duh! unaweza kusema photoshop?

Kumbe rangi za kijani za Wanamtandao na CJJ zinatoutiana!
 
Tabia waliyo nayo wana familia kwa kiasi kikubwa huathiliwa na baba wa familia,baba akiwa mwizi na watoto wataiba tu ndivyo ilivyo kwa chama cha magamba,bila ya chama cha magamba kuondoka madarakani Rushwa haiwezi kupungua kwani ndiyo siraha kubwa ya chama cha magamba kwenye chaguzi zote.
 
Clouds fm live watatoa updates muda si mrefu. Mida ya saa nane hivi.tutajua mbichi na mbivu.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom