Uchaguzi mkuu kiti cha Rais 2025 (video): Unabii waweka wazi kuwa ni Samia S. Hassan (CCM) vs Bishop Josephat Gwajima (CHADEMA)...

4. Kwa mujibu wa unabii huu, CHADEMA hawana mtu ambaye ana kibali cha Mungu - Yehova kugombea kiti cha u - Rais mwaka 2025 aliye ndani ya chama chao..
Kwa hili nakubaliana na huu unabii. Na hakuna mtu mwenye akili timamu anaweza kujiunga kwenye chadema hii ya sasa ili agombee urais!
 
Chai
 
..Samia vs Gwajima itakuwa vita ya kidini, sio kampeni za uchaguzi.
 
Msikilize Nabii feki, utapata majibu yote ya maswali yako.
Kama huna GB za kutosha, siwezi kukusaidia, kwani ukitaka kuifaidi hii mada ni lazima usikilize video hiyo. Vinginevyo utakuwa umekurupuka tu.
Nimesikiliza na kusikiza kwa makini. Sijaisikia neno Wagalatia Wala habari za msichana wa miaka 17.
 
Nimecheka kijinga sana system ipo kazini ,chadema haitafanya makosa
 
Kwa jicho jingine... Je Kama ni watu wa CCM wasiomtaka mama, wanamtisha ili asigombee, ili wao wachukue hio nafasi Wala sio Gwajima, kwamba hapa wanatumia jina la Gwaji Kama skape goat ya timu flani ndani ya chama?
Hili nalo linawezekana..

Na kusema kweli, kwa haraka haraka hata mimi nimeiona hii picha, kwamba, a smart political game is being played here..

Na hawa jamaa wanaocheza mchezo huu kwa jinsi walivyo wajinga wakidhani watu hawataajua, wanaonesha kuwa hawamtaki huyu mwanamke wao huko CCM lakini at the same time ndani ya CHADEMA wanajua kwa hakika kuwa mtu hatari na sumu kwa CCM wakati wowote ni Tundu Antipasy Mughway Lissu.

Kwa hiyo wanacheza mchezo wao kotekote kuhakikisha, huyu mama hatoboi huko CCM na wakati huohuo kujaribu kupanda mgogoro CHADEMA ili mradi mwiba wa CCM, mwanasheria, mwanaharakati na mwanasiasa nguli na machachari Tundu Lissu hapati nafasi kupambana na yeyote atakayesimama CCM mwaka kesho - 2025..

Na ukiachilia mbali hiki kinachoitwa "unabii", the fact is that, huyu mama majority ya wana CCM huko ndani mwao ukiachilia mbali sisi wananchi tusio wanaCCM hawamkubali..

Vigezo vikuu vya kutokukubalika ni vitatu hivi;

1. Si Mtanganyika, ni Mzanzibari (nchi na taifa jingine akitawala nchi nyingine ya Tanganyika)

2. Ni mwanamke. Taifa hili ni gumu, mwanamke hawezi kuliongoza. Huyu mwanamke amethibitisha hili. Na by the way this is nature. A woman can never be a head of the family unless it is by default..

3. Hatukumchagua. She is just there by constitutional default. in 2020 she was just a side chick wa John P. Magufuli. Mtu ambaye hakuchaguliwa hawezi kuwa na vision ktk uongozi wake. Siku zote uongozi wake utakuwa vogue.

Mimi namwita Lucas Mwashambwa aje huku aseme neno. Yuko kimya sana kwenye hili. Au umepigwa na kitu kizito kichwani boss na umezirai huko uliko??
 
Nakukumbusha tu,

CHADEMA haijawahi kurudia mgombea Urais.
 
Tujadliane wote..

Mimi ni mjumbe tu...

Kama ulivyoona wewe, nami hivyo hivyo nimepita huko na kukutana na hii kitu na kuamua kushea hapa ili tujadiliane..

Kwa hiyo bila shaka unaweza kuwa na mawazo/maoni yako. Vivyo hivyo wengine nikiwemo mimi tunaweza kuwa na views tofauti tofauti...

Hata hivyo, nathamini sana observation yako. Bila shaka wajumbe wengine wanaweza kutia neno...
 
Chadema ni chama kikuu cha upinzani hili halina ubishi. Tatizo la chadema kwa sasa imepoteza viongozi wenye mvuto japo hawataki kukubali. Wao wamejikita na chuki dhidi ya JPM wanadhani hichi kitawasaidia kumbe ndio kinawauwa kabisa. JPM bado anaishi kwenye mioyo ya watu wengi pamoja na makosa yake ya kibinadamu bado anakumbukwa sana kwa kazi na hulka yake na yeyote atakaye mzungumzia vizuri ananafasi kubwa ya kupenya kisiasa, hivyo basi ili imani ya watanzania kwa chadema irudi inahitaji watu watayeweza kutembelea nyota ya JPM hata kama viongozi wa juu hawataki nao hao watu wengi wao wapo nje ya chadema. Huu ni ushauri wangu.
 
Watu wajinga kama wewe huangalia mazuri machache aliyofanya mtu pasipo kujali pale aliishia, vitabu vya Mungu vinasema bora mwisho mwema kuliko mwanzo mwema..Magufuli alianza vyema badae aliharibu na matokeo yake alipata alichostahili..hata kama alifanya mazuri kiasi gani hapo mwanzo, mwisho ndio unasema kwa sauti kubwa kuliko mwanzo wake, hayo mazuri aliyofanya ni sawa na bure, Mungu alituma watu kumwambia..acha hii mambo, akakaza shingo na kiburi cha madaraka, ndio ikaishia hapo, binadamu ana uamuzi kusikia anachoambiwa bila kujali nani anasema, maskini au tajiri, mkubwa au mdogo, muislamu au mkristo au mpagani...SIKILIZA! ukikaza shingo itabaki historia!
 
Ikiwa unaanza na herufi kubwa baada ya nukta hapo ndipo nilipogundua hakuna unachoelewa.
 
Huu mchongo ukitiki basi kuanzia hapo mimi na dini tutakua maji na samaki.

Tena kwake mzee wa ufufuo na uzima nitabobea ibadan.
 
Mpeni Lisu kiti 2025 tunatoboa wallah, wapinzani wengi wana sifa chafu ila si huyu Mwana.
 
Marais wote ni chaguo la Mungu
 
Na siku zote Mungu hujibu maombi ya watu wake ktk njia tofauti kabisa na tunavyodhani sisi kama asemavyo katika Neno lake;

Moja ya point muhimu kabisa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…