Uchaguzi wa Bunge la Wananchi CHADEMA

bagamoyo

JF-Expert Member
Joined
Jan 14, 2010
Posts
24,941
Reaction score
28,869
15 December 2022

LIVE UCHAGUZI WA BUNGE LA WANANCHI CHADEMA


Wagombea waelezea jinsi wanavyoweza kulitumikia Bunge la Wananchi la CHADEMA
Source: ZAMAMPYA TV

Katika hotuba yake Mwenyekiti wa Chadema amewatambulisha wabunge wa bunge la wananchi. Hi concept nimependa Sana. Hivyo inabidi chadema waifanyie kazi na kuanzisha hata vikao vyao.

1. Litakuwa na uwezo wa kujadili Mambo yanayo wagusa wananchi moja kwa moja.

2. Litakuwa na uwezo wa kukosoa serikali kwa uwazi.

3. Litakuwa na uwezo wa kuleta bajeti mbadala.

4. Litakuwa na uwezo wa kuishauri serikali kwa uwazi.

Nawapongeza chadema kwa ubunifu huu.

15 December 2022

Mwenyekiti wa CHADEMA Mh. Freeman Mbowe azungumzia nafasi ya Bunge la Wananchi la CHADEMA
 
CDM chama Cha BRAINS.

May God bless you. Aamen
 
Unafikiri ni wazo la CHADEMA!?

HIYO move ni ya wenye NCHI WANANCHI!!
 
C
Sijutii kujiunga CHADEMA mwaka 2000. Chama chenye akili.
 
Wametumia katiba ya mwaka gani ya Chadema kuanzisha Bunge hilo? Wakifutiwa usajili wasilalamike tushawaasa!
 
Yaani CHADEMA viongozi wake ni zero brain...na ni form 4 na 6 failure...hivi mnajua mnachokifanya ni uhaini kwa nchi...?mnatumia katiba ipi?
Msajili wa vyama akikufutieni usajili msilalamike!!!

NB:MMEMDHARAU SANA MAMA ILA MAGU ANGEKUWEPO MSINGEFANYA HUO UJINGA
 
Mna vituko sana ninyi BAWACHA ,BAVICHA na BAZECHA kila siku kuja na kitu Cha kuwatia moyo. Bunge Tanzania lipo moja mengine ni magenge
 
Nawapongeza kwa kurasimisha concept ya bunge la wananchi ila sijapenda suala la Suzan Lyimo kuwa kiongozi Tena!!



Mtu ameshakua mbunge since 2010 akastaafu 2020 akakaribishwa Baraza la wazee how on earth anapewa active post??



Hili bunge ni kwa ajili ya active politics na liko kimkakati kwa wagombea wa Chadema 2025 waanze kuonekana mapema. So ni jambo jema watu kama Lumola na Shija kuibuliwa Leo ila sura zile zile kupewa Uspika sioni kama ni strategic kabisa na hapo tumefeli.



Na hii tabia haipo Chadema tu hata CCM, unakuta mtu ni waziri Bado anagombea ujumbe NEC wakati huo huo ni mbunge as if hakuna sura mpya!!



Iwekwe kanuni kwamba mtu mmoja kofia Moja haiwezekani Msigwa akawa mwenyekiti wa Kanda hapo hapo alikua mbunge hapo hapo ukute mjumbe wa kamati kuu!! Hapana waamue Moja na kingine waachie wengine nao wapate fursa ya kuonyesha uwezo wao.



Cc Erythrocyte Kalamu
 
Uhaini ni upi? Vyuo vikuu tu kuna bunge na mawaziri mpaka Marais ndio sembuse chama kikubwa kama Chadema?

Acheni kukariri maisha, hakuna kosa kuwa na bunge maana ni majadiliano tu yanafanyika hapo Wala sio kama ni jeshi kwamba Kuna risk ya machafuko
 
Great
 
👍👍👍kila la kheri
 
Hii move ni nzuri sana. Ni wakati sasa chama tuwe na kituo chetu cha Redio na Tv
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…