Uchaguzi wa Kiteto: Taarifa mbalimbali

Uchaguzi wa Kiteto: Taarifa mbalimbali

Status
Not open for further replies.
1. Chadema kuna nini? Hata hiki kiti kimoja tu mnashindwa? Au ni kusindwa tu kawaida? Kuna matatizo ndani ya Chama? Au bado ni mbinu chafu za CCM? Je Chadema hakukuwa na mbinu chafu nao? Well kwa mwelekeo huu basi Upinzani una mda mrefu kupata fursa kuongoza dola Tz- as CCM wataendelea kutawala kwa miaka mingi ijayo! Poleni, it is a challenge CHADEMA, mmejifunza, tusonge mbele!

2. Naomba ushauri- Sasa mimi kwa sasa sina Chama na ni mzalendo kweli (Halisi)..nauliza kama nataka kugombea nijiunge na Chadema au CCM?

Watu hapa tutatafuta wachawi wee,lakini ukweli ni kuwa wananchi wa Tanzania ni fools(people lacking good sense and good judgement) They deserve what they are getting because they choose to have that.
Wako tayari kutoandamana kuishinikiza serikali kuwachukulia hatua Maafisadi lakini wako tayari kwenda kuandamana kumpokea Lowassa. Tanzanians are cheap like a bunch of groundnuts.We are easly bought therefore we are cheaply treated.
 
Well, it is painful maana kila juhudi zimefanyika ili CHADEMA washinde. Bila shaka bado tuna shida ya kimkakati katika upinzani na tunahitaji kujipanga vizuri zaidi. Lakini pia naamini bado kuna issue ya kujiamini kwa upande wa wananchi kwa maana ya kuamini kwamba wana uwezo na uhuru wa kuchagua kile roho yao inataka. Kwa hiyo pamoja na umuhimu wa upinzani kukaa chini na kujipanga vizuri zaidi, bado kuna haja ya ku-intesify kabisa elimu ya siasa kwa wananchi wetu ili wafike mahala wajiamini na wafanye maamuzi bila kuogopa vitisho. Baada ya kusema yote haya, ni vigumu sana kuamini kwamba matokeo haya yanaonyesha imani walionayo wananchi kwa CCM, maybe I am wrong!

nilikuwa nikisubiri kwa hamu sababu mtazoibuka nazo


kimkakati nnakubaliana nawe kuwa watani bado hamjajipanga kiasi cha kutufanya tuhahe ila sio siri sasa tumeanza kukuangalieni macho mawili hatulali na malengo yetu chaguzi zijazo tukuwekeni benchi kabisa na hili sio utani.


kuhudu wananchi hili si kweli hata nyinyi kabla ya uchaguzi mlithibitisha kuwa wananchi wanauelewa wa kutosha na wanajua wanachokifanya.

kuwadhihaki na kuwadharau watanzania kila upinzani unaposhindwa kunakuangushieni credit mkubali wananchi wanajua kuwa wapinzani ni wapiga domo nakutaka misifa vishindo vingi wakati wa uchaguzi baada hapo hawaonekani.

jifunzeni kuwa karibu na wanachama wenu majimbo mlo nayo yafanyeni pilot ili majimbo mengine watamani kuchagua upinzani

au mpaka mbowe awe ikulu na zitto awe waziri mkubwa ndio mtaweza kuleta maendeleo?
 
Posted Date::2/25/2008
CCM, Chadema wavutana
Na Mussa Juma, Kiteto


MATOKEO ya mwanzo ya uchaguzi mdogo wa ubunge uliofanyika jana katika Jimbo la Kiteto, yanaonyesha mgombea kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Victor Kimesera, anaongoza dhidi ya mpinzani wake mkuu, Benedict Nangoro wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika uchaguzi huo.


Hata hivyo, CCM wanadai kuwa mgombea wao anaendelea kuzoa kura katika kata kadhaa, hivyo kuwa na uhakika kwamba ataibuka mshindi na kukirudisha kiti hicho mikononi mwao.


Hadi kufikia jana wakati tunaenda mtamboni, majira ya saa 3:00 usiku, Kimesera ambaye ni Mkurugenzi wa Baraza la Wazee wa Chadema, alikuwa akiongoza katika baadhi ya vituo vilivyopo katika kata saba kati ya kata 15 za jimbo hilo kwa kupata kura 6,149 na kumwacha kwa mbali mgombea wa CCM, Nangoro aliyepata kura 3,672.


Kata hizo, ni Kibaya, Bwagamoyo, Lengatei, Matui, Njoro, Olboroti na Partimbo.


Matokeo ya vituo vyote vilivyoko katika Kata ya Kibaya iliyoko mjini Kiteto, hadi kufikia jana jioni, ndiyo pekee yalikuwa yamepatikana.


Katika kata hiyo iliyokuwa na wapigakura 1,605, Kimesera alishinda uchaguzi huo kwa kupata kura 1,153 na kuwaacha kwa mbali Nangoro wa CCM aliyeambulia kura 450. Jumla ya waliojiandikisha katika kata hiyo, ni watu 3,092.


Kutokana na matokeo hayo, mamia ya wafuasi wa Chadema na wa vyama vingine vya upinzani, walimiminika mitaani na kuanza kusherehekea kwa amani ushindi huo.


Hali hiyo iliwafanya askari wa Kutuliza Ghasia (FFU) kuingilia kati na kuanza kuwatawanya wafuasi hao.


Hata hivyo, katika Kata ya Partimbo ambako ni ngome ya CCM, mgombea wao, Nangoro alikuwa akiongoza kwa kura 1,033 dhidi ya kura 787 alizopata Kimesera wa Chadema.


Taarifa hizo zinaeleza kwamba katika Kata za Dosidosi na Engusero ambayo ni maeneo ya wafugaji CCM inaongoza ingawa hazikusema kwa kiasi gani cha kura.


Hata hivyo, kwa mujibu wa Msimamizi wa Uchaguzi jimboni hapa, Festo Kang'ombe, matokeo kamili ya uchaguzi huo, yatatolewa leo saa 5:00 asubuhi.


Katika matokeo hayo ya awali ya baadhi ya vituo katika Kata ya Bwagamoyo, mgombea wa Chadema, alikuwa akiongoza kwa kupata kura 1,055 dhidi ya kura 706 alizopata mgombea wa CCM.


Katika Kata ya Lengatei, Chadema ilikuwa imepata kura 234 wakati wa CCM alipata kura 113. Kata ya Matui, Chadema (kura 1,602), CCM (kura 685), Kata ya Njoro, Chadema (kura 496), CCM (kura 307), Kata ya Olboroti Chadema (kura 822), CCM (kura 378) na Kata ya Partimbo, CCM (kura 1,033), Chadema (kura 787).


Hata hivyo, uchaguzi huo ambao ulifanyika kwa amani, ulitawaliwa na mapungufu kadhaa katika baadhi ya vituo vya kupigia kura.


Baadhi ya mapungufu hayo ni katika Kituo cha Kaloleni, zaidi ya wapigakura 50 walishindwa kupiga kura kutokana na majina yao kutoonekana kwenye orodha ya wapigakura licha ya kuwa na shahada.


Kata ya Matui ambayo ni moja ya kata yenye wapigakura wengi, kulikuwa na upungufu wa tatizo la upungufu wa fomu namba 21 'B' ya matokeo ya jumla hasa katika kituo cha Azimio.


Hata hivyo, akizungumza na mwandishi wa habari hii, Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Kiteto, Kang'ombe alikiri kuwapo na mapungufu katika baadhi ya vituo, lakini akasema mengi yalipatiwa ufumbuzi.


"Ni kweli kulikuwapo na upungufu katika baadhi ya vituo kwa wapigakura kutokana majina yao, lakini kulitokana na wao kutokuwa makini katika kutafuta majina yao na matatizo ya kibinadamu wakati wa uchapaji wa orodha ya wapigakura," alisema Kang'ombe.


Katika vituo vyote vya kupigia kura jana, kulikuwapo na askari wa FFU hali iliyosababisha uchaguzi kuwa shwari wakati wote.


Tuma maoni kwa Mhariri
 
Kwani matokeo yalishatangazwa rasmi na tume ya uchaguzi?
Wapinzani wasife moyo ni kusonga mbele,ni kujikagua walipopungua na kuanza upya kupanga mikakati kwa miezi 30 iliyobaki kufika uchaguzi mkuu wa Rais na wabunge.
Kwa kweli Vyombo vyetu vya dola vinashangaza kwa kutowajibika ipasavyo hasa katika hizi chaguzi,Sijui nao wamekuwa wanasiasa?kwa kuwa walichangia kuwadhoofisha wapinzani.Kilichonishangaza zaidi ni vyombo usalama pamoja na mkuu wa Wilaya eti kumsihi Kptn Komba kushuka jukwaani wakati hakustahili kuwepo uwanja ule wa kapteni!Liko Jeshi la polisi na usalama wa Taifa?

Jitihada ya SISIEMU kuzima hisia za wananchi haziondoi kudra ya kwa Mwenyezi Mungu kwa waja wake.Voksi populi vksi dei
 
Mimi sioni sababu ya kuendelea kusubili, usitegemee sisiem kushidwa ukizingatia wametoka kwenye kashifa ya richard monduri. Watafanya kilaliwezekanavyo either ni la haki au sio la haki ili washinde.

Kwa ufupi lazima washinde tu, kutokana na mazingira tuliojiwekea sisi watz
 
Watu hapa tutatafuta wachawi wee,lakini ukweli ni kuwa wananchi wa Tanzania ni fools(people lacking good sense and good judgement) They deserve what they are getting because they choose to have that.
Wako tayari kutoandamana kuishinikiza serikali kuwachukulia hatua Maafisadi lakini wako tayari kwenda kuandamana kumpokea Lowassa. Tanzanians are cheap like a bunch of groundnuts.We are easly bought therefore we are cheaply treated.

Chukua kwanza 5 halafu wakati namalizia nitakupa tena 5 ziwe 10..

Ni hivi: Pamoja na kuwa uchaguzi si suala la upinzani tu kushinda ndio uchaguzi uonekane wa haqq lakini kiukweli watanzania tunataka tufunguliwe mlango wa 'Maendeleo' kwa kugonga mlango ulioandikwa 'Umaskini'..hivyo sisi wenyewe ndo wachawi wa maendeleo yetu, haswa linapokuja suala la kuchagua viongozi wa kutuwakilisha..

Suala la wananchi wetu kuwa gullible masses sio la kupuuza na ndio maana ndugu yangu mmoja alishajiapiza kwa jina Mungu wake kuwa katu hatopoteza muda wake kuvote only to see his vote evaporated and outweighted by gullible masses. Hii ni serious issue kama cancer ambapo cell ambayo ilitegemewa kuwa chanzo cha uhai ndio inakuwa ya kwanza kuuondoa uhai..

Nakumbuka hata kipindi napata exposure kwenye ancient philosophy, kuna philosopher mmoja alipinga kabisa hoja ya kura- moja-mtu-mmoja kwani kuna uwezekano kuwa democracy ya aina hiyo is NOT necessarily the best way kumpata kiongozi bora haswa kwenye case ya cheap folks ..

5 nyingine hizoo
 
kushindwa kwa upinzani ni mipango mibovu waliyonayo wiongozi wao,lazima upinzani uwe na mipango ya muda mfupi na mrefu ktk kuhakikisha wanashinda ktk hizi chaguzi mbalimbali.
Ili upinzani uweze kushinda ni lazima kufanya tathimini ya uchaguzi uliopita kwa kina ilikujua kwa nini wagombea wao walishindwa ktk chaguzi hizo bila kuoneana haya.pia wanatakiwa kuhakikisha kuwa wanakuwa na watu tayari ambao wanaandaliwa kwa ajili ya kugombea hizi nafasi mbalimbali kwa kuwaandaa mapema,tunajua wazi tunauchaguzi mkuu 2010,kwa maana hiyo vyama vyote vilitakiwa kuwa na watu ambao tayari wapo ktk mkakati wa kuwania nafasi mbali mbali wakati muda muafaka utakapo fika.

Hawa watu kwa sasa wanatakiwa wawe wameshajijengea mazingira wa kukubalika ktk jamii na wawe wanafanyavitu kwa vitendo sio maneno au ahadi,hii itawasaidia kuonekana tofauti na watu wengine ktk majimbo au vitongoji vyao kwa nafasi za udiwani.
unapofika wakati wa chaguzi basi wananchi hawaulizi mara 2 kwani tayari mtu anakuwa ameshajijengea mazingira mazuri na hivyo kumrahisishia kazi ktk kinyanganyiro cha uchaguzi.
 
Kwaminchi,

Sasa kama nataka ubunge ndugu.. je nifanyeje nishinde?

Mimi nadhani Tz upinzani kuna matatizo..kimkakati, kisera, raslimali n.k.

Upinzani wa kweli CCM igawanyike na kuwapata kama Anna Malecela
20 hivi toka CCM waunde pande mbadala...otherwise hata 2010 nina wasi2 upinzani hata wakiungana basi watabagwa tena ..yaani kirahisi tu!

Angalia since 1995 kura za uraisi upinzani na hata wabunge zimekuwa zinapungua kwa kasi ya ajabu! Why? Ni kweli kuwa walikuwa hawajaungana...ila na je huu uchaguzi Kiteto CUF/NCCR/TLP/CHADEMA mbona walisimamisha mgombea mmoja?
WEWE HUONI KAMA HAWA JAMAA WA CCM WASHAGAWANYIKA MANA KUNA MAMBO WALIKUBALIANA SASA WAMESHINDWA KUYATEKELEZA WAMEMTOSA LOWASSA.SASA EL KAANZISHA MTANDAO WAKE WE SUBIRI 2010 TUTAONA MAAJABU HUKO BONGO.
 
kwa hiyo CCM wameshinda au? acha washinde tuu kama wameshinda kihalali ingawaje sipendi.
 
hallo wajukuu zangu..........

hali zenu, babu yenu nimerudi tena.kwanza niwape pole wajukuu zangu waliokamatwa kwa kuonekana wanaikandamiza serikali. mie nawaambia pole ila msirudi nyuma kwani mna kitu ambacho nafikiri hamkijui...ujasiri.hongereni sana.

pili niwapongeze ccm kwa ushindi waliopata kule kiteto. hii inaonyesha kwamba watu bado wana imani nanyi na kwamba wanataka muendelee kusafisha huu uzembe uliojaa miongoni mwa watendaji.

ninafurahisha sana na haya na kwa kweli nikupe pongezi mh. raisi na mwenyekiti wa richama hili. kwa kweli mwanawane,endelea wala usirudi nyuma. sisi wazee wako tunakuombea dua.

kwa vijana wangu wapenda mabadiliko na sio maendeleo, napenda kuwaambia kuwa kura zinawekwa kwenye box baada ya mtu kuridhika na hoja za msingi katika maisha yake.naomba muelewe watu katika utandawazi wanajua helicopter na wala hawashtuki. mnawaambia nini au mnawaahidi nini, ndicho cha msingi.

nimuunge mkono mjuu wangu , kitila mkumbo kwamba yawezekana upinzani umekosa mbinu za msingi za kuiondoa ccm madarakani.mie nakuambieni jipangeni tena kwani hawa jamaa wagumu.

aluta kontinua.....wabheja sana!
 
Well, it is painful maana kila juhudi zimefanyika ili CHADEMA washinde. Bila shaka bado tuna shida ya kimkakati katika upinzani na tunahitaji kujipanga vizuri zaidi. Lakini pia naamini bado kuna issue ya kujiamini kwa upande wa wananchi kwa maana ya kuamini kwamba wana uwezo na uhuru wa kuchagua kile roho yao inataka. Kwa hiyo pamoja na umuhimu wa upinzani kukaa chini na kujipanga vizuri zaidi, bado kuna haja ya ku-intesify kabisa elimu ya siasa kwa wananchi wetu ili wafike mahala wajiamini na wafanye maamuzi bila kuogopa vitisho. Baada ya kusema yote haya, ni vigumu sana kuamini kwamba matokeo haya yanaonyesha imani walionayo wananchi kwa CCM, maybe I am wrong!


Nakubaliana na wewe Kamanda na moja ya mikakati mibovu ni kwa Chadema ku hijjack the whole campaign na kuwa ya Ki-chadema zaidi badala ya umoja wa wapinzani.

Niliwahi kuta hadharisha kuhusu hili mwanzoni mwa thread hii, tumeshuhudia ubinafsi mkubwa wa wanachadema na matokeo yake ule ushirikiano wa vyama umekuwa hauna maana yeyote.

Kabla hamjaanza na ule utaratibu wenu wa kawaida wa kudai mmeibiwa kura, vitisho, sumu nk kwanza safisheni nyumba yenu ni chafu mno.
 
Watu hapa tutatafuta wachawi wee,lakini ukweli ni kuwa wananchi wa Tanzania ni fools(people lacking good sense and good judgement) They deserve what they are getting because they choose to have that.
Wako tayari kutoandamana kuishinikiza serikali kuwachukulia hatua Maafisadi lakini wako tayari kwenda kuandamana kumpokea Lowassa. Tanzanians are cheap like a bunch of groundnuts.We are easly bought therefore we are cheaply treated.

Wewe watukane wazee wako tu.. wakichagua chadema/wapinzani ndio wanakuwa werevu?
 
Ushindi ni mikakati na si hoja peke yake. Mikakati hupangwa na wataalamu wa mikakati (political strategists) na siyo wagombea au wanasiasa. Fani ya kampeni inahusisha sayansi na sanaa. Kwa hili CCM bado wako mbali sana kuweza kufikiwa.

Hata mikakati michafu ni mikakati katika siasa; Kwa wapinzani kutegemea wanaweza kushinda kwa kucheza michezo mizuri na kuwa waungwana inakuwa vigumu kwao kushinda. Kutegemea kushinda kwa kupigiwa kura na watu wengi zaidi bila ya kujua ni kina nani wanatakiwa kukupigia kura ni vigumu.

Hivyo, kama CCM wameshinda na ninaamini hivyo watakuwa wameshinda kwa kuwazidi wapinzani mikakati (hata mikakati mibovu) na wanaelewa kuwa siasa bado ni fani inayohusi mikakati na counter-mikakati. Kwa hili natoa pongezi kwa CCM kwa ushindi wao na kuendelea kutoa funzo kuwa hoja hujibiwa kwa hoja, na hoja za kushinda kura hujibiwa kwa mikakati ya ushindi.

Tutake tusitake, CCM bado ni chama ambacho kina mvuto wa aina yake na ambacho kutokana na vitu vingine bado kinashawishi utii wa ajabu. Hebu tuangalie kidogo ni jinsi gani mgombea wa Chadema angeweza kushinda?

Mwaka 2005, waliojiandikisha kupiga kura Kiteto walikuwa ni 74,632. Mgombea wa CCM Bw. Losorutia alishinda kwa kupata kura 30,483 sawa na asilimia 56.3 wakati mgombea wa Chadema Bw. Kimesera alipata kura 22,565 sawa na asilimia 41.7. Kimsingi CCM iliishinda Chadema kwa "double digits" yaani asilimia 14.6.

Tofauti kati ya mshindi na aliyeshindwa ni kura 7918. Hii ndiyo namba ambayo ingeweza kuleta tofauti katika uchaguzi huu, na ni namba hii ambayo Chadema walitakiwa kuishawishi kuwapigia kura. CCM haikuhitaji kuwashawishi kuwapigia kura bali kuwashawishi wanachama wake na wale waliowapigia kura kuwapigia kura tena. Hapo ndipo mkakati wa ushindi unapotokea.

Kwa kadiri ambavyo matokeo yanajulikana hadi hivi sasa ambapo CCM imeshinda, uchambuzi utakuwa ni jinsi gani Chadema waliweza kuwashawishi hao watu 7000 kuwapigia kura. Hivyo basi, ushindi wa CCM utakuwa convincing kama wameweza kuchota wapiga kura zaidi toka upinzani, kwa kushinda kwa zaidi ya kura 7000. Endapo ushindi wa CCM utakuwa chini ya kura 2000 au hata 4000 itaonesha kuwa kwa kiwango kikubwa Chadema waliweza kushawishi wapiga kura waliopigia kura CCM mwaka 2005 kuwapigia kura. Pamoja na hayo hayo hawakuweza kuwashawishi watu wengi kwani, CCM ingeweza kushinda bila kura hata moja ya walioipigia Chadema 2005, lakini Chadema isingeweza kushinda bila kura ya waliopitia CCM 2005.

Hongera CCM kwa ushindi.

Idadi ya kura imeanza kuingia, nitawapa taarifa muda si mrefu kupitia KLHN.
 
Ushindi ni mikakati na si hoja peke yake. Mikakati hupangwa na wataalamu wa mikakati (political strategists) na siyo wagombea au wanasiasa. Fani ya kampeni inahusisha sayansi na sanaa. Kwa hili CCM bado wako mbali sana kuweza kufikiwa.

Hata mikakati michafu ni mikakati katika siasa; Kwa wapinzani kutegemea wanaweza kushinda kwa kucheza michezo mizuri na kuwa waungwana inakuwa vigumu kwao kushinda. Kutegemea kushinda kwa kupigiwa kura na watu wengi zaidi bila ya kujua ni kina nani wanatakiwa kukupigia kura ni vigumu.

Hivyo, kama CCM wameshinda na ninaamini hivyo watakuwa wameshinda kwa kuwazidi wapinzani mikakati (hata mikakati mibovu) na wanaelewa kuwa siasa bado ni fani inayohusi mikakati na counter-mikakati. Kwa hili natoa pongezi kwa CCM kwa ushindi wao na kuendelea kutoa funzo kuwa hoja hujibiwa kwa hoja, na hoja za kushinda kura hujibiwa kwa mikakati ya ushindi.

Tutake tusitake, CCM bado ni chama ambacho kina mvuto wa aina yake na ambacho kutokana na vitu vingine bado kinashawishi utii wa ajabu. Hebu tuangalie kidogo ni jinsi gani mgombea wa Chadema angeweza kushinda?

Mwaka 2005, waliojiandikisha kupiga kura Kiteto walikuwa ni 74,632. Mgombea wa CCM Bw. Losorutia alishinda kwa kupata kura 30,483 sawa na asilimia 56.3 wakati mgombea wa Chadema Bw. Kimesera alipata kura 22,565 sawa na asilimia 41.7. Kimsingi CCM iliishinda Chadema kwa "double digits" yaani asilimia 14.6.

Tofauti kati ya mshindi na aliyeshindwa ni kura 7918. Hii ndiyo namba ambayo ingeweza kuleta tofauti katika uchaguzi huu, na ni namba hii ambayo Chadema walitakiwa kuishawishi kuwapigia kura. CCM haikuhitaji kuwashawishi kuwapigia kura bali kuwashawishi wanachama wake na wale waliowapigia kura kuwapigia kura tena. Hapo ndipo mkakati wa ushindi unapotokea.

Kwa kadiri ambavyo matokeo yanajulikana hadi hivi sasa ambapo CCM imeshinda, uchambuzi utakuwa ni jinsi gani Chadema waliweza kuwashawishi hao watu 7000 kuwapigia kura. Hivyo basi, ushindi wa CCM utakuwa convincing kama wameweza kuchota wapiga kura zaidi toka upinzani, kwa kushinda kwa zaidi ya kura 7000. Endapo ushindi wa CCM utakuwa chini ya kura 2000 au hata 4000 itaonesha kuwa kwa kiwango kikubwa Chadema waliweza kushawishi wapiga kura waliopigia kura CCM mwaka 2005 kuwapigia kura. Pamoja na hayo hayo hawakuweza kuwashawishi watu wengi kwani, CCM ingeweza kushinda bila kura hata moja ya walioipigia Chadema 2005, lakini Chadema isingeweza kushinda bila kura ya waliopitia CCM 2005.

Hongera CCM kwa ushindi.

Idadi ya kura imeanza kuingia, nitawapa taarifa muda si mrefu kupitia KLHN.

mkuuu ile kauli mbiu yako ya kuwa KIteto mtatufunza demokrasia imefikia wapi?


sawhib nnakupenda kwa kuruka vihunzi
 
baada ya tamaa ya fisi kuona kuwa mkono wa binaadamu utaanguka wapinzani waliona kuwa CCM ambayo kwa sasa ina kazi kubwa ya kujisafisha na kujipanga itapoteza jimbo la kiteto.

wakawa na tamaa ya kuwa CCM itaanguka tu, wakaenda kwa majigambo na kedi, wakajiamini kupita kiasi.

magazeti yakanadi hapa JF kina Mkjj na wenziwe wakajilabu vya kutosha kuwa kipindi hiki wapinzani watatoa somo ambalo CCM hawatalisahau.

lakini baada ya kuona kinyume wazee wetu wamenywea hakuna breaking news wala cha nn kimya utadhani hakuna uchaguzi.


kilichobaki ni kusubiri matetezi ya ndugu zetu wapinzani.

wapinzani jee umoja wao utadumu?

jee watasoma alama za nyakati au watasubiri huruma ya wananchi bila ya jasho?

hivi ni kweli wananchi ni wajinga wakikichagua CCM ?


lini hii jeuri ya kuwadharau wananchi itakoma kwa wananchi?


lengo la CCM ni kuhakikisha bunge la 2010 kuwe hakuna wapinzani bungeni isipokuwa wapemba tena na huko tutagawana nusu kwa nusu.


tutawafunza kuwa jeuri si maungwana na siasa si lelemama
 
Uwe na uhakika na unachosema.. umeangalia KLH News tangu jana..? ushabiki mwingine hata hauna msingi.
 
lengo la CCM ni kuhakikisha bunge la 2010 kuwe hakuna wapinzani bungeni isipokuwa wapemba tena na huko tutagawana nusu kwa nusu.


tutawafunza kuwa jeuri si maungwana na siasa si lelemama

Mtu wa pwani, unaona raha gani kwa kuwa na wabunge wa CCM tu? Watanzania wazalendo wanapongeza jitihada wa Wabunge wa upinzani japo ni wachache. achana na uccm ndugu yangu, jali maslahi ya taifa. Ni masikitiko makubwa kwa CCM kupewa kiti kingine cha ubunge licha ya blanda walizizifanya kwa kukumbatia mafisadi.
 
mkuuu ile kauli mbiu yako ya kuwa KIteto mtatufunza demokrasia imefikia wapi?


sawhib nnakupenda kwa kuruka vihunzi
tatizo lako unafikiri haya mapambano ni personal. Halafu unafikiri nimeruka viunzi; sasa ulitaka niseme vipi? jaribu kuniweka kwenye chupa ya fikra zako, bahati mbaya you can't contain me. Wenzako walijaribu.
 
Mtu wa pwani, unaona raha gani kwa kuwa na wabunge wa CCM tu? Watanzania wazalendo wanapongeza jitihada wa Wabunge wa upinzani japo ni wachache. achana na uccm ndugu yangu, jali maslahi ya taifa. Ni masikitiko makubwa kwa CCM kupewa kiti kingine cha ubunge licha ya blanda walizizifanya kwa kukumbatia mafisadi.


wapinzani bado si wanasiasa tunataka tuwape darasa la kuwa waangalizi ili wajifunze siasa na wapunguze haya maneno ya kifedhuli
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom