Uchaguzi wa Kiteto: Taarifa mbalimbali

Uchaguzi wa Kiteto: Taarifa mbalimbali

Status
Not open for further replies.
Kaka Ahsante na wewe. Inabidi nilale maana saa hizi, ni kulala kwa dakika chache si saa chache. Hayo ni matokeo ya saa 7.15 (01.15hrs) ambako CCM walikua wakiongoza kwa tofauti ya kura takriban 2000, lakini kasi ya Chadema ilikua kubwa kwani saa 6.06(00.06) CCM walikua wakiongoza kwa tofauti ya kura 4,000 ambazo baada ya saa moja za Chadema ziliongezeka. Lakini wakati huo sehemu kubwa walikua wamekwisha kuhesabu. Kuna UKIUKWAJI mkubwa wa taratibu katika uchaguzi huo na kwa hali ilivyo KAMA CCM watashinda itakua ni ushindi wa AIBU. Kwa idadi kubwa ya wabunge walionao hawakua na sababu ya kufanya yaliyotokea Kiteto, pamoja na kuwa ni MKAKATI WA kuzuia UPEPO wa MABADILIKO.

Halisi,

Asante sana kwa kutufahamisi hizo za huko Kiteto. Nafikiri CCM hawakuwa tayari kuona wimbi la mabadiliko linaendelea maana wananchi wakishajua mwisho wa CCM unakaribia, basi wangeongeza speed ya kuwamaliza.

Pia mimi nina matatizo makubwa na strategy ya CHADEMA hasa kwenye suala la umoja wa vyama. Wameenda kule kama CHADEMA zaidi badala ya umoja wa vyama. Naelewa sheria haziruhusu mgombea wa muungano wa vyama, lakini bado ningelikuwa mimi jina la CHADEMA lingeishia kwenye hizo forms na makaratasi ya kupigia kura.

Kampeni nzima ingeendeshwa kama vyama vya upinzani na ingesimamiwa na kiongozi wa chama kingine. Kwa mfano kwasababu mgombea alikuwa wa CHADEMA basi Mrema au Lipumba ndiye angeongoza kampeni, huku Mbowe anafuata nyuma.

Kuwakosa CCM wakati huu ambao kila mtu anawaona ni mafisadi naona ni pigo kubwa sana kwa upinzani. Kama waliko na mashabiki wengi, watu wachache walipiga kura, huenda hapo CCM walinunua kadi za kupigia kura na kuzichoma moto.

Kuwashinda hawa jamaa lazima upinzani wawe wamejiandaa kuwatoa CCM kwa knock out.
 
CCM wanaelekea kushinda japo kwa tofauti ndogo kama hakutakua na muujiza wowote katika maeneo machache yaliyosalia. Nadhani huu ni wakati ambao Chadema wamefanya mazoezi ya kulichukua hilo jimbo 2010 kwani CCM wakati huo kila mtu atakua anatetea jimbo lake na si wote kuhamia Kiteto. TATIZO KUBWA (SIJUI KWANINI) zaidi ya nusu ya wapiga kura hawajajitokeza kupiga kura na zaidi katika maeneo ambayo mgombea wa CHADEMA ana wafuasi wengi. Inawezekana ilikua ni mkakati maalumu wa CCM na hapo ndipo wapinzani wanapopata fundisho la kujiandaa kwa mikakati na si mambo ya "mbwembwe". CCM wanaangalia wapi ulipopasahau na hapo ndio watapita, hawana njia moja ya kupata ushindi. Wakikosa katika kampeni za kawaida watakumaliza kampeni za kimkakati, wana timu na wataalamu wa kila fani wakiwamo wanaolipwa fedha za walipa kodi (watumishi wa serikali). Tuna safari ndefu ya kutokea mabadiliko katika nchi hii.

Mtazamo safi sana halisi.
Ijapokua CCM wamesambaratika na kashfa zinazokumba nchi ni wazi kuwa upinzani wana-homework ya kufanya.This will always take time maana democracy has to mature.Pia hilo swala la watu kujitokeza kupiga kura hua lipo in most places maana ari ya kujitokeza huonekana sana wakati wa uchaguzi mkuu.
Civil Education has to be promoted through NGO's.The government itself and other organs of State.Hapo nd'o tutaweza kusema vizingiti vya demokrasia vimeanza kukita.It will take time lakini tutafika.Asanteni

Kwa muda wenu tetembeleeni: http://www.eastafricayote.com/index.php
 
mpya zilizopo kuwa chadema wameangukia pua.

tunatanguliza pole zetu kwa ndugu zetu na wamejitahidi sana ila ndio hivyo bado ni wachanga mno.

wache wajipange zaidi huenda baada ya miaka 20 wanaweza kuaminila alau kupata baadhi ya majimbo.


sasa uchaguzi umeisha tushirikiane ktk kuijenga kiteto na tanzania

Mimi nitakuwa Thomaso hadi pale nitakapoona matokeo rasmi walau kura 40,000 zikiwa zimehesabiwa na walau sisiem inaongoza kwa zaidi ya kura 10,000 ndio niweze kusema ni kweli wameshinda vinginevyo hakuna mshindi hadi sasa. Tusubiri matokeo in term of numbers sio maneno.
 
Mimi nitakuwa Thomaso hadi pale nitakapoona matokeo rasmi walau kura 40,000 zikiwa zimehesabiwa na walau sisiem inaongoza kwa zaidi ya kura 10,000 ndio niweze kusema ni kweli wameshinda vinginevyo hakuna mshindi hadi sasa. Tusubiri matokeo in term of numbers sio maneno.

no haya si maneno tu hizi ni habari za ndani/. la kama huamini subiri magazeti hapa jf ss hupokea habari in first hand.

ila nnachosubiri ndugu zangu kuja na sababu za kushindwa. huenda wakaja kutwambia alipewa sumu, komba kaimba kwenye mkutano wao, polisi walipendelea, ccm imetumia dola, na mengi ya uzushi.

nitawaona mashujaa kama chadema kukubali matokeo bila ya manung'uniko na kukubali asiekubali kushindwa si mshindani.

upinzani unahitaji kujipanga zaidi, wasikate tamaa jitahidini sana.

na usione simba karoa ukadhani kesha.
 
no haya si maneno tu hizi ni habari za ndani/. la kama huamini subiri magazeti hapa jf ss hupokea habari in first hand.

ila nnachosubiri ndugu zangu kuja na sababu za kushindwa. huenda wakaja kutwambia alipewa sumu, komba kaimba kwenye mkutano wao, polisi walipendelea, ccm imetumia dola, na mengi ya uzushi.

nitawaona mashujaa kama chadema kukubali matokeo bila ya manung'uniko na kukubali asiekubali kushindwa si mshindani.

upinzani unahitaji kujipanga zaidi, wasikate tamaa jitahidini sana.

na usione simba karoa ukadhani kesha.

Mtu wa Pwani
Huwa naheshimu hoja zako lakini kwa hili sikuamini. Sihitaji kujua source ila tuambie how those people came to conclusion that CCm imeshinda kwa maana ingine kuna numbers. Tupe hizo number vinginevyo nashawishika kuita ni habari za kidaku
 
Mtu wa pwani naomba nitofautiane na kauli yako hapo juu!!!!!!! Kumbuka kwamba uchaguzi una taratibu zake na ukiukwaji wa makusudi wa taratibu hizo basi huufanya uchaguzi huo kutokuwa huru na haki!!!!!!!!!

Chadema wanaweza kutumia mapungufu yeyote ya msingi yaliyojitokeza kupinga matokeo na hiyo ni sehemu halali demokrasia. Hivyo basi kuanza kubeza mapema kabisa namna hii wakati hata matokeo hayajajulikana ni dalili za ushabiki usiokuwa na tija na inaweza pia kuashiria kuwa aidha una chuki na chadema au wanachadema au mashabiki wa chadema.
 
Heshima mbele.....

Mi nadhani nijiunge na wengine aliotangulia na kusema, "tusiandikie mate ingali wino upo" tumengoja kwa muda wote huo itakuwa haya masaa machache tu kusikia oficial results, lets wait and see!!!

Cheers
 
Nawapa matokeo ambayo yamefanyiwa kazi kwa mujibu wa timu ya CHADEMA iliyopo Kiteto.

Kwa sasa ni kuwa mkurugenzi ndio ameingia kwenye kujumlisha na bado matokeo haya sio ya mwisho kwani kuna kata mbili na baadhi ya vituo matokeo hayajapatikana kutokana na miundo mbinu mibaya.


CHADEMA CCM PPT SAU

Bwagamoyo 1055 706 0 2

Dongo 355 900 3 18

Dosidosi 478 1100 0 0

Engusero 1007 1992 0 0

Kibaya 1153 450 1 1

Kijungu 454 1605 0 8

Lengatei 234 113 0 0

Makame 11 839 0 0

Matui 2839 2216 12 33

Ndedo 22 940 0 5

Njoro 862 1367 8 20

Olboloti 923 679 4 11

Partimbo 1360 2771 16 32

Songambele 483 899 7 16

Sunya 618 1357 0 0

TOTAL 11854 17934 51 146


USHINDI 39.53% 59.81% 0.17% 0.49%


40.14% Overall Turnout


Nawatakia kusoma na kutafakari kwa kina mpaka kieleweke,.
 
Mtu wa pwani naomba nitofautiane na kauli yako hapo juu!!!!!!! Kumbuka kwamba uchaguzi una taratibu zake na ukiukwaji wa makusudi wa taratibu hizo basi huufanya uchaguzi huo kutokuwa huru na haki!!!!!!!!!

Chadema wanaweza kutumia mapungufu yeyote ya msingi yaliyojitokeza kupinga matokeo na hiyo ni sehemu halali demokrasia. Hivyo basi kuanza kubeza mapema kabisa namna hii wakati hata matokeo hayajajulikana ni dalili za ushabiki usiokuwa na tija na inaweza pia kuashiria kuwa aidha una chuki na chadema au wanachadema au mashabiki wa chadema.

no no no, wapinzani wote hatuwachukii, ss tunawaita watani wetu sasa mtani huchukiwa?

ila mtani tunamwambia ile njozi yake ya kudhani mkono utaanguka amepwerewa pwere.

wenye kusubiri namba wasubiri ila ss tunajipongeza kwa mishkaki ya kondoo na shurba
 
vipi kuhusu majina ya wapiga kura kukosekana kwenye orodha, hasa kwenye stronghold ya chadema, tunaomba mtu wa kujustify uzembe huu wa kunyima watu haki yao ya msingi ya kidemokrasia, YA KUPIGA KURA?
 
someni matokeo kutoka kushoto kwenda kulia inaanza na CHADEMA,CCM ,PPT NA SAU.

Imegoma kuattach excel ndio maaana imekuwa hivyo wakuu samahanini.
 
someni matokeo kutoka kushoto kwenda kulia inaanza na CHADEMA,CCM ,PPT NA SAU.

Imegoma kuattach excel ndio maaana imekuwa hivyo wakuu samahanini.


wape namba wenye kutaka namba.

mie nnawasubiri watetezi wa kutokubali kushindwa.

lini tutajifunza kukubali kushindwa bila ya kulalamika?


mna hakika gani kama majina yasioonekana kuwa ni upinzani pekee?

jee suali hilo ni la ccm au tume? jee idadi yao laiti wengeipigia chadema ingebadilisha mshindi?


tunakusubirini, mie nnajua wengi wanajua matokeo yote ila wanaona haya kutoka kwa walioyasema.

sasa wanatafuta watoke vp?

mkjj na wenzenu njooni, kuvunjika kwa koleo sio mwisho wa uhunzi
 
1. Chadema kuna nini? Hata hiki kiti kimoja tu mnashindwa? Au ni kusindwa tu kawaida? Kuna matatizo ndani ya Chama? Au bado ni mbinu chafu za CCM? Je Chadema hakukuwa na mbinu chafu nao? Well kwa mwelekeo huu basi Upinzani una mda mrefu kupata fursa kuongoza dola Tz- as CCM wataendelea kutawala kwa miaka mingi ijayo! Poleni, it is a challenge CHADEMA, mmejifunza, tusonge mbele!

2. Naomba ushauri- Sasa mimi kwa sasa sina Chama na ni mzalendo kweli (Halisi)..nauliza kama nataka kugombea nijiunge na Chadema au CCM?
 
Unanichekesha, yaani unataka kujiunga katika chama kwa lengo moja tu, la kugombea ubunge? Bora ubaki hivyo hivyo, bila ya chama, uendelee kuwakebehi wapinzani.
 
Unanichekesha, yaani unataka kujiunga katika chama kwa lengo moja tu, la kugombea ubunge? Bora ubaki hivyo hivyo, bila ya chama, uendelee kuwakebehi wapinzani.

Kwaminchi,

Sasa kama nataka ubunge ndugu.. je nifanyeje nishinde?

Mimi nadhani Tz upinzani kuna matatizo..kimkakati, kisera, raslimali n.k.

Upinzani wa kweli CCM igawanyike na kuwapata kama Anna Malecela
20 hivi toka CCM waunde pande mbadala...otherwise hata 2010 nina wasi2 upinzani hata wakiungana basi watabagwa tena ..yaani kirahisi tu!

Angalia since 1995 kura za uraisi upinzani na hata wabunge zimekuwa zinapungua kwa kasi ya ajabu! Why? Ni kweli kuwa walikuwa hawajaungana...ila na je huu uchaguzi Kiteto CUF/NCCR/TLP/CHADEMA mbona walisimamisha mgombea mmoja?
 
Ni kwasababu wameshindwa... otherwise kungekuwa na zaidi ya mabandiko kumi kuhusu kiteto

Mhh. hata kama wameshindwa haifurahishi hata kidogo. tunahitaji more wabunge toka upinzani ili tusonge mbele kwa kasi.
 
1. Chadema kuna nini? Hata hiki kiti kimoja tu mnashindwa? Au ni kusindwa tu kawaida? Kuna matatizo ndani ya Chama? Au bado ni mbinu chafu za CCM? Je Chadema hakukuwa na mbinu chafu nao? Well kwa mwelekeo huu basi Upinzani una mda mrefu kupata fursa kuongoza dola Tz- as CCM wataendelea kutawala kwa miaka mingi ijayo! Poleni, it is a challenge CHADEMA, mmejifunza, tusonge mbele!

2. Naomba ushauri- Sasa mimi kwa sasa sina Chama na ni mzalendo kweli (Halisi)..nauliza kama nataka kugombea nijiunge na Chadema au CCM?

Well, it is painful maana kila juhudi zimefanyika ili CHADEMA washinde. Bila shaka bado tuna shida ya kimkakati katika upinzani na tunahitaji kujipanga vizuri zaidi. Lakini pia naamini bado kuna issue ya kujiamini kwa upande wa wananchi kwa maana ya kuamini kwamba wana uwezo na uhuru wa kuchagua kile roho yao inataka. Kwa hiyo pamoja na umuhimu wa upinzani kukaa chini na kujipanga vizuri zaidi, bado kuna haja ya ku-intesify kabisa elimu ya siasa kwa wananchi wetu ili wafike mahala wajiamini na wafanye maamuzi bila kuogopa vitisho. Baada ya kusema yote haya, ni vigumu sana kuamini kwamba matokeo haya yanaonyesha imani walionayo wananchi kwa CCM, maybe I am wrong!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom