Uchaguzi wa Kiteto: Taarifa mbalimbali

Uchaguzi wa Kiteto: Taarifa mbalimbali

Status
Not open for further replies.
Wapendwa naona mmesahau kutupatia yanayojiri. kwa wale waliopata msukosuko nawapa pole mpate nguvu kwani siku zimekaribia Wasalaam Aleykum
 
Kama ni wizi wa shahada na kumwaga damu, inavyoonekana CCM haina tofauti na PNU ya nchi jirani.
 
Tupange majeshi kwenda mbele,Bado miezi 30 tunafikia uchaguzi mkuu.Nyani lazima apigwe giladi.
Hatuwezi kubali unyama huu ktk nchi ya kistaarabu.Hakuna katiba inayoruhusu askari awanyuke raia hivyo tena wako mikononi mwao.

Nadhani sisiem mmesikia yaliyokipata cha Musharaf kule PAKISTAN? tena mnanyanyasa watu kwa dhahiri?Tulishapanga majeshi kuwakabiri,mwisho wenu umefika.Bebeni vyuma sisi twatumia hoja.Wanyamwezi/warugaruga(SASI JABELA MITWE) chini ya mtemi ISIKE walimkabiri mjerumani vilivyo pamoja na kuwa na risasi zake,lakini waliendelea na hoja zilizokuwa ktk nyimbo zao na leo tuna historia imeandikwa.HUWA INAFIKIA WAKATI HATA RISASI INASHINDWA.

Mgosi makamba mbona kimya hakanushi kuwa ni sisiem wamefanya ufedhuli?Najua nawe huko hapo kujitahidi kuzima nguvu ya CHADEMA Arusha.Kweli nimeona woga umeifunika sasa sisiem,Pamoja na kuwa na viti vya bunge zaidi ya 200 bado wanang'ang'ania hicho kimoja.Chadema oyeeeeeeeeeeeeee!

Wao wanadhani kuwa wananguvu na uwezo wa kutawala na kunyanyasa watanzania daima kwa kutumia vyombo vya dole. Tatizo hawajui kuwa kuna watu wanaona kinachofanyika na wanachoka siku hadi siku.

Siku inakuja na mwisho wao u karibu.
Kwa sasa ngoja waendelee kunyanyasa kwa kutumia vyombo vyao vya dola bila kumwogopa MUNGU. Kinachoumiza wengine wanajiita mashehe na mapadri na kujifanya ni waumini.... goooosh
 
polisi lazima washtuke kama wamejifanya wanamgambo like janja widi alafu wana zuga kwa nyimbo lazima BRUCE LEE awa HOOHAA.
 
Tena pakiwa pana ugeni mzito; na vyombo vyote vya habari vya dunia vikiwepo. Kama hali hiyo haiwezi kumfanya mtu afikirie mara mbili mbili kutenda jambo kama hili wakati huu; ni kipi asichoweza kukifanya akiwa gizani? Haitatosha bila ya Kikwete kulizungumzia na kulikaripia kwa nguvu jambo hili

Kalamu,

hii ndio tunaita arrogance.... kama ile ya Alfred Mutua wa PNU ambaye watu wanakufa yeye anaanza kutoa namba kuwa waliokufa ni chini ya asilimia 1 ya wakenya wote.

Kuna watu Afrika wanajiona miungu na kinachofanyika Kiteto sasa hivi ni uthibitisho kabisa wa hili.
 
Wakuu, sasa leteni habari za Kiteto. Naona CCM na wao wameamua kuingia na helkopta. It is good wameamua kujifunza kutoka kwa CHADEMA. Nafikiri wananchi sasa wanaweza kuanza kuelewa kuwa kuna mengi wanayokosa kwa kuendelea kuishikilia CCM. Hope wana Kiteto wanafanya kweli kesho.Mpka Kieleweke, please give us up to the minute updates from Kiteto.
 
Vurugu zazidi kurindima Kiteto

2008-02-22 09:57:20
Na Simon Mhina, Kiteto

Maofisa wa Jeshi la polisi na Askari wa Kutuliza Ghasia (FFU) jana walilazimika kumshusha jukwaani Mbunge wa Mbinga na Mkurugenzi wa kundi la sanaa la TOT, kapteni John Komba, baada ya kuibuka vurugu kubwa za kampeni za uchaguzi mdogo katika kata ya Kijungu wilayani hapa.

Vurugu hizo ziliibuka baada ya ratiba ya Tume ya Uchaguzi kuonyesha waliopaswa kufanya mkutano wa kampeni ni CHADEMA badala ya CCM ambapo Kapteni Komba alionekana kulishambulia jukwaa na bendi yake ya TOT.

Jeshi la polisi limelaumiwa kwa kushindwa kuchukua hatua za haraka kudhibiti hali hiyo licha ya viongozi wa CHADEMA kuwasilisha malalamiko hayo kwa jeshi hilo.

Katika tukio hilo, Mpiga picha wa Tanzania Daima, Bw. Joseph Zablon alinusurika kipigo baada ya kutaka kumpiga picha kiongozi wa TOT, Kapteni Komba akishushwa jukwaani.

Mara baada ya kuwasili kikosi cha FFU katika magari mawili, PT 1461, PT 1433 na gari dogo la polisi aina ya Landrover PT 1529, waliokuwa wanaongozwa na Mkuu wa Kikosi cha upelelezi mkoa wa Manyara akiwa pamoja na Mrakibu Mwandamizi wa Polisi (ASP), Ernest Sakawa, walitumia zaidi ya saa moja kumshawishi Kapteni Komba kusitisha kupiga mziki, lakini aligoma.

Hata hivyo, mara baada ya kuwasili Mkuu wa Wilaya ya Kiteto, Bw. John Henjewele na kufanya mazungumzo na maofisa hao wa polisi, walifanikiwa kumshawishi Komba kushuka jukwaani.

``Tunakuomba uzime mziki Mheshimiwa Komba na kushuka chini,`` alisikika mmoja wa maofisa wa polisi akimweleza Komba ambaye baada ya kuimba nyimbo za CCM kwa muda ndipo alishuka.

Awali, akizungumza na waandishi wa habari kijiji hapo, Mkuu wa mkoa wa Manyara, Bw. Henry Shekifu alisema amejionea tatizo hilo na kuahidi kuwa serikali itachukuwa hatua kwa kundi ambalo limevamia mkutano.

``Mimi nimeona lakini sio jukumu langu kuzuia mkutano. Kuna vyombo husika vyenye majukumu hayo nadhani wamepewa taarifa watakuja,`` alisema.

Awali, Bw. Shekifu ambaye yupo katika ziara ya kukagua na kuhamasisha miradi ya maendeleo, aligoma kupigwa picha wala kuzungumza na waandishi wa habari kwa maelezo kwamba hajatoa ruhusa na ni makosa kumpiga picha bila idhini yake.

Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Wilbroad Slaa, alifaya jitihada za kuwazuia vijana waliokuwa tayari wamebeba mawe kushambulia kundi la TOT.

Dk. Slaa aliwaeleza vijana hao ambao walikuwa katika Uwanja wa Shule ya Msingi Kijungu ambapo CHADEMA ndio walikuwa wahutubie kuwa, vurugu zinazofanywa na CCM zinalenga kutaka kusababishwa kusogezwa mbele kwa uchaguzi.

``Vijana wangu kuweni wapole tu hawa wanataka tuwavamie na kuwaondoa kwa nguvu ili vurugu zitokee wapate sababu za kuahirishwa kwa uchaguzi huu,`` alisema Dk. Slaa.

Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kushuka jukwaani na kuzima muziki, Komba alisema kilichotokea ni masuala ya siasa na ni kweli kuwa CHADEMA ndio walikuwa na mkutano katika eneo hilo.

Hata hivyo, alisema waliamua kuvamia eneo hilo sio kufanya mkutano bali ni kupiga muziki na kudai kuwa hata wao CHADEMA hupita katika maeneo yao ya mikutano na kupiga muziki.

Mgombea wa Ubunge wa Jimbo hilo kupitia CHADEMA, Bw. Victor Kimesera, aliwaomba wananchi wa Kijungu kumchagua ili aongeze nguvu katika vita dhidi ya mafisadi na kuwaletea maendeleo.

Msimamizi wa uchaguzi jimbo la Kiteto, Bw. Festo Kang`ombe, naye alikiri kwamba jana kuwa CHADEMA ndio walipaswa kufanya mkutano katika eneo hilo kwa mujibu wa ratiba na alilaumu jeshi la polisi kwa kushindwa kudhibiti vurugu zinazotokana na kukiuka ratiba za mikutano ya kampeni.

Tukio hilo limekuja siku chache tu baada ya viongozi sita wa CHADEMA kuvamiwa na kupigwa na vijana wa CCM na polisi katika kijiji hicho.

Hata hivyo, hadi jana hakuna mtuhumiwa ambaye alikuwa amekamatwa na polisi.

Wakati huo huo, Mwenyekiti wa CHADEMA, Bw. Freeman Mbowe jana alianza kampeni za uchaguzi mdogo wa Jimbo la kiteto kwa kutumia helikopta.

Mapema kabla ya kutua na helkopta bila kuzuiwa, Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Bw. Shekifu na Mkuu wa Wilaya Bw. Henjewele walifika katika Uwanja wa shule ya msingi, Kijungu ambapo helkopta hiyo ilipangwa kutua na kuwaeleza viongozi wa CHADEMA kuwa helikopta hiyo haitakiwi kutumika.

Akizungumza na viongozi hao, Bw. Shekifu alisema serikali mkoani Manyara bado haijakubali kutumika kwa helikopta hiyo kwenye kampeni, kutokana na ukosefu wa taarifa ya ujio wake.

``Hapa leo helkopta haitashuka kwani tumeipinga na hatuna taarifa nayo,`` alisema Shekifu kuwaeleza viongozi wa CHADEMA.

Naye Mkuu wa wilaya hiyo, alifanya kikao na viongozi wa CHADEMA na maofisa wa polisi waliofika katika eneo hilo la Kijungu kutuliza ghasia na kusisitiza kuwa helkopta hiyo haitakubaliwa kutua katika wilaya yake.

``Jambo hili tumelijadili na msimamizi wa uchaguzi na tumekubaliana kuzuwia helikopta hii kutumika katika kampeni,`` alisema Henjewele.

Wakati huo huo, Mwandishi Wetu jijini Dar es Salaam anaripoti kwamba Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), imeruhusu chama chochote cha siasa kuweka wakala wa mgombea wake kutoka sehemu yoyote hata kama ni nje ya Kata au Jimbo la uchaguzi.

Kwa mujibu wa taarifa ya NEC, sheria ya uchaguzi namba 1 ya mwaka 1985 haijaeleza bayana Mawakala watoke ndani au nje ya Kata au jimbo la uchaguzi.

Taarifa hiyo ya NEC iliyotolewa na Mkurugenzi wa uchaguzi wa NEC Bw. Rajabu Kiravu, ililenga kujibu madai ya msimamizi wa uchaguzi katika jimbo la Kiteto Bw. Festo Kang\'ombe, kupiga marufuku wakala wa kusimamia kura kutoka nje ya Kata au jimbo hilo.

Bw. Kiravu alisema, chama chochote kina uhuru wa kuweka mawakala wanaowataka kwa ajili ya kulinda kura za mgombea wao bila kujali kama ni mkazi wa eneo hilo au anatoka nje.

Hata hivyo, NEC imesema msimamizi wa uchaguzi katika kituo ndiyo mwenye mamlaka ya mwisho katika kutoa maamuzi na yeyote atakayeona ameonewa anatakiwa kufuata sheria na kujaza fomu husika.

Kuhusu suala la kuwaapisha mawakala, Bw. Kiravu alisema, kila wakala anatakiwa kuapa kutunza siri mbele ya msimamizi wa uchaguzi.

Alisema agizo hilo ni kwa mujibu wa sheria ya uchaguzi namba 1 kifungu cha 93 (1) ya mwaka 1985.Bw. Kiravu alisema, kesho ndiyo siku ya mwisho ya kuwaapisha Mawakala.

Naye Raymond Kaminyoge anaripoti kwamba Msajili wa Vyama vya Siasa Nchini, Bw. John Tendwa, amelitaka Jeshi la Polisi kuwakamata waliofanya vurugu katika uchaguzi wa jimbo la Kiteto, mkoani Manyara, badala ya \'kukimbizana\' na wauza gongo.

Bw. Tendwa alisema hayo jana jijini Dar es Salaam alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu vurugu zilizotokea hivi karibuni.

Alisema wanapoachia vurugu kama hizo kutokea bila kuwachukulia hatua wahusika, wanaweza kuifikisha nchi hii katika machafuko kama yaliyotokea nchini Kenya.

Alisema inashangaza kuona kuwa pamoja na vurugu zilizotokea waliofanya vurugu hawakukamatwa na kufikishwa katika vyombo vya dola badala yake imetuma maofisa kwenda kufanya uchunguzi.

``Katika kampeni za uchaguzi kunakuwa na polisi wanaolinda usalama, wilaya ya Kiteto ni ndogo inasikitisha kuona kuwa vurugu zimetokea bila watuhumiwa kukamatwa, badala yake polisi wanakimbizana na wauza gongo,`` alisema.

Aliongeza: ``Polisi wasikwepe lawama kwa tukio hilo, hatutaki waje kutufikisha katika matukio mabaya ya kuuana kama yanayotokea nchini Kenya.``

Aliviasa vyama vyote vinavyoshiriki katika uchaguzi huu kuheshimu kanuni za maadili ya vyama vya siasa ili kuepuka ubabe, vurugu na uvunjifu wa amani.

``Katiba ya nchi ibara ya 20 (2) (C) inasisitiza kuwa chama cha siasa hakiwezi kusajiliwa ikiwa katiba yake au sera zake zinakubali au kuchochea vurugu au matumizi ya nguvu kwa maana hiyo chama chochote chenye usajili wa kudumu kinaweza kupoteza sifa ya kuitwa chama cha siasa,`` alisema.

Jumapili iliyopita viongozi sita wa chama cha CHADEMA walijeruhiwa kwa kupigwa, kuchomwa visu na kupuliziwa machoni kemikali ambayo haijatambuliwa.

Kampeni za uchaguzi mdogo katika jimbo hilo unafanyika ili kuziba pengo la aliyekuwa Mbunge wa Kiteto, Bw. Benedict Losurutia aliyefariki mwishoni mwa mwaka jana.

Wakati huo huo, Chama cha CUF kimedai kuwa mashambulizi dhidi ya viongozi wa CHADEMA waliojeruhiwa jimboni Kiteto mkoani Manyara kwenye kampeni za uchaguzi mdogo unaofanyika keshokutwa, yalifanywa na CCM na polisi.

Kaimu Mkurugenzi Haki za Binadamu na Mahusiano na Umma wa CUF, Bw. Mbaralah Maharagande, alitoa madai hayo jana katika taarifa yake iliyosambazwa kwa vyombo vya habari jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi huyo alisema inasikitisha kuona kuwa CCM inakana kuhusika na vitendo hivyo na kuongeza kuwa mashambulizi yanayofanywa na chama hicho wakati wa uchaguzi yanajulikana na mifano ipo wazi na Watanzania wanaijua .

``CUF inasikitishwa na kauli ya Katibu Mwenezi wa CCM Bw. John Chiligati ya kukana vitendo vya vurugu zilizofanywa na makada wa CCM kwa kushirikiana na polisi dhidi ya viongozi wa CHADEMA katika kampeni za uchaguzi mdogo wa jimbo la Kiteto.``
 
Wakuu, sasa leteni habari za Kiteto. Naona CCM na wao wameamua kuingia na helkopta. It is good wameamua kujifunza kutoka kwa CHADEMA. Nafikiri wananchi sasa wanaweza kuanza kuelewa kuwa kuna mengi wanayokosa kwa kuendelea kuishikilia CCM. Hope wana Kiteto wanafanya kweli kesho.Mpka Kieleweke, please give us up to the minute updates from Kiteto.

hata hivyo, helkopta ya CHADEMA imeharibika usiku ktk uwanja wa ndege wa Dodoma. inawezekana kabisa kuwa ni hujuma. siyo jambo la kawaida helkopta kuharibika kirahisi hivyo. inawezekana kwamba nia yao ilikuwa ni mbaya zaidi, yaani kusababisha ajali.
Watanzania vita/mapambano ya kisiasa yawe ya hoja siyo kumwaga damu.
 
See attched latest photos....

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kwa mara ya kwanza kimelazimika kutumia usafiri wa helikopta katika kusaka ushindi wa mgombea wake wa ubunge kwenye uchaguzi mdogo wa Jimbo la Kiteto, mkoani Manyara.

Hatua hiyo ya CCM kutumia chopa, imekuja ikiwa ni siku moja tu tangu Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kianze kutumia helikopta kumnadi mgombea wake wa ubunge, Victor Kimesera anayeungwa mkono na takriban vyama vitano vya upinzani.

Helikopta hiyo ya CCM yenye namba 5Y-DTW, mali ya Kampuni ya Tropic Air ya Kenya, iliwasili jana majira ya saa 4:00 asubuhi na mara moja ikaanza kutumika katika kampeni za uchaguzi unaofanyika kutokana na kifo cha aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Benedicto Lusurutia.

Ilipowasili, makada watatu maarufu wa CCM, Kapteni John Komba, Christopher ole Sendeka na Lepilal ole Moleimet, ndio walioanza kuitumia kwa ajili ya kampeni.

Katika tukio ambalo lilionyesha dhamira ya wazi ya chama hicho tawala kujibu mapigo ya CHADEMA ambayo tangu mwaka 2005 imekuwa ikitumia helikopta katika kampeni zake, CCM walitumia chopa hiyo jana kupita maeneo yale yale alimopita Kimesera aliyekuwa akinadiwa na Mwenyekiti wa taifa wa chama chake, Freeman Mbowe na Katibu Mkuu wa chama hicho cha upinzani, Dk. Willibrod Slaa.

Wakati CCM wakitamba na helikopta jana, CHADEMA kwa upande wao walijikuta wakipata wakati mgumu baada ya chopa yao kushindwa kuruka.

Tukio hilo la helikopta ya CHADEMA ambayo ililala katika Uwanja wa Ndege wa Dodoma mjini kushindwa kuruka, lilisababisha Mbowe ashindwe kurejea Kiteto kwenye kampeni za ubunge hadi majira ya jioni jana.

Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA (Tanzania Bara) ambaye pia ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe akizungumzia suala hilo mjini hapa alisema, kumekuwa na hofu ya kufanyika kwa hujuma dhidi ya chopa yao kwa nia ya kuzorotesha makali ya kampeni zao.

Akizungumza na Tanzania Daima kutoka Uwanja wa Ndege wa Dodoma jana, Mbowe alisema tayari mafundi kutoka Nairobi nchini Kenya walikuwa wameshaitwa kwa ajili ya kuifanyia matengenezo chopa hiyo kwa ajili ya kufanya kampeni kesho.

Alisema hali imekuwa ni ya wasiwasi mkubwa kuhusu kushindwa kuruka kwa helikopta hiyo ambayo juzi jioni ilitua salama Dodoma baada ya kuitumia kwa kampeni kwa siku nzima.

“Bado hatujajua ni kitu gani hasa kimetokea na kusababisha chopa iwake, lakini ikashindwa kuruka. Tunasubiri uchunguzi wa mafundi kutoka Nairobi na wao ndio watakaotoa majibu iwapo kulikuwa na hujuma zozote zimefanyika au ni matatizo ya kiufundi,” alisema Mbowe.

Pamoja na hilo, Mbowe alisema bado chama chao jana kiliendelea na kampeni zake nzito za ubunge kikiwatumia wabunge wake wote waliosambaa katika maeneo mbalimbali ya Jimbo la Kiteto wanaofanya kampeni wakisaidiwa na viongozi wa juu na makada wengine cha chama hicho.

Mbowe alisema alikuwa anaamini kuwa, mara baada ya chopa hiyo kutengemaa, chama hicho kilikuwa kikitarajia kupita katika kata zote 15 za Jimbo la Kiteto kumnadi mgombea wao wa ubunge ambaye alisema wana imani ataibuka mshindi.

Akihutubia mikutano ya hadhara ya kampeni juzi, Mbowe alitumia muda mwingi katika kampeni zake kumtaka Kimesera kujiandaa kuwatumikia wananchi wote wa jimbo hilo bila kujali itikadi za vyama.

Akizungumza wakati wa mkutano wa kampeni katika kata nne tofauti, Mbowe alisema kuwa wote ni Watanzania na wapo katika maisha magumu, hivyo ni wakati wao sasa kufanya mabadiliko ili kubadili maisha yao.

Alimtaka Kimesera kuzingatia hilo pale atakapopata fursa ya kuingia bungeni, kwani kutokana na mwamko walioonyesha watu wa jimbo hilo, wana matumaini makubwa kwake hivyo ni dhahiri kuwa watampa kura zao kesho.

“Kimesera, uende bungeni kuwatumikia hawa wananchi sio kusubiri posho,” alisema Mbowe na kuongeza kuwa, CHADEMA haina itikadi bali kuwatumikia wananchi ambao kipindi kirefu walidanganywa kuwa CCM ni ya kwao, kumbe ni chama cha matajiri wachache.

Alisema kuwa wananchi wa kata za jimbo hilo wanapaswa kuonyesha mshikamano kwa kuikataa CCM ambayo licha ya miaka 42 ya uhuru, imeshindwa kubadilisha hali zao za maisha, hivyo kuwafanya walio wengi kujikuta wakiwa katika maisha ya hovyo bila uhakika wa elimu bora, huduma za matibabu na miundombinu mibovu ya barabara.

Mbowe akiwa katika Kijiji cha Lengasai alieleza kuwa, katika kijiji hicho kuna shule ambayo ina madarasa hadi ya saba, lakini kuna walimu wawili ambao alihoji kuwa watawatoa wapi wasomi watakaoleta maendeleo ya jimbo hilo.

Akiwa katika Kijiji cha Sunya, alimuita mtoto mmoja aliyekuwepo katika mkutano huo ambaye alisema ana miaka 13 na kuwa hakuwa anasoma, jambo lililoonekana kumsikitisha na kusema kuwa tayari maisha ya mtoto huyo yameishavurugwa.

Alisema kuwa kwa kipindi kirefu viongozi wa chama tawala wameshindwa kuwathamini watu hao jambo ambalo linavuruga maisha yao na ya watoto wao.

“Katika hali kama hii, hebu niambie kuna wasomi watakaopatikana kutoka katika kata hiyo?” aliuliza.

Mwenyekiti huyo alisema kuwa anasema hivyo kutokana na takwimu za Shirika la Umoja wa Mataifa la Sayansi Elimu na Utamaduni (UNESCO), ambazo zinabainisha kuwa kati ya watu 100 watakaofikia elimu ya chuo kikuu, asilimia 99 maisha huwa mazuri.

Alibainisha kuwa, idadi kama hiyo kwa wanaoishia kidato cha sita wanaofanikiwa kimaisha huwa ni asilimia sitini wakati kwa kidato cha nne kati ya mia huwa ni asilimia 40 wanaofanikiwa wakati kwa wahitimu wa darasa la saba asilimia 99 huishia katika umaskini mkubwa.

Aliwataka wakazi wa jimbo hilo kutambua kuwa, CHADEMA na vyama vingine vya upinzani vipo kwa ajili ya watu maskini, hivyo ni wajibu wao kuvipa ushirikiano na kwa kuanzia wafanye mapinduzi kwa ajli ya vizazi vyao kwa kumchagua Kimesera.

Akitumia helikopta, Kimesera na Mbowe walifanya mikutano katika kata za Kijungu, Lengasai, Sunya na Dongo.
 

Attachments

  • helikopta.jpg
    helikopta.jpg
    81.6 KB · Views: 53
  • mbowe.jpg
    mbowe.jpg
    178.8 KB · Views: 55
  • image002.jpg
    image002.jpg
    51.4 KB · Views: 49
See attched latest photos....

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kwa mara ya kwanza kimelazimika kutumia usafiri wa helikopta katika kusaka ushindi wa mgombea wake wa ubunge kwenye uchaguzi mdogo wa Jimbo la Kiteto, mkoani Manyara.

Hatua hiyo ya CCM kutumia chopa, imekuja ikiwa ni siku moja tu tangu Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kianze kutumia helikopta kumnadi mgombea wake wa ubunge, Victor Kimesera anayeungwa mkono na takriban vyama vitano vya upinzani.

Helikopta hiyo ya CCM yenye namba 5Y-DTW, mali ya Kampuni ya Tropic Air ya Kenya, iliwasili jana majira ya saa 4:00 asubuhi na mara moja ikaanza kutumika katika kampeni za uchaguzi unaofanyika kutokana na kifo cha aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Benedicto Lusurutia.

Ilipowasili, makada watatu maarufu wa CCM, Kapteni John Komba, Christopher ole Sendeka na Lepilal ole Moleimet, ndio walioanza kuitumia kwa ajili ya kampeni.

Katika tukio ambalo lilionyesha dhamira ya wazi ya chama hicho tawala kujibu mapigo ya CHADEMA ambayo tangu mwaka 2005 imekuwa ikitumia helikopta katika kampeni zake, CCM walitumia chopa hiyo jana kupita maeneo yale yale alimopita Kimesera aliyekuwa akinadiwa na Mwenyekiti wa taifa wa chama chake, Freeman Mbowe na Katibu Mkuu wa chama hicho cha upinzani, Dk. Willibrod Slaa.

Wakati CCM wakitamba na helikopta jana, CHADEMA kwa upande wao walijikuta wakipata wakati mgumu baada ya chopa yao kushindwa kuruka.

Tukio hilo la helikopta ya CHADEMA ambayo ililala katika Uwanja wa Ndege wa Dodoma mjini kushindwa kuruka, lilisababisha Mbowe ashindwe kurejea Kiteto kwenye kampeni za ubunge hadi majira ya jioni jana.

Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA (Tanzania Bara) ambaye pia ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe akizungumzia suala hilo mjini hapa alisema, kumekuwa na hofu ya kufanyika kwa hujuma dhidi ya chopa yao kwa nia ya kuzorotesha makali ya kampeni zao.

Akizungumza na Tanzania Daima kutoka Uwanja wa Ndege wa Dodoma jana, Mbowe alisema tayari mafundi kutoka Nairobi nchini Kenya walikuwa wameshaitwa kwa ajili ya kuifanyia matengenezo chopa hiyo kwa ajili ya kufanya kampeni kesho.

Alisema hali imekuwa ni ya wasiwasi mkubwa kuhusu kushindwa kuruka kwa helikopta hiyo ambayo juzi jioni ilitua salama Dodoma baada ya kuitumia kwa kampeni kwa siku nzima.

“Bado hatujajua ni kitu gani hasa kimetokea na kusababisha chopa iwake, lakini ikashindwa kuruka. Tunasubiri uchunguzi wa mafundi kutoka Nairobi na wao ndio watakaotoa majibu iwapo kulikuwa na hujuma zozote zimefanyika au ni matatizo ya kiufundi,” alisema Mbowe.

Pamoja na hilo, Mbowe alisema bado chama chao jana kiliendelea na kampeni zake nzito za ubunge kikiwatumia wabunge wake wote waliosambaa katika maeneo mbalimbali ya Jimbo la Kiteto wanaofanya kampeni wakisaidiwa na viongozi wa juu na makada wengine cha chama hicho.

Mbowe alisema alikuwa anaamini kuwa, mara baada ya chopa hiyo kutengemaa, chama hicho kilikuwa kikitarajia kupita katika kata zote 15 za Jimbo la Kiteto kumnadi mgombea wao wa ubunge ambaye alisema wana imani ataibuka mshindi.

Akihutubia mikutano ya hadhara ya kampeni juzi, Mbowe alitumia muda mwingi katika kampeni zake kumtaka Kimesera kujiandaa kuwatumikia wananchi wote wa jimbo hilo bila kujali itikadi za vyama.

Akizungumza wakati wa mkutano wa kampeni katika kata nne tofauti, Mbowe alisema kuwa wote ni Watanzania na wapo katika maisha magumu, hivyo ni wakati wao sasa kufanya mabadiliko ili kubadili maisha yao.

Alimtaka Kimesera kuzingatia hilo pale atakapopata fursa ya kuingia bungeni, kwani kutokana na mwamko walioonyesha watu wa jimbo hilo, wana matumaini makubwa kwake hivyo ni dhahiri kuwa watampa kura zao kesho.

“Kimesera, uende bungeni kuwatumikia hawa wananchi sio kusubiri posho,” alisema Mbowe na kuongeza kuwa, CHADEMA haina itikadi bali kuwatumikia wananchi ambao kipindi kirefu walidanganywa kuwa CCM ni ya kwao, kumbe ni chama cha matajiri wachache.

Alisema kuwa wananchi wa kata za jimbo hilo wanapaswa kuonyesha mshikamano kwa kuikataa CCM ambayo licha ya miaka 42 ya uhuru, imeshindwa kubadilisha hali zao za maisha, hivyo kuwafanya walio wengi kujikuta wakiwa katika maisha ya hovyo bila uhakika wa elimu bora, huduma za matibabu na miundombinu mibovu ya barabara.

Mbowe akiwa katika Kijiji cha Lengasai alieleza kuwa, katika kijiji hicho kuna shule ambayo ina madarasa hadi ya saba, lakini kuna walimu wawili ambao alihoji kuwa watawatoa wapi wasomi watakaoleta maendeleo ya jimbo hilo.

Akiwa katika Kijiji cha Sunya, alimuita mtoto mmoja aliyekuwepo katika mkutano huo ambaye alisema ana miaka 13 na kuwa hakuwa anasoma, jambo lililoonekana kumsikitisha na kusema kuwa tayari maisha ya mtoto huyo yameishavurugwa.

Alisema kuwa kwa kipindi kirefu viongozi wa chama tawala wameshindwa kuwathamini watu hao jambo ambalo linavuruga maisha yao na ya watoto wao.

“Katika hali kama hii, hebu niambie kuna wasomi watakaopatikana kutoka katika kata hiyo?” aliuliza.

Mwenyekiti huyo alisema kuwa anasema hivyo kutokana na takwimu za Shirika la Umoja wa Mataifa la Sayansi Elimu na Utamaduni (UNESCO), ambazo zinabainisha kuwa kati ya watu 100 watakaofikia elimu ya chuo kikuu, asilimia 99 maisha huwa mazuri.

Alibainisha kuwa, idadi kama hiyo kwa wanaoishia kidato cha sita wanaofanikiwa kimaisha huwa ni asilimia sitini wakati kwa kidato cha nne kati ya mia huwa ni asilimia 40 wanaofanikiwa wakati kwa wahitimu wa darasa la saba asilimia 99 huishia katika umaskini mkubwa.

Aliwataka wakazi wa jimbo hilo kutambua kuwa, CHADEMA na vyama vingine vya upinzani vipo kwa ajili ya watu maskini, hivyo ni wajibu wao kuvipa ushirikiano na kwa kuanzia wafanye mapinduzi kwa ajli ya vizazi vyao kwa kumchagua Kimesera.

Akitumia helikopta, Kimesera na Mbowe walifanya mikutano katika kata za Kijungu, Lengasai, Sunya na Dongo.
 
Salaam toka nyumbani kwangu Kijichi na naomba kujua kama leo Helikopta iweza kukatiza mawingu baada ya kupigwa zongo.
 
What was CCM thinking with Komba????LOL...mbunge wetu maskini!!! :-( ndo mtu kama huyo anaweza kumsikiliza raia wa kawaida matatizo yake? je atapigania haki na maendeleo ya mbinga kama anavyo sijiusisha na ugomvi na chadema?? Inasikitisha na Aibu kwa wale waliompigia kura..tutafika kweli??
 
hata hivyo, helkopta ya CHADEMA imeharibika usiku ktk uwanja wa ndege wa Dodoma. inawezekana kabisa kuwa ni hujuma. siyo jambo la kawaida helkopta kuharibika kirahisi hivyo. inawezekana kwamba nia yao ilikuwa ni mbaya zaidi, yaani kusababisha ajali.
Watanzania vita/mapambano ya kisiasa yawe ya hoja siyo kumwaga damu.


Unajua nashangaa sana siasa za Tanzania .CCM ina wasi wasi gani ? Chama hiki na watu hawa wako madarakani tangia Tanganyika na sasa Tanzania .Kama walikuwa wanatenda mema naamini mema yao yangali umaliza upinzani na woa kuchukua kura bila ya matusi , fujo , wizi ama kuwatumia polisi na Usalma wa Taifa na hata wakuu wa mikoa na Wilaya .CCM haifanyi kazi ndiyo maana wana haha hadi Komba anaonyesha kiburi mbele ya dola .Lakini siku zao zina hesabiwa
 
Waangalizi EU wawasili kushuhudia uchaguzi mdogo Kiteto
*CCM na Chadema wakabana koo kwa helkopta
*FFU, polisi kibao wamwangwa kulinda amani


Na Waandishi Wetu Kiteto, Dar


UCHAGUZI mdogo wa Jimbo la Kiteto unafanyika JUmapili baada ya vyama vya CCM na Chadema vyenye wagombea wanaochuana vikali vikihitimisha kampeni zao mbwembwe za helkopta.


Uchaguzi huo mdogo unaofanyika kuziba nafasi ya mbunge wa zamani wa jimbo hilo Benedict Losurutia aliyefariki dunia mwishoni mwa mwaka jana.


Katika uchaguzi wa leo, wapiga kura wanaamua kati ya Benedict Ole Nangaro (CCM) na Victor Kimesera (Chadema) ambapo kati yao mmoja atakuwa mbunge atakayekamilisha kipindi kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2010. Katika orodha ya wagombea pia kuna Juma Saini wa PPT-Maendeleo na Mashaka Fundi wa SAU.


Nangaro anakabiliwa na kazi kubwa kwa kuwa hakuwa mzungumzaji mzuri wa jukwaani bali ana sifa ya kuanzisha miradi mbalimbali ya maendeleo katika hilo.


Kwa upande wa Kimesera, yeye ni maarufu jukwaani huku akiwania jimbo hilo kwa safari ya nne. Wagombea wote wawili wa CCM na Chadema wanaelezwa kuwa marafiki wa karibu.


Tangu jana asubuhi, vyama vyote viwili kupitia kwa wawakilishi wao vilikuwa katika harakati za kuhamasisha wananchi kujitokeza kwa wingi kupiga kura ambapo kulikuwa na magari kadhaa ambayo yalikuwa yakifanya kazi hiyo.


Kwa mujibu wa tume ya uchaguzi chini ya msimamizi wa uchaguzi huo Festo Kang'ombe, wapo wapiga kura 74,418 ambao watapiga kura katika vituo 222. Jimbo la Kiteto lina jumla ya Kata 15, ambazo ni; Kibaya, Bwagamoyo, Partimbo, Kijungu, Lengatei, Sunya, Dongo, Songambela na Dosi dosi.


Nyingine ni; Engusero, Matui, Njoro, Makame, Kiperesa na Ndedo. Kwa mujibu wa


KUKAMILISHA KAMPENI


Jioni ya jana vyama vyote vilikamilisha kampeni zao kwa kufanya mikutano ya hadhara. Chadema kilihitimishia kampeni zake katika uwanja wa mpira wa Kibaya, wakati CCM walikamilisha kampeni hizo katika uwanja wa Shule ya Msingi Kibaya.


Helkopta za vyama vyote zilikuwa zikizunguka katika anga la Kiteto na hivyo kuandika historia ya kuwa uchaguzi wa kwanza kukutanisha vyama vinavyotumia helkopta, huku CCM ikionyesha kuiga mtindo huo ulioanzishwa na Chadema licha ya kwamba chama hicho kiliwahi kupinga matumizi ya helkopta katika kampeni kwa kusema hayaendani na umaskini wa nchi.


Hata hivyo juzi helkopta ya Chadema iliharibika mjini Dodoma na kisha kufanikiwa kutengenezwa na jana ilifanikiwa kufanya kazi sambamba na ile ya CCM.


Kulikuwepo na vikosi kadhaa vya askari wa FFU wapatao 500 waliotoka mikoa ya jirani ambao waliongozwa na magari yapatayo 15. Hata hivyo askari hao walikuwa wakiwaeleza wananchi kuwa kuwepo kwao Kiteto ni kwa ajili ya usalama na si vinginevyo.


VITUKO VYA KAMPENI


Kulikuwepo vituko kadhaa wakati wa kuhitimisha kampeni hizo jana. Kubwa kabisa itabakia matumizi ya helkopta ambapo mashabiki wa vyama vyote walionyesha kutambiana.


Helkopta hizo zilikuwa zikiruka maeneo mbalimbali kwa lengo la kuvutia mashabiki kuhudhuria mikutano.


Tena kulikuwepo na taarifa kuhusu mwenyekiti mmoja wa CCM kukamatwa na shahada nne za kupigia kura ambazo kwa mujibu wa viongozi wa Chadema waliomkamata, walieleza kuwa alikuwa na lengo la kuziuza. Mwenyekiti huyo alifikishwa polisi juzi na hadi jana alikuwa hajaachiwa huku akilalamika kwamba, shahada hizo zilikuwa za ndugu zake na yeye alikuwa kawashikia kabla ya viongozi wa Chadema kutumia mbinu za kumnasa.


Shahada za Kura ambazo zilikamatwa ni za majina, ya Namanyani Lengima ambaye

ilikuwa na namba 12740377,Ngongoni Saturo shahada namba 12749791,Meri Mamela

shahada namba 12706591 na Ndoye Lengela namba 12706589.


Kulikuwepo pia tukio la baadhi ya mashabiki wa vyama vya CCM na Chadema kugombea kupiga picha kwenye helkopta hizo huku wale wa CCM wakionekana kuwa na shauku kubwa kufuatia chama chao kutumia helkopta kwa mara ya kwanza.


Wakati huo huo Joyce Mmasi anaripoti kutoka jijini Dar es Salaam kuwa, tume iliyoundwa na jeshi la polisi kuchunguza vurugu zilizotokea wakati wa kampeni za uchaguzi mdogo wa jimbo la Kiteto haiwezi kumaliza kazi hiyo katika kipindi kifupi kufuatia kuwepo na mambo mengi ya kuchunguza.


Msemaji wa jeshi la polisi nchini Isaka Mgassa aliliambia gazeti hili juzi kuwa, tume iliyoundwa na jeshi hilo ipo wilayani Kiteto ikifanya kazi hiyo na kwamba haiwezi kumaliza kazi ndani ya siku mbili.


�Tume iliyoundwa bado ipo huko, inaendelea na kazi, unajua ile sio kazi ya siku mbili, nadhani muwe na subira kwa kuwa itachukua muda kidogo� alisema Mgasa.


Wiki iliyopita Mkuu wa Jeshi la polisi Said Mwema aliunda Tume ya kufuatilia vurugu zilizotokea katika jimbo la Kiteto baada ya wafuasi wa Chadema kudai kushambuliwa na wafuasi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wakishirikiana na jeshi la polisi.


Wafuasi hao wa Chadema pamoja na viongozi wa Chama hicho katika wilaya ya Kiteto walipigwa na kati yao kuumizwa vibaya na kudai kuwa walipigwa na wafuasi wa CCM na walipoenda kituo cha polisi nao walipigwa zaidi hadi walipokuja kutolewa kwa dhamana na viongozi wao wa kitaifa.


Tuma maoni kwa Mhariri




Habari katika picha na Matangazo
 
Hali zenu ,na poleni kwa kukosa kutoka uwanja wa mapambano.

Leo uchaguzi umeanza majira ya saa moja kamaili na watu wengi wanaendelea kujitokeza kupiga kura kwenye vituo vyao.

BAADHI YA MATATIZO .
1. kata ya kibaya kituo cha shule ya msingi palitokea hisia kuwa kuna kituo kimeongezeka lakini ukweli ni kuwa hakipo kitu kama hicho.
2.kata ya bwagamoyo .kituo cha kaloleni shule ya msingi pamekuwa na tafrani ndogo ndogo kati ya vijana wa chadema na diwani wa CCM aliyekuwa naashawishi watu kituoni ila vijana wamefanikiwa kumtoa mbio diwani huyo. Pia aliingia kada ambaye jina lake halijajulikana bado akiwa amevalia sare ya ccm na wananchi pamoja na mawakala wakamtoa mbio.

3.kata ya sunya kituo cha ndiliti mtendaji wa kata alikuwa amewazuia mawakala wa CHADEMA kuingia kituoni ila baada ya tafrani wameruhusiwa kuingia vituoni na wanaendelea na kazi.
4.kata ya matui ni kuwa kuna tatizo la vituo vya Ostetibugan na Nkole kuhamishwa na kupelekwa kusikojulikana ,ila mgombea wa CHADEMA ameenda kujua tatizo na ataweza kutupatia taarifa za kina zaidi kuwa nini kinaendelea huko.

5.kata ya Njoro, ilisemekana kuwa kuna tatizo la kituo hewa kinajulikana kama ndorokony ila baada ya Zitto kwenda na kukagua kila kona taarifa hizo hazijadhibitishwa hadi wakati huu.

Mengine nitawapasha baadae kadiri yatakavyojiri
 
Shukrani mpaka kieleweke,
Naona upinzani wamejipanga vilivyo na naamini hapa leo hakuna cha kuiba kura.

Hivi mtu akifanya kampeni au kuvalia nguo zinazoshawishi watu kumpigia kura mgombea fulani siku ya uchaguzi ni kosa. Kwa nini huyo Diwani na huyo kada wasishitakiwe kwa kosa la kukiuka sheria za uchaguzi badala ya kumfukuza tu na kuishia hapo?
 
Ni kweli wamejipanga vya kutosha na naona pia hata observers wa jumuiya ya ulaya wako hapa na kila kitu kipo sawa na kinaendela vizuri so far.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom