Hata miye, tangu lilipoanza kuuza kwa headlines za urongo kama ya HamzaRAIA mwema gazeti la udaku sinunui kabisa Siku hizi
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hata miye, tangu lilipoanza kuuza kwa headlines za urongo kama ya HamzaRAIA mwema gazeti la udaku sinunui kabisa Siku hizi
Kama kweli katiba ilikiukwa juu ya kupatikana spika basi Mahakama kuu itende haki na uchaguzi wa spika usifanyike. Mahakama iwe huru na kufanya kazi yake.View attachment 2094670
Aiseee! Hivi vifungu vya sheria visikilizie huko mbali kwa jirani. Matobo yake ni sawa na matundu ya neti.Au kishafanya,, maana katiba haibanishi kwamba lazima mtangaziwe[emoji23]
Wakati katibu wa Bunge amethibitisha kuipokea barua? Au ilikuwa lazima aambatane na kila mmoja wetu kama uthibitisho wa kufanya hivyo?Katiba inasema vyote viwili sura 148(1) inasema barua iandikwe na isaniniwe kwa mkono wa mhusika. Baadaye kipengele (c) inasema hiyo taarifa (iliyo katika barua) ipelekwe bungeni!! Ndugai hakufanya hivyo!!
Ndivyo watakavyojibu. Japo kwa mujibu wa Katiba ya JMT, mhimili wa mahakama, ndio the custodian wa Katiba. Bunge lilitunga sheria
batili ya kipengele cha mgombea uongozi kudhaminiwa na chama cha siasa, Mtikila akafungua kesi Mahakama Kuu kupinga kipengele hicho, akashinda, Mahakama Kuu ikatoa uamuzi kipengele hicho ni batili kwasababu kinakwenda kinyume cha katiba. Serikali ikakata rufaa, ikashindwa.
Ili kumkomoa Mtikila na kuidharau mahakama, Serikali ikapeleka bungeni sheria ya mabadiliko ya katiba kwa hati ya dharura na kukichomeka kipengele hicho batili ndani ya katiba, ili kuhalalisha sasa kiko kikatiba. Mtikila akapinga tena na akashinda tena kwa mahakama kutamka mabadiliko hayo ya katiba ni mabadiliko batili.
Serikali ikakata rufaa na mahakama ya rufaa Tanzania ikafikia uamuzi wa ajabu kuwahi kutokea Tanzania, ikatamka Mahakama haina uwezo wa kuliingilia Bunge na
kupinga kipengele chochote Bunge lilichokiingiza kwenye ndani ya katiba!.
PShurti la kudhaminiwa na chama kugombea uchaguzi, ni shurti batili kwa mujibu wa Katiba, linatutia hasara, tulifute!.
Wanabodi, Shurti la Mgombea Uongozi wa Umma, Kudhaminiwa na Chama cha Siasa ni Sheria Mbovu, ni... Kinyume cha Katiba, Kinyume cha Universal Declaration of Human Rights Kinyume cha The United Nations Human Rights Committee, Kinyume cha African Chatter of People and Political Rights Inaminya...www.jamiiforums.com
Pascal Mayalla unatukosea sana sisi wafuasi kindakindani wa Sisiemu. Inakuaje ^maigizo^ wakati tumefuata taratibu zote kama chama? Maigizo, by definition, ni kitu ama jambo lisilo halisi. See?Mkuu Consultant, nchi inaendeshwa kwa mujibu wa Katiba, sheria, taratibu na kanuni. Kilichofanyika katika uteuzi wa Dr. Tulia Akson ni utaratibu tuu ndani ya CCM. Baada ya utaratibu wa CCM kufuatwa, kila chama kitaleta mgombea wake aliyepatikana kwa mujibu wa taratibu za vyama na kumleta Bungeni ambapo sasa kanuni za Bunge kumchagua Spika lazima zifuatwe na Spika kuchaguliwa na hivyo Spika kuapa mbele ya Bunge na kuwa amepatikana kwa mujibu wa sheria, taratibu na kanuni.
Japo baada ya uteuzi wa CCM, huyo ndiye Spika, kinachofanyika ni maigizo tuu ya kukamilisha tuu taratibu za uchaguzi wa Spika wa Bunge kwa mujibu wa sheria na kanuni.
P
Bunge ni mhimili, kufuatia kutokuwepo checks and balance, mahakamani yetu sio tuu haita entertain hiyo kesi, bali haita thubutu hata to summon the legistlature with a court summons, hata Bunge livunje vipi katiba!.
Hivyo mchakato wa kukamilisha tuu taratibu za kumthibitisha Spika Tulia utaendelea as if nothing happened.
Rejea
P,Nani Zaidi Kati ya Bunge na Mahakama?!. The Doctrine of "Separation of Powers" Nothing, Just a Myth!
Wanabodi, Leo Tarehe, 26/11/2014 ni siku ya kihistoria kwa taifa letu la Tanzania, kwa sababu siku hii, inaanza kwa mtanange muhimu kuliko hata mjadala wa katiba, huu ni mtanange wa kupimana ubavu kati ya vyombo vikuu viwili vya Dola, Bunge, na Mahakama, Nani Zaidi?!. Bunge limetangaza...www.jamiiforums.com
Mkuu Jasmoni Tegga , ninawakoseaje CCM wakati mimi mwenyewe ni kada wa CCM?. Kosa langu ni kuwa ukweli daima, mimi ni CCM Nyerere type, kinataka viongozi wachaguliwe kwa ushindani wa haki based on merits na sio mgombea kubebwa kwa karata ya gender!. Tulitaka spika bora na sio bora Spika, Dr. Tulia Akson ni Bora Spika, but she has a chance to be Spika Bora na hili nimelisema hapa Je, Wajua, Naibu Spika, Chini ya "Bora Spika", Anaweza Kuwa "Spika Bora?". Dr. Tulia, "Ukitulia, Una Fursa ya Kuwa Spika Bora Sana!" Hongera Sana!Pascal Mayalla unatukusea sana sisi wafuasi kindakindani wa Sisiemu. Inakuaje ^maigizo^ wakati tumefuata taratibu zote kama chama? Maigizo, by definition, ni kitu ama jambo lisilo halisi. See?
Mkuu Consultant, nchi inaendeshwa kwa mujibu wa Katiba, sheria, taratibu na kanuni. Kilichofanyika katika uteuzi wa Dr. Tulia Akson ni utaratibu tuu ndani ya CCM. Baada ya utaratibu wa CCM kufuatwa, kila chama kitaleta mgombea wake aliyepatikana kwa mujibu wa taratibu za vyama na kumleta Bungeni ambapo sasa kanuni za Bunge kumchagua Spika lazima zifuatwe na Spika kuchaguliwa na hivyo Spika kuapa mbele ya Bunge na kuwa amepatikana kwa mujibu wa sheria, taratibu na kanuni.
Japo baada ya uteuzi wa CCM, huyo ndiye Spika, kinachofanyika ni maigizo tuu ya kukamilisha tuu taratibu za uchaguzi wa Spika wa Bunge kwa mujibu wa sheria na kanuni.
P
Basi utaratibu wa CCM ni wa kibabe sana. Wabunge wa CCM bado watapaswa kufanya igizo la kupiga kura kuchagua kati ya Tulia na kivuli cha Tulia? Madness!Mkuu Consultant, nchi inaendeshwa kwa mujibu wa Katiba, sheria, taratibu na kanuni. Kilichofanyika katika uteuzi wa Dr. Tulia Akson ni utaratibu tuu ndani ya CCM.
Kama nisingesoma chote, basi ningeandika tu kifungu kidogo "c" kinasemaje lakini nimeanzia palipoandikwa "Mtu yeyote mwenye dhamana ya kazi yoyote iliyoanzishwa na Katiba hii.....ndipo nikaja ku-drop kifungu c: iwapo mtu huyo ni Spika au Naibu wa Spika wa Bunge, basi taarifa hiyo ya kujiuzulu ataiwasilisha kwenye Bunge;,Soma muktadha/context vizuri. Anaposema TAARIFA HIYO YA KUJIUDHURU ana-refer taarifa iliyoandikwa na kuwekwa sahihi kwa mkono wa spika!! Lazima hi hk kifungu cha 149 (1) c kisomwe chote kwa pamoja ili kupata muktadha vizuri!!
Uchaguzi wa Spika utafanyika kwa sababu kesi aliyopeleka mahakamani Mh. Mbatia , ni ya kumtaka Spika aliyepita ajiuzulu kkwa utaratibu. Mh, Mbatia si kwamba anahitaji Spika aliyepita arudi madarakani, hapana bali anamtaka ajiuzulu kwa kufuata utaratibu kama ambavyo Mh. Mbatia anavyodhani kuwa ni sahihi. Sasa hapa kuna hoja gani ya kuzuia uchaguzi usifanyike?
Mh. Mbatia hajapeleka mahakamani shauri la kuzuia uchaguzi wa Spika usifanyike na hivyo uchaguzi utafanyika kama ilivyopangwa.
Assuming angekuwa ameamua kuacha kazi na asiandike barua ya kuacha kazi, Spika asingechaguliwa? Kama kweli angekuwa hakujiuzulu kwa kufauata utaratibu, basi ingeweza hata kuchukuliwa kuwa amefukuzwa kazi halafu mambo mengine yanaendelea. Kutokufuatwa utaratibu na aliyejiuzulu, kwa namna yoyote ile haku-compromise nafasi ya mwingine anayetakiwa kuchukua nafasi yake.Kama ikithibitika hakufuata sheria zakujiuzuru huoni atakayechsguliwa automatic atakuwa batili?