Uchambuzi huru: Hotuba ya Rais Samia Suluhu ya Aprili 22, 2021

Uchambuzi huru: Hotuba ya Rais Samia Suluhu ya Aprili 22, 2021

Maoni ya rais kuhusu matumizi ya mbinu za kisasa katika Kilimo, kuna hatari kubwa ya nchi yetu kurudi kutawaliwa tena Kiuchumi kutokana na ujio wa mbegu za maabara ambazo zitaondoa kabisa rutuba ya Ardhi yetu, ubora wa mbegu zetu (Organic) na kubwa zaidi kumikilisha Mashirika ya nje nguzo za Uchumi wetu Kitaifa.

Maasalaam,
- Ramadhan Kareem
Mzee mwenzangu; na mimi napitia taratibu hotuba nzima niisikilize; sidhani kama nitakuwa mbali sana na maoni yako. Kulikuwa na vitu nasubiri kuvisikia katika hotuba zake hizi mbili...
 
Kwa rehma zake Mwenyezi Mungu ni matumaini yangu sote tutaumaliza Mwezi huu Mtukufu wa Ramadhan salama salimin na hakika yeye ndiye mwenye kurehemu riziki zetu kubwa na ndogo na hapana mwingine apaswaye kuabudiwa. Tumuombe sote atuepushe na kila lisokuwa na kheri kwetu. Ameen.

Nina hakika siku ya leo tutasikia SIFA kemkem za mafuta ya tin na zaitun zitamiminika kupamba na kusifia hotuba ya rais wa JMT Mama Samia Suluhu Hassan kwa sababu imewagusa watu wote katika mazingira tofauti katika mwelekeo mpya wa dira ya Awamu hii ya sita ikitekeleza kauli mbiu ya KAZI IENDELEE.

Mimi binafsi, niseme ukweli wangu kutoka moyoni ya kuwa sii mshabiki wa rais Mama Samia Suluhu Hassan toka hotuba yake ya kwanza alipo apishwa kama rais wa Awamu ya sita. Huu ndio ukweli wangu! Na sababu zangu ni ndogo kabisa, nilimsoma toka mwanzo mwelekeo na Dira yake Kitaifa, dira ambayo Kiitikadi, mimi sii muumini wake na hupingana na nadharia zinazofungamana zaidi na UBEPARI badala ya UJAMAA wa Mwafrika.

Hivyo unaponisoma hapa ni muhimu Uzingatie kuwa mimi ni muumini wa UJAMAA wa Mwafrika na naamini Maendeleo ya Tanzania yataletwa na WATANZANIA wenyewe badala ya WAWEKEZAJI kutoka nje. Imani ya kwamba maendeleo yetu yanahitaji kuweka masharti rahisi ili kuvutia Wawekezaji ni sawa na fikra za.Kitumwa za Mababu zetu walokubali kupewa na wakoloni Shanga na vilemba ili tupendeze huku wagenu wakiondoka na madini mali ghafi na nyara zetu za Kitaifa.

Niseme wazi kwamba binafsi yangu naiona tofauti kubwa sana baina ya Hayati rais wa awamu ya Tani John Pombe Magufuli na Mama Samia Suluhu Hassan na kwamba hawa sii kitu kimoja hata kidogo. Tofauti zinazotokana na ahadi za mabadiriko makubwa ya SERA na SHERIA ambazo Chama cha Mapinduzi na Hayati Magufuli walizitumia kupata ushindi mkubwa katika Uchaguzi wa mwaka 2020. Niseme kwa nini nasema hivi?

Haina Shqka kabisa, Hayati Magufuli alikuwa rais anayepigania maslahi ya Wananchi Wanyonge kwa maana ya Watanzania Maskini dhidi ya Wawekezaji Mabeberu tofauti kabisa na Dira na Mwelekeo wa Mama Samia anayetazama zaidi viwashwishi kwa maslahi ya WAWEKEZAJI pamoja na dhana ya UKUONGEZA UZALISHAJI wa Mazao kwa WINGI zaidi (Quantity) badala ya fikra za Magufuli kudhamiria Kuanzisha viwanda vya ndani ili Kuongeza thamani ya Mazao yetu ya Asili yalokuwa BORA zaidi (Quality).

Nimalizie tu kwa kusema, rais wetu Mama Samia Suluhu Hassan awe makini sana na dhana hizi, kwani hatukuanza jana wala juzi. Tulifuata mrengo ule toka wakati wa Rais Ally Hassan Mwinyi, akaja Mh. Benjamin Mkapa na Mwishowe mstaafu Jakaya Kikwete, na kote huko nyuma tulifanya makosa mengi sana kwa dhana ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Biashara. Matokeo yake tukaunda Matabaka ya Walionacho na wasiona nacho baina ya Wainanchi wenyewe. Ndipo Ufisadi na rushwa viliposhamiri kwani hapana alotaka kubakia katika kundi la wasionacho (Maskini)

Maoni ya rais kuhusu matumizi ya mbinu za kisasa katika Kilimo, kuna hatari kubwa ya nchi yetu kurudi kutawaliwa tena Kiuchumi kutokana na ujio wa mbegu za maabara ambazo zitaondoa kabisa rutuba ya Ardhi yetu, ubora wa mbegu zetu (Organic) na kubwa zaidi kumikilisha Mashirika ya nje nguzo za Uchumi wetu Kitaifa.

Maasalaam,
- Ramadhan Kareem
Nakubaliana na wewe kwa msingi kwamba uvutiaji wa wawekezaji uwe katika miradi ya kimkakati ambayo utatuwesha kutufungulia masoko ya nje kama kwenye utalii, na mboga mboga Matunda, na vyakula vingine ikiwezekana tuwe na sisi tuna hisa katika uwekezaji huo.
Sio uwekezaji wa wenye nguvu kuleta watu wao na sisi kuwa watazamaji kwenye ardhi yetu wenyewe, na kuishia na kazi za vibarua.
Pia kuhakikisha hatutoi mianya ya ukwepaji kodi na utoroshaji wa fedha na mitaji kwa kupitia "creative accounting " ambayo wana siasa wetu wengi hawajui au ndio njia wanayotumia kupitishia mambo yao.

Mara nyingi hii miradi wana siasa huwa na hisa zao hivyo kuweka sera za kumpatia mwekezaji faida kubwa au monopoly katika biashara zao, design ya Tiscan, iliyokuwa voda, walivyo binafsisha ttcl, na ujio wa celtel na kuwa sasa airtel, au mkataba ya madini, dhahabu na Gesi, iptl, richmond
 
Umejitahidi kuchambua japo Uchambuzi wako ni wa Masikini Jeuri, wa kua na Mawazo Makubwa bila ya Uwezo wa Kutenda.

Mama Samiah anataka tufanye tunachoweza kufanya sasa wakati tunaendelea kujenga Uwezo wa kufanya hayo unayoyaelezea.

Tunahitaji Uwekezaji wa Ndani na pia tunahitaji Uwekezaji kutoka nje ili kuendelea kujenga Uwezo wa kujenga Uchumi wa Kujitegemea.
Mkuu wala.usisumbuke sana maana muda bado. Hapa panaitwa MTAKUJA iwe leo, kesho au keshokutwa. Kila nilisemalo hutokea ilivyo toka enzi za Hi5, Nyenzo, Bcstimes na Jamboforums. Yawezekana wewe ndio mgeni..

2015 Niliwaasa Chadema wakati wa Lowassa dhidi ya Dr. Slaa nikapuuzwa sana ikapita na Nikasema Magufuli atakuwa rais wa mfano nikapigwa vita vile vile pande zote. Kwa hiyo nimezoea, miaka yote mimi hapa Jamiiforuns nimekuwa nikipingwa kwa hoja zangu maana kwenu hazingii akilini. Mnachoshindwa kujua ni kwamba, mimi nimebobea katika Siasa, nazijua.mbivu mbichi chachu n.k
 
Mkuu Mkandara habari za siku nyingi?

Binafsi nimefurahi sana kuona wajenga hoja wazuri kama wewe wanaanza kurudi kwenye mijadala. Hii peke yake ni hatua nzuri inayoashiria kuwa tumepiga tena hatua na kurudi kwenye awamu ya hoja kwa hoja na si hoja kwa ngumi.

Kuhusu hotuba, kwa upande wangu nilitegemea kusikia niliyoyasikia na zaidi kidogo. Hata hivyo yaliyosemwa yamesemwa vizuri na ambayo nilitaraji yatasemwa zaidi na hayakusema naamini ipo siku yatasemwa. Kila kitu ni hatua.

Kuhusu approach za uwekezaji, mama yupo sahihi sana. Unapozungumzia habari za ujamaa na ubepari, inawezakana huelewi vyema implications ya dhana hizo katika ulimwengu wa sasa.

Suala hili la uwekezaji na nadharia za ujamaa na ubepari kama ulivyoliweka ni mjadala unaohitaji utulivu na ulivyouweka, umeuweka kijuu juu mno kiasi kwamba ni rahisi amma kutoeleweka vyema au kupotosha mambo kadhaa. Nikitulia nitarudi tujadiliane jambo hili kwa kina.
Mkuu nimeishi na hawa watu miaka 33 leo hii halafu unanambia sijui approach ipi? Halafu watu wenyewe wanaoshindana ni Wamarekani na Wachina? Nani kamzidi mwenzake hapo mkuu..
 
Natilia shaka kinywaji unachotumia.

Kama tu maoni umeyaita uchambuzi... Kweli awamu ile tulipigwa!
Kichwa cha habari hiyo kimerekebisha na Admin wa Jamiiforums kwa nia njema pengine. Kwa hiyo AKILI KUBWA husoma yaliyomo na kutafakari, sii ku judge by the cover or heading..huo ni Utindiga..
 
I like this one though you missed some points.

Kila mtawala huja na vipaumbele vyake, so It doesnt matter ana ideology kinachoangaliwa ni suala zima la maendeleo yatafikaje na kwa wakati gani!!!!!

Lakini pia serikali ni wananchi, unaposikiliza kero zao na kuzitafutia majibu, kwa mwanasiasa huu ni mtaji. Nadhani Mama Samia anatafuta njia fulani zitakazofanya aimbwe kwenye midomo ya watu ilihali anakamilisha ilani za chama chake.
Kila mtawala una maana gani ? Kwani wananchi walipigia kura MTU au Dira na mwelekeo wa chama kwa miaka mitano ijayo? Labda nikuulize wewe unadhani haya mabadiriko unayosema yangetangazwa na CCM na rais Magufuli ametutoka kabla ya Uchaguzi wa 2020 unadhani CCM ingeshinda Uchaguzi?
Na ikiwa kila rais anaweza kuja na mwekeleo wake basi kuna haja gani ya kuwa na Vyama vya siasa? Kwa nini kila mgombea Urais asiwe mtu binafsi, akishinda achague watu wake kama anavyofanya Mama Samia. Tuna Wasomi na Watalaam.kibao hawahitaji kuwa CCM wala Chadema na kutungiwa Ilani ya chama wakati wao wana mrengo wao kichwani.
 
Wewe ni miongoni mwa watu wenye upeo wa chini sana! Itakuchukua miongo mingi sana kujua anachoongea Mama Samia !

Wanyonge unaowazungumzia Rais Magufuli aliwapigania je ni pamoja na Paulo Makonda akiyekuwa akipora fedha za watu huku akitembelea Range Rover na Lamborghini?!

Rais Magufuli aliwahi kumkemea Paulo Makonda kuhusu tabia zake hizo?
Ndugu hujitambui na wala huijui Dunia tuliyonayo sasa.

Rais Magufuli alikuwa na nia nzuri ya kujenga Taifa Ila alikuwa na mawazo primitive sana ( mawazo ya kizamani) na hakuwa na "exposure" kubwa kuhusu Dunia inavyo operate!

Mama Samia inaonekana anayo "exposure" na anajua Dunia inavyo operate tunasubiri usimamizi wake.
Kama atakuwa na usimamizi mzuri atamfunika Rais Magufuli asubuhi sana!
Rais Magufuli alikuwa anajenga Nchi kwa jasho na damu la Watanzania!

Watu walikuwa wameshachoka sana,mlibaki wewe na akina Makonda mnafurahia matunda ya Nchi hii!

Nimependa hapo kwa wanyonge. Hivi huwa wanamaanisha nn hasa wanaposema wanyonge? Au ni hao mama na baba lishe wanaowalisha wananchi wetu uchafu kwa kuvunja sheria za nchi? Jpm kwangu mm ni the most divisive president ever kwa Tanzania. Kizazi cha akina makonda, sabaya etc walikuwa juu ya sheria enzi za jpm why? Jpm hajawahi kuwa rais wa wanyonge alikuwa rais wa kikundi fulani na wale brain washed aliokuwa anawagawia pesa barabarani.

Mama Samia yuko exposed na part of ipi kwa kuwa amefanya kazi kwenye NGOs kubwa Znz kwa zaidi ya 20 yrs kama sikosei. Yule mwingine im sorry ila ushamba wake umetucost sana kama nchi kwa kweli.
 
Kila mtawala una maana gani ? Kwani wananchi walipigia kura MTU au Dira na mwelekeo wa chama kwa miaka mitano ijayo? Labda nikuulize wewe unadhani haya mabadiriko unayosema yangetangazwa na CCM na rais Magufuli ametutoka kabla ya Uchaguzi wa 2020 unadhani CCM ingeshinda Uchaguzi?
Naunga mkono mengi uliyoandika humo kwenye mada, kwani nami mlengo wangu ni huo huo wa "Watanzania kujiletea maendeleo yao wenyewe">

Ila hiki kipande nilicho'quote hapo juu kuhusu uchaguzi: hivi unaandika kuhusu uchaguzi gani, huo wa 2020?

Ule kweli unaweza ukauita uchaguzi?
 
Kwa rehma zake Mwenyezi Mungu ni matumaini yangu sote tutaumaliza Mwezi huu Mtukufu wa Ramadhan salama salimin na hakika yeye ndiye mwenye kurehemu riziki zetu kubwa na ndogo na hapana mwingine apaswaye kuabudiwa. Tumuombe sote atuepushe na kila lisokuwa na kheri kwetu. Ameen.

Nina hakika siku ya leo tutasikia SIFA kemkem za mafuta ya tin na zaitun zitamiminika kupamba na kusifia hotuba ya rais wa JMT Mama Samia Suluhu Hassan kwa sababu imewagusa watu wote katika mazingira tofauti katika mwelekeo mpya wa dira ya Awamu hii ya sita ikitekeleza kauli mbiu ya KAZI IENDELEE.

Mimi binafsi, niseme ukweli wangu kutoka moyoni ya kuwa sii mshabiki wa rais Mama Samia Suluhu Hassan toka hotuba yake ya kwanza alipo apishwa kama rais wa Awamu ya sita. Huu ndio ukweli wangu! Na sababu zangu ni ndogo kabisa, nilimsoma toka mwanzo mwelekeo na Dira yake Kitaifa, dira ambayo Kiitikadi, mimi sii muumini wake na hupingana na nadharia zinazofungamana zaidi na UBEPARI badala ya UJAMAA wa Mwafrika.

Hivyo unaponisoma hapa ni muhimu Uzingatie kuwa mimi ni muumini wa UJAMAA wa Mwafrika na naamini Maendeleo ya Tanzania yataletwa na WATANZANIA wenyewe badala ya WAWEKEZAJI kutoka nje. Imani ya kwamba maendeleo yetu yanahitaji kuweka masharti rahisi ili kuvutia Wawekezaji ni sawa na fikra za.Kitumwa za Mababu zetu walokubali kupewa na wakoloni Shanga na vilemba ili tupendeze huku wagenu wakiondoka na madini mali ghafi na nyara zetu za Kitaifa.

Niseme wazi kwamba binafsi yangu naiona tofauti kubwa sana baina ya Hayati rais wa awamu ya Tani John Pombe Magufuli na Mama Samia Suluhu Hassan na kwamba hawa sii kitu kimoja hata kidogo. Tofauti zinazotokana na ahadi za mabadiriko makubwa ya SERA na SHERIA ambazo Chama cha Mapinduzi na Hayati Magufuli walizitumia kupata ushindi mkubwa katika Uchaguzi wa mwaka 2020. Niseme kwa nini nasema hivi?

Haina Shqka kabisa, Hayati Magufuli alikuwa rais anayepigania maslahi ya Wananchi Wanyonge kwa maana ya Watanzania Maskini dhidi ya Wawekezaji Mabeberu tofauti kabisa na Dira na Mwelekeo wa Mama Samia anayetazama zaidi viwashwishi kwa maslahi ya WAWEKEZAJI pamoja na dhana ya UKUONGEZA UZALISHAJI wa Mazao kwa WINGI zaidi (Quantity) badala ya fikra za Magufuli kudhamiria Kuanzisha viwanda vya ndani ili Kuongeza thamani ya Mazao yetu ya Asili yalokuwa BORA zaidi (Quality).

Nimalizie tu kwa kusema, rais wetu Mama Samia Suluhu Hassan awe makini sana na dhana hizi, kwani hatukuanza jana wala juzi. Tulifuata mrengo ule toka wakati wa Rais Ally Hassan Mwinyi, akaja Mh. Benjamin Mkapa na Mwishowe mstaafu Jakaya Kikwete, na kote huko nyuma tulifanya makosa mengi sana kwa dhana ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Biashara. Matokeo yake tukaunda Matabaka ya Walionacho na wasiona nacho baina ya Wainanchi wenyewe. Ndipo Ufisadi na rushwa viliposhamiri kwani hapana alotaka kubakia katika kundi la wasionacho (Maskini)

Maoni ya rais kuhusu matumizi ya mbinu za kisasa katika Kilimo, kuna hatari kubwa ya nchi yetu kurudi kutawaliwa tena Kiuchumi kutokana na ujio wa mbegu za maabara ambazo zitaondoa kabisa rutuba ya Ardhi yetu, ubora wa mbegu zetu (Organic) na kubwa zaidi kumikilisha Mashirika ya nje nguzo za Uchumi wetu Kitaifa.

Maasalaam,
- Ramadhan Kareem
Umeanza vizuri umeanza kutoa boko ulipoanza kusema kuhusu mama anataka quantity hayo umesema wewe husimuekee mama maneno mdomoni, mama anachotaka production iongezeke with the best out come and best quantity ilikuuza adi nje sasa tasfiri yako sijui umeipata wapi shekh. Hivi unajua mda gani inatokea ili kuua nutrition ya land? Waulize wanaofanya kilimo mfano mdogo Hiroshima land imekufa sasa watatumia almost the same components kwenye kuzalisha?Tufike mda tukabali dunia ni kijiji tusiogope kuingia soko la dunia kama wachina wanaleta adi samaki huku nini kinatushinda kupeleka tunapotaka. Common sense brother.

Sent from my 601SO using JamiiForums mobile app
 
Kwahiyo huu ndiyo uchambuzi au maoni yako
Toa na wewe uchambizi wako tofauti badala kukashifu bila kuonyesha wapi panakiwa kusahihishwa au kuongezewa. Mimi nimeona huo ni uchambuzi mahiri.
 
Mkuu wewe ni yule Rufufu Mkandara mchambua mikanda ya video? Yaani hapa ndio umechambua hotuba ya Rais Samia? Haki ya nani Kanda ya Ziwa inatapatapa!! Uliposikia anasema kuongeza uzalishaji wewe ukenda kwenye GMO? Mbona mama alikuwa wazi kabisa kwamba wataiongezea uwezo (mtaji) ASA ili izalishe mbegu za kutosha kuliko kutegemea mbegu za kutoka nje! ASA haizalishi GMO mkuu! Naona mnahaha!!
Jikite kwenye uchambuzi acha ukabila.
 
Kuna mifumo ya kizamani dunia ilipokuwa ni kama inaanza na kila mtu alikuwa hana kitu, was the big struggle....kwa sasa dunia imeendelea sana kwenye mambo mengi na vitu vingi hupatikana kwa urahisi..

Tunapozungumzia uwekezaji tunazungumzia watu wenye mitaji kuanzia ya hela, akili na teknolojia...watu hawa wako mbele miaka mingi kwa kila kitu....kuwaalika na kuchangamana nao maana yake tunachangamsha uchumi wetu na watu wetu wanapata mitaji, akili, maarifa, teknolojia nk vitu hivi vikifika kwa watu wetu nao watapata uwezo wa kuwekeza hapa na kwingineko....China tunayoiona imekua kwa uwekezaji kutoka ulaya na kujifunza maarifa kutoka ulaya..
Nakubaliana na mengi, lakini la mwisho siyo kweli. China haijaendelea kwa mitaji ya nje, ila imeendelea kwa kuwapeleka wachina wengi nje na kurudi kuendesha gurudumu la maendeleo. Wachina maelfu na malaki wamesoma USA, Ujermani, Ufaransa, Urusssi, na Ulaya yote. Wengi wao walibaki wakifanya kazi huko na baada ya miaka waliondoka na teknolojia ambayo wameitumia kwao kuirusha China kimaendeleo.

katika miaka ya 90 Cgina ilikuwa na tenda ya kununua skrepa za computer za jeshi (USA). Waamerika hawakutambua kuwa wao walikuwa wanaenda kuzusambaratisha na kuiba siri za teknoljia kutoka hard drve. Walikujatambua wachina wameishaiba siri nyingi, ndiyo maana China ili pickup haraka katika miaka 80/90.
 
Kwa rehma zake Mwenyezi Mungu ni matumaini yangu sote tutaumaliza Mwezi huu Mtukufu wa Ramadhan salama salimin na hakika yeye ndiye mwenye kurehemu riziki zetu kubwa na ndogo na hapana mwingine apaswaye kuabudiwa. Tumuombe sote atuepushe na kila lisokuwa na kheri kwetu. Ameen.

Nina hakika siku ya leo tutasikia SIFA kemkem za mafuta ya tin na zaitun zitamiminika kupamba na kusifia hotuba ya rais wa JMT Mama Samia Suluhu Hassan kwa sababu imewagusa watu wote katika mazingira tofauti katika mwelekeo mpya wa dira ya Awamu hii ya sita ikitekeleza kauli mbiu ya KAZI IENDELEE.

Mimi binafsi, niseme ukweli wangu kutoka moyoni ya kuwa sii mshabiki wa rais Mama Samia Suluhu Hassan toka hotuba yake ya kwanza alipo apishwa kama rais wa Awamu ya sita. Huu ndio ukweli wangu! Na sababu zangu ni ndogo kabisa, nilimsoma toka mwanzo mwelekeo na Dira yake Kitaifa, dira ambayo Kiitikadi, mimi sii muumini wake na hupingana na nadharia zinazofungamana zaidi na UBEPARI badala ya UJAMAA wa Mwafrika.

Hivyo unaponisoma hapa ni muhimu Uzingatie kuwa mimi ni muumini wa UJAMAA wa Mwafrika na naamini Maendeleo ya Tanzania yataletwa na WATANZANIA wenyewe badala ya WAWEKEZAJI kutoka nje. Imani ya kwamba maendeleo yetu yanahitaji kuweka masharti rahisi ili kuvutia Wawekezaji ni sawa na fikra za.Kitumwa za Mababu zetu walokubali kupewa na wakoloni Shanga na vilemba ili tupendeze huku wagenu wakiondoka na madini mali ghafi na nyara zetu za Kitaifa.

Niseme wazi kwamba binafsi yangu naiona tofauti kubwa sana baina ya Hayati rais wa awamu ya Tani John Pombe Magufuli na Mama Samia Suluhu Hassan na kwamba hawa sii kitu kimoja hata kidogo. Tofauti zinazotokana na ahadi za mabadiriko makubwa ya SERA na SHERIA ambazo Chama cha Mapinduzi na Hayati Magufuli walizitumia kupata ushindi mkubwa katika Uchaguzi wa mwaka 2020. Niseme kwa nini nasema hivi?

Haina Shqka kabisa, Hayati Magufuli alikuwa rais anayepigania maslahi ya Wananchi Wanyonge kwa maana ya Watanzania Maskini dhidi ya Wawekezaji Mabeberu tofauti kabisa na Dira na Mwelekeo wa Mama Samia anayetazama zaidi viwashwishi kwa maslahi ya WAWEKEZAJI pamoja na dhana ya UKUONGEZA UZALISHAJI wa Mazao kwa WINGI zaidi (Quantity) badala ya fikra za Magufuli kudhamiria Kuanzisha viwanda vya ndani ili Kuongeza thamani ya Mazao yetu ya Asili yalokuwa BORA zaidi (Quality).

Nimalizie tu kwa kusema, rais wetu Mama Samia Suluhu Hassan awe makini sana na dhana hizi, kwani hatukuanza jana wala juzi. Tulifuata mrengo ule toka wakati wa Rais Ally Hassan Mwinyi, akaja Mh. Benjamin Mkapa na Mwishowe mstaafu Jakaya Kikwete, na kote huko nyuma tulifanya makosa mengi sana kwa dhana ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Biashara. Matokeo yake tukaunda Matabaka ya Walionacho na wasiona nacho baina ya Wainanchi wenyewe. Ndipo Ufisadi na rushwa viliposhamiri kwani hapana alotaka kubakia katika kundi la wasionacho (Maskini)

Maoni ya rais kuhusu matumizi ya mbinu za kisasa katika Kilimo, kuna hatari kubwa ya nchi yetu kurudi kutawaliwa tena Kiuchumi kutokana na ujio wa mbegu za maabara ambazo zitaondoa kabisa rutuba ya Ardhi yetu, ubora wa mbegu zetu (Organic) na kubwa zaidi kumikilisha Mashirika ya nje nguzo za Uchumi wetu Kitaifa.

Maasalaam,
- Ramadhan Kareem
Mzee Mkandala, huo ni uchambuzi maoni au ni maoni yako madogo kwenye hotuba...!!?
Sasa umechambua nini hapo mkuu?
😁😁😁😁😁
 
Back
Top Bottom