Mkuu
Mkandara habari za siku nyingi?
Binafsi nimefurahi sana kuona wajenga hoja wazuri kama wewe wanaanza kurudi kwenye mijadala. Hii peke yake ni hatua nzuri inayoashiria kuwa tumepiga tena hatua na kurudi kwenye awamu ya hoja kwa hoja na si hoja kwa ngumi.
Kuhusu hotuba, kwa upande wangu nilitegemea kusikia niliyoyasikia na zaidi kidogo. Hata hivyo yaliyosemwa yamesemwa vizuri na ambayo nilitaraji yatasemwa zaidi na hayakusema naamini ipo siku yatasemwa. Kila kitu ni hatua.
Kuhusu approach za uwekezaji, mama yupo sahihi sana. Unapozungumzia habari za ujamaa na ubepari, inawezakana huelewi vyema implications ya dhana hizo katika ulimwengu wa sasa.
Suala hili la uwekezaji na nadharia za ujamaa na ubepari kama ulivyoliweka ni mjadala unaohitaji utulivu na ulivyouweka, umeuweka kijuu juu mno kiasi kwamba ni rahisi amma kutoeleweka vyema au kupotosha mambo kadhaa. Nikitulia nitarudi tujadiliane jambo hili kwa kina.