Uchaguzi 2020 Uchambuzi: Tundu Lissu anaweza kumshinda Dkt. Magufuli na Maalim Seif anaweza kuibuka kidedea Zanzibar

Uchaguzi 2020 Uchambuzi: Tundu Lissu anaweza kumshinda Dkt. Magufuli na Maalim Seif anaweza kuibuka kidedea Zanzibar

SHANTI

JF-Expert Member
Joined
Mar 16, 2011
Posts
296
Reaction score
365
Wasalaam wanabodi,

Kampeni za uchaguzi mkuu zinaelekea ukingoni siku mbili zijazo nchi nzima. Tumeona Kila mgombea akijinadi kwa style yake na upekee kulingana na malengo na mikakati thabiti waliyojiwekea.
Chama tawala CCM walianza kwa kishindo kikubwa pale dodoma na kuonesha ukubwa wa idadi ya wafuasi wake walijipanga kutetea kiti Chao. Kadiri siku zilivyozidi kwenda utamu wa kampeni za chama tawala ulinoga kupita zilizotangulia.

Msingi wao mkubwa ulikuwa nyomi la watu na uwezo wa kufika vijijini zaidi. Tofauti na miaka yote mgombea wao amefika MAENEO mengi ya mijini zaidi kuliko vijijini ukilinganisha na 2015. Ukifanya SWOT Analysis utayaona haya:

Strength:
CCM huwezi kuitenganisha na Sola na pia huwezi kuitenganisha na serikali , na hapo ndipo utagundua kwa Nini NEC Ni watiifu Sana kwa CCM.

WEAKNESS
Kundi kubwa Lina wageni ambao sio wajuvi wa siasa za majukwaa na uwezo wa kubashiri yajayo kwa uyakinifu. Hii imewagharimu Sana kiasi hawajui kuwa mbaya wao Ni Seif sharrif Hamad au Tundu Lissu au ubovu wa kumsimamisha Mwinyi.

Si hivyo tu pia kushindwa kujua kuwa Kuivuruga CUF, CHADEMA na kununua wabunge wa upinzani ingelikuwa njia nyepesu ya wao kushinda Bila kupingwa au kushinda kwa kishindo kikubwa. Mpaka Sasa timu ya kampeni ya CCM imeshinda kuondoa udhaifu huu na unawagharimu kwenye field sababu kubwa walisahau kuwa upinzani Ni mioyo na hisia za watu na sio vyama. Hivyo mziki wa upinzani bado unagonga spika zao kwa Kasi Sana.

NGUVU YA UMMA
Inaonekana wazi LISSU na SEIF hawatanii hata kidogo jinsi walivyojipanga kutumia nguvu ya Umma. Kwa mwenye macho mapana .Umma haujawahi kushinda DHIDI ya watawala na Kama kweli basi hiki kitisho kikubwa Sana kwa CCM.

OPPORTUNITY
Fursa kubwa na ya pekee Ni kutumia Dola .

Pili mtaji wa fedha na rasilimali watu

TECHNICALLY
Hapa namaanisha MBINU za kiufundi za kushinda uchaguzi siku ya uchaguzi. MBINU ya kwanza NEC,hii imewapa wabunge zaidi ya 20

NEC na CCM ni watu wamoja wanaongea lugha Moja pia wanaweza kwa hiyari tu Kuivuruga ngome ya wapinzani na matokeo Yao kwa sababu hawana pa kushtakiwa popote kwa kuwa wao wanatoa tamko la mwisho.(namaanisha wakurugenzi) na dalili zishaonekana tayari.

CHADEMA NA ACT
Wote kwa pamoja na wajadili Bila kuwatenganisha ili nihitimishe vizuri. Ni ukweli usiopingika kuwa Zambarau wameiteka Zanzibar na CDM wameiteka Tanganyika.

Ubora wa viongozi wao wakuu wawili MBOWE & SEIF SHARRIF HAMAD umejidhihirisha wazi kwenye uchaguzi huu kwa kuruka mamii ya vihunzi na kuilaghai serikali mchana kweupeeee.

Hebu nikurudishe nyuma kidogo, siku Maalim Seif alipokwenda ikulu kumsalimia Rais huku MBOWE akipambana kesi ya Akwilina. Kila mtu alijua Maalim ameunga juhudi mkono na shughuli anayo mwamba. Sasa ndio nang'amua kwamba kumbe Ile Ni MBINU ya kimedani ya kuwalaghai watawala waamini upo pamoja nao. Ile ndio siku ya USHINDI wa SEIF Kama ikitokea atashinda Zanzibar kesho kutwa.

Hisia zinaniambia kwamba mwamba na mwalimu waliwaingiza Chaka CCM na Membe wao huku wakijua wamemficha mfukoni Lissu.
Tuachane na hayo hebu tuwafanyie SWOT na wao wapoje.
STRENGTH

NGUVU YA UMMA
Umma umewaelewa Sana ACT &CHADEMA na ushahidi wa Watanzania kuwachangia pesa wahalifu wasiende jela badala yake walipiwe faini na warudi uraiani Ni ishara Tosha upo tayari kufanya lolote lenye kuwalinda Chadema kwa upande wa bara. Jambo Hili liliwatia kiwewe IKULU na kesho yake Rais aliamua kumlipia msigwa kuonesha Kwamba Rais Ana huruma na wapinzani. Kama watu walichanga dusko dusko namaanisha kiasi Cha 1k -10k kinyume chake hizi buku buku Ni idadi ya wapiga kura wa upinzani. Sasa kazi yako chukua kikokotoo halafu tafuta majibu Ni watu wangapi wanasapoti Chadema. Zenji siongei Kila mtu ameona NGUVU ya Maalim kaondoka na wanachama wake kwenda ACT so like amevimbisha msuli kwa mamlaka.

UWEZO WA KUNUSA HATARI
Tukio la Membe kuachwa kwenye mataa na hajielewi linathibitisha uwezo wa wapinzani KUNUSA HATARI.
Waliujua mtego wa CCM na wao wakatega wa kwao kwenda ikulu na kuleta picha kwamba Seif Ni mshkaji na MBOWE mkorofi kumbe Ni mtego wa Kumlinda LISSU na kunifanya Membe aonekane punguani asiyejua anataka nn.
Membe Ni ujio hatarishi kwa upinzani na Lissu anatafutwa na watesi wake asirudi kwenye siasa. Inaonesha wazi Kuna makubaliano kwamba ACT na CDM wote waingize wagombea ili mmoja akikatwa aungwe mkono mwingine na ndicho kinachoendelea Sasa.

Wanachama 9M according to MBOWE

WEAKNESS
Hawana Dola Wala serikali na hawajahi kushinda uchaguzi ngazi ya Rais

NEC haipo upande wao

UWEZO mdogo wa ulinzi na USALAMA wa viongozi wake, Ni rahisi kumteka au kumkata au kuzuia mkutano wa upinzani.

Ukosefu wa rasilimali fedha

OPPORTUNITY
MPASUKO wa CCM baada ya kura za MAONI. Huu Ni mtaji mkubwa Sana wa upinzani na dalili zimeonekana wazi Kanda ya ziwa na Zanzibar. Maamuzi ya Dodoma huenda yakawafanya CCM kupoteza majimbo 35-50 ya uchaguzi wasipotumia utemi.

KULINDA KURA VITUONI
Wakiwekeza NGUVU imara ya KULINDA KURA CCM hawana Chao. Naamini Lissu anamaanisha na ujumbe umewafikia walengwa. Wameanza kujibu maneno

MAKUNDI MAALUM YALIYOUMIZWA NA SERIKALI
Hapa nawaweka wahanga wote wa utawala wa awamu ya tano. Wafanyakazi hewa,waliobomolewa,waliotoswa walimu, wafanyakazi wa serikali, waliokosa mshahara n.k

Hawa Ni game changers watatoa USHINDI 5%-7% kwa Lissu sababu Wana maumivu Yao.

TECHNICALLY

MAANDAMANO YASIYO KIKOMO
Ukifuatilia vizuri utagundua MBINU pekee ya wapinzani kuingia ikulu Ni MAANDAMANO YASIYO na KIKOMO. Hii ndio MBINU ya kiufundi yenye chanya na imewasaidi wapinzani wa nchi jirani kuingia na kushika serikali punde tu baada ya uchaguzi.

Hakuna serikali ya kiafrika imeyashinda MAANDAMANO YASIYO KIKOMO. Kiufundi wapinzani wako vyedi.

MATAMKO NA VITISHO VYA VIKWAZO
tangu wiki iliyopita mataifa makubwa yamekuwa na spidi ya MATAMKO na baru ya into kwa serikali ya Tanzania Ni wazi wapinzani kwenye MBINU hii wako mbali Sana. Yakitokea tusiyoyaomba wanatusua mapema.

Baaada ya mtazamo huo Sasa najikita kueleza kwa Nini Lissu 49% na Magufuli 47%.

Sympathy
Umaarufu wa Magufuli umeporomoka Sana baada ya kura za MAONI. Wakati huohuo umaarufu wa Chadema umekuwa mkubwa kupindukia sababu watu waliaminishwa kuwa upinzani umekufa na kinyume chake umekuwa zaidi kwa sababu ya huruma kuwa wanaonewa.

Kifungo Cha viongozi wa Chadema mwezi Machi kiliibua hisia za huruma kwa wananchi na kuamsha Ari ya huruma kwa wapinzani. Ujio wa Lissu umeikuza sympathy ya Chadema na ACT kwa pamoja na hivi tunavyoongea waliopewa kazi kushughulika na wapinzani wanalala na viatu.Hii itawapa kura sawa na 21%

Waislamu
Hapa Sina lengo la udini Ila hakuna asiyejua michango ya waislamu hapa bongo. Ujio wa sheikh Ponda Ni pigo kwa CCM na faida upinzani.

Sheikh ponda kashawagawa na Hili litawapa wapinzi USHINDI Zanzibar na pwani na mikoa ya kusini ambapo CCM imewakwaza kwa kiasi kikubwa kupitia korosho. Hili litapunguza 45% kwenye kura za waislam zilizotakiwa kwenda ccm

KOROSHO
sekeseke la korosho linaonekana Ni shida kubwa Sana kiasi Cha kuitikisa ngome ya CCM na hii ikikutana na impact ya ponda itawaumiza CCM zaidi na kuwanufaisha wapinzani.

Low turnover
Mwitiko mdogo wa wapiga kura siku ya uchaguzi, Ni pigo kingine kwa CCM na msaada kwa upinzani. Kuna uwezekano turn over ya wapiga kura ikawa watu 9M -11M

Hapa ndio kifo Cha CCM kinaanzia na hiili litawapunguzia 50% kura zote walizotarajia kupata kwenye uchaguzi huu.hii Ni faida kwa upinzani kwa sababu wao wanategemea sababu za hapo juu kupindua meza.

Common interest za Wazanzibar
Ikumbukwe watu wa visiwani wakitaka Lao hawashindwi licha ya utofauti wa vyama. Ni wazi CCM na ACT wote Lao Ni Moja ingawaje kwa nje wanashambuliana Jana kwamba wanapigana Vita ya 3 ya dunia. Seif anakwenda kushinda uchaguzi kwa sababu wazenji wote Wana ongozwa na common interest kuiona CCM Ni kikwazo kwao so best way Ni kumpa seif na sio Mwinyi.

Tutarajie mchuano mkali.

Karibuni kwa mjadalaa
 
Uchambuzi mzuri Ila free and fare election lissu anashinda kwa zaida ya 60%

Yaani toka mama yangu ambaye ni kada wa jumuiya ya wazazi ccm anihakikishie kumpigia kura Tundu lissu pia akawa anasema kamati yao nzima wamesema hawana Imani na Magufuli

Jinsi alivyo mfia chama halafu anamchinja mwenyekiti wake

Ndio niliona kabisa kwamba Magufuli Hana chake mwaka huu.
 
Lissu huyu mbeba maono ya mabeberu au mnaongelea kitu gani?

Uchaguzi 28/10 ni siku ya mapumziko na siku inayofuatia itakuwa sikukuu ya MAULID kabla ya pilau ya maulid hajaiva tayari Lissu atakuwa amegeuzwa kibra. Kesho yake atakuwa anajiandaa kuhamishia kijiwe KISUTU kujitetea kwa nini asipigwe mvua za kutosha kwa uchochezi
 
Hizi ni ndoto za mchana. Mmejaribu kumnadi Lissu lakini watanzania wamemkataa, hawataki wakala wa mabeberu. Watanzania wameamua kwenda na JPM kwamiaka mingine mitano. Utafiti uliofanywa kisayansi juzi na Taasisi ya IBC Research International imegundua JPM anashinda kwa 89.5 na Lissu ataambulia tu 8.2% ya kura zote. Nakuhurumieni sana wana Ufipa, pengine ndoto hizi za mchana unazokuja nazo ni sehemu yenu ya kujifariji. Kila Mahali ni kura ya ndiyo kwa JPM. Hakuna mtanzania wa kumchagua Lissu . Tunakwenda na JPM .
 
IMG_8634.jpg
 
Kuna mtu kanambia ana uhakika Lissu atashinda nikamwambia mimi sio mwanasiasa wala mtabiri ila Magufuli atashinda.
Nikamuomba tuweke dau la milioni mojamoja ili ambae kauli yake itakua ilikua yakweli achukue milioni mbili kakataa nikajua kumbe ananiambia maneno asio na uhakika nayo kabisa na anaujua ukweli.

Sent from my Infinix X603 using JamiiForums mobile app
 
Uwezekano wa Tundu Lissu kushinda uchaguzi upo lakini je atatangazwa kama kashinda kweli.
Kwa Zanzibar Hilo halina majadala Maalimu seif atashinda je atatangazwa au ndiyo yaleyale ya Jeche 2015.
 
Wasalaaam wanabodi,

Kampeni za uchaguzi mkuu zinaelekea ukingoni siku mbili zijazo nchi nzima. Tumeona Kila mgombea akijinadi kwa style yake na upekee kulingana na malengo na mikakati thabiti waliyojiwekea.
Chama tawala CCM walianza kwa kishindo kikubwa pale dodoma na kuonesha ukubwa wa idadi ya wafuasi wake walijipanga kutetea kiti Chao. Kadiri siku zilivyozidi kwenda utamu wa kampeni za chama tawala ulinoga kupita zilizotangulia.

Msingi wao mkubwa ulikuwa nyomi la watu na uwezo wa kufika vijijini zaidi. Tofauti na miaka yote mgombea wao amefika MAENEO mengi ya mijini zaidi kuliko vijijini ukilinganisha na 2015. Ukifanya SWOT Analysis utayaona haya:

Karibuni kwa mjadalaa
Asante kwa uchambuzi mzuri na mahiri, hii ya Lissu atashinda, naomba usubirie tarehe 28 October, utashangaa!.
P
 
Mjadala mzuri sana. Asante kwa uchambuzi wako. Hii ndio njia iliyobaki. Niko nje ya Tanzania (bahati mbaya). Nimekuwa nikiongea na ndugu zangu walioko huko vijijini. Kwa majuma mawili hizi usikivu kwa simu ni mbaya mtu. Simu zinakatika katika. Inaonekana kuna mtu hataki watu wawasiliane kipindi hiki. Pale nilipoweza kuwasiliana, wanasema Magufuli hatakiwi hata huko vijijini. Imeshutua. Mama yangu wa miaka kati ya 70-80 naye anasema atampigia kura Lissu. Imenishangaza sana kwa vile mama alianza na TANU zamani sana. Leo hii anasema hana habari na CCM.

CCM hawawezi kuondolewa kwa kura. Mfumo wote wa serikali sasa hivi CCM imeuchukuwa kwa manufaa yake. Zaidi ni mtangaza mshindi. I do not see NEC/Kaijage akimtangaza mtu mwingine zaidi ya Magufuli. Wananchi wako tayari. Wanachohitaji ni kuongozwa. TL, Zitto na Maalim Seif - hapa ndipo wanapotakiwa kutoa uongozi. Hii ni nafasi nadra kwa wapinzani. Wakiacha ikapita hivi hivi, inaweza isitokee tena. Watu wameichoka CCM. Wanahitaji tu kuongozwa.
MAANDAMANO YASIYO KIKOMO

ukifuatilia vizuri utagundua MBINU pekee ya wapinzani kuingia ikulu Ni MAANDAMANO YASIYO na KIKOMO. Hii ndio MBINU ya kiufundi yenye chanya na imewasaidi wapinzani wa nchi jirani kuingia na kushika serikali punde tu baada ya uchaguzi.

Hakuna serikali ya kiafrika imeyashinda MAANDAMANO YASIYO KIKOMO. Kiufundi wapinzani wako vyedi.
 
Back
Top Bottom