Elections 2015 Uchambuzi wa ahadi za mgombea urais kwa tiketi ya CCM, Dr. John Pombe Magufuli

Elections 2015 Uchambuzi wa ahadi za mgombea urais kwa tiketi ya CCM, Dr. John Pombe Magufuli

Kuna maswali mengi kuliko majibu!
Matatizo au kero zinazoelezwa na Mhe. Magufuli zinatatanisha sana. Hivi Tanzania ina serikali? Kama serikali ipo, inaongozwa na chama gani?

Kero anazoongea kama chama chake kimeshindwa kuzitatua kwa miaka kadhaa, je yeye ataweza kwa miaka 5 au 10?

Itakuwa vigumu sana kwa watu wanaojua kuchambua maswala ya kisiasa kukubaliana na staili ya Mhe. Magufuli. Hawezi kulaumu chama chake na viongozi waliomtangulia na akaonekana ataleta tofauti yoyote wakati akichaguliwa atafanya kazi na watu walewale. Naona kama vile Mhe. Magufuli ameiba sera ya upinzani na amesahau lawama ni za chama chake.

Kwa hotuba anazozitoa, kama kweli kuna upinzani, CCM imeshawapunguzia 50% ya muda wao wa kampeni. Kama watu wanaiba dawa, wananyanyasa raia, matumizi mabaya ya ofisi, ufisadi, nk. ni nani wa kulaumiwa? Bila shaka si Upinzania maana wamekuwa wakitoa shutuma hizo kwa serikali ya CCM.

Hii ni dalili mbaya kwa CCM na upinzani wachukue haya mapungufu kwa kujizatiti.

Anjo
 
Jamani watanzania KIKWETE alisema Tanzania Yenye Neema inawezekana je Watanzania mmeipata hiyo NEEMA au kaipata RIDHIWANI?
 
kaeni msipige kampeni, naona hukumsikia aliposema "Kila zama na kitabu chake"!Unadhani kwa nini mamvi na wfanyabiashara wenzie wamekimbia ccm na kwa udi na uvumba wanataka kumzuia Magufuli asiingie ikulu!?Subiri muone huu mziki, twende tingatinga twende, tuko pamoja mpaka kieleweke
 
ccm inajimaliza yenyewe na hapa ndio unagundua jinsi chama hicho kinavyoingilia maamuzi mbali mbali hapa nchini....inakufa na haina pa kutokea.
 
Magufuli hana jipya nawala sio kiongozi mzuri, Magufuli is hana mission wala vision, na wala sio mtu wa mikakati na mipango ni mpenda sifa tu. Kiongozi imara anasema neno na linatendeka kiongozi dhaifu kama Magufuli inabidi ashinde site ili neno litendeke. inabidi uwe kichaa ili uamini mabadiliko kupitia kwa Magufuli.
 
Napenda kuuliza sijui wenzangu kama mliona jipya katika hotuba ya huyu magufuli?, mimi binafsi niliona ni yaleyale ya CCM ya miaka yote na hakuna jipya wala alichokuja nacho. Pia mengi ni uongo uleule wa CCM usiotekelezeka, ni yaleyale ya MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA ya Kikwete badala yake yakawa magumu zaidi. Nimekatishwa tamaa na huyu mgombea, sasa CCM basi siitaki tena. Mwenye kuweza kunishawishi kwamba mna kitu ndani ya Magufuli na amwagike hapa
 
CCM haina jipya! Ni masikitiko tu kwamba watanzania wanaendelea kupumbazwa tu miaka nenda rudi bila kujitambua!
 
Kusemakweli inasikitisha kuona chama kikongwe kama ccm kinakosa dira badala yake kinakuja na ahadi za uongo ambazo aziwezi kitekelezeka, Mpaka sasa watu vijijni wanakunywa Maji machafu ambayo hata magufuli mwenyewe hawezi kunawa ili ale chakula lakin ndo huyohuyo anayesema et kila kijiji atakipa 50mln, MSD wenye jukumu la kupereka madawa kwenye hospital za serikali wanaidai serikali pesa chungu mbovu lakini magufuli anashangaa eti kwann hospital hakuna dawa, et ataboresha mishahara ya manesi na madaktari wakat madaktari waliomaliza chuo kikuu wameambiwa wafanye kazi bure kwa kujitolea Mpaka baada ya mwaka mmoja ndipo waanze kulipwa mishahara, je MTU/ daktari wa nmna hiyo akikutana na madawa yatanusulika kweli? je atashindwa kuomba hongo toka kwa mgonjwa?.Ccm ni vyema wakasema kwa miaka hii 5 hatuna ahadi mpya labda tutamalizia alizoahidi jk miaka 10 iliyopita.
 
Katika hali isiyooeleweka Magufuli amezidi kumwaibisha Rais wake kwa kusema yafuatayo:- (1) Nitahakikisha madawa yanapatikana katika vituo vyote vya Afya (2) Nitapambana na watumishi wala rushwa (3) Nitapambana na watumishi wazembe. Yote aliyoyasema ndo yanatokea sasa hivi. Madawa hakuna, Rushwa kama kazi, Watumishi bado ni wazembe sana. JE ATAWEZA KAMA SERIKALI YA CCM IMESHINDWA YOTE HAYA.
 
Samia suluhu amesema atagawa boda boda thelathini marangu endapo wakishinda boda boda 2m kwa hiyo milioni sitini hii nadhani wangeweza kugawa sasa hivi kwa sababu wako madarakani vinginevyo ni ULAGHAI.
 
Kampeni zake na msemo wake nashangaa kuona osptal Madawa hamna anashangaa kana kwamba alikua aishi Tanzania maahadi kibao mpaka yale aliyoshindwa mheshimiwa amejitwishwa yeye ataweza?
Na ahadi nyinge eti kila kijiji nitatoa million hamsini huu ni ukweli au naota mana naona kama ndoto binafsi yangu bado hujanisawishi ahadi zingine kwa Tanzania naona azitekelezeki ajira kwa vijana imefeli hii kweli itawezekana
 
kampeni ni zake lakini system zinaonyesha kuwatengenezea njia wapinzani mana kila ahadi inaonyesha kuikosoa serikali yake
 
Mbona hujamshangaa lowassa anabeba magunia tandale? Pumbavu Sana
 
Back
Top Bottom