Uchawa unadumaza maendeleo ya nchi, unalinda ufisadi na kubariki kutokuwajibika. Taifa linaangamia

Uchawa unadumaza maendeleo ya nchi, unalinda ufisadi na kubariki kutokuwajibika. Taifa linaangamia

Kwanini unaona uchawa wa sasa hivi ni mbaya kuliko uchawa wa kipindi cha mwendazake?.Au kwavile sio zamu yako kulamba asali.Kipindi ambacho wewe ulikua mfuasi wa mtu hukuona kama hicho kitendo ni kibaya,au kwavile aliyepo sasa huna maslahi naye ndo unaibuka na hoja yakujifanya huupendi uchawa.Siku tutakayoamua kuacha unafiki na kuamua kusimama na nchi badala ya mtu ndio siku tutakayoanza kupiga hatua yakulisaidia hili taifa.sasa hivi watu bado wanapokezana kulamba asali.
Umeshaacha uchawa kwa mboye??
 
Mtu akikamata tu maiki anaanza "tunamshukuru......". Hata kama hahusiki moja kwa moja
Tunamshukuru nani hii kwa kutuletea maji.

Bila juhudi zake tusingepata maji.
 
Haya yalianza na mwendazake. Hawa wengine wanaiga tu. Wakati tunapiga vita hii tabia, tutafakari kwanini mwendazake alipenda sana kusifiwa hata kwa vihoja hadi kupelekea kuasisiwa kwa tabia ya uchawa
Mfumo ovu ndiyo umetufikisha hapa
 
Kuna wajinga wanaamini uchawa ni uzalendo.
Uzalendo ni kuhoji watanzania watanufaika nini katika hili?
Hiyo kitu ilitake effect awamu iliyopita. Ku a wimbi fulani ambalo lilifanya hadi wasomi wakawa kama mazombi fulani.
Hii kitu usipodhibitiwa tutapa viongoz wa ajabu huko mbeleni
 
Kuna ajira mpya ya kisiasa imezuka katika Taifa letu nayo inaitwa uchawa.

Uchawa ni kitendo cha kuwa mfuasi kindaki ndaki wa mtu kwa matendo na kauli zake bila kujali uhalali wa kile kinachofanywa.

Mtu huyo anaweza kuwa Kiongozi mkuu wa nchi au mwanasiasa yeyote mwenye ushawishi.

Kiongozi mwenye dhamana ya kuliongoza Taifa anao wajibu wa kikatiba kulinda maslahi ya watu wake hivyo inategemewa kwamba kila anachokifanya maslahi ya uma yanapewa kipaumbele.

Ila inapotokea kiongozi huyo akakengeuka katika maamuzi yake basi kwa mifumo ya kiutawala tuliyonayo wananchi wana haki ya kumkumbusha wajibu wake.

Kwa kutambua umuhimu wa kuwa na nafasi za kukosoana na kushauriana Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere alituasa vijana tuwe na hulka ya kuhoji , kwamba pale tunapoona kuna jambo linafanyika na tunaamini linafanyika sio kwa maslahi yetu ya Taifa basi tunapaswa kuhoji.

Hali sasa ni tofauti kabisa, kizazi cha kuhoji kinapotea na ni kama hakipo kabisa kwani watu wamegeuka wabinafsi na kuangalia maslahi yao binafsi.

Kijana anaona kuliko kuhoji na kukosa fursa kwa kuonekana mtukutu bora akubaliane na kila jambo la nwanasiasa au kiongozi wa kitaifa ili akumbukwe kwa favours mbali mbali wanaita kulamba asali.

Kitendo hiki kina faida za muda mfupi ila hasara kwa muda mrefu wa vizazi vijavyo kwani kunauwezekano wa matendo ya wanasiasa kuwa ya kuliangamiza Taifa.

Kijana au mtu mwingine yeyote anapamua kuwa chawa anashiriki kuliangamiza Taifa lake kwani kiongozi husika hatakuwa na woga wa kufanya jambo lolote kwani anajua hakuna wa kumhoji kwa lolote.

Hivyo basi ni vyema tukaondoa dhana hii ya uchawa kwani inaliangamiza Taifa.
Kuna wanaouzidi uchawa waliokuwa wakiufanya Sabaya na Bashite enzi zile za miaka ya ujima(medieval era)?😝😝😝😝😝
 
Sifa zimezidi.

Ukisikiliza hotuba za wanasiasa ni kusifu tuu kila kitu.

Sijui wana mpango gani na Taifa hili??

Sijui vizazi vijavyo watatuona vipi kwa Tabia hizi za ajabu kabisa.
Hivyo vizazi vijavyo vinatokana na sisi, kama wazazi wao wanaishi kwa uchawa na wao watapita mulemule tu.

labda tukibadili fikra zetu Sasa huenda na wao wakawa watu wenye kutumia mno bongo zao kufikiri badala ya kutumia tumbo kufikiri.
 
Kuna ajira mpya ya kisiasa imezuka katika Taifa letu nayo inaitwa uchawa.

Uchawa ni kitendo cha kuwa mfuasi kindaki ndaki wa mtu kwa matendo na kauli zake bila kujali uhalali wa kile kinachofanywa.

Mtu huyo anaweza kuwa Kiongozi mkuu wa nchi au mwanasiasa yeyote mwenye ushawishi.

Kiongozi mwenye dhamana ya kuliongoza Taifa anao wajibu wa kikatiba kulinda maslahi ya watu wake hivyo inategemewa kwamba kila anachokifanya maslahi ya uma yanapewa kipaumbele.

Ila inapotokea kiongozi huyo akakengeuka katika maamuzi yake basi kwa mifumo ya kiutawala tuliyonayo wananchi wana haki ya kumkumbusha wajibu wake.

Kwa kutambua umuhimu wa kuwa na nafasi za kukosoana na kushauriana Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere alituasa vijana tuwe na hulka ya kuhoji , kwamba pale tunapoona kuna jambo linafanyika na tunaamini linafanyika sio kwa maslahi yetu ya Taifa basi tunapaswa kuhoji.

Hali sasa ni tofauti kabisa, kizazi cha kuhoji kinapotea na ni kama hakipo kabisa kwani watu wamegeuka wabinafsi na kuangalia maslahi yao binafsi.

Kijana anaona kuliko kuhoji na kukosa fursa kwa kuonekana mtukutu bora akubaliane na kila jambo la nwanasiasa au kiongozi wa kitaifa ili akumbukwe kwa favours mbali mbali wanaita kulamba asali.

Kitendo hiki kina faida za muda mfupi ila hasara kwa muda mrefu wa vizazi vijavyo kwani kunauwezekano wa matendo ya wanasiasa kuwa ya kuliangamiza Taifa.

Kijana au mtu mwingine yeyote anapamua kuwa chawa anashiriki kuliangamiza Taifa lake kwani kiongozi husika hatakuwa na woga wa kufanya jambo lolote kwani anajua hakuna wa kumhoji kwa lolote.

Hivyo basi ni vyema tukaondoa dhana hii ya uchawa kwani inaliangamiza Taifa.

As long as the president is everything in this country, chawa wataendelea kuwa kikwazo kikubwa katika nchi hii. Most, if not all, ministers and their deputies, PSs and their deputies, RCs, DCs, RASs, DASs, DEDs, etc. are chawas!
 
Kuna ajira mpya ya kisiasa imezuka katika Taifa letu nayo inaitwa uchawa.

Uchawa ni kitendo cha kuwa mfuasi kindaki ndaki wa mtu kwa matendo na kauli zake bila kujali uhalali wa kile kinachofanywa.

Mtu huyo anaweza kuwa Kiongozi mkuu wa nchi au mwanasiasa yeyote mwenye ushawishi.

Kiongozi mwenye dhamana ya kuliongoza Taifa anao wajibu wa kikatiba kulinda maslahi ya watu wake hivyo inategemewa kwamba kila anachokifanya maslahi ya uma yanapewa kipaumbele.

Ila inapotokea kiongozi huyo akakengeuka katika maamuzi yake basi kwa mifumo ya kiutawala tuliyonayo wananchi wana haki ya kumkumbusha wajibu wake.

Kwa kutambua umuhimu wa kuwa na nafasi za kukosoana na kushauriana Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere alituasa vijana tuwe na hulka ya kuhoji , kwamba pale tunapoona kuna jambo linafanyika na tunaamini linafanyika sio kwa maslahi yetu ya Taifa basi tunapaswa kuhoji.

Hali sasa ni tofauti kabisa, kizazi cha kuhoji kinapotea na ni kama hakipo kabisa kwani watu wamegeuka wabinafsi na kuangalia maslahi yao binafsi.

Kijana anaona kuliko kuhoji na kukosa fursa kwa kuonekana mtukutu bora akubaliane na kila jambo la nwanasiasa au kiongozi wa kitaifa ili akumbukwe kwa favours mbali mbali wanaita kulamba asali.

Kitendo hiki kina faida za muda mfupi ila hasara kwa muda mrefu wa vizazi vijavyo kwani kunauwezekano wa matendo ya wanasiasa kuwa ya kuliangamiza Taifa.

Kijana au mtu mwingine yeyote anapamua kuwa chawa anashiriki kuliangamiza Taifa lake kwani kiongozi husika hatakuwa na woga wa kufanya jambo lolote kwani anajua hakuna wa kumhoji kwa lolote.

Hivyo basi ni vyema tukaondoa dhana hii ya uchawa kwani inaliangamiza Taifa.
Pasco ujumbe unakuhusu
 
As long as the president is everything in this country, chawa wataendelea kuwa kikwazo kikubwa katika nchi hii. Most, if not all, ministers and their deputies, PSs and their deputies, RCs, DCs, RASs, DASs, DEDs, etc. are chawas!
Katiba imemlimbikizia madaraka makubwa mtu mmoja hivyo lazima wengine wajikombe kwake kupata fursa.
 
Kwenye hoja kama hizi huwezi kumuona Pascal Njaa

Jamaa anatia kinyaa sana, kutoka kuwa mwandishi nguli mwenye hoja elimishi zilizoshiba hadi kuwa kuwa chawa wa Halima!!!
 

Attachments

  • images (32).jpeg
    images (32).jpeg
    30 KB · Views: 4
Back
Top Bottom