cocastic
JF-Expert Member
- Nov 30, 2019
- 96,456
- 156,324
Babuuh nna babeeh wangu, anatokea pande hizo sasa napatwa wasi wasi kuanza kufanya mafekeche yangu akanistukia, daaah.Babu anakulinda USIOGOPE mjukuu
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Babuuh nna babeeh wangu, anatokea pande hizo sasa napatwa wasi wasi kuanza kufanya mafekeche yangu akanistukia, daaah.Babu anakulinda USIOGOPE mjukuu
Kirenga busuchawi upo zaidi ugweno,usangi na lomwe..
muulize rais wa awamu ya 2.
nadhani hata kwenye kitabu chake hakusalimia na hataki kukumbuka!
aliporudi pwani akatafuta wataalam waliobobea akawatuma kule wakasafishe vijiji vya kishirikina!
ilitokea kasheshe kubwa sana wakati huo ikawa ndio habari ya mjini kipindi hicho!
kuna mzee ana mabasi yatokayo moshi-usangi (sitamtaja)huyo mzee ni fire.
ametesa sana matrafiki waliokuwa wanasumbua basi zake.
kuna trafik alizoea kupiga mkono basi zake hadi leo mkono umebakia kauunyosha juu.hapana chezea huyo mzee!
hiyo ni ruti yake na kila ijumaa usafiri ni bure ole wako konda uchkue nauli unajikuta secret parts hazipo...!
Wenye hizo mbinu hawajitangazi.Nimeshakwambia USIOGOPE nipo nitakupa kinga asione kitu[emoji3][emoji3][emoji3]
Sasa ni wakati Mshana unipe konnection ya pande hizo na mtaalamu.Ni kinga tu nampa[emoji2]
INimezaliwa Makanya
Nimekulia na Kusomea Makanya kuanzia chekechea, shule ya msingi mpaka Kidato cha nne,
Niliondoka Makanya nilipofaulu Kidato cha nne.
Makanya ndio kwetu, Makanya ndio watu wangu, nami ni mtoto wao.
Hayo unayosema yapo Kwa kiasi,
Makanya Ushirikina na Uchawi upo na unaathari labda Kwa wageni wasio wazawa.
Makanya inamchanganyiko wa Makabila kutokana na kilimo cha zao la Mkonge.
Wenyeji wengi ni Wapare,
Lakini pia kuna
Wamasai, wasambaa, Wachaga kidogo, Warundi, Wanyambo, Wasukuma, NK.
Pia wapo wanyiramba.
Uchawi Kwa kiasi kikubwa unapatikana Milimani ambapo ipo Mashariki mwa kamji Ka Makanya.
Wasambaa na watu wa Tanga wameongeza nafasi ya UCHAWI katika mji huo wenye ukame.
Makanya ndio Makao makuu ya Biashara ya Mirungi Afrika Mashariki.
Mirungi hiyo itokayo Milimani hasa Tae, Suji, Parane na Chime ina ladha inayopendwa na watumiaji ukilinganisha na Mirungi ya Kenya na Somalia.
Uchawi pia unaisaidia Biashara hiyo ya Mirungi kuendelea kuexist mbali na Rushwa.
Polisi Wanoko wasiotaka Rushwa hukipata cha mtema kuni wakifuatilia Wauza Mirungi huko Milimani.
Hivyo hujikuta wanapata madhara na kuamua kuacha au huamishwa kabisa kituo cha kazi.
Kipindi nakua, baadhi ya ajali za barabarani zilihusishwa na Uchawi na Ushirikina.
Makanya pia ni moja ya miji iliyojaliwa Madini ya Mawe ya Nasi(Gypsum stone) ambapo hutumika kutengeneza Saruji(Cement).
Ipo dhana katika mji huo kuwa Migodi ya Jasi inaathiri unyeshaji wa Mvua.
Watu wa Makanya kipindi nakua waliamini kuwa Mvua inahamishwa na wenye Migodi ya Mawe Jasi.
Ni kawaida Makanya Wingu Jeusi kutanda lakini upepo ukatokea na kupeperusha mawingu hayo na mvua kugoma kunyesha.
Hata hivyo, kitaaluma Tabia nchi ya Makanya na tambarare ya magharibi ya wilaya ya SAME ni SEMI-ARID DESERT.
Hivyo sifikiri uhaba wa Mvua Makanya unaotokana na uchawi na Ushirikina Bali ni tabia ya nchi ya eneo hilo
AINA ZA UCHAWI ULIOPO MAKANYA KULINGANA NA ASILI;
1. Uchawi wa Wapare wenye asili ya Milimani sio Tambarare
2. Uchawi wa kisambaa
3. Uchawi wa kizigua na Kibondei
4. uchawi wa Kimasai unaotokea magharibi ya Mji wa Makanya ambapo kuna Mji wa Ruvu.
5. Uchawi wa Kirundi kutokana na Wakazi wa Makanya wenye Asili ya Burundi ambao wengi walikuja kufanya vibarua kwenye mashanba ya Mkonge
6. Uchawi wa Wanyambo na Wasukuma. Hawa pia walikuja Kama vibarua vya Mkonge.
7. Uchawi chotara
Ambao kutokana na mchanganyiko wa Makabila Makanya kuna uchawi chotara.
Wachimba Jasi wanaotaka Maeneo mengine ya Tanzania wamechangia kiasi katika uchawi huu.
Msamiati Kama Zongo ni moja ya maneno ya kawaida Makanya.
Kuvunja Jungu, n.k
Makanya na Hedaru ni moja ya miji Maarufu wilayani Same na pia inaongoza Kwa ujanja ujanja.
Sisi Wana Makanya tunapendana mno,
Mwafrika hata akishika dini bado aachi asili.Maeneo yote hayo uliyoyataja asilimia kubwa ni dhehebu la wasabato
Inakuwaje na mambo hayo ya giza?
Tae ni wasabato tupuDini ya sabato ilipoingiaTanzania wamishionari wa kwanza walifika milima ya upare...sijawahi fika upareni lakin nasikia Kuna maeneo Ni watu wa dini Sana hasa linapokuja suala la kutunza sabato..Kama kweli huko viongozi wa dini Ni washirikina mbona wakiwa miji mingine Kama dar etc Ni wasabato haswaaaa na wanashika sabato sanaaa na hawana ushirikina?
Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
Mkuu hapa nyamnyusi wife wangu aliwahi kufundisha hebu nipe kidogoNenda Kasulu Nyamnyusi Utajiridhisha
Hayo Mambo Ni Magumu Ila Yapo Sana
Mchawi na jambazi ni watu wema Sana machoni kwa jamii.Dini ya sabato ilipoingiaTanzania wamishionari wa kwanza walifika milima ya upare...sijawahi fika upareni lakin nasikia Kuna maeneo Ni watu wa dini Sana hasa linapokuja suala la kutunza sabato..Kama kweli huko viongozi wa dini Ni washirikina mbona wakiwa miji mingine Kama dar etc Ni wasabato haswaaaa na wanashika sabato sanaaa na hawana ushirikina?
Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
HakikaMchawi na jambazi ni watu wema Sana machoni kwa jamii.
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]Sasa ninaowasimamia waniloge ili niwapende, nyumbani dada yako aniloge nimpende, mchepuko uniloge ili nizidi kutoa hela, bosi aniloge nisifikirie kuacha kazi, hapo mgahawani nilogwe nisihame mgahawa mwisho niwe zombi kwa mchanganyiko wa madawa. Nitakomaa na huyu mwana hadi kieleweke"[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Kuna Jamaa Alikuwa Anauguliwa Na Mke WakeMkuu hapa nyamnyusi wife wangu aliwahi kufundisha hebu nipe kidogo