Hivi umemesoma vizuri kituko alichokuuliza? Ungesema tu ndiyo au hapana...
Hapa chini ni bandiko la Mohamed Said
Au ulikuwa una maana ya muasisi wa 'wa jina TANU' kama alivyosema kituko?
Wanaukumbi, John Rupia, Said Chamwenyewe, Oscar Kambona, Paul Bomani, Ali Tambwe Mwinyi, Mchango wao TANU ni upi.
Naunga mkono
Nyara hizo hapo chini zinatosha au niongeze nyingine?
R.M. Kawawa, Comments on Dr Mwanjisi Speaks to TAGSA, 28 th December, 1951. Sykes' Paper's
Doctor Mwanjisi Speaks to TAGSA 22 nd December, 1951. Sykes' Papers
The Secretariat Ref. 38515/265 8 th February, 1952. Sykes' Papers.
Sykes to TAGSA Honorary Secretary, to The Honourable Chief Secretary to the Government; Ref. No.1/52/3 10 th January, 1952. Sykes' Papers.
Yericko Nyerere,Nimetoa tafsiri ya mwasisi hapo juu hebu isome mkuu
Mkubwa Ahsante sana.
Vipi TANU iliundwa inabidi urudi nyuma miaka 25 hadi 1929 pale ilipoasisiwa African Association.
Usiishie hapo uje hadi 1933 ilipoasisiwa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika mwaka 1933.
Vyama hivi viwili viongozi wake walikuwa wamoja.
Nadhani umeona kuwa safari ya Nyerere ya UNO mwaka 1954 aliyekuwa anakusanya fedha
alikuwa Idd Faiz Mafongo ambae alikuwa mweka hazina wa Al Jamiatul na mweka hazina wa TANU
kwa wakati mmoja.
Hii inataka maelezo kwa nini ilikuwa hivi.
Ukitaka mfano hai ni kama vile mweka hazina wa Parokia ndiyo mweka hazina wa TANU.
Jambo kama hili haliji bila sababu.
Sasa kuhusu kuasisiwa kwa TANU azma ilikuwapo miaka mingi toka Vita Kuu Vya Pili na Abdu ndiyo
akishawishi wenzake kuunda chama cha siasa.
Mwaka wa 1950 akiwa katibu aliunda TAA Political Sub Committee.
Hili nimelizungumza sana katika mnakasha huu.
Hiki kilikuwa moja ya kituo katika safari ya kuunda TANU.
Nyerere hayumo katika hiyo kamati.
Mpango wa Abdu ilikuwa kumleta Chief Kidaha Makwaia katika TAA kisha kuunda TANU.
Chief Kidaha hakutaka kujiunga na TAA kwa sababu ambazo ziko wazi.
Mwaka 1952 Nyerere akapelekwa kwa Abdu na Kasella Bantu akiwa na barua kutoka kwa
Hamza Mwapachu ambayo ilieleza sifa za Nyerere.
Kama alivyotoa ile rai ya uongozi kwa Chief Kidaha, Abdu aliitoa ile rai kwa Nyerere.
Nyerere aliafiki na hivyo akawa rais wa TAA mwaka 1953.
Mwaka wa 1954 TANU ikaundwa.
Katika kitabu changu nimesema maneno haya:
[TABLE="class: MsoNormalTable"]
[TR]
[TD] ...it was during this time that Abdulwahid, for the second time, advised Nyerere to resign from teaching so as to concentrate fully on the work of the Association.
This idea did not appeal to Nyerere, just as it had not appealed to Chief Kidaha Makwaia four years earlier.
But Nyerere had gone a step further than Chief Kidaha. He had at least accepted leadership of TAA.
Nyerere was also aware that TAA was being sustained by patriots who did not number more than four and that he would live on their charity, whatever their good intentions.
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 601"] What drove the TAA inner circle to insist on Nyerere's assuming TAA's leadership on full-time basis was first, that the Association was then operating more or less as a political party and the governor was aware of it; secondly, the plan was in operation to register as a political party before the end of the year.
TAA was busy working on the draft of the constitution for the new party and plans were under way for the president of the proposed political party to travel to the United Nations to appear before the Trusteeship Council as Japhet Kirilo had done two years before.
It was important that there should be a full-time president when the new party was founded. [/TD]
[/TR]
[/TABLE]
Yapo mambo mengi aliyofanya Abdu Sykes na mengi yakihitaji uwezo mkubwa sana wa fedha
kukamilisha.
Naacha wazi akili ya msomaji aamue mwenyewe katika hali kama hii vipi Nyerere aweze kuunda
TANU kwenye mji kama wa Dar es Salaam ile ya 1950.
Nimetoa tafsiri ya mwasisi hapo juu hebu isome mkuu
Hatuwezi shindana nao kwa midomo, vita yetu iko shuleni watakaohitimu hawatawasikiliza tena na Jua lao hao linaelekea kuzama.
Bwana Mohamed Said.
Simulizi za maisha binafsi ya wazee wako na harakati za ukombozi wa Tanganyika, zinaweza kuwa sahihi kabisa. Kama "unatusoma" between lines. Utaona kwamba hatupingi kuwepo kwa hao wazee wako, au ushiriki wao katika kupigania uhuru wa Tanganyika. Hata kama ukiandika "Sykes alikula mapapai matatu", au "Salum Abdalah alikuwa anakula Nsasa na matoborwa", kama ulivyosimuliwa, sisi hatukupingi.
Mengi ya tunayopinga yapo katika "premises" ambazo zimejengwa katika hisia. Ni katika hisia hizo, ndipo ULIPOLAZIMISHA kuwepo kwa uadui kati ya Nyerere na Wakristo kwa upande mmoja, na waislam kwa upande mwingine. Umetumia maneno, " inasemekana Mwalimu alikuwa hapendi hiki au kile", , "it is said that church lobby did this or that"
Na mara nyingine umekuwa uki-cook conclusions zako ukizifanya kama vile facts, wakati hazina msingi wowote wa tafiti za kisayansi,. Kwa mfano unasema: "the truth is that Muslims were not better off than they were 30 years before" Wakati hauoneshi tafiti zozote zinazo support hiyo "truth" yako.
Na wakati mwingine, umekuwa kama mtabiri, ambaye unaamini kuwa unayajua mawazo ya watu. Mara nyingi hapa umeonesha kama vile ulikuwa unajua mambo ambayo Nyerere alikuwa anawaza. Nafikiri hii ni hulka yako, ndio maana hata hapa jamvini, mara kadhaa unafikiri unajua tunachowaza, mara "ooh, wamestushwa", mara " ooh, walikuwa hawajawahi kumsikia huyu na yule" Kwa ujumla haya ndio tunapingana nayo. Premises za namna hii ndizo ulizotumia kupandikiza chuki katika jamii. Chuki hii iko very personal. Ya kwako dhidi ya Nyerere na wakristo (Chanzo cha chuki tunakijua). Lakini ukaona uitumie kupatia pesa kwenye mihadhara, na safari za kimataifa, huku ukishawishi waislam wote wamchukie Nyerere na wakristo. Na hapo hatukubani na wewe.
Sasa tukikubana kwenye hizo "angles" unasema " ooh mimi nasimulia habari za wazee wangu", " na nyie andikeni kitabu" " sijibu maswali yasiyo na tija" "Mwalimu shaffi alinifundisha nisibizane na wajinga"
Halafu wewe mwenyewe unashangaa kwamba kwa miaka kumi na tano baada ya kutoa kitabu chako, serikali na kanisa hawajakujibu … kwani wao ndio wanalazimishwa "kujibizana na wajinga"???
nanren,
ndugu yangu hata wewe huna sababu ya kujibizana na mjinga.
Hiki kitabu ni cha miaka mingi sasa.
Kisikushughulishe.
Mkuu baadae sijuhi walishtuka nini walikukuja rekebisha kidogo msemo huo ukuwa "ZIDUMU FIKIRA SAHII ZA MWENYEKITI WA CCM" wakaongezea neno sahihi!!! Mtu uwezi kuamini kama tulikuwa tunaishi in real au virtual WORLD wakati huo!Nikiikumbuka Tanzania nakumbuka ZIDUMU FIKRA ZA MWENYEKITI WA CCM. Na wakti huo Mwenyekiti ni CCM ni Nyerere. Kwa kufikiri kidogo tu utaona huyu alikuwa Mungu mtu yaani zidiume fikra zake zote hata zikiwa za kuangamiza Taifa lake.Kweli enzi za Nyerere tulijifunza na kuona mengi
nimetoa tafsiri ya mwasisi hapo juu hebu isome mkuu
Mkubwa Mohamed Said, napenda kufahamu mengi kuhusu historia ya nchi yetu, nimeshtuka kidogo kuhusu hicho kisa cha kuchoma nyaraka za TANU. Ukipata wasaa tujuze kaka.
Si kweli!Nilichogundua wengi hawajui maana ya Mwasisi/kuasisi has hasa katika dhana ya vyama vya siasa!
Katika dhana ya siasa, "kuasisi" ni kuongoza kwa mara ya kwanza kundi lenye malengo fulani
Hivyo kiongozi wa awali huitwa mwasisi na waambata wake pia huitwa waasisi wa cha chama hicho, lakini katika uso wa wengi, ni kiongozi tu ndie huonekana zaidi!
Ikiwa ni kampuni au NGOs basi mwasisi wake huwa ni mmoja tu!
umemjibu vema sana,japo wao wanakuja kwa jazba na kejeli ili wakutoe kwenye mstari ila nakupongeza sana kwa jins unavojituliza na kuwajuza wajinga mambo wasiyoyajua,,
stil hatujaona criticisms zenye tija kutoka kwao.
Sina lakini najua kama wamejiwekea asilimia zakupitisha hakuna shida.Una uhakika sio NECTA?
Nyaraka hizo hapo chini zinatosha au niongeze nyingine?
Annual Report of the Secretary of Tanganyika African Association, 7 January, 1951. Sykes' Papers.
R.M. Kawawa, Comments on Dr Mwanjisi Speaks to TAGSA, 28 th December, 1951. Sykes' Paper's
Doctor Mwanjisi Speaks to TAGSA 22 nd December, 1951. Sykes' Papers
The Secretariat Ref. 38515/265 8 th February, 1952. Sykes' Papers.
Sykes to TAGSA Honorary Secretary, to The Honourable Chief Secretary to the Government; Ref. No.1/52/3 10 th January, 1952. Sykes' Papers.
Julius K. Nyerere, President Tanganyika African Association to Governor Edward Twining, 10 th August, 1953. Sykes Papers.