Unaona ulipojikwaa? Na mzee Mohamed Said naye alijikwaa hapohapo. Kama Mohamed Said hakufanya utafiti kwa mapadre/viongozi wa dini wa kikistu , ilikuwaje akaweza kuwaweka kwenye kitabu/papers zake? alikwenda kuwauliza au amenukuu tu kutoka kutoka kwa waandishi wengine? Nyerere nae alihojiwa?Nafikiri Kazimoto wewe ujawahi kufanya utafiti wowote. Ngoja nikusaidie kidogo.
Ili mtu uweze kufanya utafiti ni lazima ujue unataka kufanya utafiti wa Nini. Huwezi kufanya utafiti wa kila kitu.
Al Akhiy Mohamed Said alitaka kufanya utafiti wa Mchango wa wazee wake katika kupigania uhuru wa Tanganyika. Na hilo ameliweka wazi kila mtu analijua hilo. sasa asingeweza kwenda mpaka kwa hao mapadri au hata kwenda kwa chifu Rumanyika wa kule Bukoba. yeye amejikita zaidi kwa wazee wake wa Dar katika kupigania uhuru wa Tanganyika na reference yake kubwa ilikuwa Kijitabu cha Kivukoni ambacho kilisahau mchango wa wazee wake.
sasa na wewe unaweza chukua kijitabu cha Kivukoni kuhusu historia ya Uhuru wa Tanganyika na kile cha Mohamed Said kuangalia kama kuna watu wamesahaulika basi na wewe ukatoa kijitabu chako. Hiyo ni ruhsa kabisa kuliko kutoa shutuma na lugha za kejeli kwa al akhiy Mohamed Said kwa kazi yake nzuri.
Pole sana.
Ningekuelewa kama angekuwa ameandika simulizi TU za wazee wazee wake wa gelezani...