Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar


Mkuu Ngongo,

Unauliza swali wakati jibu lipo wazi kila mmoja anaeleza madhira yake, alichofanya Mohamed Said kaeleza madhira yaliyowakumba wazee wake ambao ni waislam.

Ni kweli Kambarage aliwatosa hawa madaktari na wengine wakakimbia nchi, familia za hawa wazee wazalendo zipo mpaka sasa ndiyo wanajua madhira walioyofanyiwa wazee wao na Kambarage.

Lakini kwanye ili sidhani kama Nyerere atapata lawama kisa kawafanyia wakiristu wenzake.
 
Last edited by a moderator:
Huyo ndiye wa kwanza na ndiye alikuwa mweka hazina wa Jammiatul Islamiya na ndiye aliyefanya safari ya kwenda Tanga kuzileta fedha zilizomuwezesha nyerere kusafirishwa kwenda New York, bado tu huuoni umuhimu wake?

Zomba,

Hebu tujikumbushe:

Kumbukumbu zinaonyesha kwamba Idd Faiz Mafongo alihudhuria mkutano wa uzinduzi wa TANU katika Ukumbi wa Arnautoglu.

Haifahamiki kwa hakika hasa ni lini Idd Faiz alijiunga na TANU kwa sababu kadi yake ya kwanza ya uanachama ilipotea na akapewa
kadi nyingine iliyokuwa na namba 915 iliyotolewa tarehe 28 Agosti, 1954.

Lakini kwa kukisia tu kutokana na kadi ambayo Idd Faiz mwenyewe aliitoa kwa kaka yake Idd Tosiri ambayo ilikuwa kadi namba 25
na yenye saini yake kama afisa aliyetoa kadi hiyo, inaweza kuchukuliwa kwa uhakika kuwa Idd Faiz alikuwa miongoni mwa wale
watu wa mwanzo kabisa kuingia TANU na huenda akawa miongoni mwa wanachama ishirini wa mwanzo.

Ukichukua katika fikra ukweli kwamba Ali Mwinyi Tambwe aliyekuwa katibu wa Al Jamiatul Islamiyya aliingizwa TANU na Mtemvu
katikati ya mwezi Agosti, 1955, huenda Ally Mwinyi kama katibu wa Al Jamiatul Islamiyya na Idd Faiz akiwa mweka hazina, wote
wawili waliingia TANU wakati mmoja.
 
Tufahamishe kwa nini Chifu Kidaha Makwaia, alifungwa na Wilbard Mwanjisi kwa nini alikimbia nchi.
Kwa kweli sijui lakini kumbukumbu za mahakama zipo. Mzee Mwanjisi ndugu na jamaa zake wapo.
 

WC,

Niwie radhi sina hizo katiba.
 
Mkuu Ritz ndiyo ushangae walioshindwana na Mwl Nyerere walikuwa wengi,watu wa makabila yote,watu wa dini zote Mohamed Said hakuliona hilo kaamua kuchagua kundi lake la wazee wa Gerezani kumbe wapo wahaya,wachagga,wapare,wanyakyusa,wapemba,wakristo,waislam na wengine wengi.


 
Last edited by a moderator:
Huyo ndiye wa kwanza na ndiye alikuwa mweka hazina wa Jammiatul Islamiya na ndiye aliyefanya safari ya kwenda Tanga kuzileta fedha zilizomuwezesha nyerere kusafirishwa kwenda New York, bado tu huuoni umuhimu wake?
Hilo tu? Kwa hiyo fisadi Rostam Aziz ni muhimu sana kwa URAIS wa Rais wetu JK?
 
Mze Saidi..wale Wazuru kina Sykes walipokuja na Weissman walikuwa tayari wameshasilimu?
 
Ritz,
Unawafahamu waweka hazina waliopita wangapi wa TANU? Kwa nini Idd Faiz pekee ndie akumbukwe? Kwa DINI yake?
WildCard,

Idd Faiz Mafongo ndiyo mweka hazina wa kwanza TANU na alihudhuria mkutano wa uzinduzi wa TANU katika ukumbi wa Arnautoglu.

Kaka yake na Idd Faiz, Idd Tosiri ambae alikuwa na kadi namba 25 ndiyo alikuwa afisa ambaye anatoa kadi za TANU.

Mwaka 1953 Idd Faiz alikuwa na umri wa miaka 43. Huyu ndiyo aliyempeleka Nyerere Bagamoyo kwa Sheikh Mohamed Ramia, pitia hotuba ya Nyerere hapo juu kuhusu safari yake ya kwenda Bagamoyo kufanyiwa dua.

Idd Faiz alikuwa akifuatana na Nyerere katika za awali za kuitangaza TANU, akihutubia mikutano jukwaa moja na Nyerere.

Huyu ndiye aliyekuwa mkusanyaji wa pesa za kumpeleka Nyerere UNO. Kasafiri mpaka Tanga kukisanya michango tukuwekea picha yake.

Mkuu unawajua marais wa TAA waliyopita kabla ya Nyerere.
 
Last edited by a moderator:
Duh WildCard ha ha ha ha jamaa alikuwa busy kuandika habari za wazee wake wa Gerezani na kuiita historia ya uhuru wa Tanganyika.Na mimi naandika historia ya wazee wangu wa Arusha ambao Mwl Nyerere kawasahau kabisa.Nani anamkumbuka Mzee Maeda mwaafrika wa kwanza kujenga ghorofa Arusha mjini alikuwa akimpokea Nyerere na kumlaza hotelini mwake mikutano yote ya TAA/TANU ilifanyika nyumbani kwake wakoloni walimsumbua sana hadi kuyumbisha biashara zake za mabus na mahotel.Kasahaulika mzee wa watu kwasababu ya dini yake ya kikristo.

Acha utani Mzee Mohamed. Hauwezi kuandika HISTORIA ya TAA, TANU na NCHI yetu bila kupitia document muhimu kama hizi! Utakuwa umetudanganya sana. Ni aibu.
 
Last edited by a moderator:

Walioshidwa vipi?
 
Last edited by a moderator:
zomba,
naamini akili yako ni pana zaidi ya haya unayoyaandika hapa. Hebu ushughulishe ubongo wako kidogo tu.
 
Mkuu Ngongo,
Ndiyo vizuri ukiandika hiyo historia ilikuwa mwaka gani?
 
Last edited by a moderator:

zomba mzee wa hints..!

umenifurahisha sana mkuu,
jamaa anataka kukimbia na sadaka yetu sio??
Aje aimwage elimu yake hapa na sisi tufaidike,aache zake hizo..
 

N,

Ndugu yangu nimefika Library of Congress.
Ikiwa huamini basi.

Si jambo kubwa.
Mimi Allah kanifungulia dunia Alhamdulilah.

Nimetembea kwingi sana.

Mimi na kaka yangu sote tumezaliwa Kipata.
Yeye ni Prof. Ph D Genetics.

Iko siku tunakula dinner Cape Town na wake zetu.
Nikamwambia, ''Kaka from Kipata to Cape Town...''

Tuliangalia tulikotoka Kipata, Gerezani leo tuko Cape Town...

Ngoja nikuage na hii.

Nimewahi kuzuiwa Heathrow kuingia Uingereza kwa sababu tu passport yangu
ilikuwa imeingia nchi nyingi sana.

Walidhani mie Mzungu wa Unga...
Baada ya kujiridhisha wakaniachia.

Wewe inakutisha hiyo Washington DC kuwa sijaingia Library of Congress...

Nimefika hadi New York Columbia University kwenda kuona alikosoma shemeji yako...
Nilipokelewa na walimu wake na walinialika hadi nyumbani kwao New Jersey...

Mie si limbukeni nijisingizie nijikwaze...
Haya naeleze kukata kibri chenu.

Kwa kawaida sie huwa hatujinasibu.
 
Acha utani Mzee Mohamed. Hauwezi kuandika HISTORIA ya TAA, TANU na NCHI yetu bila kupitia document muhimu kama hizi! Utakuwa umetudanganya sana. Ni aibu.

WC,

Hapana ugomvi.
Hilo lichukulie utakavyo.
 
Ama Kwa Hakika Ndug Moh Said ni Bingwa na Mjuvi wa Minakasha..

uliaga na ukasema unaondoka wakaanza kulalamika na kukutaka urudi ya kwamba walikumis,,

sasa unazid kumwaga NONDO Wanaanza Kupata STRESS..!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…