Jina la kitabu
HISTORIA YA KWELI YA TANGANYIKA
Waadishi ni Yericko Nyerere, Mag3, Mzee Mwanakijiji, Nguruvi3, Nyambala, nyiondo, WildCard, kibol, Jasusi,
Kitabu kipo njiani wakati wowote kitatoka. Watanganyika jiandaeni kuisoma historia yenu jopo la waandishi vichwa wa JF kwa pamoja wanaunganisha nguvu kuandika kitabu.
Nisahihi kabisa, labda kwakuongezea tu nikuwa tutawajumuisha watanzania wenzetu akina Mohamed Said, Ritz, Zomba, Boko Haram, Kichwangumu nk!
Sisi waswahili wauza kahawa wenye akili za madrasa tutakichafua kitabu chenu.
Hakuna uchafu ulio uchafu mtupu,Sisi waswahili wauza kahawa wenye akili za madrasa tutakichafua kitabu chenu.
Hakuna uchafu ulio uchafu mtupu,
Huwa siamini katika usisi na unyinyi!
Naamini katika umoja tu!
waswahili sisi tangu lini mambo haya?
wataanza kutumia kikristo (kiingereza) ambacho sisi hatujui mpaka tutumie google translate
hivi kama red maana yake ni hiyo blue, kwanini usingetumia hiyo red tu au blue tu?Alamat'l Munafik Thalatha. Alama za mnafik ni tatu. Jee, unazijuwa?
Mkuu, huyo Ritz ni mfuta viatu wa mkombozi wao Mohamed Said, hawezi kukujibu zaidi yakumpigia makofi Mohamed Said
hivi kama red maana yake ni hiyo blue, kwanini usingetumia hiyo red tu au blue tu?
dini yenu lazima ukitaja sentesi kwa lugha ya kiarabu lazima utafsili ndo utaeleweka?
Zomba,Sisi mpaka sasa tuna Maalim Mohamed Said tuna Dr. Hamza Njozi ambae kitabu chake Nkapa kakipiga marufuku lakini kinasomwa kwa sana tu, bado tunatoa nao. Nyinyi kusanyikeni wote na mje na kitabu chenu, tena naona mnachelewa, mwaka wa kumi na tano huu kitabu cha Mohamed Said kinatamba.
Na kuna vingine vinashuka hivi karibuni, kaeni chonjo.
WC unajua ukiamini masimulizi ni rahisi sana kupotezwa. Simulizi zima la vita vya Kagera limelenga katika kumtuhumu Nyerere na udini dhidi ya Idd Amin ambaye hata Waganda wanaishukuru sana Tanzania hadi leo.Hiyo vita ndio hatuwezi kuongopeana kabisa uwadanganye hawa vijana waliozaliwa miaka ya '70 kuelekea '80. Uongo mzuri ni kama wa mzee Mohamed aliouficha kwenye kanzu na barghashia za wazee wake wa Kariakoo.
WC unajua ukiamini masimulizi ni rahisi sana kupotezwa. Simulizi zima la vita vya Kagera limelenga katika kumtuhumu Nyerere na udini dhidi ya Idd Amin ambaye hata Waganda wanaishukuru sana Tanzania hadi leo.
Hao wanaoamini vita ya Kagera hawajui kuwa kulikuwa na mtafaruku mkubwa 1973 uliosuluhishwa na Marehemu Haile Selasi wa Ethiopia. Hawaelewi kuwa Mwanza ilishawahi kushambuliwa kwa mabomu.
Uktaka kumpata Mtanzania basi tunga jambo halafu chomeka harufu ya udini kila mmoja ataingia kichwa kichwa.
Tatizo la taifa letu ni watu kutopenda kutafuta elimu kwa kujisomea. Kila jambo limekuwa ''mission town'' hata elimu watu wanaifanya hivyo
Zomba,
Si kila mtu ana kipaji cha uandishi. Mohamed kajaliwa kipaji hicho. Lakini kwa sababu Mohamed kaandika kitabu akijikita zaidi kwa michango ya Waislamu, hakuna sababu yangu mimi kuandika kitabu cha michango ya Wakristo. Lakini wakati huo huo tunayo haki, kama wasomaji, wa kupinga yote anayosema Mohamed kwa sababu kwa kanuni za uandishi, yeye ameegemea zaidi upande mmoja tu, kwa kuzingatia simulizi za wazee wake. Kuna vitabu vingi tu vimeandikwa ambavyo ni more balanced, na tumevisoma na ndiyo sababu tuko hapa kumwonyesha Mohamed ni wapi amepindisha na ni wapi anapotosha kwa malengo yake.
Hamtachafua, kwanini unapenda kusema chenu ama chetu?
Kitabu kitakuwa cha watanzania wote mimi, wewe na wale!
Acha ubora mimi ndugu!
Mohamed, Mag3 ameelezea kuhusu mzozo wa nyumba uliomhusisha D.Cameron.Nguruvi3,
Tuendelee na mjadala:
Mapema mwaka wa 1930 katika juhudi za kuikiimarisha chama,
Kleist akawa anasimamia ujenzi wa jengo la makao makuu ya
African Association, New Street (sasa Mtaa wa Lumumba) ambalo
wananchi walikuwa wakijenga ofisi yao kwa kujitolea nguvu zao
wenyewe.
Hili ndilo jengo ambalo TANU ilikuja kuzaliwa tarehe 7 Julai, 1954.
Nyumba hii ipo hadi leo ingawa si kama ilivyojengwa hapo hapo
mwanzo.
Hivi sasa jengo hilo ni katika majengo ya hapo mwanzo makao
makuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na hivi sasa ni ofisi yake
ndogo.
Ile nyumba ya zamani ilikuwa imejengwa kwa chokaa, udongo na
mawe kama ilivyokuwa desturi ya ujenzi wa wakati ule.
Chokaa ndiyo iliyokuwa ikitumika badala ya sementi.
Akiwa bado mtoto mdogo, Abdulwahid anakumbuka kumuona
baba yake na wenzake wakijenga nyumba hiyo kwa kujitolea
siku za Jumapili.
Vilevile alimuona baba yake akifanya mikutano na akishughulika na
uongozi wa harakati za Kiislam na vyama vya wafanyakazi.
(Kutoka ''Maisha na Nyakati za Abdulwahid Sykes...'')
Kuna picha ndani ya kitabu ya ufunguzi wa jengo hilo iliyopigwa 1933
Gavana Cameron yupo pamoja na Kleist, Mashado Plantan, Mwalimu
Mdachi Shariff na wanachama wengine wa African Association.
Cecil Mtola alikufa mwaka 1933 na Mzee bin Sudi akachaguliwa kushika
nafasi yake.
Nakaa kisha nainamisha kichwa kushoto natafakari sana, kisha najiuliza hivi wanaounga ngano za Mohamed Said wanaunga kwakusimamia ukweli wa historia au wanasimamia ukweli wa imani zao?
Kwanini imani iwalazimishe waukane ukweli na kuziabudu ngano hizo?
Kweli napata tabu sana kichwani mwangu, sijui niamue kuwaweka kundi gani hawa watanzania wenzangu?!
Sijui niwasaidieje, nazidi kuwaombea kwa Jah awape ufahamu na waifahamu kweli nayo kweli iwaweke huru!
Mohamed, Mag3 ameelezea kuhusu mzozo wa nyumba uliomhusisha D.Cameron.
Katika maelezo yako unaelezea ujenzi wa nyumba hiyo tu.
Bado hoja haijajibiwa kwa ukweli kuwa hujakanusha kuwepo kwa mzozo.
Labda tuulize tena, Je, ni kweli kulikuwa na mzozo wa Nyumba iwe hiyo au iwayo kama alivyosema Mag3?
Mpaka sasa hamjafanikiwa. Hapo sasa.
Wewe ndiyo umeleta hizi ngano unaulizwa maswali huna majibu zaidi ya matusi hata ukichukia kazi bure kitabu kipo toleo la tatu...saizi sikusikii tena ukija kama rais wa JF Mohamed Said kaamua kushinda JF, kulala JF, kula JF, kuweka wazi historia ya wazee wazalendo waliosahulika.
Kazi iliyobakia kwako ni kupromosha matusi tu.