Yericko Nyerere
JF-Expert Member
- Dec 22, 2010
- 17,005
- 20,425
- Thread starter
-
- #5,481
Mohamed Said anakuja na data na facts za kutosha katika kuelezea historia ya wazee wake nyie wengine mnakuja na maneno matupu.
Hii ndiyo tofauti yenu ndiyo maana nyie mnaepinga kila kitu mnaishia kumuuliza maswali huyo mnayempinga.
Kitu kikubwa mnacho mshinda Mohamed Said ni lugha za kejeli na dhihaka.
Ndio tofauti ya mtazamo na fikra tengefu za Mwalimu Nyerere na wazee wenu na sasa nyinyi mmeriithishwa,heshima ingetakiwa ianzie kwake kama yeye alishindwa kuwapa kipaumbele waliompokea hayo ndio matokeo yake
heshima ingetakiwa ianzie kwake kama yeye alishindwa kuwapa kipaumbele waliompokea hayo ndio matokeo yake
Ulitaka awape kipaumbele gani? Hivi unajua ni wazee wangapi wa Jijini Dar amb ao walipewa kipaumbele katika serikali (na watoto wao) kulinganisha na wazee wengine? Ulitaka afanye nini awajengee chumba Ikulu?
Unajua maana ya kuja na data?
Kuja na data maana yake ni kuja na vielelezo visaidizi nje ya wewe mtuhumiwa/muhusika!
Sasa lieleze jukwaa hili ni data zipi ambazo Mohamed Said amekuja nazo hapa kujibu hoja zetu nje ya aliyoyaandika yeye mwenyewe na kibaya zaidi ni kuwa data hizo ndizo tunazozipinga hapa!
Kaka yangu Jasusi,Zomba,Kama wewe kweli unaamini Nyerere aliondoka Magomeni kwenda sokoni Kariakoo kuwanunulia watoto wake chakula huku hana hata senti tano mfukoni basi ama wewe ni mwendawazimu au Nyerere ndiye alikuwa na wazimu.Na hotuba za Nyerere, hasa ile ya kwanza UN tunajua aliiandika mwenyewe. Kama TANU walimpa point of references na draft hilo ni jambo jengine ambalo Mohamed hakusema kabisa. Alitaka tuamini kuwa aliisoma kama kasuku huko UNO.
Mimi nilidhani mjadala tumeshaufunga baada ya kuweka mambo kadha wazi na Bw. Said hajayakanusha.
a. Hakufuata kanuni za uandishi wa historia (historical method) katika kujaribu kusimilia "historia"
b. Katika hilo la (a) alichagua vyanzo vyenye kukubaliana na nadharia yake na hivyo kutafuta ushahidi wa yale yanayoendana na hisia zake. Lolote lililopingana na hisia hizo aliliweka pembeni.
c. Ametegemea ushahidi wa watu rafiki tu na wa karibu kama ushahidi pekee wa msingi huku ushahidi wa vyanzo vyenye kuweza kujua zaidi akiviacha pembeni.
d. Vyanzo vile ambavyo ameweza kuvinukuu karibu vingi tayari vimetangulia mbele ya haki. Hakuna mahali popote ambapo amewarekodi hao anaodai aliwasikia ili watu wengine waweze kupima ukweli wa wanachodaiwa kusema (mfano mzuri ni nukuu yake kuhusu Ditopile akielezea suala la Mshume Kiyate)
e. Madai yake yake kuwa yeye ndiye amekuwa wa kwanza kuwataja 'wazee wake' hadharani na kuhusika kwao kwenye harakati za uhuru yamethibitika kuwa si ya kweli kwani wapo wengi waliowataja kabla yake; John Illife na August Nimtz ni mfano tu ambao waliutaja kwa usahihi kabisa mchango wa wazee wa Kiislamu katika harakati za Uhuru - bila kujaribu kumfanya Nyerere duni ili wapande kwenye mabega yake.
KUtokana na hayo yote a-e ni wazi kuwa soma maandishi ya Bw. Said at your own risk lakini ukiwa na open mind kuelewa kuwa unachosoma siyo historia bali ni HISTOHIA - yaani historia inaposimuliwa chini ya mwanga wa hisia za msimulizi.
Mimi nilidhani mjadala tumeshaufunga baada ya kuweka mambo kadha wazi na Bw. Said hajayakanusha.
a. Hakufuata kanuni za uandishi wa historia (historical method) katika kujaribu kusimilia "historia"
b. Katika hilo la (a) alichagua vyanzo vyenye kukubaliana na nadharia yake na hivyo kutafuta ushahidi wa yale yanayoendana na hisia zake. Lolote lililopingana na hisia hizo aliliweka pembeni.
c. Ametegemea ushahidi wa watu rafiki tu na wa karibu kama ushahidi pekee wa msingi huku ushahidi wa vyanzo vyenye kuweza kujua zaidi akiviacha pembeni.
d. Vyanzo vile ambavyo ameweza kuvinukuu karibu vingi tayari vimetangulia mbele ya haki. Hakuna mahali popote ambapo amewarekodi hao anaodai aliwasikia ili watu wengine waweze kupima ukweli wa wanachodaiwa kusema (mfano mzuri ni nukuu yake kuhusu Ditopile akielezea suala la Mshume Kiyate)
e. Madai yake yake kuwa yeye ndiye amekuwa wa kwanza kuwataja 'wazee wake' hadharani na kuhusika kwao kwenye harakati za uhuru yamethibitika kuwa si ya kweli kwani wapo wengi waliowataja kabla yake; John Illife na August Nimtz ni mfano tu ambao waliutaja kwa usahihi kabisa mchango wa wazee wa Kiislamu katika harakati za Uhuru - bila kujaribu kumfanya Nyerere duni ili wapande kwenye mabega yake.
KUtokana na hayo yote a-e ni wazi kuwa soma maandishi ya Bw. Said at your own risk lakini ukiwa na open mind kuelewa kuwa unachosoma siyo historia bali ni HISTOHIA - yaani historia inaposimuliwa chini ya mwanga wa hisia za msimulizi.
Ulitaka awape kipaumbele gani? Hivi unajua ni wazee wangapi wa Jijini Dar amb ao walipewa kipaumbele katika serikali (na watoto wao) kulinganisha na wazee wengine? Ulitaka afanye nini awajengee chumba Ikulu?
Mjadala haujafungwa kama wewe umechoka au unakereka na michango ya Mohamed Said unaweza kukaa pembeni kuna umati wa Watanzania wanafuatilia huu mjadala.
Ulitaka awape kipaumbele gani? Hivi unajua ni wazee wangapi wa Jijini Dar amb ao walipewa kipaumbele katika serikali (na watoto wao) kulinganisha na wazee wengine? Ulitaka afanye nini awajengee chumba Ikulu?
Tarehe 27 Aprili, 1985 Nyerere akijulikana kama Baba wa Taifa katika sherehe kubwa Ikulu alitoa Medali 3,979 kwa Watanzania waliochangia maendeleo ya Taifa letu.
Katika waliopewa Medali alikuwa Sheikh Abdallah Chaurembo peke yake.
Sasa wewe Mwanakijiji hebu jiulize hawa wazee wengine wa Dar es Salaam waliyomsaidia siyo wazalendo.
Angalau nakufahamu kidogo Mzee Mohamed. Mtu ambaye hakuwa upande wa wazee wako huyo lazima alikuwa kibaraka wa wakoloni. Mtu ambaye alikuwa upande wa Mwalimu, hata kama ni Muislam mwenzako kama akina Rashid Kawawa, huyo naye ni kibaraka wa mfumokristo! Mtu wa ajabu sana mzee wewe ambaye unadhani uko sahihi wakati wote.Ritz,
Hawa ndugu zetu ni watu wa kuonewa huruma kwa maana
wanakikimbilia chombo kinachozama.
Walimleta Martin Kayamba na kumtaka awe shujaa wao.
Kwa kweli mimi nilitingisha kichwa kwa masikitiko na huruma.
Najiuliza hivi hawa wanamjua huyu Martin Kayamba?
Wewe ukawaambia huyu bwana umaarufu wake ulikuwa kufuga
kuku pale Muheza.
Mimi nikawaeleza wenzake walikuwa wanamuonaje - kibaraka
wa Waingereza aliyependa kujikomba kwa bwana.
Siku nyingi nikijua kuwa hawa ndugu zetu hii historia ya Tanganyika
hawaijui lakini kinachowasukuma kuitetea ni ule mshtuko uliowapiga
baada ya kusoma yale waliyokuwa wamefichwa kwa miaka mingi.
Hivi kweli Rais wa NCHI anaweza kuhangaika kujua nani apate medali? Awape medali hata waliompelekea maharage na dagaa kule Magomeni? Masuala ya medali hayaandaliwi na ofisi ya Rais jamani. Nchi haiendeshwi hivi. Hata familia zetu sio kilakitu ni baba.Tarehe 27 Aprili, 1985 Nyerere akijulikana kama Baba wa Taifa katika sherehe kubwa Ikulu alitoa Medali 3,979 kwa Watanzania waliochangia maendeleo ya Taifa letu.
Katika waliopewa Medali alikuwa Sheikh Abdallah Chaurembo peke yake.
Sasa wewe Mwanakijiji hebu jiulize hawa wazee wengine wa Dar es Salaam waliyomsaidia katika harakati za uhuru siyo wazalendo.
Hapo juu kwenye hotuba yake mwenyewe anakiri walimsaidia sana.
Unajua maana ya kuja na data?
Kuja na data maana yake ni kuja na vielelezo visaidizi nje ya wewe mtuhumiwa/muhusika!
Sasa lieleze jukwaa hili ni data zipi ambazo Mohamed Said amekuja nazo hapa kujibu hoja zetu nje ya aliyoyaandika yeye mwenyewe na kibaya zaidi ni kuwa data hizo ndizo tunazozipinga hapa!
Unataka Mohamed Said ajibu hoja gani tena wakati wewe ndiyo umeanzisha huu uzi kuwa Mohamed Said ni mchochezi wewe ndiyo unatakiwa uthibitishe uchochezi wake.
Bila Mohamed Said wewe usingejua kama John Hatch kutoka chama cha Labour cha Uingereza alifanya mkutano mkubwa sana Mnazi Mmoja kuunga mkono ukombozi wa watu weusi watu 20,000 walihudhuria huo mkutano Ally Mwinyi Tambwe alikuwa mkalimani, pembeni yupo Oscar Kambona na Denis Phombeah. Nyerere alikuwa yupo Musoma.
Bila Mohamed Said ungewajua hawa Schneider Plantan, Liwali Yustino, I. C. Chopra. Charles Philips, Robert Makange, Arthur Lewis.
Hebu na wewe tupe data na facts ambazo unazo kutoka AA, TAA, TANU.
Mohamed Said kaja na kitabu, wewe umekuja na shutuma, wewe ndio ulitakiwa ulete ushahidi wa tuhuma zako, umeshasahau hii mada imeanzishwa na nani na kwa nini?
Kaka yangu Jasusi,
Hakuna asiyefahamu umahiri wa Mwalimu katika hotuba hata kama haijaandikwa. zomba hataki kuelewa kwa makusudi tu. Muulize kama aliwahi kuona au kusoma kokote hotuba ya Abdulwahid Sykes. Elimu ya Mwalimu na Abdu ilikuwa tofauti kama kichuguu na mlima Kilimanjaro. Mwalimu kwa jeuri yake na kujiamini alikokuwa nako asingeweza kuandikiwa hotuba na mtu kama Abdu ambaye hata elimu yake Mzee Mohamed Said haiongelei sana zaidi ya kumsifia kuwa alikuwa na akili sana! Hotuba hii ninayoinukuu hapa chini aliitoa mwaka 1995 kwenye Mkutano Mkuu wa CCM ambao hatimaye ulimteua Mkapa kuwa mgombea Urais kwa tiketi ya CCM. Hakuwa ameiandika popote:
"Ukabila bado upo. Kwa hiyo, ukabila lazima uendelee kupigwa vita. Hapana kukaa na kusema "Tanzania hatuna ukabila". Hapana. Watu hatujawa Watanzania bado. Kwa hiyo, lazima tuendelee kuupiga vita. Na watu wana udini dini. Kuna watu kabisa wanatamani nchi hii iwe ya Kikristu, wajinga. Kuna watu wanatamani nchi iwe ya Kiislamu, wajinga. Natumia neno zuri wajinga, sisemi wapumbavu. Wajinga.
Tunataka rais wetu, akiwa Mkristu, ajue hatumchagui kwa sababu ya Ukristo wake. Akiwa Muislam, ajue hatukumchagua kwa sababu ya Uislam wake. Hatumchagui awe rais wa Wakristu wala awe wa Waislam, na tunataka hilo alikubali kwa dhati na alisimamie na ndiye kiongozi wetu. Alisimamie kwa dhati bila woga, ndiye kiongozi wetu.Katika nchi changa namna hii, ambayo watu haraka sana hukimbilia ukabila, haraka sana hukimbilia udini, tunataka kiongozi awe imara kabisa katika mambo haya." Niishie hapo kunukuu na ni mshukuru MSOMAJI RAIA wa Raia Mwema ya leo.
Ajabu sana..!Mohamed Said kaja na kitabu, wewe umekuja na shutuma, wewe ndio ulitakiwa ulete ushahidi wa tuhuma zako, umeshasahau hii mada imeanzishwa na nani na kwa nini?