Wanajamvi,
Habari ambazo nimezipata kutoka chini ya kapeti(sina uhakikanazo sana) Mzee Mohamed Saidi ni muakilishi wa kikundi cha kigaidi cha Al-shabab hapa nchini kwa kufadhiliwa na serikali ya Irani. Inasemekana makutano na mipango yao yote huwa
inafanyika Zanzibar kwenye makazi ya kiongozi mmoja wa Uamusho....serikali inafatilia.
BD,
Sikutaka kukujibu lakini kwa hili nitakujibu kukuondoa wasiwasi.
Wala hizo taarifa hazihitaji kuwa za chini ya kapeti.
Zanzibar nakwenda sana.
Nikifika Zanzibar lazima kwanza nikamsabahi Sheikh Mselem bin Ali,
Sheikh Farid na wote masheikh vijana.
Uamsho wananifahamu vizuri sana na ninatafakhari kujuana na watu
kama hawa.
Sisi malezi yetu tumefunzwa kufanya usuhuba na watu wema.
Na hakika hawa ni watu wema sana kwangu.
Hakika nikifika Zanzibar kila mtu anataka kukutana na mimi na katika
mialiko hii ya chai, chakula huwa tunazungumza mengi sana kuhusu
dini yetu.
Huwa siishii katika Uislam.
Napata mialiko mingi kutoka kwa wanasiasa huwa wana hamu ya ''kupigizana''
kelele na mimi.
Huenda hili hulijui lakini mimi ni mzungumzaji mzuri sana tena wa kuvutia hisia.
Ukikutana na mimi mara moja tu.
Tutaunga urafiki wa maisha.
Na ninao marafiki wa namna hii dunia nzima.
Turudi Zenj.
Hakika Zanzibar ni nyumbani kabisa.
Unajua mimi nilikuwa mtafiti msaidizi katika kile kitabu maarufu kuhusu historia
ya mapinduzi ya Zanzibar - ''Kwaheri Ukoloni Kwaheri Uhuru...'' cha Dk Ghassany.
Kwa hiyo ushajua ushawishi wangu kwa Wazanzibari.
Kuhusu Iran nimealikwa Iran na Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje na tulikuwa ujumbe
mkubwa tu kutoka Tanzania pamoja na maofisa wa serikali na watu wa magazeti na TV.
Hilo na Al Shaabab wala sitalizungumza hilo nakuachia wewe...
Hizi anga ni zako na Mwanakijiji mie siingii humo nachelea kuwa kichekesho.