Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

mzee Ms,

Kwanini sasa kwenye kitabu chako usiweke mambo sawa?
Kwani asilimia kubwa iwe misikitini uswahilini wanajuwa mwl kafundishwa kuvaa salawili na wazee wako. Na wewe unaandika hiyo historia inamaana hujawahi kusikia? kwanini usiliweke hili jambo kwenye maandishi yako?

Mgashi,

Usisikize maneno yasiyo na maana.

Kitabu unapoandika ni kuwa wewe
unachukuliwa ni mtu wa maana.

Ikiwa maudhui yako ni matusi na kashfa...
Hata ''publishers'' watakukwepa.

Ningeliandika upuuzi leo tusingekuwa hapa
JF tunajadili.

Nadhani umefahamu.
 
Mohamed Said "mtoto wa magorofani"kama unavyojiita,ukisoma Dandy na Beano -umeshaulizwa humu wewe vikwazo hivi vya elimu ulivipita vipi-ulipenya vipi katika "mfumo kristo".Elimu ufuata damu-yaonekana wewe ulikuwa expectation to the rule-tujuze tukate kiu
 
Last edited by a moderator:
Mohamed Said "mtoto wa magorofani"kama unavyojiita,ukisoma Dandy na Beano -umeshaulizwa humu wewe vikwazo hivi vya elimu ulivipita vipi-ulipenya vipi katika "mfumo kristo".Elimu ufuata damu-yaonekana wewe ulikuwa expectation to the rule-tujuze tukate kiu

Son...

Iko siku nitakueleza ngoja kwanza tumalize haya yaliyoko mezani.

Kuna movie ya John Wayne ''North to Alaska'' ilikuja Empire Cinema
enzi hizo za 1960s na ipo nyimbo yake kaimba somebody Haton?

Sina uhakika na jina ni miaka mingi.
 
Son...

Iko siku nitakueleza ngoja kwanza tumalize haya yaliyoko mezani.

Kuna movie ya John Wayne ''North to Alaska'' ilikuja Empire Cinema
enzi hizo za 1960s na ipo nyimbo yake kaimba somebody Haton?

Sina uhakika na jina ni miaka mingi.

hiyo empire ndio drive in
 
hiyo empire ndio drive in

Son...

Mtaa wa Azikiwe kwenye kona na Jamhuri baada ya bank nyumba ya pili kama unaelekea
picha ya Bismini (Askari Monument) pale ndipo ilipokuwa Empire Cinema.

I have many fond memories of the place...
1964... siku ya Eid Fitr ndiyo kwa mara ya kwanza niliona movie ''Blue Hawaii'' ya Elvis Presley.

Siku ya pili asubuhi nakunywa cha na baba yangu nikamueleza habari za Elvis.

Yeye akanambia alipokuwa mdogo alikuwa anatazama movie za Bing Crosby na Abdu Sykes na
mdogo wake Abbas pale Avalon Cinema.
 
G,

Amani itasimama na kudumu katka jamii ambayo haki
inathaminiwa.

Hapana mabwana na watwana.
Hapana dhulma.

Hiki ndiyo sote tunachokililia.
Hebu basi tuangalie wafaidika wa keki ya taifa kwa ufupi,
Kikwete na familia yake na jamaa zake lowasa na familia yake na jamaa zake hivyo hivyo kwa wengineo kama sita, membe, mwinyi, mwandosya, magufuli mpaka wasio na dini kama kingunge nk.
Hawa ndo wala keki ya taifa ni kama asilimia 10 tu ya wtz wote.
Sasa mzee kwanini usiziandame familia za hawa watu kuliko kupandikiza chuki kwa wtz wote?
kwanini kuwaaminisha waslam wanaonewa wakati shida ipo kwa wtz wote? Kama we ni jasili pambana na limia 10 ya hao nilokutajia kama utasubutu wakati kikwete ndo mfadhili wenu.
Bisha kikwete hakuwafadhili kina ilunga kwenda tz nzima wakimtukana baba wa taifa na cdm na maaakofu.
 
...........Jaffari alikumbushwa na wale waliomlisha yamini kuwafikiria Waafrika milioni tisa nchini Tanganyika waliokuwa wanamtegemea Nyerere kama mkombozi wao..........
haya ni maneno yako MS.
 
Son...

Mtaa wa Azikiwe kwenye kona na Jamhuri baada ya bank nyumba ya pili kama unaelekea
picha ya Bismini (Askari Monument) pale ndipo ilipokuwa Empire Cinema.

I have many fond memories of the place...
1964... siku ya Eid Fitr ndiyo kwa mara ya kwanza niliona movie ''Blue Hawaii'' ya Elvis Presley.

Siku ya pili asubuhi nakunywa cha na baba yangu nikamueleza habari za Elvis.

Yeye akanambia alipokuwa mdogo alikuwa anatazama movie za Bing Crosby na Abdu Sykes na
mdogo wake Abbas pale Avalon Cinema.

Mohamed Said,

Umenikumbusha mbali Impire Cinema nakumbuka Movie moja inaitwa Midninight Express nimeiona pale.
 
Mohamed Said,

Umenikumbusha mbali Impire Cinema nakumbuka Movie moja inaitwa Midninight Express nimeiona pale.

Ritz,

Kile kisa ni cha kweli kilitokea Uturuki yule kijana walimkamata na bangi
akafungwa.

Ni movie nzuri sana.
Ninayo katika archive yangu.

Mimi ni mpenzi wa movie.
 
Muulize mzee wako Mohamed Said maana yeye ndie mnae muamini zaidi kwa kuwa ni mmanyema mwenye tambo na muislam safi anayeweza kujenga miskiti kila anakokwenda.

Punguza munkali Uislam wa Mohamed Said unakusumbua sana wewe mbona ATHEIST watu hawakusumbui.

Tunategemea mengi kutoka kwako kutupasha habari za wapigania uhuru.
 
haya ni maneno yako MS.

Z,

Hayo ni maneno ya Bilal Rehani Waikela.

Kisa cha Tabora na Kura Tatu wazee wa Tabora niliwafanyia
mahojiano kama jopo.

Walikuwapo Bilal Waikela, Mohamed Mangiringiri, Abdallah Kassongo,
Ramadhani Singo na wengine wengi.

Kikao kilikuwa nyumbani kwa Waikela Gongoni.

Huyu Waikela ndiye aliyemsomea Nyerere hotuba mashuhuri ''Moto wa
Waislam Ukiwaka'' katika sakata la kwanza la EAMWS kwenye mkutano
uliofanyika Dar es Salaam 1963.
 
Z,

Hayo ni maneno ya Bilal Rehani Waikela.

Kisa cha Tabora na Kura Tatu wazee wa Tabora niliwafanyia
mahojiano kama jopo.

Walikuwapo Bilal Waikela, Mohamed Mangiringiri, Abdallah Kassongo,
Ramadhani Singo na wengine wengi.

Kikao kilikuwa nyumbani kwa Waikela Gongoni.

Huyu Waikela ndiye aliyemsomea Nyerere hotuba mashuhuri ''Moto wa
Waislam Ukiwaka'' katika sakata la kwanza la EAMWS kwenye mkutano
uliofanyika Dar es Salaam 1963.
mkuu hiyo risala aliyosomewa Nyerere inapatikana?
pia naomba kama una katiba ya EAMWS utuwekee jamvini.
 
Ritz,

Kile kisa ni cha kweli kilitokea Uturuki yule kijana walimkamata na bangi
akafungwa.

Ni movie nzuri sana.
Ninayo katika archive yangu.

Mimi ni mpenzi wa movie.

Nasikia hiyo movie ndiyo ilisababisha mpaka Amnest International kuishitaki Uturuki jumuiya ya Ulaya jela zao zimejaa mateso mpaka wakapunguza mateso miaka 1976.
 
Punguza munkali Uislam wa Mohamed Said unakusumbua sana wewe mbona ATHEIST watu hawakusumbui.

Tunategemea mengi kutoka kwako kutupasha habari za wapigania uhuru.
Aaa Ritz, uislam wa Mohamed utanisumbuaje mie? kinachonisumbua mimi ni tabia ya Mohamed Kutumia uislam kwa maslahi binafsi, kuchochea chuki na kuhatarisha amani yetu. Wewe na mimi tunatakiwa kuungana kukemea tabia hii mbaya bila kujali imani zetu. Machafuko yakitokea Mohamed anapakukimbili, bila shaka hata wewe, zomba, Dullah, Boko Haram et al mnaweza mkawa na pakukimbilia yaani kwa wafadhili wenu. Mimi nitakimbilia wapi?
 
Hebu basi tuangalie wafaidika wa keki ya taifa kwa ufupi,
Kikwete na familia yake na jamaa zake lowasa na familia yake na jamaa zake hivyo hivyo kwa wengineo kama sita, membe, mwinyi, mwandosya, magufuli mpaka wasio na dini kama kingunge nk.
Hawa ndo wala keki ya taifa ni kama asilimia 10 tu ya wtz wote.
Sasa mzee kwanini usiziandame familia za hawa watu kuliko kupandikiza chuki kwa wtz wote?
kwanini kuwaaminisha waslam wanaonewa wakati shida ipo kwa wtz wote? Kama we ni jasili pambana na limia 10 ya hao nilokutajia kama utasubutu wakati kikwete ndo mfadhili wenu.
Bisha kikwete hakuwafadhili kina ilunga kwenda tz nzima wakimtukana baba wa taifa na cdm na maaakofu.

Mgashi,
Niwekee hapa kile unachokiona ni kupandikiza chuki.
 
Aaa Ritz, uislam wa Mohamed utanisumbuaje mie? kinachonisumbua mimi ni tabia ya Mohamed Kutumia uislam kwa maslahi binafsi, kuchochea chuki na kuhatarisha amani yetu. Wewe na mimi tunatakiwa kuungana kukemea tabia hii mbaya bila kujali imani zetu. Machafuko yakitokea Mohamed anapakukimbili, bila shaka hata wewe, zomba, Dullah, Boko Haram et al mnaweza mkawa na pakukimbilia yaani kwa wafadhili wenu. Mimi nitakimbilia wapi?

Gwalihenzi,

Sisi hatujapata kuwa na mfadhili.
Chunguza utamuona nani ana wafadhili.

Unajua kuwa kila mfadhili aliyejaribu kuwasaidia
Waislam wa Tanzania alifurushwa?

Tuanze na Chuo Kikuu Cha EAMWS kilichotaka kujengwa
mwaka 1968.

Unamjua aliyekihujumu?

Miaka ya 1980 OIC ilitaka kujenga Chuo Kikuu Tanzania
serikali ikakataa kutoa kibali.

Chuo hicho kikajengwa Mbale Uganda.

Darul Iman walitaka kujenga chuo cha ufundi Kibaha na ardhi
wakanunua na fidia kulipwa.

Ikaja kampeni ya magazeti maarufu tuliipa jina ''Waarabu Wapora
Ardhi.''

Darul Iman wakakunja virago wakaondoka na fedha zao.

Ukitaka mifano zaidi Insha Allah nitakupatia.

Maslahi yangu binafsi ni yapi hayo?
Nifahamishe.
 
Aaa Ritz, uislam wa Mohamed utanisumbuaje mie? kinachonisumbua mimi ni tabia ya Mohamed Kutumia uislam kwa maslahi binafsi, kuchochea chuki na kuhatarisha amani yetu. Wewe na mimi tunatakiwa kuungana kukemea tabia hii mbaya bila kujali imani zetu. Machafuko yakitokea Mohamed anapakukimbili, bila shaka hata wewe, zomba, Dullah, Boko Haram et al mnaweza mkawa na pakukimbilia yaani kwa wafadhili wenu. Mimi nitakimbilia wapi?

Sisi wauza kahawa hatuna wafadhili tungekuwa na wafadhili tusingeuza kahawa.
 
Tumekuomba uweke historia umesema huna. Bado unaendelea kuumanisha ulimwengu kuwa ilikuwa maarufu hata pale usipo na ushahidi.

Nguruvi,

Nimekuambia hapakuwa na hiyo hotuba katika karatasi.
Waikela alinieleza nini alisema katika hiyo hotuba.

Ndugu yangu hebu tuache hivi vitu vidogo vidogo mie
napenda kukupa majibu lakini kwa staili hii itafika nitakuwa
nakusoma napita.

Na hii habari ya kutaka ushahidi nishakueleza kwani mimi na
wewe tuko mahakamani kuwa nikupe ushahidi?

Nishasema mimi siko hapa kushinda hoja niko hapa kuwapa
hawa wasikizaji 80, 000 ambao hawajapatapo kusikia historia
hii.

Kwangu wewe ni njia tu ya kuwafikia hao wasikilizaji wangu.
 
Sisi wauza kahawa hatuna wafadhili tungekuwa na wafadhili tusingeuza kahawa.
Tupo pamoja jamaa yangu, tuungane mkono kuwakataa watu kama Mohamed Saidi wanaohatarisha umoja wetu kama taifa na kutishia amani yetu.
 
Back
Top Bottom