Mag3,
Jibu langu lipo katika historia yetu kuanzia tunapigania uhuru hadi ulipopatikana.
Baada ya uhuru ndipo matatizo yakaanza kwa kubwa kuvunja EAMWS wakati ilipokuwa
inatayarisha mipango ya kujivua na dhulma zilizosababishwa na ukoloni.
Kuanzia hapa Waislam hawakuruhusiwa kujioganaizi nje ya BAKWATA na serikali ikahakikisha
maisha BAKWATA itaendeshwa na vibaraka na watu wajinga.
Wakati haya yakiendelea taasisi za Kikristo TEC na CCT ziko huru zikitekeleza mipango ya
maendeleo kama kujenga shule na hospitali.
Kwa upande wa Waislam kila aina ya msaada ulotoka nje kujaribu kuwasaidia Waislam
ulihujumiwa.
Mfano Chuo Cha Kikuu Cha Kiislam kilichotaka kujengwa Tanzania na OIC serikali ilikataa
kutoa kibali chuo kikajengwa Mbale Uganda, Darul Iman ilitaka kujenga chuo cha ufundi
Kibaha wakapigwa vita wakaondoka na kuacha ardhi ambayo tayari walishanunua.
Hii ni mifano michache.
Wakati haya yakiendelea Wakristo wanaendeleza yale yale walokuwa wakifaidi wakati wa
ukoloni.
Hili si swali la kuwa na Waislam 10 katika nafasi ndiyo ikawa wakunyooshewa kidole kuwa
Waislam wana nafasi.
Angalia watendaji katika nafasi zote katika mashirika ya umma na serikali yenyewe na vyuo
vikuu na kwengineko nani wamehodhi fursa zote.
Lakini kubwa la kusikitisha hii leo badala ya serikali juu ya kupelekewa taarifa za dhulma na
Waislam serikali iko kimya na wanaotoa maswali na kutaka maelezo kutoka kwa Waislam ni
Mag3 na mfano kama wake.
Mohamed nichangie katika kundi la ''mfano kama wa Mag3'' ha ha ha.
Kwanza kabisa hujajibu maswali muhimu sana yaliyoulizwa.
Katika maswali hayo umeulizwa, kwa vile wakuu wa taasisi na vitengo muhimu kama usalama wa taifa, Polisi, Mahakama na taasisi ya Urais ni waislam, ni vipi basi mfumokristo unaweza kuwa bado unafanya kazi?
Pili, unaposema watendaji ni wakristo na hapa nisema umeshafuta dai la uongozi, je ni kwanini basi viongozi wakuu na wenye uwezo wa kuvunja mfumo huo wameshindwa? Kama Inspekta wa Polisi ni sehemu ya mfumo kristo kwanini IGP ashindwe kumwadabisha katika njia ya haki.
Tatu, Umesema nafasi katika vyuo vikuu zimehodhiwa na mfumokristo, swali ni kuwa ili mtu awe profesa au mhadhiri, je anateuliwa au inatokana na academic qualification zake.
Na vipi basi katika mfumo huo kandamizi tumeweza kupata watu kama Shivji, Haroub(mwenyezi amrehem), Bushir Ally, Profesa Safari, profesa Lipumba n.k. ambao ung'aro wao umevuka mipaka na kuingia anga za kimataifa?
Nne, Umesema TEC CCT wamekuwa na mipango ya kujenga shule na Hospitali. Hebu tuanzie hapa katika Hospitali.
Ni taasisi gani ya kiislam ilitaka kujenga Hospitali na kukataliwa na sababu zilikuwa zipi za kukataliwa.
Tano, kwa vile Chuo kikuu cha kiislam kilikataliwa na badala yake kikahamishiwa mbale,hivi ujenzi wa Chuo kikuu ulikataliwa na serikali iliyoongozwa na nani na kwasababu zipi.
Sita, Darul Islam walitaka kujenga chuo cha ufundi Kibaha, ni vita gani walipigwa ili nasi tuyaone maonevu hayo?
Na je wale waliojenga shule ''WHIPAS'' ya watoto wa kike wa kiislam pale kibaha iliponaje na choko choko na dhulma hiyo iliyofanyiwa Darul Islam.
Saba, Je, ni wanafunzi wangapi wa kiislam wanaodhamiwa na taasisi za kiislam kwenda kusoma Mbale?
Nane,ili kutoa fursa sawa kwa wote ungeshauri mfumo gani utumike katika ajira.
Tisa, na kuzingatia 8 hapo juu na ujio wa soko huria hilo litawezekanaje na kwa utaratibu gani.
Kumi, nafasi za masomo kwa waislam katika nchi za kiislam kama Turkey na kwingineko zinatolewa kwa utaratibu gani?
Je utaratibu huo unakubaliwa na waislam na kwamba ni wa haki zaidi ya huu wa mfumokristo?
Ni vijana wangapi waliopewa scholarship ambao wamerejea na kuendeleza jamii yao.