ntamaholo
JF-Expert Member
- Aug 30, 2011
- 12,938
- 6,942
Na zaidi ya hapo, kuandika maandishi ikiwa ni pamoja na takwimu ambazo leo tunajua hazina ukweli huku ukiwaaminisha watu kwa miaka 15 si bahati mbaya ni makusudi.
Siamini katika vyuo ulivyotoa mihadhara na wasomi uliokutana nao hakuna hata mmoja aliyewahi kukueleza kuhusu mapungufu ya takwimu za utafiti wako. Bahati mbaya inaweza kuwa miezi au mwaka siyo miaka 15.
Lakini pia Mohamed anasababu! mathalan kumsema Kawawa kama makamu wa kwanza wa rais ilikuwa kutia uzito wa hoja zake. Pengine angekuwa hakukusdia angelieweza kurudi maktaba na kujiridhirisha kuwa hicho alichokiandika au kusudia kukisema kina ukweli.
Kuwaambia watu kwa miaka 15 kwamba Nyerere alifundishwa siasa na Sykes huku ukijua kuwa alikuwa msomi na alianza harakati hizo siku nyingi si bahati mbaya ni makusudi ili kufikia lengo.
orodha ni ndefu but the bottom line is, Mohamed anachokifanya ni makusudi wala si mapungufu.
Huwezi kuniambia amejua leo kuwa Maryknoll walitoa ticket au Nyerere alikuwa katibu wa AA Tabora kabla ya kukutana na Sykes! no! ni makusudi ambayo leo anakiri ni mapungufu ya kibinadamu. No thank you Sir!
anachonikera ni pale anasema anaaandika kuhusu historia, halafu anakuja anasema ni mawazo yake. Hivi ni lini historia ya mtu au kitu iliwahi kuelezwa kwa hisia na mawazo ya mtu? nini maana ya historia? si kuandika au kuelezea kile kilichotokea? iweje yeye aandike hisia na mawazo yake tu?