Sawa, lakini hayo ni maoni ya aina moja tu; mtu mwingine anaweza (kwa kuangalia facts zile zile) kufikia hitimisho tofauti na kumwasha msomaji aamue mwenyewe. Sasa kujibu hoja zako nyekundu wacha na miye nikupatie toka Wikipedia huko huko:
Lakini tunaweza kwenda mbali zaidi kutoka huko huko Wikipedia:
Kumbe utaona kuwa 'territory' ya Holy See ambayo yenyewe ndio sovereign ni Vatican City State. Lakini hata bila ya kuwa na territory imewahi kuendelea kuwa sovereign!
Swali la jumbe kwa namna limekosewa; kama ana maanisha kuwa ni kwanini tuna Uhusiano wa Kibalozi na Holy See jibu liko wazi - tuna mahusiano na serikali ya Kipapa ambaye ni mkuu wa Vatican City. Serikali hii ndiyo Holy See.
Jibu lako ni partially true; kuna mahusiano ya karibu kati ya Holy See na nchi hizo zote ukiondoa kuweka mahusiano rasmi ya kibalozi. Hili si jambo geni; nchi kutokuwa na mahusiano ya kibalozi haina maana haiitambui ile nchi nyingine kuwa ni nchi au kuwa hakuna mahusiano mengine ya karibu chini kidogo ya yale ya Ubalozi. Marekani haina balozi Cuba wala Cuba haina balozi Marekani lakini nchi hizo hazina mahusiano? Well..
Angalia na hapa:
Utaona ni nchi tano tu duniani ambazo hazina KABISA mahusiano yoyote (katika level yoyote) na Holy See - hizi ni Bhutan (sidhani kama wana ubalozi Tanzania au sisi kwao), Maldives, North Korea, China na nchi ambazo hazijatambulika Rasmi (kama Somaliland n.k)
Sasa, nchi zaidi ya 180 zina mahusiano ya kibalozi na Tanzania nii mojawapo. Hawa wote wametambua na wanatambua nafasi ya Holy See licha ya maswali ambayo unayo na ambayo labda wengine walishauliza. Nchi hizi zote hazijakosea. Tanzania haijakosea. Na nchi hizi zote haina maana zimebadilisha dini zao (Saudi Arabia bado ni ya Kiislamu, Malaysia bado ni ya Waislamu, Falme za Kiarabu bado ni nchi ya Kiislamu, Bahrain bado ni nchi ya Kiislamu, Misri bado ni nchi ya Waislamu wengi, Kuwait bado ni nchi ya Kiislamu hujasikia wameanza kusali Rozali!; Pakistan bado ni nchi ya Waislamu wengi hujasikia watu wanaandamana ati Pakistan sasa imegeuzwa nchi ya Wakatoliki!
Kuendelea na hoja yako hii jinsi ilivyo kunaonesha ni kutokutaka kujua au kukubali ukweli hata kama unakutumbulia macho. Nchi 180 (za Kikristu, Kiislamu, Sekula, Orthodox n.k) zimetambua Holy See kama entity ambayo ni nzuri kuwa nayo na mahusiano ya Kibalozi. Nchi 80 kati ya hizo zina mabalozi wa kudumu Vatican! Vatican yenyewe ina mabalozi zaidi ya 100 kwenye nchi hizo. Sasa, kusema ati kwa vile tuna Uhusiano wa kibalozi na Vatican (Holy See) basi Tanzania imekuwa nchi ya Kikristu ni kutokujua, kutokupenda kujua na kuwa mgumu kujua.
Sasa unaweza usipende hili kwa sababu Holy See inawakilisha Kanisa Katoliki (serikali ya Kanisa Katoliki chini ya Papa) na hili linakukwaza lakini wewe kukukwaza haina maana halipo. Mwenyewe umeona mabadiliko ya Papa tu dunia nzima inapeleka waandishi zaidi ya 5000 kufuatilia; it is not about the church my friend, it is about history of Western Civilization. Nchi hizi za Magharibi nyingi zimechota katika elimu, tamaduni n.k kutoka kwa Kanisa Katoliki. Utambue kuwa Kanisa Katoliki limekuwa ni sehemu ya utawala wa nchi za Magharibi kwa karibu miaka 1000.
Sasa una haki ya kuchukia uwepo wa Ubalozi wa Holy See na kile inachosimamia; unaweza kabisa kuona huu ni upendeleo lakini hili peke yake halibadili ukweli kuwa uongo. Kuendelea kubishania hili ni kujaribu kupigana na ukuta wa historia. Na wakismama watu kama wewe kuzungumza kwa mamlaka ya kisomi ati hawatambui Holy See au sovereignty ya Vatican City watatuabisha sisi wengine.