Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar


Mzee Saidi mwalimu unayetusomesha hapa unaonaje tumalize kwanza ule mjadala wa sensa 1957/ 1967?
 
Soma hiyo hotuba ya maandishi ya rangi ya bluu, ukiiamini hiyo hutahitaji video tena.

Hiyo hotuba ya maandishi kaileta JokaKuu na sisi tukakuambia kuna sehemu imechakachuliwa wewe mwenyewe ndiyo ukaja na ahadi kuwa utaenda TBC kuichukua uiweke humu leo miezi 4.

Ulisema inauzwa watu tukajitolea kuinunua tukakuambia sema kiasi gani kimya mpaka leo.

Mwenzako naye Son, alisema ndani ya masaa 24 hotuba itakuwa humu leo miezi 4.

Leo tena unakuja na habari zingine hutaki tena hotuba ya TBC.
 
Hiyo hotuba imekuwa bidhaa adimu? au Yericko bado yuko njiani kufuatilia TBC? hata na RITZ alishajitolea kulipia gharama ili Yericko akaichukue lakini kaishia mitini!

Kadogoo,
Suala halikuwa kutajwa Abdu katika hotuba ya muago wa Nyerere pale Ukumbi
wa Diamond.

Suala ni kuwa Nyerere alisema hakumbuki Abdu alikuwa na cheo gani katika TAA.

Kwangu mimi wala hili halinishughulishi.
 

Ritz,
Wahurumie hawa ndugu zetu.
 

Mzee Saidi mwalimu unayetusomesha hapa unaonaje tumalize kwanza ule mjadala wa sensa 1957/ 1967?

Nyambala,
Elimu yangu mie si ya kufanya ubishi na watu.

Naeleza kitu kile ninachokijua na ikiwa atakuja mwingine na taarifa kinyume na ya
kwangu hapana ugomvi wala sitalazimisha kuwa taarifa yangu ndiyo yenyewe, la hasha.

Ubaya wa ubishi ni kuwa unapoteza muda.
Wewe uko hapo hapo lakini angali mie nishatoa darsa ngapi na kuhusu mangapi.

Mengi katika hayo wasikizaji hawakupata kuyasikia popote.
Leo watazamaji wamefika 130,000 and counting...

Basi nibaki na sensa, sensa, sensa, sensa...
Sahani ya santuri imekwama kwenye gramafoni.

Tija iko wapi?
 
Na ndiye huyo huyo anayesemwa alikuwa na uzoefu wa siasa kuliko ''debate'' za shule za Nyerere! please Mo
 

Ooh C'moon Mzee Saidi, this is too low of you. Is this a new normal? Leo hili unaliona halina maana kwa sababu unafahamu litachambuliwa nje ndani? Nani aliyeanzisha hizi mada za sensa? Sasa ulitaka utuhumu na kuongopa mambo yaachwe tu hewani hewani? Not here Mzee Saidi.

I tell you what tatizo ni kuwa wewe uliamini kabisa kuwa haya masuala ni wewe tu unayeyafahamu na umeshazungumza hivyo mara kadhaa. It's the first tyme I can see unaanza ku-tread carefully and safely. It's good though kwa ustawi wa mjadala unaondelea. Sasa unaweza kukiri hadharani mbele ya wanajukwaa kwamba hadithi ulizokuwa ukizisimulia kuhusu sensa ya 1957 na 1967 ni za uongo?

Mzee Saidi mimi sipo hapa kwa ubishi, kazi yangu moja tu kuweka records straight kwa yale nnayoyafahamu ndiyo maana hata lile la uandishi bayografia ya Nyerere kuwa ilitokana na kitabu chako nikajitokeza na kuweka records straight kwamba ulichokuwa ukikisema ni uongo, the same kuhusu kuwa na kitabu ndani ya library of congress, the same kuhusu eti Darul Iman walikatazwa kujenga chuo cha ufundi Kibaha, The same kuhusu Sokoine, the same kuhusu historia kamili ya wapi uhuru wa Tanganyika ulijadiliwa kwa mara ya kwanza, the same kuhusu hili la sensa na mengine mengi yaliyowekwa na wajumbe wengine. The list is endless. I will always be gone lakini likiwekwa jambo lisilo kweli nalolifahamu ntajitokeza.
 
Wakati mwingine uwa nacheka sana watu wanatumia mabandiko ya John Iliffe kama ushahidi wakati John Illife miaka ya mwishoni ya 1960 akiwa idara ya historia ya chuo kikuu cha Dar es Salaam, aliweza kukusanya habari nyingi sana na muhimu kutoka kwa mmoja wa wanafunzi wake mtoto wa Abdulwahid Sykes, Daisy Sykes.

Binti huyu alimfahamisha John Iliffe kuwa habari alizokuwa akiandika katika semina kuhusu historia ya Tanganyika alikuwa akizipata kwa baba yake.

John Illife alichota sana Ilm kutoka kwa mtoto wa Abdulwahid Sykes na kumshauri aandike historia ya maisha ya babu yake Kleist Sykes.

Leo hii Mohamed Said anatoa Ilm bure kabisa kupitia JF.

Lakini kuwa watu wanapinga na kusema hizo habari za Gerezani kwa wanywa gahawa washinda vibarazani lakini John Illiffe akija na habari za Wazee wa kariakoo hakuna tatizo. Msomeni John Iliffe kwenye kitabu chake "A Modern History of Tanganyika."
 
Mohamed, kaa kitako na pata funda la maji. Mnyambala ana point muhimu sana.
Hapa hatuangalii quantity tunaangalia quality. Pengine ni jambo linalokushtua maana hukuzoea kupata hoja mbadala.

Suala la sensa ni muhimu sana kwasababu umekuwa ukilitumia katika harakati zako kama silaha ya uonevu.
Hapa tupo kuweka mambo sawa tofauti na kule ulikozoea kupita ukipewa credit hata za uzushi.

Kwa watu wenye akili suala la sensa ni muhimu sana vinginevyo ufute madai yako na ukubali upotoshaji.
Zimewekwa data hapa tukatoa nafasi nawe utupe zako, hukuweza unatupa zile ulizojifingua chumbani na mshauri wako mkaamua kutuletea.

Hapa si mahali pa kutupa namba tu! Mohamed Said Suala la sensa ya mwaka 1957 na 1967 unasemaje baada ya zana kuwekwa hadharani?

Hakuna kukimbia kwa maneno ya kijanja janja halafu baada ya wiki unarudi na namba zile zile zializothibitishwa kuwa hovyo! we want to set the record clear.

Hoja ya sensa ipo mikononi mwako sasa, upande mwingine umeleta zao.
 

Mzee Saidi kwa taarifa yako mimi si mwanahistoria wala mwanasiasa mimi ni mtaalamu wa uhandisi migodi nnayepractice in the first world arena and that is my area. Kama unataka tucheze huko kwenye timu yako tujaribu na huku kwangu. I am ready any time sir.
 
Kadogoo,
Suala halikuwa kutajwa Abdu katika hotuba ya muago wa Nyerere pale Ukumbi
wa Diamond.

Suala ni kuwa Nyerere alisema hakumbuki Abdu alikuwa na cheo gani katika TAA.

Kwangu mimi wala hili halinishughulishi.
Ndio maana tulisema wapi ushahidi? Wewe ulimnukuu akisema, kuna wengine hawakusikia sasa prove kwao kuwa ndivyo ilivyokuwa. Kama ulisikia una proof tatizo ni nini?
Unataka video! ulipomnukuu Nyerere ulikuwa na mkanda wa video na kama hukuwa nao unahitaji wa nini.

Jokakuu kaweka hotuba! kanusha kuwa si kweli
 
Geeky,
Huyo jamaa anaropoka hajui maingiliano ya watu wa Dar es Salaam.

Angelikuwa ananijua mimi vizuri hata asingesema hayo.
Wala sina haja ya kusema mengi katika hilo.

Yeye anamjua Rupia leo.
Wazee wetu wamekuwa na maingiliano ya miaka.
Kadogoo rafiki yangu, ebu njoo uone matumizi ya neno hili "anaropoka" lilivyotumika na mzee wako Mohamed. Hivi mtu anayeropoka huitwa nani? Sisi kule kwetu mtu huyo huitwa mropokaji. Hivi mimi Gwalihenzi nikisema mzee wenu Mohamedi Said amekuwa akiropoka na kwahiyo ni MROPOKAJI nitakuwa nimemtukana?
 

Hiyo hotuba ya maandishi siku ilipowekwa tu mimi nilisema kuna sehemu imechakachuliwa kilichoandikwa na tulichokisikia RTD ni vitu viwili tofauti.
 
Sio kweli,

John Iliffe katika utafiti wake na uandishi wa historia ya Tanganyika hakumtumia Daisy Syke kama rejea kuu bali alimtumia kama kiambata tu tena cha 0.001 ya taratibu za utafiti wa kihistoria.

Yasome mandishi ya Historia ya Tanganyika ya mwanazuoni huyu Mr J. Iliffe na kisha rejea kwenye vielelezo vyake utaona Daisy Sykes sio alama kuu ya maandishi yake.
 
Ndicho wengi tunachokitaka akifanye hapa,

Aikanushe au aikubali hutuba hiyo yamaandishi
 
Hiyo hotuba ya maandishi siku ilipowekwa tu mimi nilisema kuna sehemu imechakachuliwa kilichoandikwa na tulichokisikia RTD ni vitu viwili tofauti.

Kilete hapa hicho mlichokisikia nyinyi RTD ili nasi tujiridhishe,

Sisi tumeshaweka hotuba hiyo katika maandishi, sasa ni jukumu lenu kuleta hotuba mbadala mnayodai mliisikiliza RTD ambayo ni tofauti na hii,
 

Umesema vyema...

Ila hapo mwisho, Yeye akisema Yesu ni Mungu, wewe ukimwambia Yesu si Mungu, utakuwa umeamua kutokuwa mvumilivu kama ulivyosema. Kwasababu mtaanzisha mabishano ambayo mwisho wake hamuujui.

Ila ukiamini moyoni kuws Yesu si Mungu, ni Mtume tu, na Mohammed (S.W) ndo Mtume wa Mwisho. Na ukaendelea na shughuli zako, now that is uvumilivu na kuheshimu imani ya Mtu.
 

Wapi nimekuambia Iliffe alimtumia Daisy Sykes kama rejea. Nimeandika kuwa John Iliffe aliweza kukusanya habari nyingi sana na muhimu kutoka kwa mmoja wa wanafunzi wake. Unabisha bila kujua "The Townsman Kleist Sykes" ipo kwenye kitabu gani.

Wewe unabisha ili hujue au unabisha kubisha tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…