Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Nguruvi,
Tujadili mambo yetu.

WML hawapo tz na huyo Rukara halikadhalika.

Mohamed, tunachotaka kujua ni namna WML ilivyofanya shughuli zake katika nchi ya mfumo kristu.

Hata kama WML na Rukara hawapo sasa lakini hatuzuiwi kuangazia uwepo wao nchini na utendaji kazi zao Katika nji ya mfumo kristu, tena unathibitisha kabisa kuwa serikali (yamfumo kristu) ilitoa baraka zake
 

Dr. Sivalon anaseme hali ilivyo ni kuwa hujui ikiwa hili la kanisa au la serikali.
 
Nguruvi,
Tujadili mambo yetu.

WML hawapo tz na huyo Rukara halikadhalika.

Mohamed, tunachotaka kujua ni namna WML ilivyofanya shughuli zake katika nchi ya mfumo kristu.

Hata kama WML na Rukara hawapo sasa lakini hatuzuiwi kuangazia uwepo wao nchini na utendaji kazi zao Katika nchi ya mfumo kristu, tena unathibitisha kabisa kuwa serikali (yamfumo kristu) ilitoa baraka zake
 
Mundungus Fletcher;

Hatubishani, tunajadiliana na kuelimishana!

Kadogoo

Kipi tutaelimishana kwenye Imani?

Mimi namuamini na naamini Yesu ni Mtu Kweli na Mungu Kweli. Sijui kitu gani utaniambia au kwakutumia nini utanishawishi i believe the contrary.

Na wewe Unamuamini Mtume Mohammed (S.A.W).

sidhani kama tutaelimishana katika hilo, Ila naamini tunaweza kuheshimiana katika kuamini. Mimi naheshimu unachoamini na ninaomba kwa Mungu (naamini pia ni Mungu mmoja) atupime kwa matendo yetu pia si Imani peke yake.
 
Hizi fitna kama hizi ndizo zinazotuumiza waislamu kwa miaka mingi.Siku za karibuni tumepiga hatua kuzijibu kwa ufanisi mkubwa na kila aliyetusikiliza alikubaliana na hoja zetu.Baada kuona hivyo mfumokristo umepania kuturudisha kule kule,kutufunga kamba huku wakitupiga magumi.Redio Imaan imefungwa kwa utaratibu huu na TV Imaan sijui kama itapewa kibali cha kurusha matangazo yake.Sasa huo ushujaa wenu ni upi?.Wa kuamua kutupiga tu na kulazimisha sisi tusijibu.
Hivi nyinyi hamuoni aibu kwa kujitangazia ushindi kila siku huku mkiwafunga kamba waislamu wasirudishe mapigo?.
Suala la Kuchinja limepotoshwa sana.Baada ya fujo za Mwanza TV imaan ilihojiana na watu muhimu na kule na kurusha taarifa ile hewani.Hapakuwa na shaka kuwa mpango mzima wa kupinga uchinjaji ni harakati ya maaskofu kuitumbukiza nchi katika machafuko bila sababu.Utashangaa badala kukubali ukweli TV hiyo ikaamriwa isitishe matangazo yake kwa mtutu wa bunduki na waislamu walioshiriki kulieleza tatizo lile wakafuatwa na kuwekwa ndani?.
Hizi habari za sheikh wa kiburundi na World Muslim League ni mfano huo.Hakuna cha waislamu kinachofanyika kisibughudhiwe.Muislamu mwenye maarifa asitumie maarifa yake kufanya jambo la maana atapata madhila na kusingiziwa mengi.Lakini kama ni mkristo hata akiwa ni mzungu,si muafrika na akaonekana wazi wazi kuhamashisha machafuko nchini basi haguswi kwa lolote kama ilivyo kwa suala la uchinjaji.

Hao akina Jumanne na Shukuru na Kikwete ni waislamu wanapokuwa nje ya serikali na watakapostaafu tu na ikiwa wako kwenye pensheni za uraisi wanakuwa ni wale wale.Lakini kikawaida wakiwa kwenye madaraka wanayosema ni yale yale ya mfumokristo. Kila wanachofanya kwanza wanajali maaskofu watawapokeaje.
Kuwa kwenye nafasi hizo wanaona wamefadhiliwa,Na kweli ni hivyo kwani huwa wamewekwa ili kuutia nguvu ukristo dhidi ya uislamu.Mfumokristo umewafanya wasahao mchango wa mababu zao katika kupigania uhuru wa nchi hii.Ukifanikiwa kuiua historia ya Mohammed Said viongozi wa namna hiyo wataendelea kuwatafuna waislamu wenzao mpaka mwisho kwa kulishwa maneno na kuyatapika hadharani.
Nashangaa sana mnapojaribu kufuta ukweli kuwa hotuba ya Nyerere aliyotoa UNO aliandikwa na watu wa chini yake wakati mpaka leo Kikwete bado anaandikiwa na kutiliwa maneno mdomoni ya kuwakandamiza waislamu wenzake.Kama angelikuwa mwenyewe asingewakanusha na kuwabeza waislamu wenzake kwa 100%..
Wale waliokuwa wakimwandikia Nyerere kabla ya uhuru walikuwa na uzalendo lakini hawa wa Kikwete ni watu wabaya sana.
Hili la World Muslim League halitaisha hivi hivi. Itabidi tuangalie shirika na wakuu wake maana lina uhusiano mkubwa sana na yale yaliyotokea EAMWS kwa ulinganifu na litatupa mwanga zaidi wa habari hii..
Hili nalo bi idhniLlaah litaisha hivi hivi kama lilivyoisha lile la Africa Events na Definition ya Mfumokristo
 

Nguruvi,
Hii ni kwa kuwa wewe ni rifiki yangu ndiyo nakujibu.

Wakati Rukara anakuja Dar ofisi za WML zilikuwa Starlight
baada ya kuhama IPS Building.

Nijuavyo mie WML hawapo nchini walifunga ofisi.
 

JokaKuu,

Unaweza kutupa takwimu Tanzania wanaokataa shule ni Waislam.

Hapa umetumia maneno ya Maghembe kama ushahidi lakini sisi tukitumia maneno ya Kitwana Kondo, Prof Njozi, Prof Kigoma Malima, mnasema ni hisia tu.

Hebu jiulize kwani iwe watoto wa Kiislam wa Pwani tu ndiyo hawataki shule wasiwe watoto wa Uturuki, India, Pakistani, Indonesia, Dubai, Iran, Saudi Arabia, Misri, Singapore, Qatar.
 
Last edited by a moderator:

Ritz
Mimi nafikiri wewe ndiye ujiulize ni kwa nini Watoto wa Pwani wanakataa shule. Mtoto wako akiwa hapendi shule
na jirani akakwambia Mtoto wako hapendi shule, huwezi kumuuliza tena jirani ni kwa nini. In first place wewe
ndiye unayepaswa kujiuliza.
 
Nguruvi,
Hii ni kwa kuwa wewe ni rifiki yangu ndiyo nakujibu.

Wakati Rukara anakuja Dar ofisi za WML zilikuwa Starlight
baada ya kuhama IPS Building.

Nijuavyo mie WML hawapo nchini walifunga ofisi.

WML Walifukuzwa nchini au ilikuwaje wakafunga ofisi?
 
Nguruvi3,

Bana nimependa msosi wako umetisha kaka unakula ndezi ngongwe...ha haa haaa vipi muhogo hauna nazi.

Mkuu Ritz, kila mtu hupenda kula vya kwao! Nungekuwa kwetu, ningekuwa nakula Mteke kwa Ugali wa kivunde.
Mnakasha unatupeleka mbali sana.
 
Last edited by a moderator:

Ni mie nikuulize wewe unaamini Tanzania nzima watoto wa Pwani ndiyo hawataki kusoma kutokana na Uislam wao.
 
Mkuu Ritz, kila mtu hupenda kula vya kwao! Nungekuwa kwetu, ningekuwa nakula Mteke kwa Ugali wa kivunde.
Mnakasha unatupeleka mbali sana.

Wimana,

Hapo ndugu yangu umenipoteza Mteke ni chakula gani nipe darsa kaka.
 
Ni mie nikuulize wewe unaamini Tanzania nzima watoto wa Pwani ndiyo hawataki kusoma kutokana na Uislam wao.

Hiyo kutokana na Uislam wao umeweka kibwagizo (si vibaya).Pengine ungeanza wewe kujiuliza hivi ni kwa nini Pwani watoto
wanaacha sana shule,? Umeshajiuliza hilo? ........halafu mjadala utakuwa mzuri.
 

Again you reavel your true color, Sheikh Said; hate against Nyerere!
Unaweza kuthibitisha kuwa huo ni mtandao wa Nyerere?
 
Kadogo,
Mbona mgumu wa kuelewa? Umeambiwa Nyerere hupuuza mambo ya kipuuzi na ambayo hayana tija kwake.
Na alimjibu kambona kulingana na hadhi na umri wa kambona.
Hakuona haja kuhangaika na hadisi za Ms, ndo maana alimpuza tu, na ujuwe Mwl, aliwapuuza wengi sana si Ms, peke yake.
 
Kadogoo,
Ujue hakuna alie mkamilfu labda wewe tu, ccm kila siku wanatudanya unasemaje?
Lejea ahdi za kikwete nyingi sio uongo? Kama tren la umeme, kigoma kuwa dubai, meli kubwa kuliko mv victoria?...... Nk.
 

Wewe hu-fit kwa Mzee Mwanakijiji japo unajitahidi sana uone kama atakujibu ila mwisho wa siku unajikuta wewe ndo umejivua nguo hadharani na maneno yako ya Taarabu,,wewe saizi yako Mzee Yusuph nilishakwambia huko nyuma Taarabu inakufaa sana.
 
Last edited by a moderator:
Huyu alikuwa mfadhili big time,na wala humsikii popote-huyu ufadhili wake sio kibaba cha mchele bali ni megabucks-wewe ushangai nimekuja na hiyo 33% na MS aja doubt

Inasemekana mfadhili mkubwa wa TANU alikuwa Abdu Sykes alikuwa na "kabati" la hela nyumbani kwake!!

Ni nini kilitokea hela ya safari UN ikapungua mpaka atokee John Rupia kuokoa Jahazi?!
 
Hiyo kutokana na Uislam wao umeweka kibwagizo (si vibaya).Pengine ungeanza wewe kujiuliza hivi ni kwa nini Pwani watoto
wanaacha sana shule,? Umeshajiuliza hilo? ........halafu mjadala utakuwa mzuri.

Pitia bandiko la JokaKuu utakutana na neno Waislam.

Hivi wale watoto wanaokataa shule kule Makete, Ludewa, Magu, Nansio, Mwitongo, Nkasi, Kizi, Nyanguge, Njombe, Katoro, Ngudu, Tarime, wote ni Waislam.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…