Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Nguruvi,
Tujadili mambo yetu.

WML hawapo tz na huyo Rukara halikadhalika.

Mohamed, tunachotaka kujua ni namna WML ilivyofanya shughuli zake katika nchi ya mfumo kristu.

Hata kama WML na Rukara hawapo sasa lakini hatuzuiwi kuangazia uwepo wao nchini na utendaji kazi zao Katika nji ya mfumo kristu, tena unathibitisha kabisa kuwa serikali (yamfumo kristu) ilitoa baraka zake
 
Hapa ndipo nashindwa kabisa kuelewa lengo la Mohamed Said ni nini anapotoa madai ya uongo kama haya baada ya kujifungia chumbani na kutunga upuuzi kama huu na kuuita ukweli na kuna watu wanaamini hizi ngano. Ni kweli Julius Nyerere alikuwa Mwalimu katika shule ya St. Francis Pugu, shule iliyomilikiwa na Kanisa Katoliki lakini hakuwa mwajiriwa wa Kanisa, alikuwa mwajiriwa wa serikali na alilipwa na serikali (He was a civil servant) Ni serikali ndiyo haikufurahishwa na yeye kujiingiza katika siasa na katu si Kanisa...Kanisa liliendelea kushirikiana naye na kumpa msaada ilipolazimu katika harakati zake za kisiasa hata baada ya kujiuzulu Ualimu. Ni uongo, ni ulaghai na ni udanganyifu usiovumilika kwa mtu anayedai kafanya utafiti kuhubiri upuuzi huu.

Kwanza ni serikali iliyowapiga marufuku watumishi wake kujihusisha na mambo ya siasa na pili, uamuzi wa kujiuzulu ulikuwa ni wa kwake na hakupata shinikizo lolote kutoka kwa Kanisa. Mohamed Said hupenda kuhusisha Kanisa na maamuzi ya serikali na leo yeye ndiye mpiga debe mkuu wa harakati eti za kupambana na mfumoKristo... masikini hajui kwamba hata huo Ukristo sio Ukatoliki pekee! Mwalimu angeweza kabisa kuamua kuendelea kufundisha akiwa mwajiriwa wa Kanisa kama angependa ila kulingana na maneno yake mwenyewe, hangepata muda wa kutosha kuwapa huduma ya elimu wanafunzi wake jinsi angependa. Hata baada ya kujiuzulu aliporudi kijijini Butiama aliombwa na padre wa Katoliki afundishe lugha ya Kizanaki kwa malipo...

Dr. Sivalon anaseme hali ilivyo ni kuwa hujui ikiwa hili la kanisa au la serikali.
 
Nguruvi,
Tujadili mambo yetu.

WML hawapo tz na huyo Rukara halikadhalika.

Mohamed, tunachotaka kujua ni namna WML ilivyofanya shughuli zake katika nchi ya mfumo kristu.

Hata kama WML na Rukara hawapo sasa lakini hatuzuiwi kuangazia uwepo wao nchini na utendaji kazi zao Katika nchi ya mfumo kristu, tena unathibitisha kabisa kuwa serikali (yamfumo kristu) ilitoa baraka zake
 
Mundungus Fletcher;

Hatubishani, tunajadiliana na kuelimishana!

Kadogoo

Kipi tutaelimishana kwenye Imani?

Mimi namuamini na naamini Yesu ni Mtu Kweli na Mungu Kweli. Sijui kitu gani utaniambia au kwakutumia nini utanishawishi i believe the contrary.

Na wewe Unamuamini Mtume Mohammed (S.A.W).

sidhani kama tutaelimishana katika hilo, Ila naamini tunaweza kuheshimiana katika kuamini. Mimi naheshimu unachoamini na ninaomba kwa Mungu (naamini pia ni Mungu mmoja) atupime kwa matendo yetu pia si Imani peke yake.
 
Kwahiyo baada ya mkataba wake kwisha alirudi Burundi. Kuna mahali anaunganishwa unganishwa sana na harakati za waasi. Anyway sijui. Sasa ilikuwaje huyu alikuwa anaratibu shughuli za ndani za misikiti kupanga mikakati akiwa mfanyakazi tu wa washirika la ''Kimataifa''.

Na hawa world muslim league waliwezaje kuingia na kufanya shughuli hapa nchini maana kwa maandiko yako Tanzania ikiwa chini ya mfumo hairuhusu kujiunga na mashirika ya kiislam.

Hawa World Muslim league walikuwa wanafanya shughuli gani kiasi kwamba mfumokrkristo ambao hauruhusu Tanzania kuwa na mahusiano na mashirika ya dini ya kiislam ukawasahau.
Na vipi huyu mfanyakazi wa kigeni aliweza kumiliki Nyumba na kujihusisha na shughuli za harakati za waislam nchini.

Mohamed, hili tuliweke sawa lisije likaleta utata kwa vizazi vijavyo kama la EAMWS.

cc Mwanakijiji, Mag3, JokaKuu, Jasusi, Ritz, Platoozom, Wickama, Raphaerl,Big show
Hizi fitna kama hizi ndizo zinazotuumiza waislamu kwa miaka mingi.Siku za karibuni tumepiga hatua kuzijibu kwa ufanisi mkubwa na kila aliyetusikiliza alikubaliana na hoja zetu.Baada kuona hivyo mfumokristo umepania kuturudisha kule kule,kutufunga kamba huku wakitupiga magumi.Redio Imaan imefungwa kwa utaratibu huu na TV Imaan sijui kama itapewa kibali cha kurusha matangazo yake.Sasa huo ushujaa wenu ni upi?.Wa kuamua kutupiga tu na kulazimisha sisi tusijibu.
Hivi nyinyi hamuoni aibu kwa kujitangazia ushindi kila siku huku mkiwafunga kamba waislamu wasirudishe mapigo?.
Suala la Kuchinja limepotoshwa sana.Baada ya fujo za Mwanza TV imaan ilihojiana na watu muhimu na kule na kurusha taarifa ile hewani.Hapakuwa na shaka kuwa mpango mzima wa kupinga uchinjaji ni harakati ya maaskofu kuitumbukiza nchi katika machafuko bila sababu.Utashangaa badala kukubali ukweli TV hiyo ikaamriwa isitishe matangazo yake kwa mtutu wa bunduki na waislamu walioshiriki kulieleza tatizo lile wakafuatwa na kuwekwa ndani?.
Hizi habari za sheikh wa kiburundi na World Muslim League ni mfano huo.Hakuna cha waislamu kinachofanyika kisibughudhiwe.Muislamu mwenye maarifa asitumie maarifa yake kufanya jambo la maana atapata madhila na kusingiziwa mengi.Lakini kama ni mkristo hata akiwa ni mzungu,si muafrika na akaonekana wazi wazi kuhamashisha machafuko nchini basi haguswi kwa lolote kama ilivyo kwa suala la uchinjaji.

Kadogoo,

..mimi sijui kwanini hali iko hivyo, kwamba tangu kabla ya uhuru na mpaka leo miaka 50+ biashara zote kubwa ni za Waasia tu?

..naomba umsome Prof.Maghembe hapa anazungumzia Waislamu na elimu dunia:

"Suala la elimu ya Dunia pia ni muhimu lakini mfano mzuri wa elimu kushuka ni katika mikoa ya pwani ambapo ndio ilipoanzia mwaka 1995 wanafunzi walioanza darasa la kwanza walikuwa 35,000 lakini walikuja kumaliza darasa lasaba9000 hapa inaonesha kua waislamu tunarudi nyuma badala kwenda mbele,"alisema Profesa Maghembe.

..Sasa hebu tafakari hayo maneno ya Prof.Jumanne Maghembe. Waislamu wa aina yako mnatumia muda mwingi kujenga fitina na chuki ktk jamii badala ya kushughulikia matatizo ya Waislamu.
Hao akina Jumanne na Shukuru na Kikwete ni waislamu wanapokuwa nje ya serikali na watakapostaafu tu na ikiwa wako kwenye pensheni za uraisi wanakuwa ni wale wale.Lakini kikawaida wakiwa kwenye madaraka wanayosema ni yale yale ya mfumokristo. Kila wanachofanya kwanza wanajali maaskofu watawapokeaje.
Kuwa kwenye nafasi hizo wanaona wamefadhiliwa,Na kweli ni hivyo kwani huwa wamewekwa ili kuutia nguvu ukristo dhidi ya uislamu.Mfumokristo umewafanya wasahao mchango wa mababu zao katika kupigania uhuru wa nchi hii.Ukifanikiwa kuiua historia ya Mohammed Said viongozi wa namna hiyo wataendelea kuwatafuna waislamu wenzao mpaka mwisho kwa kulishwa maneno na kuyatapika hadharani.
Nashangaa sana mnapojaribu kufuta ukweli kuwa hotuba ya Nyerere aliyotoa UNO aliandikwa na watu wa chini yake wakati mpaka leo Kikwete bado anaandikiwa na kutiliwa maneno mdomoni ya kuwakandamiza waislamu wenzake.Kama angelikuwa mwenyewe asingewakanusha na kuwabeza waislamu wenzake kwa 100%..
Wale waliokuwa wakimwandikia Nyerere kabla ya uhuru walikuwa na uzalendo lakini hawa wa Kikwete ni watu wabaya sana.
Hili la World Muslim League halitaisha hivi hivi. Itabidi tuangalie shirika na wakuu wake maana lina uhusiano mkubwa sana na yale yaliyotokea EAMWS kwa ulinganifu na litatupa mwanga zaidi wa habari hii..
Hili nalo bi idhniLlaah litaisha hivi hivi kama lilivyoisha lile la Africa Events na Definition ya Mfumokristo
 
Mhh, Mohamed huyu sheikh Rukara hakuwepo hapo kariakoo kweli na ofisi zake. Ni wewe umesema Rukara alikuwa na world muslim league na ninakubaliana nawe kabisa.
Ukasema mambo mengine iulizwe wizara ya mambo ya ndani! sasa kama hawapo Tanzania kwanini tuulize wizara mambo yasiyohusika.

Mohamed, huu mnakasha unachimbua kila jambo ili liangaliwe kwa undani wake.
Tumeona ya EAWMS na kutimuliwa kwa sheikh Amir. Mbona la Rukara linaonekana kama siri.

Wewe ni mwenyeji wa hapo kariakoo, tuthibitishie kuwa hawapo au hawakuwepo, I mean WML.

Nguruvi,
Hii ni kwa kuwa wewe ni rifiki yangu ndiyo nakujibu.

Wakati Rukara anakuja Dar ofisi za WML zilikuwa Starlight
baada ya kuhama IPS Building.

Nijuavyo mie WML hawapo nchini walifunga ofisi.
 
Kadogoo,

..mimi sijui kwanini hali iko hivyo, kwamba tangu kabla ya uhuru na mpaka leo miaka 50+ biashara zote kubwa ni za Waasia tu?

..naomba umsome Prof.Maghembe hapa anazungumzia Waislamu na elimu dunia:

"Suala la elimu ya Dunia pia ni muhimu lakini mfano mzuri wa elimu kushuka ni katika mikoa ya pwani ambapo ndio ilipoanzia mwaka 1995 wanafunzi walioanza darasa la kwanza walikuwa 35,000 lakini walikuja kumaliza darasa la saba 9000 hapa inaonesha kua waislamu tunarudi nyuma badala kwenda mbele,alisema Profesa Maghembe.

..Sasa hebu tafakari hayo maneno ya Prof.Jumanne Maghembe. Waislamu wa aina yako mnatumia muda mwingi kujenga fitina na chuki ktk jamii badala ya kushughulikia matatizo ya Waislamu.

JokaKuu,

Unaweza kutupa takwimu Tanzania wanaokataa shule ni Waislam.

Hapa umetumia maneno ya Maghembe kama ushahidi lakini sisi tukitumia maneno ya Kitwana Kondo, Prof Njozi, Prof Kigoma Malima, mnasema ni hisia tu.

Hebu jiulize kwani iwe watoto wa Kiislam wa Pwani tu ndiyo hawataki shule wasiwe watoto wa Uturuki, India, Pakistani, Indonesia, Dubai, Iran, Saudi Arabia, Misri, Singapore, Qatar.
 
Last edited by a moderator:
JokaKuu,

Unaweza kutupa takwimu Tanzania wanaokataa shule ni Waislam.

Hapa umetumia maneno ya Maghembe kama ushahidi lakini sisi tukitumia maneno ya Kitwana Kondo, Prof Njozi, Prof Kigoma Malima, mnasema ni hisia tu.

Hebu jiulize kwani iwe watoto wa Kiislam wa Pwani tu ndiyo hawataki shule wasiwe watoto wa Uturuki, India, Pakistani, Indonesia, Dubai, Iran, Saudi Arabia, Misri, Singapore, Qatar.

Ritz
Mimi nafikiri wewe ndiye ujiulize ni kwa nini Watoto wa Pwani wanakataa shule. Mtoto wako akiwa hapendi shule
na jirani akakwambia Mtoto wako hapendi shule, huwezi kumuuliza tena jirani ni kwa nini. In first place wewe
ndiye unayepaswa kujiuliza.
 
Nguruvi,
Hii ni kwa kuwa wewe ni rifiki yangu ndiyo nakujibu.

Wakati Rukara anakuja Dar ofisi za WML zilikuwa Starlight
baada ya kuhama IPS Building.

Nijuavyo mie WML hawapo nchini walifunga ofisi.

WML Walifukuzwa nchini au ilikuwaje wakafunga ofisi?
 
Nguruvi3,

Bana nimependa msosi wako umetisha kaka unakula ndezi ngongwe...ha haa haaa vipi muhogo hauna nazi.

Mkuu Ritz, kila mtu hupenda kula vya kwao! Nungekuwa kwetu, ningekuwa nakula Mteke kwa Ugali wa kivunde.
Mnakasha unatupeleka mbali sana.
 
Last edited by a moderator:
Ritz
Mimi nafikiri wewe ndiye ujiulize ni kwa nini Watoto wa Pwani wanakataa shule. Mtoto wako akiwa hapendi shule
na jirani akakwambia Mtoto wako hapendi shule, huwezi kumuuliza tena jirani ni kwa nini. In first place wewe
ndiye unayepaswa kujiuliza.

Ni mie nikuulize wewe unaamini Tanzania nzima watoto wa Pwani ndiyo hawataki kusoma kutokana na Uislam wao.
 
Mkuu Ritz, kila mtu hupenda kula vya kwao! Nungekuwa kwetu, ningekuwa nakula Mteke kwa Ugali wa kivunde.
Mnakasha unatupeleka mbali sana.

Wimana,

Hapo ndugu yangu umenipoteza Mteke ni chakula gani nipe darsa kaka.
 
Ni mie nikuulize wewe unaamini Tanzania nzima watoto wa Pwani ndiyo hawataki kusoma kutokana na Uislam wao.

Hiyo kutokana na Uislam wao umeweka kibwagizo (si vibaya).Pengine ungeanza wewe kujiuliza hivi ni kwa nini Pwani watoto
wanaacha sana shule,? Umeshajiuliza hilo? ........halafu mjadala utakuwa mzuri.
 

Sintofahamu,

Hawa ndugu zetu wana tatizo kubwa sana la saikolojia.

Nimesoma hapa mengi sana ya kustaajabisha na wao yanawataabisha sana.
Ngoja nikupe mfano.

Abdu Sykes ''contemproraries'' wake wote pamoja na baba yangu wanajua TANU
kwa hakika imeundwa na Abdu na harakati zile aliaanza muda mrefu.

Marehemu Mzee Mavemba wa Mtaa wa Mahiwa kila siku akilieleza hili.

Hawa wote wanajua mchango wa baba yake Abdu katika kuanzisha African Association
1929.

Hawa wanajua haya kwa kuwa wamekulia Dar es Salaam na haya yote yametendeka wao
wakiyaona kwa macho yao.

Ndugu zangu wanakuja na hoja kuwa TANU imeasisiwa na Nyerere 1954.
Kuna mtandao mmoja wa Nyerere umeandika kabisa kuwa TANU .....

Again you reavel your true color, Sheikh Said; hate against Nyerere!
Unaweza kuthibitisha kuwa huo ni mtandao wa Nyerere?
 
Mzee Mwanakijiji:

Naona unataka twende mbali zaidi: hivi mila yenu ndiyo inawafundisha hivyo? kumposa msichana na kubaka wapi na wapi? au Mwanakijiji hujui maana ya neno posa? Mtu mzima na heshima zako unaenda kumposa Mwanamwali, kaona haya kwa kunyamaza huku anaangalia chini wewe unamrukia na mkubaka? hii mila ya wapi tena jamani? hujui kuposa ni hatua ya mwanzo kabisa kufikia jiko?
Msichana kama alinyamaza unatakiwa kwenda kwa baba ake na kupeleka posa kwani mwanamwali alishakubali pale mwanzo ulipomtaka kumuoa! sasa wewe na hii habari ya kubaka umeitoa wapi?

Halafu kwa taarifa yako ukiona mtu hataki kukujibu basi fahamu kuwa aidha hataki majibizano na wewe, au katahayari na kufadhaika au kakiri na kukubali kimya kimya ila hana ubavu wa kukujibu!
Sasa kwa upande wa Mwalimu hayo mawili ya mwisho yanamhusu kwasababu aliyotaja Mohamed Said ni makubwa,
yalimdhalilisha na kumsononesha! Kwa hulka yake Mwalimu asingeweza kunyamaza ndio maana mwaka 1992 Kambona alipomtaja ktk uwanja wa Jangwani kuhodhi utajiri mkubwa yeye na Amir Jamal na Rashidi bila kuchelewa alimjibu na kukiri kuwa kama ni yeye anakubali ya Kambona kwasababu si ajabu yeye kuhodhi utajiri kwani alipata medali na zawadi tele!

Akiwajibu waandishi wa habari huku akicheka Mwalimu alimsikitikia sana Kawawa kusingiziwa na Kambona kwani kwa anavyomjua Rashidi hana utajiri wa aina hiyo!
Sasa kama alimjibu Kambona kwa kumtaja hadharani tena siku moja tu! kwanini asijibu hoja za Mohamed Saidi za tangu mwaka 1998 mpaka Profesa haroub Othman aende kumhoji? na zaidi kwanini chama chake alichoasisi CCM mpaka leo kimeshindwa kujibu hoja hizo ila tunaona na kusikia mitandaoni mashabiki na wakereketwa wa Chadema ndio wako mstari wa mbele kukipinga kitabu cha Mohamed Saidi!
Kadogo,
Mbona mgumu wa kuelewa? Umeambiwa Nyerere hupuuza mambo ya kipuuzi na ambayo hayana tija kwake.
Na alimjibu kambona kulingana na hadhi na umri wa kambona.
Hakuona haja kuhangaika na hadisi za Ms, ndo maana alimpuza tu, na ujuwe Mwl, aliwapuuza wengi sana si Ms, peke yake.
 
Katika hayo machache ya uongo miongoni mwa mengi yenye ukweli kama la kukamatwa kontena la kura bandia mpakani na Zambia na la yeye alishinda urais mwaka 2010 ni miongoni mwa uongo huo? au haya ni miongoni mwa ukweli wake au unaweza kututajia mfano mmoja tu wa machache ya uongo wake?
Kadogoo,
Ujue hakuna alie mkamilfu labda wewe tu, ccm kila siku wanatudanya unasemaje?
Lejea ahdi za kikwete nyingi sio uongo? Kama tren la umeme, kigoma kuwa dubai, meli kubwa kuliko mv victoria?...... Nk.
 
Kivukoni IdeologicalCollege, Historia ya Chama Cha TANU 1954-1977,Dar es Salaam, 1981.
[2] Oscar Kambona to Baldwin Rogers, 18 th October, 1955 Party Archives, Fabian Colonial Bureau File No.202.
[3] Ulotu A. Ulotu, Historia ya TANU, (1971) p. 11.
[4] Julius Nyerere, Freedom and Unity, Dar es Salaam, 1966, p. 38.
[5] Kirilo Japhet and Earle Seaton, The Meru Land Case, Nairobi, 1966, p.16.
[6] John Hatch, Two African Statesmen, London 1976, p.17.
[7] M.H.Y. Kaniki, TANU, ‘The Party of Independence and National Consolidation’ in G. Ruhumbika (ed) Towards Ujamaa, Twenty Years of TANU Leadership,Nairobi, 1974, pp.1-2.
[8] Julius K. Nyerere, TanganyikaAfrican Association, to Governor Edward Twining, 10 th August, 1953. Sykes' Papers.
[9] H.A.K. Mwenegoha,Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Nairobi, 1976, p. 5.
[10] Secretary Tanganyika African Association to Chairman and members of the African Association 7 th January, 1951. Sykes' Papers.
[11] Julius K. Nyerere President Tanganyika African Association to Governor Edward Twining, 10 th August, 1953. Sykes' Papers.
[12] Nyerere, op. cit. p. 38.
[13] Hatch, op. cit. p.17.
[14] Ibid. p. 91
[15] John Kabudi, ‘The Party System and Socialism in Tanzania’(1986 Seminar Paper).
[16] Kaniki, op. cit. Also see Uamuzi wa Busara, Idara ya Habari ya Chama, p. 2.
[17] John Iliffe, ‘The Role of the African Association in the Formation and Realization of Territorial Consciousness in Tanzania’.Mimeo. University of East Africa Social Sciences Conference, 1968, p. 24.
[18] S.A. Kandoro, Mwito wa Uhuru, Dar es Salaam, 1981.
[19] Judith Listowel, The Making of Tanganyika,London, 1965.
[20] Yash Tandon, ‘In Defence of Democracy’ Inaugural Lecture Series No. 14, Dar es Salaam, 1979, pp. 47-48.
[21] Daily Nation, 16 th April, 1986.
[22] New African, London, June, 1985; Africa Events,London, March/April, 1988, September, 1988.
[23] John Cartwright, Political Leadership in Africa,New York, 1983, p. 164. Also I.G. Shivji, Law State and The Working Class in Tanzania, London and Dar es Salaam, 1986, p.174.
[24] Yash Tandon, op. cit. pp. 47-48.
[25] I.G. Shivji, Law, State and the Working Class in Tanzania,London and Dar es Salaam1986, pp. 174.
[26] F. Engels, Manifesto of the Communist Party,1848.
[27] Richard L. Sklar ‘The Nature of Class Domination in Africa’ in JMAS Vol. 17 No.4, 1979, p. 544.
[28] Daisy Sykes Buruku, ‘The Townsman: Kleist Sykes’, in Iliffe (ed) Modern Tanzanians, Nairobi, 1973, pp. 95-114.


Bado wakipewa references kama hizo wao hawaoni umuhim wa kutuliza akili na kuweka kitako kusoma na kudadisi wamekalia kejeli na mipasho..
ni hasara kuwa na watu sampuli ya MWANAKIjiji
,kujiona kama analo analojiua kumbe ni kama kichwa box asie na kitu kichwani,tunawaambia status wenzenu wanazitafuta,wasijiona kupata exposure mitandaoni na kuandika makala za kuwakosoa mafisadi wa CCM basi wajione kuwa wamemaliza,wanajidanganya sana.
darja la Moh Said ni kubwa sana,si size yao..

Wewe hu-fit kwa Mzee Mwanakijiji japo unajitahidi sana uone kama atakujibu ila mwisho wa siku unajikuta wewe ndo umejivua nguo hadharani na maneno yako ya Taarabu,,wewe saizi yako Mzee Yusuph nilishakwambia huko nyuma Taarabu inakufaa sana.
 
Last edited by a moderator:
Huyu alikuwa mfadhili big time,na wala humsikii popote-huyu ufadhili wake sio kibaba cha mchele bali ni megabucks-wewe ushangai nimekuja na hiyo 33% na MS aja doubt

Inasemekana mfadhili mkubwa wa TANU alikuwa Abdu Sykes alikuwa na "kabati" la hela nyumbani kwake!!

Ni nini kilitokea hela ya safari UN ikapungua mpaka atokee John Rupia kuokoa Jahazi?!
 
Hiyo kutokana na Uislam wao umeweka kibwagizo (si vibaya).Pengine ungeanza wewe kujiuliza hivi ni kwa nini Pwani watoto
wanaacha sana shule,? Umeshajiuliza hilo? ........halafu mjadala utakuwa mzuri.

Pitia bandiko la JokaKuu utakutana na neno Waislam.

Hivi wale watoto wanaokataa shule kule Makete, Ludewa, Magu, Nansio, Mwitongo, Nkasi, Kizi, Nyanguge, Njombe, Katoro, Ngudu, Tarime, wote ni Waislam.
 
Back
Top Bottom