Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Hii ya TANU kaunda Abdu inafanana na ile ya CHADEMA kaunda Mtei! Angalau wewe sio mtu wa kufikiri kwa ufupi namna hiyo. Usimpende Abdu kwa kumdunisha Mwalimu. Unaujua vizuri uwezo mkubwa wa Mwalimu katika SIASA na UONGOZI. Mwalimu hakuwa mtu kusubiri Abdu aunde TANU. Kwamba Abdu hakuutaka URAIS wa chama alichokiunda yeye, halafu akawa mgombea, hilo tuwaachie wenye akili walitafakari.

Shukran Wild Card: Wajua Mimi ni maskini kwa vile wewe ni tajiri?; Wild Card, hivi kama sio mimi kukupokea na kukupa malazi nani angekujua hapa Arusha???????; Aisha nilikuoa ukiwa katika hali duni sana, sasa nimekulisha chakula changu na kukuvisha hadi umependeza kisha unaanza kunijibisha? wajua fadhila wewe?; Kwenye ibada; Wenzangu nawaaseni kuishi na watu kwa subira na haki na matendo mema. Kuweni wakarimu, hakika Mwenyezi hukipangia kila kiumbe riziki yake!!!!!! na saidieni yatima, wasafiri, wanyonge na watu kama hao. Fanyeni hayo yote kwa kumtanguliza Mungu na malipo yapo kwa huyo aliyekwezesha wewe. TUKO PAMOJA WILD CARD? BASI, JIONI NJEMA
 
Kama Abdul ndiye aliteunda TANU kwanini asiwe na kadi namba moja? Kwa heshima yake?

Swali hili linaulizwa na mtu mwenye weledi kweli?
Lina mantiki?kwahiyo kama Abdul alikua muasisi basi ni sharti angekuwa na kadi namba moja sio?
Lakini ulishajibiwa swali hilo,sema unajitoa ufaham kwa makusudi kabisa..
 
Hivi wewe mpumbavu kwanini usijitoe kwenye huu mnakasha na ukabaki msomaji wa hoja za wenzio? Hivi huu upumbavu unao uandika hapa unadhani nani anaufurahia zaidi ya huyo mzee wako mpuuzi na mchochezi MOHAMED!


Tumeusiwa katika uislam kutowajibu watu wapumbavu,kwan mpumbavu ukijibishana nae huwa hachagui ya kuongea,mwsho wa siku analeta athari kubwa hata kwa wasiohusika,
kujibu hoja yako kumesababisha mimi kumtukanisha mwalimu wangu Moh Said,
kosa hili sitalirudia tena,japo ww ndio umekuwa kinara wa kunifata fata kila napozungmza na wenzangu humu jamvini..
Nakurudisha kwenye daraja lako lile lile la kupuuzwa..
 
Mohamed Said,

Hii mipini unayoweka ni ushahidi tosha kuwa historia za AA, TAA, TANU, zote zinaanzia Dar es Salaam.

Kama kuna mtu anataka kujilidhisha amsome Nyerere hapo juu kwenye maandishi ya blue anakiri mwenyewe kuwa kaanza siasa za Dar es Salaam na wazee wa Dar es Salaam.

Hakika tumejua mengi kupitia darsa lako Inshaa'Allah tutajua zaidi ya haya.

Ritz shukran. Usiipunje Dar Bwana. Dar ndio kila kitu Ritz. Taa za kuongoza magari za kwanza tanganyika (dar), Magorofa (dar), vilabu maarufu vya kandanda (dar), misikiti/makanisa makubwa makubwa (dar). Wanazuoni wanaouujua uislamu vizuri kuliko wengine WOTE tanganyika (dar), waumini wacha Mungu kupita wengine (dar), madereva werevu zaidi tanganyika-dar (yaani kuchomekea-akifika sekenke/lukumburu anaomba aendeshewe), siasa za kueleweka (dar), mapato ya serikali (dar), gesi (dar/kusini?), NECTA (dar), vijana "wanaoshinda" mashindano ya kuhifadhi kurani (dar?), vyuo vikuu (dar), wakina mama wenye maadili safi sana (dar). Usiipunje dar Ritz. Mwisho wa siku ni kuwa haya ni maisha. Tumekutana mji huo kwa mahitaji na mikasa tofauti. Ridhika na hiyo lakini usijejidanganya hata siku moja kuwa familia ya kawaida hapo dar ina maisha bora zaidi ya ile ya Arusha/Bukoba/Nyamongo/Namanga au Kahama mjini.
 
Winama,
Yericko hana alichoandika.

Huo si uandishi ni vichekesho.

Msome Mohamed Said na tatizo la ugaidi kama alivyoeleza katika mkutano we maudhui hiyo Chuo Kikuu Cha Ibadan mwaka 2006:

The United States ismore concerned with international terrorism while Africa is obsessed withdomestic terrorism.

The question which the United States should reflect upon isthat why is it that the United States is considered a legitimate target for attackby terrorists?

In the answer probablylies the key to solving the problem. It is a pity that terrorism as a field ofi nquiry is yet to be taken up by actual victims of terrorism.

The inquiry has been monopolised by scholars from societies which at most have suffered one or two bomb attacks.

This erodes the realities of the subject as would beperceived by the actual victims of terrorism whose lives have seen nothing but sufferings.

Selective sampling will always as a rule provide wrong premise.

Today the world knows what took place in Auschwitz from the victims who went through the extermination camps during the Holocaust.
[1]

We are yet to get first hand experience of terrorism from those who had lived andexperienced it in Vietnam, Afghanistan, Iraq, Nicaragua etc. documented withthe same intensity as the world had documented the holocaust.

Why do Muslims’ eyesfill with tears when they watch on TV fighter bombers of the United States Army raining bombs on Iraq and Afghanistan; or Israel American made fighter bombersraining bombs on refugee camps in Gaza.

Why do some Muslims rejoice sometimeswith chants of ‘Takbir Allahu Akbar’ when a suicide bomber strikes?

Why some Muslims do not show remorse when asuicide bomber kills?

Why is it that we now have ‘refuseniks’ - soldiers in theIsrael Defence Force (IDF) who refuse to kill for unjustified cause?

This belief is also encroaching into the United States forces in Iraq.

Why a suicide bomber is romanticised in certainparts of the world and is rejoiced as a hero while an American soldier is seenas a villain?

The United States should reflect on these sentiments. Reasons for the reign of terror in Kenya,Uganda and Zanzibar, Rwanda and other places are known.

The United States withits array of social scientists and research centres should be able to come upwith conclusive findings on the root cause of terrorism and why America has become a terrorist target.

Post-independence Kenya has experienced bomb attackswhen in 1975 a bus stand was bombed in Nairobi followed by another bomb attack on Norfolk Hotel in 1980.
[2]

Mtwara a small town in southern Tanzania was bombed several times by Portuguese war planes during the struggle for liberation of Mozambique.

Neither Kenya nor Tanzania internationalised the bombing of its territory because both countries knew why they were under attack.

Tanzania was being attacked by the Portuguesewith the cognisance of the United States because it was the spring board forguerrillas fighting White supremacy and foreign domination in Mozambique, Angola Namibia and South Africa.

Is it really difficult for the United Statesto know why it is now being targeted?


[1] See‘The Last Days of Auschwitz 50 Years Later:Untold Stories From the Death Camp,’ Newsweek,January 16, 1995.
[2]Norfolk Hotel was bombed on New Year's Eve 1980. 15 people werekilled, including 2 Americans, 85 were injured, and half the hotel wasdestroyed. The owners are members of a Kenyan Jewish family. It seemed theattack was motivated by revenge against Kenya by the Palestinians for aidingthe Israeli commando team that rescued hostages hijacked by Palestinians to Entebbe airport in Uganda in July1976.



Moh Said tunakusoma sana,
Hatubanduki hapa 24/7,labda ubanduke wewe,
Tafadhwali Mwaga Darsa Huru ikhuan..
 
Ritz shukran. Usiipunje Dar Bwana. Dar ndio kila kitu Ritz. Taa za kuongoza magari za kwanza tanganyika (dar), Magorofa (dar), vilabu maarufu vya kandanda (dar), misikiti/makanisa makubwa makubwa (dar). Wanazuoni wanaouujua uislamu vizuri kuliko wengine WOTE tanganyika (dar), waumini wacha Mungu kupita wengine (dar), madereva werevu zaidi tanganyika-dar (yaani kuchomekea-akifika sekenke/lukumburu anaomba aendeshewe), siasa za kueleweka (dar), mapato ya serikali (dar), gesi (dar/kusini?), NECTA (dar), vijana "wanaoshinda" mashindano ya kuhifadhi kurani (dar?), vyuo vikuu (dar), wakina mama wenye maadili safi sana (dar). Usiipunje dar Ritz. Mwisho wa siku ni kuwa haya ni maisha. Tumekutana mji huo kwa mahitaji na mikasa tofauti. Ridhika na hiyo lakini usijejidanganya hata siku moja kuwa familia ya kawaida hapo dar ina maisha bora zaidi ya ile ya Arusha/Bukoba/Nyamongo/Namanga au Kahama mjini.

Mie sipo huko unapoelekea mimi nimejikita kwenye maneo ya Nyerere hapo juu.

Wapi nimekuambia Dar watu wana maisha mazuri kuzidi sehemu zingine?

Mnakasha huu unaelezea habari za AA, TAA, TANU, huwezi kuiweka Dar pembeni wakati ndiyo makao makuu ya harakati kama nimekukwanza kuitaja Dar niwe radhwi kaka.

Tulizana kunywa maji fundo tatu munkari ushuke kisha rudi kwenye mnakasha.

Karibu gahawa nipo barazani huku nacheza dhumna.
 
Tumeusiwa katika uislam kutowajibu watu wapumbavu,kwan mpumbavu ukijibishana nae huwa hachagui ya kuongea,mwsho wa siku analeta athari kubwa hata kwa wasiohusika,
kujibu hoja yako kumesababisha mimi kumtukanisha mwalimu wangu Moh Said,
kosa hili sitalirudia tena,japo ww ndio umekuwa kinara wa kunifata fata kila napozungmza na wenzangu humu jamvini..
Nakurudisha kwenye daraja lako lile lile la kupuuzwa..
Wewe sio muislam ila ni muganga njaa tu unayeishi kwa kujinasibisha na uislam! ungekuwa muislam usingekaa kutwa nzima hapa ukiwatukana watu wanaotofautiana fikra na Mohamed Saidi! Umemshambulia kwa mitusi Mzee Mwanakijiji kwa sababu ya kuandika Riwaya ambayo hata hujaisoma! ukamshambulia Yeriko Nyerere mpaka kumuita hana adabu ati kwanini ameandika kitabu! na hilo zee lako likaja na majivuno yasiyo na maana ati Yericko hawezi kuandika kitabu! ebo nyie mijitu mkoje? mnawezaje kujiita waislam safi wakati tabia zenu ni mbovu kuliko hata hao mnaowaita makafiri? Kwa muda mrefu sana nilikuwa nje ya mji kikazi nikawa natumia simu kuingia hapa jamvini, wewe na wapumbavu wenzako mkaandika humu mkiniulizia niko wapi na mkokoteni wangu! cha ajabu hilo umelisahau unakuja na ujinga wako uliokomaa ati nakufuata futa! Nitakufuatia nini wewe ambaye huna hata chembe ya maarifa zaidi ya kushangilia ujinga wa huyo Mohamed wenu? Kaa kando mjinga wewe huna unalolijua zaidi ya ushabiki wa kidini ambayo unaitumia kujinasibu nayo wakati huna hata chembe ya maadili yake!
 
Wanajamvi tunaomba majibu yenu kupitia huu mnakasha.

Chadema wanasema Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) kuna udini mkubwa.

Ni kweli tunaomba michango yenu.
 
Nguruvi,
Waamerika wana kitu wanaita "shit list."Humo wanatiwa watu ambao si waungwana
Mohamed, kama nipo katika ''shit list'' yako wala hilo halina tabu. Lisikupe wasi wasi, wewe endelea kuoga na vijana wako mtoni.

Sioni orodha yako ninayo fit.
Ile ya kukaa katika baraza au mkeka na kukubali kuwa Tanzania ni mwanachama wa commonwealth kwasababu ya mfumokristo! please

Tuendeelee na manakasha, ila sirudi nyuma wakati napiga katika mfupa.
Sihitaji kuwa muungwana kwa kukubali kuwa Warioba alianza siasa kutoka machungani,wala uungwana eti nisiseme Mohamed na Rukara ni maswahiba kama alivyo Mohamed na Ilunga. Unajua hilo

Hii ndio list yako unayofikiri kuniweka? Ilunga,Ponda, Rukara, Farid. Please usinitukane Mohamed.
 
Narudia tena kuuliza Chadema wanasema Chuo Kikuu cha Dodoma kina udini wa kutisha ni kweli kama kuna yeyote ambaye anafahamu jambo hili ni vizuri atujuze.

Kuna wajuvi humu wanakataa Tanzania hakuna mfumo kirsto vipi kuhusu UDOM kiongozi wa Chadema Mkirsto anasema kuna udini.

Hili mnakasha wetu wa uchochezi uende mbele zaidi tupeni michango yenu.
 
Moh Said tunakusoma sana,
Hatubanduki hapa 24/7,labda ubanduke wewe,
Tafadhwali Mwaga Darsa Huru ikhuan..

The Big Show,
Ahsante ndugu yangu.

Hii ni hidaya kutoka kwake Allah.
Tuna wajibu wa kuisomeesha bure.

Katika Uislam elimu haiuzwi.

Ndipo nilipomwambia ''publisher'' siwezi kuacha
kuandika JF.

Mchapaji anafikiria faida ya kitabu atakachotoa kapata
wasiwasi maana namwaga mchele wote hadharani.

Mimi siandiki kupata fedha naandika jina la Allah liwe juu.
 

Angalia kijana aliyepata pongezi nyingi za Invisible alivyopigwa mwereka


Baada ya kupata hiyo ya kichwa.Vimulimuli vimemfanya Nguruvi asijue kipi kianze mwanzo na kipi kije mwisho.Jee akubali kushindwa au aombe radhi kwanza.Badala yake ameropokwa lisilohusika.


Eti Makorora nako ukisema "Nakusihi usirudie tena neno hili" ni tusi pia.Kwa hivyo anaona tusi alilotoa kwa Mohammed kwa kumsingizia habari za Rukara ndio limejibiwa na maneno ya Makorora.
Hapa pamoja na kukoma kuendelea na habari za Rukara ulitakiwa uombe radhi pia na kuahidi kutorudia.
Anayojua Mohammed mengi ametuwekea wazi lakini kwa makusudi mnajaribu kuyapindisha.

Ami, hivi michango na hoja za namna hii nazo utazingizia kuwa sababu ni Nyerere, Ukatoliki na Mfumo Kristo kweli?

Nasikitika sana kusema kuwa Sheikh Said amekosa watu wenye uwezo wa kumuunga mkono kwa hoja na badala yake wanarusha vijembe tu na mipasho!

Pamoja na vurugu zote na mara nyingine kwenda nje ya hoja, ni Ritz pekee na Gombesugu ndio wanajitahidi kuja na kujenga hoja za kumuunga mkono Sheikh Said. Wewe Ami na The Big Show naona ni wanogeshaji tu wa kijiwe.
 

Wld Card,

Unazungumza kwa kuwa hapa ipo nafasi ya yeyote kusema atakacho.

Abbas huwezi kumfananisha na kaka yake Abdu.
Hebu soma hapa chini:

There is a very famous photograph of TANU founding members.

In that photograph three founder members are out of sight; Ally Sykes, Tewa Said Tewa and Kasella Bantu.

These were civil servants and in the British tradition of separation of politics from civil service government,
employees were not allowed to participate in politics.

Any African who contravened that sacred regulation was liable for summary dismissal.

Therefore when the photograph was taken the threeopted out.

The photograph was taken by Gomes, a very famous Goan photographer in those days.

Abdulwahid had arranged for Gomes to come to the TAA headquarters to take the historic photograph.
Gomes did not come on time.

Getting impatient with waiting, Abdulwahid asked his young brother Abbas to goand fetch Gomes from
his studio at Acacia Avenue (now Samora Avenue) in the town center.

The only means of transport for TAA was a beaten old bicycle.

While Abbas was paddling towards the town center to fetch Gomes, the photographer came and took the
group photograph.

And this is how Abbas Sykes missed the group photograph.


Wild Card,

Hapo juu nimekuonyesha kuwa Abbas alikuwa ni bwana mdogo tu mbele ya kaka yake kiasi alikuwa wa
kutumwa na baskeli katika mkutano ule wa kuasisi TANU.

Lakini picha kamili ni hii.

Nyerere alipojiuzulu ualimu na kuja kuishi na Abdu nyumbani kwake pale Mtaa wa Stanley, Abdu alimuhamisha
Abbas chumbani kwake ampishe Nyerere chumba kile.

Wild Card,
Nadhani unakumbuka mgogoro wa ''kabati la fedha'' la Abdu hata ikabidi nieleze fedha zile zikitoka wapi.

Fedha zile zilikuwa zikiletwa pale na Abbas ambae yeye ndiye alikuwa meneja wa Kituo kile cha mafuta,
kituo ambacho kilikuwa mali ya kaka yake.

Abdu alikuwa kati ya vijana maarufu wa Dar es Salaam ya wakati wake na hii ndiyo sababu kubwa haikuwa
tabu kumuuza Nyerere.
Mzee mo,

Kuna msemo usemao kizuri.....!
Kibaya chajitembeza.
Wewe na umaalufu wako na uislam wako kwanini usijitolee umuuze lipumba achukue ichi hii?
Ni miaka mingapi anahangaika?
Mzee wangu kukiuza kitu lazima kiwe kinauzika.
 
Mohamed, kama nipo katika ''shit list'' yako wala hilo halina tabu. Lisikupe wasi wasi, wewe endelea kuoga na vijana wako mtoni.

Sioni orodha yako ninayo fit.
Ile ya kukaa katika baraza au mkeka na kukubali kuwa Tanzania ni mwanachama wa commonwealth kwasababu ya mfumokristo! please

Tuendeelee na manakasha, ila sirudi nyuma wakati napiga katika mfupa.
Sihitaji kuwa muungwana kwa kukubali kuwa Warioba alianza siasa kutoka machungani,wala uungwana eti nisiseme Mohamed na Rukara ni maswahiba kama alivyo Mohamed na Ilunga. Unajua hilo

Hii ndio list yako unayofikiri kuniweka? Ilunga,Ponda, Rukara, Farid. Please usinitukane Mohamed.


Nguruvi3,
umepanic sana,kuoga na watoto mtoni ndio kipimo cha kauli zako zilizochuja kimantiki..
Mission yako imefeli,ushahid dhidi ya uchochez wa Moh Said haujaonekana hadi saiz.mmebaki kubwabwaja tuh..
Victory Won..!
 
Swali hili linaulizwa na mtu mwenye weledi kweli?
Lina mantiki?kwahiyo kama Abdul alikua muasisi basi ni sharti angekuwa na kadi namba moja sio?
Lakini ulishajibiwa swali hilo,sema unajitoa ufaham kwa makusudi kabisa..

The Big Show,
Ungemwambia tu kuwa kadi ya kwanza alipewa Nyerere kwa ajili ya heshima
ya yeye kuwa ndiye rais wa TANU.

Kadi zilizofuatia za akina Dome Budohi, Bi Titi, Idd Faiz Mafongo na ndugu yake
Idd Tosiri, Boi Selemani, Dossa Aziz, Marsha Bilal, Schneider Abdillah Plantan na
ndugu yake Ramadhani Mashado Plantan, Mshume Kiyate, Shariff Attas, Tatu biti
Mzee ndiyo hao tena waliokuwapo mstari wa mbele nk. nk.
 
Mzee mo,

Kuna msemo usemao kizuri.....!
Kibaya chajitembeza.
Wewe na umaalufu wako na uislam wako kwanini usijitolee umuuze lipumba achukue ichi hii?
Ni miaka mingapi anahangaika?
Mzee wangu kukiuza kitu lazima kiwe kinauzika.

Mgashi,
Hii naona ufungue uzi mpya hapa itakuwa hatufaidi.

Wasemaje mkuu?
Hivi mie maarufu?
 
The Big Show,
Ahsante ndugu yangu.

Hii ni hidaya kutoka kwake Allah.
Tuna wajibu wa kuisomeesha bure.

Katika Uislam elimu haiuzwi.

Ndipo nilipomwambia ''publisher'' siwezi kuacha
kuandika JF.

Mchapaji anafikiria faida ya kitabu atakachotoa kapata
wasiwasi maana namwaga mchele wote hadharani.

Mimi siandiki kupata fedha naandika jina la Allah liwe juu.
Nikweli kabisa unamtetea Alah kwa kuchoma makanisa inelekea una nguvu kuliko yeye
 
Wewe sio muislam ila ni muganga njaa tu unayeishi kwa kujinasibisha na uislam! ungekuwa muislam usingekaa kutwa nzima hapa ukiwatukana watu wanaotofautiana fikra na Mohamed Saidi! Umemshambulia kwa mitusi Mzee Mwanakijiji kwa sababu ya kuandika Riwaya ambayo hata hujaisoma! ukamshambulia Yeriko Nyerere mpaka kumuita hana adabu ati kwanini ameandika kitabu! na hilo zee lako likaja na majivuno yasiyo na maana ati Yericko hawezi kuandika kitabu! ebo nyie mijitu mkoje? mnawezaje kujiita waislam safi wakati tabia zenu ni mbovu kuliko hata hao mnaowaita makafiri? Kwa muda mrefu sana nilikuwa nje ya mji kikazi nikawa natumia simu kuingia hapa jamvini, wewe na wapumbavu wenzako mkaandika humu mkiniulizia niko wapi na mkokoteni wangu! cha ajabu hilo umelisahau unakuja na ujinga wako uliokomaa ati nakufuata futa! Nitakufuatia nini wewe ambaye huna hata chembe ya maarifa zaidi ya kushangilia ujinga wa huyo Mohamed wenu? Kaa kando mjinga wewe huna unalolijua zaidi ya ushabiki wa kidini ambayo unaitumia kujinasibu nayo wakati huna hata chembe ya maadili yake!

Nani wa kukuulizia wewe kwa lipi lamaana uliloliweka hapa brother uwe na adabu wala hakuna mtu alikuwa anataka kujua ulikuwa wapi hayo mambo ya kikazi ni kwa faida yako na familia yako ,ohh mzee MS mpumbavu,mchochezi,mjinga baba humuwezi mzee MS umegonga ukuta:frusty: hakuna mtu anayefurahia unayoyafanya kwenye huu mnakasha :nono::nono: nakueleza kwa mara nyingine unapopiga kichwa ukuta sikitikia kichwa chako usisikitikie ukuta!!!!!!!!!!
 
The Big Show,
Ungemwambia tu kuwa kadi ya kwanza alipewa Nyerere kwa ajili ya heshima
ya yeye kuwa ndiye rais wa TANU.

Kadi zilizofuatia za akina Dome Budohi, Bi Titi, Idd Faiz Mafongo na ndugu yake
Idd Tosiri, Boi Selemani, Dossa Aziz, Marsha Bilal, Schneider Abdillah Plantan na
ndugu yake Ramadhani Mashado Plantan, Mshume Kiyate, Shariff Attas, Tatu biti
Mzee ndiyo hao tena waliokuwapo mstari wa mbele nk. nk.

Mohamed Said,

Naona unaweka mambo Mubashar hadhwarani haya yote tungeyajua wapi hiyo orodha ya wanachama wenye kadi haipo kwenye kitabu cha Kivukoni kuna wanachama 19 tu.

Tupe darsa nani alipewa jukumu la kuchapa kadi za TANU na nani alikuwa anauza hizo kadi.
 
Last edited by a moderator:
Wild Card,
Inawezekana ni ujuvi.
Inawezekana pia ni kutojua historia ya Tanganyika.

Halikadhalika inawezekana na hasad na mengine mengi
kwako wewe kufananisha siasa za kikoloni na siasa hizi
za wakati huu tulionao.

Hakika mimi nakubaliana na wewe Nyerere si mtu wa
kusubiri Abdu Sykes aunde TANU Nyerere unavyoona
wewe ni mtu wa kuunda chama chake.

Tatizo liko hapa inawezekana kweli Nyerere alikuwa na
fikra ya kuunda TANU toka Butiama.

Na ikiwa utakuja ushahidi wa hilo labda alipata fikra hizi
kwa baba yake Chief Burito au kwa namna yoyote ile nani
atapinga?

Abdu mimi nasema kaunda TANU kwa sababu historia yake
yote kuanzia kwa baba yake ndiyo hiyo za siasa za mapambano
na ukoloni.

Huo mfano wa yeye na Chief Kidaha ni mmoja wa mifano hiyo.
Ukitaka mingene na iko mingi utarudi nyuma kwa baba yake na
yeye mweyewe katika maisha yake hadi TANU ikaaundwa 1954.

Ikiwa Nyerere aliunda TANU uwanja ndiyo huu uletwe ushahidi.

Isiwe Nyerere kuunda kwake TANU unafungamanishwa na historia
yake na Abdu Sykes na TAA pale New Street.

Lameck Bugohe mmoja wa waasisi wa TANU alipata kuandika makala
katika Raia Mwema akasema yeye alikuwa na fikra ya kuunda TANU
Mwanza katika miaka ya awali ya 1954.

Mimi niliandika makala ya kumuunga mkono.

Katika makala ile alilaumu wana historia kujikita kwa Nyerere bila ya
kufanya utafiti kwa wanasiasa wengine wa wakati ule yeye akiwa
mmojawapo.

Kuasisi TANU si milki ya Abdu Sykes peke yake yawezekana wako wengi
walikuwa na fikra kama zake.

Huu ni wakati muafaka kwa sisi kusikia habari za wazalendo hawa pamoja
na historia ya Nyerere katika juhudi zake za kuasisi TANU ama iwe Butiama,
Makerere au Tabora.


Wanabarza,
Yapo makosa kidogo katika simulizi za TANU zinazochapwa hivi sasa.
Mathalan Mzee Bogohe anasema kuwa Mhasibu Mkuu wa kwanza wa TANU alikuwa Julius Mwasanyangi.

Ukweli ni kuwa mweka hazina wa kwanza wa TANU alikuwa Iddi Faizi Mafongo aliyekuwa mhasibu vilevile wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika.

Iddi FaiziMafongo ndiye aliyekuwa na jukumu la kukusanya fedha za safari ya Nyerere kwenda Umoja wa Mataifa mwezi Machi 1955.

Katika nafasi yake ya kuwa mweka hazina wa vyama hivyo viwili Iddi Faizi alitoa fedha katika hazina ya za AlJamiatul Islamiyya na kuzitia katika mfuko wa TANU ili kufanikisha safari ile.

Iddi Faizi ana historia nzuri sana na ni jukumu lao sasa wanahistoria kuzitafuta habari zake. Iddi Faizi, Sheikh Suleiman Takadir na Nyerere ndiowaliotembea Jimbo la Mashariki mwaka 1958 kuwahamasisha wana -TANU wasisusekuingia katika Uchaguzi wa Kura Tatu.

Iwe itakavyokuwa nyaraka za historia zinaonyesha kuwa alotoa jina la TANU alikuwa marehemu Abdulwahid Sykes na jina hilo alilitoa Kalieni Camp India mkesha wa Christmas mwaka 1945 akiwa askari wa 6 Batallion, Burma Infantry katika King's African Rifles (KAR) wakati wa Vita Kuu ya Pili.

Kalieni Camp ndipo askari waKAR walipokuwa wamekusanywa wakisubiri kurudishwa makwao baada ya kumalizikavita. Ukienda katika shajara yake ya mwaka huo taarifa hizi utazikuta.

Juu haya hilo haliondoi ukweli kuwa huenda na Mzee Bogohe na yeye vilevile alikuwa na wazo la kuanzisha chama cha siasa hata kama si kile cha TANU.

Ala kuli hali muhimu ni kwa wanahistoria kuwatafuta wazee hawa na kupokea hazina ambayo si muda mrefu itatoweka.

Wangapi leo wanajua kuwa ni Hamza Mwapachu na Abdulwahid Sykes ndiyo waliomsukuma Nyerere katika ulingo wa siasa?

Au wangapi wanajua historia ya madaktari watano – Dr. Vedasto Kyaruzi, Joseph Mutahangarwa, Dr Wlibard Mwanjisi, Dr Michael Lugazia na Dr Luciano Tsere na mchango wao katika kusukuma mbele harakati za TAA kati ya 1948 – 1950?

Kwa kumaliza napenda kumuuliza msomaji wangu kuwa je, haishangazi kuwa historia ya kutukuka kama hii ya wazalendo na mashujaa wetu leo imetupwa na haipewi thamani?

Kama inashangaza je, haiwi vyema tukajiuliza kwa nini imekuwa hivi?

Ni nini viongozi wetu wanachokiogopa katika kuwaenzi mashujaa wa uhuru wa Tanganyika?
Je ndiyo tuchukulie kuwa Tanzania ni nchi isiyokuwa na mashujaa wake?

Wasomaji hamkubaliani nami kuwa kuna haja kubwa sana ya kuandika upya historia ya uhuru wa Tanganyika na kuwaenzi wale wote waliotoa mchango katika vita vya uhuru?

Kwa kumaliza makala haya namshukuru Mzee Lameck Bogohe kwa kufunua kinywa na kutueleza yale anayoyajua katika kuanzishwa kwa TANU na kuonyesha kidole kwa yale ambayo ameyaona yanapotosha historia hiyo.

Nitafurahi sana Insha Allah kama watajitokeza wengine na kuandika wanayoyajua kuhusu mashujaa wetu wa uhuru ambazo habari zao hazijulikani na wengi. Je hapana hajaya kuiuliza CCM hivi hadi lini wataiacha historia yao inapotoshwa na kupotea?
 
Back
Top Bottom