Wickama
JF-Expert Member
- Mar 8, 2009
- 1,466
- 1,196
Hii ya TANU kaunda Abdu inafanana na ile ya CHADEMA kaunda Mtei! Angalau wewe sio mtu wa kufikiri kwa ufupi namna hiyo. Usimpende Abdu kwa kumdunisha Mwalimu. Unaujua vizuri uwezo mkubwa wa Mwalimu katika SIASA na UONGOZI. Mwalimu hakuwa mtu kusubiri Abdu aunde TANU. Kwamba Abdu hakuutaka URAIS wa chama alichokiunda yeye, halafu akawa mgombea, hilo tuwaachie wenye akili walitafakari.
Shukran Wild Card: Wajua Mimi ni maskini kwa vile wewe ni tajiri?; Wild Card, hivi kama sio mimi kukupokea na kukupa malazi nani angekujua hapa Arusha???????; Aisha nilikuoa ukiwa katika hali duni sana, sasa nimekulisha chakula changu na kukuvisha hadi umependeza kisha unaanza kunijibisha? wajua fadhila wewe?; Kwenye ibada; Wenzangu nawaaseni kuishi na watu kwa subira na haki na matendo mema. Kuweni wakarimu, hakika Mwenyezi hukipangia kila kiumbe riziki yake!!!!!! na saidieni yatima, wasafiri, wanyonge na watu kama hao. Fanyeni hayo yote kwa kumtanguliza Mungu na malipo yapo kwa huyo aliyekwezesha wewe. TUKO PAMOJA WILD CARD? BASI, JIONI NJEMA