Ritz
Kwanza hizo percentages nina wasi wasi nazo. Huwa mna kawaida ya kupika na kuleta data from your own imaginations halafu mnazifanya ni factual data. Hivi umeisha andika hapa, baadaye data za 92% na 8% zitaanza kuonekana kwenye alnuur, na baadaye kwenye toleo la nne la Moh Said ilhali umezitengeneza wewe chumbani kwako.
Uchache au uwingi watu wa dini fulani hau-define udini.
Mzee Mwinyi, Rais Shein sio wadini
Lakini wewe na Moh said, mnaqualify kuitwa wadini japo nyie wanne wote ni waislam.
Statement kama "alhamdullilah, I have never seen a christian manyema" ya Moh Said, ni statement inayoashiria udini.
Haya lete data za maana zaidi tujadili.
Nanren,
Ulikuwa unazungumza na Ritz lakini nami umenitaja.
Kwa kuwa umenitaja nami nitakujibu.
Hakika nimesema, ''Alhammdulilah hakuna Mmanyema Mkristo.''
Kwa ufupi nimeshukuru kwa hilo.
Kwa nini nimeshukuru?
Naam nimeshukuru kwa kuwa Uislam ni nema na ni kitu ambacho
nakutamania hata wewe uwe Muislam.
Kushukuru kwangu si kuwa siwapendi Wakristo wala huo si udini.
Ikiwa wewe ni Muislam na ukawa mdini kwa maana ya kuwabagua
wasio Waislam hapo umekwenda kinyume na mafunzo ya Allah.
Utakuwa umedhulumu na Allah ameharamisha dhulma kama
alivyoharamisha kukubali kudhulumiwa.
Kumtamania mtu kuwa angekuwa Muislam ni kumtakia mafanikio hapa
duniani na kesho akhera.
Ingeliikuwa sisi Waislam tumeshika madaraka ya serikali ya Tanzania na kisha
Wakristo wakawa wanalalamika kuwa tunawabagua kwa udini wetu kama hivi
leo Waislam tunavyolalamika basi sie Waislam wote wa Tanzania tungekuwa
masuul mbele ya Allah.
Kwa ufupi tungekuwa na kesi ya kujibu kwani Allah hapendi dhulma.
Nimejitahidi kukueleza haya ili uelewe kwa nini nashukuru kuhusu Uislam.
Na ikiwa itakuja siku Insha Allah Nanren ukanambia, ''Mzee Mohamed mimi
nimesilimu sasa ni Muislam, neno nitakalosema kwako ni, ''Alhamdulilah.''
Maana yake, ''Shukurani zote zinamstahiki Allah.''