Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

RITZ;
Watakuja na kauli za kudai Waislamu wengine hutumia majina ya Kikristo na Wakristo hutumia ya Kiislamu! wakatihuo huo humtaja JK, Bilali, Said Mwema, Jaji Mkuu na wengine kuwa wamehodhi nyadhifa kubwa nchini na huo ni udini!

Kadogoo,

Wasomaji wa huu mnakasha ndiyo watapima mambo haya.
 
Last edited by a moderator:
Ha ha haaa...mbavu zangu! Mbona unajidhalilisha? Mhasibu Mkuu na mweka hazina wapi na wapi! Kama kawaida unapewa "like" na wale walee! Kweli mgema akisifiwa tembo hulitia maji, napita tu...

...Bado natafakari ile ya "shit list", kwa mbali nimesikia inatumika tu huko Marekani! Mohamed Said, you do know exactly where to direct your messages and the "likes" from the ever faithful start streaming , hongera!
 
Last edited by a moderator:

Huyo rafiki yako ni Mtanzania? Kama una picha yake naomba unitumie.
 
Picha yake sina, lakini ninayo namba yake ya simu. Ukitaka nikuunganishe sema.

nimemuandika barua pepe, akichelewa kujibu nitaomba hiyo namba asap

aisee ile ahadi nimeshindwa kuitimiza, mimi mvivu sana wa ku-scan vitu
 

Ritz
Kwanza hizo percentages nina wasi wasi nazo. Huwa mna kawaida ya kupika na kuleta data from your own imaginations halafu mnazifanya ni factual data. Hivi umeisha andika hapa, baadaye data za 92% na 8% zitaanza kuonekana kwenye alnuur, na baadaye kwenye toleo la nne la Moh Said ilhali umezitengeneza wewe chumbani kwako.

Uchache au uwingi watu wa dini fulani hau-define udini.
Mzee Mwinyi, Rais Shein sio wadini
Lakini wewe na Moh said, mnaqualify kuitwa wadini japo nyie wanne wote ni waislam.

Statement kama "alhamdullilah, I have never seen a christian manyema" ya Moh Said, ni statement inayoashiria udini.


Haya lete data za maana zaidi tujadili.
 
Last edited by a moderator:

Nanren,
Ulikuwa unazungumza na Ritz lakini nami umenitaja.

Kwa kuwa umenitaja nami nitakujibu.

Hakika nimesema, ''Alhammdulilah hakuna Mmanyema Mkristo.''

Kwa ufupi nimeshukuru kwa hilo.
Kwa nini nimeshukuru?

Naam nimeshukuru kwa kuwa Uislam ni nema na ni kitu ambacho
nakutamania hata wewe uwe Muislam.

Kushukuru kwangu si kuwa siwapendi Wakristo wala huo si udini.

Ikiwa wewe ni Muislam na ukawa mdini kwa maana ya kuwabagua
wasio Waislam hapo umekwenda kinyume na mafunzo ya Allah.

Utakuwa umedhulumu na Allah ameharamisha dhulma kama
alivyoharamisha kukubali kudhulumiwa.

Kumtamania mtu kuwa angekuwa Muislam ni kumtakia mafanikio hapa
duniani na kesho akhera.

Ingeliikuwa sisi Waislam tumeshika madaraka ya serikali ya Tanzania na kisha
Wakristo wakawa wanalalamika kuwa tunawabagua kwa udini wetu kama hivi
leo Waislam tunavyolalamika basi sie Waislam wote wa Tanzania tungekuwa
masuul mbele ya Allah.

Kwa ufupi tungekuwa na kesi ya kujibu kwani Allah hapendi dhulma.

Nimejitahidi kukueleza haya ili uelewe kwa nini nashukuru kuhusu Uislam.

Na ikiwa itakuja siku Insha Allah Nanren ukanambia, ''Mzee Mohamed mimi
nimesilimu sasa ni Muislam, neno nitakalosema kwako ni, ''Alhamdulilah.''

Maana yake, ''Shukurani zote zinamstahiki Allah.''
 

Nanren,

Wewe unasema huna data kuhusu UDOM nakupata unasema una wasiwasi nazo.

Chukua na hii pale UDOM wafanyakazi-Wanataaluma Wakirsto 96% Waislam 4%.

Wafanyakazi waendeshaji Wakiristo 86% Waislam 14%.

Lau kama unaona Ritz, muongo mnywa gahawa na kashata na ana akili za madrasa hauwezi kuwa mkweli basi ukipata wasaa chukuwa source hii utazipata ( UDOM Website, announcements of admission) nikipata wasaa tashusha orodha nzima ya viongozi wa Chuo Kikuu UDOM.

Nanren, ndugu yangu umenitaja mie kama mdini unaweza kuniambia udini wangu ni upi halafu kwa nini kwenu huwa hakuna Mkiristo mdini.
 
Last edited by a moderator:
Barubaru, ulikuwa na sababu gani za kuukana utanzania wakati moyo wako bado unaihusudu Tanzania yetu?
 
Mohamed Said,

Nakukumbusha darsa kuhusu kadi za TANU nani alikuwa anazigawa au kuziuza na rangi ya kadi za TANU ilikua rangi gani.
 
Last edited by a moderator:

Mag3,

Si wewe ndiyo ulisema humu jamvini kuwa mikutano mingi ya TANU ilikuwa inafanyika nyumbani kwa Nyerere Pugu, na haya maneno nayo utayakana na kukimbilia kwa Invisible, ili nipigwe BAN

Ninamnukuu Nyerere maneno yake mwenyewe kutoka hapo juu yenye maandishi ya blue.

Nyerere alisema hivi "Miezi minne baada ya kuanza kazi Pugu nikawa ninakuja Dar es Saalam kwa miguu kila jumamosi, baadaye Wazee wakanipa baiskeli ni kawa nakuja mjini kukutana na wenzangu kufanya mikutano". Mwisho wa kunukuu.

Hakuna kitu ambacho Mungu akipendi kama mzee kuwa muongo.
 
Last edited by a moderator:
Hata na wao hawako salama.Pamoja na kwamba hata maneno wanayozungumza ya kutiliwa vinywani mwao lakini kila siku wanaelekezwa vidole kwa udini.
Hata udini wa Kikwete unaomkera mpaka Mkapa hauna takwimu yoyote.Ni wivu na fitna za mfumokristo

 
One among the point which should be taken into consideration is the political situation which obtained in 1969.By 1965,it was quite clear to the Muslims that the Christian-dominated goverment was not interested at all in resolving the Muslim Question.Musilm decided to depend solely on their own efforts.They reorganised themselves under the East African Muslim Welfare Society(EAMWS),Westerlund(1980)said that it would probably never be known why Nyerere decided to ban that Muslim organisation.
Sivalon(1992) has revelead that it was actually the church leaders who requested Nyerere to ban tha Muslim body which actually he did,
Nyerere Went on to impose a puppet oganisation on the Muslims.
Bakwata was formed in December 1968 and adopted TANU's constitution by substituting the word TANU with Bakwata.Many Muslim sheikhs who opposed that puppet organisation were secretely arrested(Westerlund,1980,).It was against that background Nyerere who was all along opposed to the nationalisation of church schools hurriedly took that step.It was essentially meant to please the angry Muslims rather than to rectify the imbalances..
THIS IS THE MUSLIM QUESTION AS SEEN BY MUSLIMS..
 
Mtu mmoja anaundaje chama? Anachotaka kutuaminisha Mzee Mohamed ni kuwa AA ni mali ya Sykes; TAA ni mali ya Kleist; TANU ni mali ya Abdu! Hakuna siku wala saa mzee Mohamed atakiri kuwa RAIS wa KWANZA na pekee wa TANU alikuwa Mwalimu. Hasad mbaya sana hii sijui inatokana na Umanyema au UDINI wake.
 
Assalam Aleykum.

Attitude can take away your beauty no matter how good looking you are or it could enhance your beauty, making you adorable.

Cc.. gombesugu,

Ritz,

Waalayka Salaam Al Akhiy. Niwie radhi kiduchu,nimepata ile bayana yako lakini tangu siku chache zilizopita nimepata uzito kiduchu maana nina ugeni wa Khaloo yangu na Aunt yangu wapo hapa toka huko Unguja kwa matibabu na mapumziko kiduchu.

Wallahi nina furaha iso mfano kuona umerejea. Ni wajibu wetu kila mmoja baina yetu kipatwa na madhila basi soote tuwe na simanzi.

I noted what you said,always remember that;not every person is going to understand you and that's ok. They have a right to their opinion and the so called facts and you have every right to ignore it.

Insha Allah,tuendelee na hii shughuli.

Ahsanta.
 
Mzee Mohamed,
Unataka ushahidi gani wa Mwalimu kuwa mmoja wa waliounda TANU? Yeye ndie mwenye kadi namba moja; Mwalimu ndie RAIS wa KWANZA na pekee wa TANU tangu ilipoundwa hadi tunarudishiwa uhuru wetu; Mwalimu hakumpigania mkoloni kama walivyofanya babu, baba na Abdu mwenyewe; Abdu alipotea kabisa kwenye siasa za TANU baada kuanguka Urais.
"Kuasisi TANU si milki ya Abdu Sykes peke yake yawezekana wako wengi
walikuwa na fikra kama zake." Haya ndio maneno. Wala Abdu hakuunda TANU.
 

WildCard,

Hakuna mahala popote Mohamed Said amesema kuwa TANU ni mali ya Abdul na Ally Sykes wala AA mali ya Kleist.

Mohamed Said kaeleza kwingi kuhusu waasisi wa AA, TAA, TANU, ametaja majina mengi ya wazee ambao walikuwa waasisi.
 
Last edited by a moderator:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…