Kwani wewe hapa umefanya nini?
Wacha uongo wewe, kama hakukua na vita, akina Milambo ma Mkwawa walipanuaje milki zao za utawala? au unamaanisha nini unaposema hakukuwa na vita hapo zamani?Nilipo Bold.
hapo ndio kiini cha tatizo. Kwani historia inayofundishwa Tanzania ni ile ya kumsifia Nyerere mpaka kufika kusema yeye kaleta amani Tanzania . Jambo ambalo si kweli kwani amani ya nchi yenu ni urithi toka kwa mababu zenu. Hakukuwa na vita vya makabila toka zamani. Sasa najiuliza Nyerere huyu alileta amani gani huko Tanzania?
Kwa kumtukuza huko wanafichwa hata wale vinara wa ukombozi na wapigania uhuru waliojitoa muhanga kwa mali zao na nguvu zao jambo ambalo Al Akhiy MS umeliweka bayana mpaka leo tunamjua Abdu na nduguze na hata akina Mz Mshume kihate na mashikh wetu takadir na tambaza na wengine katika kupigania uhuru.
Mimi naamini huwezi ficha historia na ukweli siku zote unasimama. Allah akubarik ana Al akhiy MS kwa kututoa matongotongo ya historia iliyofichwa
Peleka chuki zako binafsi kwa wapumbavu wenzako!Nimetoa hoja za kuthibitisha kwamba ama Nyerere ni MNAFIKI au ni CHIZI. Sasa wewe chagua moja kati ya sifa anayostahili ama MNAFIKI au CHIZI. Kama una hoja ya kumnusuru kutoka kwenye sifa mojawapo kati ya hizo alizojijengea mwenyewe kutokana na hotuba yake kama ilivyowewekwa na muanzisha thread hii, basi mnusuru kwa hoja.
Peleka chuki zako binafsi kwa wapumbavu wenzako!
Wickama, mimi nimewekwa kwenye "shit list" ya Mohamed Said na sasa nadokezwa kuwa na gombesugu naye anatayarisha "shit list" yake, nitashangaa kama sitakuwamo humo. gombesugu anadai kuwa Mohamed Said ametufunza mengi hapa tulokua hatuyajui.Mzee MS; The movie ya the Bridge on river Kwai ninayo na i see none of its role here. Nyerere stole nobodys identity. Ila naona sana maneno ya Nicholas Cage 'IT WONT BRING THEM BACK". Ni kuwa despite your absolute denial you HATE NYERERE kuliko unavyompenda Khomein.
Simulizi zako mwenyewe za kuonyesha one scenario A.Sykes anataka TAA waingie wasomi halafu on another scene yeye na swahiba yake wanamteta Nyerere kuwa watamwachiaje mtu wasiemjua (Nyerere) chama, ina m-potray A.Sykes kama MNAFIKI na mteta watu. You dont seem to realize this. You have also potrayed ile election ya TAA kama a planned sham. Lengo kum-demean (Nyerere) kama vile alipewa ushindi mezani hali wewe huyo huyo unasema uchaguzi ulikuwa very close.
Umesahau hata hiyo episode inazidi kuonyesha A. Sykes kama a hypocrite. Haya huwezi kuyaona kwa vile "cross-hairs" zako zimelenga Mkatoliki Nyerere. Hiyo episode pia imeonyesha Nyerere akipata only benefit ya kampeni ya meneja wa hall la Anartoglu peke yake. Kwa anayejua kupima mambo ni kuwa Sykes alijiimarisha zaidi Dar akasahau kuwa kura watapiga toka mikoa yote. Hapa ni funzo kuwa tanganyika ilikuwa komavu toka zamani.
All along you are very bitter and hateful against Nyerere japo una-camouflage your hate. WELL HE IS DEAD. wengine huna haja ya kutusimulia mkeka aliolalia ulitoka kwa nani au nani alimnunulia kabichi. Kama unahisi dhuluma subiri, pana miaka 50,000 tutakua mbele ya Muumba wetu tukihukumiwa, utapata fursa ya ku-spill your case against him and your sadness kuhusu jinsi alivyohujumu EAMWS. Ukimshinda utaambiwa uchote katika thawabu zake ujaze kwenye kapu lako.
In the meantime no amount of books will change matokeo ya Anatoglu. That event is cast in stone. Your hate notwithstanding.
Masikini gombesugu, hajui kwamba ni Mohamed Said ndiye kapata funzo humu...kwake historia sahihi ilikuwa ni ya "wazee wangu" mpaka pale tulipomuelimisha kuwa "wazee wetu" walishirikiana bila kubaguana kwa misingi yoyote ile.Gombesugu said:Mfano nagundua hata Mag3, nae siku hizi anatumia neno Wazee Wetu!
Ukweli ukipiga hodi, uongo hutokomea!Mohamed Said said:Sihitaji kuthibitisha chochote kwa yeyote awaye yule. Nithibitishe nini ili iwe nini na kutaka nini?
Uongo! Mwaka 1929 Raisi alikuwa Cecil Matola.Mohamed Said said:TAA ilitokana na African Association chama kilichoanzishwa na Kleist Sykes 1929 yeye akiwa katibu na rais akiwa Mzee bin Sudi.
Uongo! Hiyo ilikuwa TANU ya kufikirika, TANU iliasisiwa 7/7/1954Mohamed Said said:Kuwa baba yangu alikuwa akijua kuwa Abdu alikuwa akaifanya mipango ya kuunda TANU toka 1950 na akimdokeza mambo yalivyokuwa yanakwenda?
Uongo! Mwalimu alishaikanyaga Dar miaka ya 1940 na kukutana na wenyeji wa mji kama Dossa Aziz.Mohamed Said said:Abdulwahid ndiye aliyempokoea Dar es Salaam ile ya miaka ya 1950 na akamjulisha kwa wenyeji wa mji. Wapenzi wa Nyerere hadi leo ukiwauliza Nyerere alisema nini kuhusu ukweli kuwa si yeye aliyeasisi TANU wamekuwa kimya.
Uongo na upuuzi! Mtu atoke nyumbani kwake kununua kitoweo Kariakoo bila senti mfukoni!!Mohamed Said said:Mwalimu Nyerere told Mshume Kiyate that he was going to Kariakoo Market to buy provisions but he did have a single sent in his pocket. Mshume Kiyate dipped his hand into his pocket and gave Mwalimu Nyerere two hundred shillings.
Uongo! Kwa nini uchaguzi wa kumtafuta Rais wa TAA ufanyike miezi michache baadaye?Mohamed Said said:Ndiyo maana haikuwa ajabu kuwa Nyerere alipofika Dar es Salaam 1952 ilibidi na yeye aingie nyumba ile akatambulishwe kwa Abdulwahid Sykes Rais wa TAA. Ile nyumba ndiyo yalikuwa makazi ya Rais wa TAA. Ndiyo ilikuwa "Ikulu" yao kwa wakati ule.
Uongo na Upuuzi! Lakini kama inasemekana, aliyekusimulia alikudanganya!Mohamed Said said:Inasemekana Mzee Mshume alipata kumpa Nyerere fedha nyingi sana kwa matumizi yake na ya familia yake ili asihangaike na atie nguvu zake zote katika kupigania uhuru.
Uongo na upuuzi. EAMWS ilikuwa ina wenyewe hadi ilipovamiwa na AMNUT!Mohamed Said said:Waislam walikuwa wanajenga Chuo Kikuu mwaka 1968 chini ya uongozi wa Mufti Sheikh Hassan bin Amir na East African Muslim Welfare Society (EAMWS). Kanisa Katoliki hawakupendezewa na hili na kwa kumtumia Nyerere EAMWS ikapigwa marufuku kuwa si chama halali na Sheikh Hassan bin Amir akafukuzwa nchini.
Uongo, upuuzi na aibu! Huku ni kujikweza, yaani Mwalimu aliyepambana na viongozi wakuu wa dunia kwa nguvu za hoja afyate kwa Mohamed Said!Mohamed Said said:Hili nililijua mimi kwa mara ya kwanza mwaka 1987 wakati Usalama wa Taifa walipokusanya gazeti zima la Africa Events (London) kwa kuwa ndani kulikuwa na makala yangu ikieleza mchango wa Waislam katika uhuru wa Tanganyika.
Hapo ndipo nilipopata nguvu ya kujua udhaifu wa Nyerere kuwa ala! kumbe si simba kitu anaweza akatiwa hofu na akaogopa!
Uongo! Kwa nini alipotua Dar baada ya vita hakufanya kweli? Je alikuwa na wadhifa gani AA kabla ya mwaka 1948?Mohamed Sykes said:Abdulwahid Sykes akiwa jeshini wakati wa Vita Kuu ya Pili ndipo alipokuja na wazo la kuasisi TANU. Hii ilikuwa tarehe 25 December 1945 na fikra hii aliandika katika shajara yake (diary).
Uongo, thubutu! Mambo ya kujitungia tu.Mohamed Sykes said:Mwisho utamkuta Bibi Titi Mohamed ndani ya Kamati Kuu ya TANU alivyotoleana maneno na Nyerere na Titi akamwambia Nyerere "Mimi namuogopa Allah simwogopi yoyote." Ugomvi wao ni kuwa Titi alikuwa anapinga kufungiwa kwa EAMWS akisema imekuwapo kabla ya TANU na ina manufaa makubwa kwa Waislam na Uislam na Nyerere akishinikiza EAMWS ivunjwe.
Loo! Kumbe ndio maana wazee walisononeka! Linalogomba ni uongozi wa nchi!Mohamed Said said:Ndiyo maana Prof. Haroub Othman alimuomba Nyerere ajibu shutuma kwenye kitabu changu ili Waislam wajue ni kwa nini aliipiga marufuku EAMWS ni kwa woga, husda na fitna ya kuwa Waislam wakiwa na
Chuo Kikuu na zile shule walizokuwa wakijenga nchi nzima kwa msaada wa Aga Khan watatoa changamoto
kwa kanisa au palikuwapo na jingine?
Hofu kuwa Waislam wakisoma watachukua uongozi wa nchi?
Alaa kumbe!Mohamed SaidMimi nimendika historia ya [B said:wazee wangu[/B] watu niliokuwa nikiwajua toka utoto
wangu. Bila shaka huko kwenu nanyi mna wazee hebu andikeni habari zao tuzisome.
Badala ya kutaka kwa ulazim na kwa haraka haraka kukubali hayo mapungufu ya kitabu cha Sheikh Mohammed,nijaalie muda kiduchu tuangalie atakapoishia na soote kwa pamoja, ndo tukate shauri la kujua nani mkweli na nani ni mrongo/alokosea. Halafu ndipo pia tutarejea tena kujua huko kukosea, je kunahalalisha na kutosheleza malengo ya hii mada kama ilivyoletwa hapa jamvini na Yericko Nyerere!?
Kwa kifupi,haya yoote tusumbukayo hapa jamvini,lakini la muhimu zaidi ni kuthibitisha shutuma dhidi ya Sheikh mohammed Said. Na pia tuangalie,je hata kama hizo shutuma dhidi yake tukizithibitisha,alizifanya kwa makusudio au ni tafran na dhahama tu za kiuandishi zilimzidi kimo,lakini moyoni mwake alikua na bado anayo makusudio mema kwa Watanzania wenzie na nchi yake!?
Ahsanta.
Aya ya kwanza Mohamed anaonyesha kuwa uchache (under representation of muslims in the Parliament) unasababu.Sweke34,
Nakuwekea hapo chini kutoka paper niliyotoa Chuo Kikuu Cha Ibadan mwaka 2006 kuhusu ugaidi:
Tanzania passed the Prevention of Terrorism Act of 2002, which in all intentand purpose replicated the United States Patriot Act of 2001. Due to underrepresentation of Muslims in parliament the Act sailed through without any difficulties notwithstanding Muslim opposition outside the parliament.
Whatconcerned Muslims more was the fact that the law was not only draconian butalso targeted Muslims. Muslims realised that with the Act in force any conflict between them and the government could be tried under that legislation and this would have very dire consequences.
The Prevention of Terrorism Act was a piece of legislation, which was imposed on Tanzania with the intention to open up the country for covert operations against enemies of theUnited States. Although the act does not say so in so many words but it is clear the legislation is meant to protect United States and provide it with political and legal powers to expand its military hegemony in countries, which it did not enjoy, such freedom before. On 17[SUP]th [/SUP]May 2003 with the anti terror legislation in place the police in collaboration with the FBI (who were already in the country waiting for the president to assent the bill) arrested Muslims suspected to be ‘terrorists.'
But those arrested had nothing to do with terrorism; they were Muslims leaders who the government arrested for being ‘opponents' of the government and ruling partythe Chama Cha Mapinduzi (CCM). Among those arrested were leaders of various Muslim charitable organisations -foreign oriented and local, who have distinguished themselves in providing social services to Muslims like building mosques, schools, orphanages etc.
These were targeted for being ‘terrorist sympathisers' or for being directly involved in ‘terrorist activities' or for ‘providing logistic support toterrorists;' and bank account of one prominent Muslim school – Al Furqan was frozen for suspicion of being a conduit of funds from abroad to support terrorism. In response tothese arrests Muslims staged a mass demonstration against the government andthe United States opposing the mass arrests of the Muslim leadership,harassment by the local police, the FBI and against the Anti – Terrorist Legislation. The demonstration was the first of its kind, as never before had Muslims shown such solidarity against a foreign power.
Ignoring the feeling of Muslims the then United States Ambassador to Tanzania Robert Royall addressedthe Tanzanian Parliament expressing his government's satisfaction in Tanzania'ssupport in its war against terrorists and pledged USD 100m in aid to East African governments to help combat terrorism. Investigations revealed that none of the arrested Muslims had any kind of military training whatsoever or had in anyway engaged in terrorist activities and they were quietly released without being charged.
Investigations also failed to prove that the account of AlFurqan had at any one time used to transfer funds from abroad for illegal use. All this notwithstanding there was no apology from the government, the FBI or the police.
Hapana unajiita hivyo kwa sababu ya uduni wako wa kufikiri!Najua mkiishiwa hoja mankimbilia kutukana matusi. Mimi sina alergy ya kutukanwa. Ndio maana naitwa Zali la Mentali.
Gombesugu ndugu yangu; twende taratibu:
c. Kitu pekee kipya ambacho Mohammed Said amekifanya na kufanikiwa sana ni kuingiza dini katika historia. Katika hili ni mwandishi pekee hadi hivi sasa aliyeiangalia historia yetu kwa mwanga wa dini. Bahati mbaya sana ukienda kwenye historia yenyewe au maandishi ya kipindi kile (cha kuanzia 1920s hadi 1961) hukuti wazee wetu wakiangalia harakati za Uhuru kwa misingi ya dini zao. Kina Saadan Kandoro, Ali Ponda, Shehe Mohammed Ramiya, John Rupia, Martin Kambanga na wengine wengi hutawakuta wakituliza dini zao kama kichocheo cha kumkataa ukoloni. Hukuti HATA MARA moja wazee wa Kiislamu wa Dar wakibagua wenzao kwa sababu ya dini zao.
ISIPOKUWA mara moja ambapo kikundi cha wazee wa Kiislamu wa Dar walianzisha upinzani dhidi ya Nyerere kwa sababu ya Ukatoliki wake. Kikundi kikiongozwa na Shehe Takadir na baadhi ya wazee ambao baadaye waliunda AMNUT. Masalia ya kikundi hiki na vizazi vyao ndio wamekuja kufufua ule udini ambao wazee wetu mashujaa wa Uhuru walifanikiwa kuuzika. Na kikundi hiki sasa kimepata wafuasi.
Ni kweli wazee wa wakati ule hawakuwa wadini lakini Nyerere alikuwa mdini aliyekubuhu.
Ushahidi uliowekwa na muanzisha thread hii kwamba Askofu Maranta alikwenda kwa Sheikh Issa ili aone jinsi Kanisa linavyoweza kuingia rasmi kwenye kinyang'anyiro cha kudai uhuru hapo mwaka 1948 na kushauriwa ajiunge kwenye vyama vilivyopo ni dhahiri kwamba Sheikh Issa alikuwa analikalibisha Kanisa kwenye African Association ambapo Masheikhs walishajitambulisha na hicho chama tangu kinaanzishwa mwaka 1929. Na inaonekana hapa kwamba mipango ya Kanisa Katoliki kuanza mikakati ya kumpandikiza Nyerere kwenye TAA ilianza kusukwa hapa kwani Kanisa halikuwa na sababu yeyote ya msingi ya kutaka kuonana na Masheikhs kujadiliana nao jinsi gani Kanisa litaingia kwenye harakati za kudai uhuru wakati Kanisa lilishafanya uamuzi kwamba hawawezi kujiunga na vyama ambavyo havina wasomi. Haiingii akili kwenda kumuona mtu ambaye tayari umeshamuhukumu kwamba hafai!!!!
Nyeree alificha makucha yake ya udini uliokubuhu wakati wa zoezi zima la yeye kuingia kwenye kwenye Siasa kupitia TAA. Makucha yake alianza kuyaanika mara baada ya kufanikiwa kujipenyeza ndani ya TAA na hatimaye kupata Urais wa nchi. Ndipo hapo Nyerere aligeuka kuwa zaidi ya Mdini. Alikuwa Mmadhehebu wa hatari sana. Alianza kuweka mikakati ya kuwapendelea Wakatoliki dhidi ya dini zingine na madhehebu mengine ya Wakristo. Akaanza mikakati ya kuuuwa Uislam.
Kitabu cha Jan P. Van Bergen kilimnukuu Nyerere akisema maslahi ya kanisa lake (Roman) yanakuja kwanza na hatokwenda kinyume na kanisa lake.
Alipokufa Pope Yohana wa 23 bendera ya taifa ilipepea nusu mlingoti nchi nzima!
Kabla ya kifo chake Pope Yohana wa 23 alimletea Mheshimiwa Nyerere barua ya pongezi kwa kuupanua Ukristo- barua ambayo ilitiwa saini na Pope mwenyewe. Barua hiyo imetangazwa kwenye gazeti la Tanganyika Standard.
Gazeti la Reporter la Kenya la tarehe 20/6/1963 lilitangaza katika ukurasa wake wa mbele:
"KUIBADILI AFRIKA YA MASHARIKI KUWA KATIKA DINI YA ROMANI CATHOLIC".
Ndani ya gazeti hilo ukurasa wa 18 liliwataja waliopewa dhamana ya kufanikisha jambo hilo kuwa ni: Uganda - Kiwanuka, Kenya - Mboya na Tanganyika Mheshimiwa Nyerere.
Mwaka 1970 Nyerere aliwaalika Ikulu aliyekuwa Katibu Mkuu wa Tanzania Episcopal Conference Fr. Robert Rweyemamu na muwakilishi wa Papa Tanzania Mgr. Giovano Cerrano na Nyerere aliwaambia wageni wake alikuwa anafanya kila liwezekanalo katika mamlaka yake kuuimarisha Ukatoliki Tanzania. Aliwaomba pia waende kuwafahamisha ma bishops kwamba ameanzisha idara ya elimu ya siasa kwenye TANU na kwamba amemteua Mkristo Reverend kuwa mkuu wa idara hiyo sio kwa sababu ya uwezo wake katika siasa bali kwa sababu ya imani yake thabiti kwenye Ukristo. Jukumu lake ni kuongoza na kudhibiti muelekeo wa kisiasa wa chama. Aliwafahamisha vilevile kwamba katika Kamati Kuu ya Chama (NEC) wajumbe wawili ni Reverends. Alisema anaamini hiyo ndio njia nzuri ya kuhakikisha kwamba chama kinapata watu wazuri!!!!!! (van Bergen, 1981:333-336).
Si ajabu kutokana na agano lake hilo hapo juu kwamba Sivalon (1992:49) anaripoti kwamba katika mwaka huo huo aliotoa ahadi Wakatoliki walikuwa asilimia 70 ya asilimia 75 ya Wakristo wote waliochaguliwa kuwa wabunge. Kati ya wabunge 108 waliochaguliwa 5 walikuwa wanaamini kwenye dini zetu za asili, 23 walikuwa wanaamini kwenye Uislam, 24 walikuwa wanaamini katika madhehebu mengine ya Kikristo yasiyokuwa Katoliki na 56 walikuwa wanaamini katika Ukatoliki. Hivyo utaona Wakatoliki walikuwa zaidi ya nusu ya wabunge wote!!!!!!!!
Nyerere ndio mtu aliyetumika na Kanisa katika mikakati yao ya kuumaliza Uislam (Crusade). Hii inadhihirishwa na mpango wake wa kufanya mapinduzi Zanzibar kwa kumtumia mtu katili na mdini mwenzake Okello ili kuusambaratisha Uislamu ambapo zaidi ya watu 20,000 waliuawa kikatili na watu wasiopungua 200 walichomwa moto kwenye tanuri wakiwa hai!!!!!
hii ndio inatoa picha halisi ni jinsi gani uongozi kwa maslahi ya umma ulivyo na changamoto kubwa. Kile kitendo cha mtu kuwa na upeo wa kutokuangalia dini, kabila, eneo bali binadamu si wote tunaweza kuufikia. Asante kwa ufafanuzi[/B]Nimemsoma Mohammed Said kwa kina sana na kwa werevu wote unaohitajika. Naweza kusema pasi ya shaka kabisa kuwa maandishi yake ni ya kichochezi (provocative) na yenye lengo la kupandikiza jazba miongoni mwa jamii ya Kiislamu kwa kuwaaminisha kuwa wanaonewa na ndugu zao Wakristu. Lengo lake ni kupandikiza uadui dhidi ya Kanisa kwa kulipa nguvu lisilookuwa nalo.
Mimi na wewe hatujui kilichomo moyoni mwake; tunajua kile anachokisema hadharani tu. Maandishi yake yanathibitisha kuwa lengo lake si jema kwa Watanzania. Kumbuka ukimsoma vizuri ndugu kwake na jamaa zake wa Karibu na ambao maslahi yao ana yajali sana ni ya Waislamu. Kwake Waislamu ni walio bora kuliko wengine; dhulma dhidi yao ni mbaya zaidi kuliko kudhulumiwa wengine, mafanikio yao ni muhimu zaidi kuliko mafanikio ya Watanzania wengine. Kwamba anajali "Umma wa Waislamu" kuliko Umma wa Watanzania wote hili liko wazi na ndio kiini cha histohisia yote.
Jamii anayoijali yeye katika Tanzania si ya Watanzania wote bali ni ya Waislamu wa Tanzania. Maandishi yake hayamuoneshi hata kidogo kama mtu anayetaka haki usawa na utu wa Watanzania wote uzingatiwe.
gombesugu,
Kwa kweli nikisoma bayana zako humu jamvini walaahi najisikia murua raha mstarehe.
Hawa ndugu zetu wanasema tusitumie neno "sisi" au "nyie" wanasema siyo uzalando wakati huo huo hao wanaotoa kauli hizo ndiyo wanaotuita sisi wafuasi wa Mohamed Said na wale wote wanaopingana na fikra za Nyerere.
Kwa maana hivyo hawa wote ambao ni Wakirsto ni wafuasi wa Nyerere. Sisi watu wa madarasa akili zetu na fikra zetu zinafanana kama machinas..ha haa haa.
Kuna jamaa mmoja humu yeye alienda mbali zaidi akasema kuwataja hao wazee wa kariakoo humu jamvini kwake ni matusi makubwa huyu huyu ndiye anatoa darsa kwa Waislam, ha ha haaa.
Kuna mwingine yeye bingwa wa tambo na majingambo anawaita wazee wetu "mwanameka" yeye anaita kukata kisu na mfupa, ha haa ha.
Karibu sana mie napata uji wa shurba na mkate wa ufuta.
Alnuur al taqiyya!
Aya ya kwanza Mohamed anaonyesha kuwa uchache (under representation of muslims in the Parliament) unasababu.
Kwa mtu wa Ibadan Nigeria au average Tanzanian hili atalijua kama sehemu ya uonevu.
Mohamed anajaribu kuonyesha kuwa wabunge wanateuliwa na si kupigiwa kura.
Hii ni sehemu ya madai yake kuwa mfumo umetawala kila mahali.
Lakini basi Mohamed anapaswa ajiulize, je bajeti inayopitishwa bila kupingwa kwa majority ya CCM au mswada wa kuanzisha machakato wa katiba uliopita bila kupingwa nao pia ulihusu wingi wa watu wa imani fulani.
Mtu anaweza kudhani Mohamed ana upungufu wa maono, la hasha anajua anachokifanya na kundi alilolenga.
Kwa wale wanaouliza wapi uchochezi wa Mohamed, mambo ni kama haya.
Ni huyu huyu Mohamed alisema walipita wakinong'onezana waichague CCM.
Ni CCM hiyo ndiyo ina majority kuanzia zama hizo anaandika paper.
Sasa inakuwaje tena analalamika under-representation ya jambo lile alilounga mkono?
Aya ya pili anaongelea kuhusu waislam kwa ujumla. Mohamed hajui kuwa katika waislam wapo BAKWATA, Ismailia, Bohora, Shia na Sunni na kwamba hicho anachokiongelea ni kikundi chake na wala si waislam.
Jitihada zake ni kuonyesha ulimwengu uzito wa jambo hili kama tutakavyoona.
Aya ya tatu, inapaswa kumshangaa Mohamed. Yeye anasema Marekani ilishinikiza sheria ya ugaidi ili iweze kuweka nguvu za majeshi yake, nguvu ambayo hawakuwa nayo siku za nyuma.
Na kwamba siku sheria ilipopitishwa FBI kwa kushirikiana na Polisi walikuwa tayari kuwakamata waislam.
Mohamed anasahau kuwa Tanzania ilikuwa na tukio la Ugaidi wa ubalozi kabla ya hapo(twin mbombing).
FBI walikuja na kumkamata Mohamed Ghailan pale kwao.
Sikwamba FBI walianza kuwepo wakati huo, walikuwepo siku zote.
Mohamed hajiulizi mabalozi wa Marekani wanateuliwaje, mashirika yao ya misaaada yanafanya kazi vipi.
Kama angelijua hilo basi asingeandika alichoandika kwasababu FBI hawahitaji ruhusa kuingia popote! wanaingia wakitaka.
Mohamed, hii forum si ya kutupa tupa unachodhani!
Aya ya nne anasema wale waliokamatwa hawakuhusika na mambo ya kigaidi isipokuwa wapinzani wa CCM.
Wapinzani wa chama kile kile alichokipigia upatu kwa kunong'nezana nadhani kuanzia zama hizo.
Kama si hivyo lini uswahiba wa ''waislam akina Mohamed'' na CCM ulianza?
Kaendele kusema, miongoni mwa waliokamatwa ni wale wa mashirika ya misaada kama ya kusaidia kujenga shule, afya na yatima. Kwa mtu anyewakilisha paper alitakiwa aeleze nani na washirika gani.
Aeleze kwasababu akitokea mtu akasema World Muslim League ni mojawapo Mohamed atapingaje wakati yeye haijui?
Kwa kiwango cha paper hii ni tatizo kubwa sana la mzee wetu, kuandika vitu kwa ujumla bila kuwa na specific pengine kukwepa ukweli. Akataja shule ya Al Faruq ili kujaza jazba bila kutaja mashirika.
Aya inayofuata amedai balozi za Marekani zilitoa pesa kwa nchi za EA, na kudai kuwa balozi wa Marekani ilihutubia bunge! Kwa hili yawezekana anajua undani wa kile kilichoongelewa.
Tunachomuuliza Mohamed ni kuwa lini balozi huyo alihutubia bunge?
Tunauliza ili kuondoa dhana ya kuwa suala hilo la waislam wa Mohamed lilikuwa kubwa kiasi hicho.
Ni mazoe ya Mohamed kutaja watu au mahali katika kuongeza nguvu za hoja zake hata kama hakuna ukweli.
Mohamed alishawahi kusema kuwa katika baraza la Idd mwaka 1988 aliyehudhuria alikuwa makamu wa rais mzee Kawawa.
Hilo alilisema makusudi kuonyesha nguvu ya hoja yake. Ni kutokana na mwiba huo uliotuchoma ndio maana tunamuuliza Mohamed, balozi alihutubia lini Bunge! Swali hili ni muhimu kwasababu limebeba paper nzima.
Mohamed, lini balozi alihutubia Bunge?
Nguruvi,
Ndugu yangu punguza ghadhabu, jitulize na andika kwa utulivu na kwa adabu.
Vinginevyo utageuka kuwa Lancelot Gobbo.
Si unamkumbuka huyu mtu katika ''Merchant of Venice'' ya William Shakespeare?
Nilieleza habari zake hapa JF.
Umesema mengi lakini nitakujibu moja.
Hili la Balozi Robert Royall.
Balozi Royall alihutubia Bunge la Tanzania tarehe 15 May 2003 na mada yake
ilikuwa ''Blood Money and Financing Terrorism.''
Nitakuongeza kitu.
Hiyo paper yangu iliyozua swali lako ndiyo lilikuwa jibu la hotuba ya Robert Royall
na ndiyo sababu ya kukumatwa uwanja wa ndege Dar es Salaam mwaka 2007
nilipokuwa narejea kutoka Tehran.
Nakutakia siku njema na utulivu wa fikra.
Barubaru unaishi sayari gani mwenzetu? HIvi kweli mchango wa Nyerere katika kuleta amani na umoja wa Taifa letu unaweza kupuuza na kuufanya duni? Kama hujui historia ya Tanganyika vizuri ni bora kuisoma. Kama hujui mambo ambayo Nyerere alifanya ili kuhakikisha umoja wa taifa unadumu tutakufundisha. Kama unafikiri wazee wetu ndio walileta amani jiulize tena. Unasema hatujawahi kuwa na vita vya makabila? really? Umesoma historia ya Makabila Tanzania?
BY Nguruvi3""Aya ya pili anaongelea kuhusu waislam kwa ujumla. Mohamed hajui kuwa katika waislam wapo BAKWATA, Ismailia, Bohora, Shia na Sunni na kwamba hicho anachokiongelea ni kikundi chake na wala si waislam.
Jitihada zake ni kuonyesha ulimwengu uzito wa jambo hili kama tutakavyoona. ""
Usichanganye mambo na kuweka histohisia zako nguruvi3,bakwata ni chombo chenu kilichowekwa na nyerere kusimamia maslahi yenu na si maslahi ya waislam..
hilo lipo wazi na tunalitamka kwa kifua mbele kabisa,tatizo lako unajikanyaga kanyaga,unapiga hatua tano mbele kisha unarud hatua 25 nyuma,jitulize,hebu tulizana..
Ha ha ha..!,
Kuna 'sisi' na 'wao',tena waanzilishi wa hali hii ni wao..
VIPOPOOO LEO UMESAHAU??