Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Dah ! Wickama na Wilcard leo mumenisoma kutoka huko mliko, nawashukuru sana. Kila mlichosema ndicho nilichotaka kusema.

Leo huwezi kusikia mwandishi mwenye akili nzuri akiandika kuhusu Mandela alivyobeba mitondoo huko Robben. Hata usaliti wa Winnie kwa huyu mzee unaandikwa kwa staha yake.

Mohamed kaenda hadi kufikia kusema wapi Nyerere alipunzika. Hivi Mama yetu Maria au watoto wake wakisikia hili wanajisikiaje. Wickama umesema vizuri sana kuhusu usengnenyaji, sasa huyu ndiye mtu anayetaka haki na anayesema anasimama kwa ajili ya uislam ule ule asio u-practice.

Tulimwambia siku nyingi kuwa kuna mambo katika uandishi unayaangalia na impact yake. Wapi Nyerere alilala na kitoweo alipata wapi ingeweza kuandikwa kwa namna ya staha kama kweli ilitokea hivyo. Lakini katika kuhakikisha kuwa anamdhalilisha Nyerere katika kiasi anachoweza Mohamed amekwenda mbali kumzulia hata mengine ya uongo.

Mohamed, this is too low! Kwa wajinga na wasiojua dini au ustaarabu wa mwanadamu hizi ni habari njema. Kwa mwenye kutumia asilimia 10 ya ubongo wake hii ni dhalilili kubwa sana katika fani ya uandishi wako.
 

Duuh,
Kama mitazamo ya watu ndiyo hii hamna haja ya watu tulio na akili timamu kujibizana hapa.
 

Mag3,

Wallahi,sisi soote tumepata simanzi kuona umetuhusisha na laana za kilevi. Makwetu hayo ni mambo ya kijaaluta yaso mipaka. Tafadhali itakulazim ututake radhi ndugu yangu,hasa kwa Sheikh Mohammed Said. Sisi pia tunampa hishma kubwa mno kuliko ile wewe umpayo Nyerere.

Ni kama vile jamaa zako walivyompa challenge Sheikh Mohammed Said kuhusu "Mmanyema Mkristo",na mimi binafsi nakupa challenge ndugu yangu Mag3;yakuwa sijapata kuona Muislam mlevi ijapokuwa sijawahi kufika Tarime kuona vitimbi vya huko.

Mbona zile LIKE zako na jamaa zako Mwanakijiji na Nguruvi3 hazikushughulishi? Huoni nawe pia unatumia ukabila na udini. Ama kwa hakika umenihuzunisha ndugu yangu. Hata zile nguvu za kukuombea utolewe kwenye ile "Shit List" ya Sheikh Mohammed Said zimenisha.

Lakini haina neno bado nakupenda na kukuheshimu sana ndugu yangu.

Cc;Ritz,Barubaru,Kadogoo,Boko Haram,The Big Show,Ami
 
Wakati nakunywa juisi ya muwa bariidi kama nilivyo aswa nikasikia sauti ya ngurumo hii hapa Nikahisi nahitaji vijiko vitatu vya asali (ushauri wa Ritz) kwasababu mtafiti hakufanya utafiti lakini anabaki kuwa mtafiti kama anavyothibitisha hapa Nikimalizia kijiko cha tatu ndipo nikasikia kishindo hiki
Sikumbuki kama ni ile ngurumo au kishindo vilivyonichanganya, ninakumbuka kusikia kwa mbali kama sauti za umati zikigutia liar! liar! liar!Mo stop this, please! case dismissed.
 
Thanks Mzee Mwanakijiji: Ni kweli MS ni mchonganishi. Sipati picha hapo Ibadan walivyotuona Watanzania baada ya
kuambiwa Balozi amepewa nafasi ya kuhutubia Bunge letu. MS hajali, anachonganisha Waislam na Wakristo, ameandika uongo mwingi na mifano iko chungu nzima, anawagawa hata Waislam wenyewe kwa madaraja (Manyema, Zulu fist class),
anawasimanga hata Marehemu na zaidi hata ile heshima kidogo ya Nchi iliyobaki anai-damage huko nje ili tu a-achive his
mission. Sijui hili baadaye atasema "typo error".

Hata huo Uislam anaodai kuutetea inaweza kuwa geresha. Ni chuki tu.
Hapa chini Wickama amemwelezea kwenye "angle' nyingine.

 
Unnecessary pomps from someone who thinks that because he was born in Dar or Tanga or Zanzibar then he is a better and more knowlegeable muslim than those muslims from Kigoma, Kondoa and Tabora. Pathetic "mipasho" style!

Ndio yale yale 'madharau' ya kibaguzi.
Wtu w Bara waliwadharau sana watu wa Pwani kwa kuwaita 'Waswahili' na watu wa Pwani vivyo hivyo kuwaita watu wa Bara: Wabara au Wakuja!

Ubaguzi huu kwa kawaida huendelea kiwango kwa kiwango, Walipobaki watu wa Tanga wenyewe, walidharauriana na wale wa Pwani wakawadharau Wasambaa hata kuja na msemo 'Msambaa mmoja havunji soko'! Huendelea vivyo hata wanapobaki wa dini moja pekee, mfano ni UK ambapo katika 'Ukristo' wao wakaanza kubaguana kati ya Waanglikana na Wakatoliki hadi kusababisha via vya kidini.
 

Kadogoo,

Salaam. Nilipenda saana ile minyambulisho ya masuala ya elimu mlofanya hapa na JokaKuu. Ilikua ni kwa bashasha na ustaarabu mzuri baina yenu. Nafikiri ile pia ni fundisho kwa wengine wenye kupenda kutuumiza vichwa kwa fedhuli zisizo maarifa.

Kwa ufupi nakutumia bayana yangu hii adimu kwako kukufahamisha kuwa si lazim kila swali uwajibu hawa jamaa,mengine waachie wenyewe tu. Najua kuna wakati wanatumia Psychological warfare ili kukuchosha,nawe inakua unaharibu bure effort na energy yako. Niwie radhi najua unayafahamu haya lakini ni uzuri pia kukumbushana.

Nimeona hivi mchana kutwa ulipokua unalumbana nao kuhusu masuala ya udhalimu wa Amerika. Jinsi baadhi yao walivyokua wakikujibu nahisi labda hata hawafahamu kiundani ile inner workings of American Military Complex and Geo-Political Orientation.

Ahsanta na Mola takupia fadhila zako Insha Allah.
 

Mag3, this is a good and helful summary to those who have embarked in this dialogue/ debate few weeks ago.
Your arguments and comments are highly appreciated. Thanks.
 
 

Nguruvi3,

Ndugu yangu tafadhali usipoteze bure maguvu yako kushangilia,mbona hii shughuli bado ni pevu mno. "Ndo kwanza mpopo unaalika maua"

Kwa hiyo tufanye sabra na utuvu,bado mambo ni mengi mno. Nakwambia hivi sababu mimi nakustahi sitaki uje adhirika mbele ya umma halaiki. Nafikiri umenifahamu.

Na pia utafanza vyema ukiwafahamisha jamaa zako wapunguze kidogo tashtit,la si hivyo mtasababisha ile orodha ya Sheikh Mohammed Said iongezeke bila sababu.

Tuendelee na mnakasha.
 
Gwalihenzi;

Najua wewe umeelewa maelezo ya Lisu kupitia nguvu za ufunuo! mimi mswahili mla kashata na gahwa uwezo huo wa kumuelewa Lisu ntaupata wapi? sisi tunateswa na hisi tu!
Kadogoo, wacha kejali, nguvu za ufunuo ndio zipi hizo?
 

Gombesugu,
Mnakasha umenoga.

Ugomvi ni kuwa Balozi wa Marekani hakuzungumza na Bunge bali
na wabunge wachache.

Sina ugomvi na hilo.
Ninachoshangaa ni kwa nini hili limewahamakisha kiasi kile.

Wanaona aibu kuwa Balozi wa Marekani kufika pale Dodoma au kitu
gani?

Sasa tatizo ni kuwa yale mengine niliyowaambia Waamerika wao
hawana haja ya kuyasikia wala kuyazungumza ila hili la halikuwa
Bunge bali wabunge wachache kama vile ingebadili msimamo wao.
 
Safi sana kijana uliyezaliwa katika familia ya waislam safi wenye kumcha Allah! ukafundishwa kujenga kitu unachokiita hoja kwa kusoma hotuba kwa chuki zako na kufikia kutukana matusi matamu ya kiislamu ati mtu mwenye umri wa kumpita hata babu yako tena marhemu ati ni MNAFIKI au CHIZI. Mzee Mohamed angekuwa na chembe ya busara angekukemea mara moja kwamba huo si uislam!
 
Kwani kushika nyadhifa ndio hoja unamjua mtu anayeitwa ABDU JUMBE chunguza mambo yaliyo mkuta ndio utajua baba yako wa taifa alichokifanya kasome kitabu kinachoitwa THE PARTNERSHIP.
Boko, kubishana na wewe ni kupoteza muda, mzee muovu Mohamed Said kesha iua kabisa akili yako. Nadhani anapousoma ujinga wako huu atakuwa anashangilia kwa ushindi alio upata.
 
Mkuu, siumeona walivyopongezana! kwao wao huo ulikuwa ushindi mnono kama ule wa timu ya ujerumani (B.Munich) kuwachapa bao nne Barcelona jana!Ama kweli hasidi Mohamed Said kailamba ilivyo akili ya jamaa hawa!
 
Mag3, this is a good and helful summary to those who have embarked in this dialogue/ debate few weeks ago.
Your arguments and comments are highly appreciated. Thanks.

Wimana,

Ikiwa unapenda turudi nyuma katika kitabu changu na yote nilisema hapa
basi tuanze taratibu nami nakuwekea hii hapa na nitaweka bold kwa msisitizo:

Nyerere alishinda uchaguzi huo dhidi ya Abdulwahid kwa kura chache sana.

Huu ulikuwa ndiyo mwanzo wa Nyerere kujulikana katika siasa zaTanganyika.
Kuanzia siku ile historia ya Tanganyika ikabadilika na siasa zaTanganyika zikachukua sura nyingine kabisa.

Siasa zilichukua sura nyingine kwasababu walingia watu katika harakati ambao waligeuza mwelekeo kudai
haki kwavipaji vya kuhamasisha watu ambavyo Tanganyika ilikuwa haijapata kuona.

Hapa ndipo unapokutana na Titi Mohamed,
[1] Tatu bint Mzee, Said Chamwenyewe,[2] Sheikh Suleiman
Takadir,
[3] na wengine wengi lakini kwa bahati mbaya hawa wote historia imewasahau hawatajwi kabisa.
Nyerere mwenyewe kamwe hajazungumzia kuhusu uchaguzi huu au namna alivyokuja kuongoza TAA Dar es Salaam.

Kiasi cha karibusana alichofika kumhusisha Abdulwahid na historia yake kilikuwa katika ile hotuba ya mwaka
wa 1985 ya kuwaaga wazee Dar es Salaam, na kwa bahati mbaya Nyerere alipojaribu kumueleza Abdulwahid, a
lishindwa kwa kuwa kwa kauli yakealisema hakumbuki cheo alichokuwa akishika Abdulwahid katika TAA wakati
yeye Nyerere alipojiunga na chama mwaka 1952.

Hata hivyo gazeti la serikali, "DailyNews" lilijaribu kurekebisha historia kwa kutaja cheo cha Abdulwahid, ingawakwa
makosa, kwa kusema kuwa Nyerere alipojiunga na TAA makao makuu Abdulwahid alikuwa katibu.

Ukweli ni kuwa Nyerere alimkuta Abdulwahid akiwa rais wa TAA.
Nini sababu ya mparaganyiko huu?


[1]Titi Mohamed alianza kuhutubia mikutano ya TANU katika viwanja vya Mnazi Mmoja kabla
hajamjua Julius Nyerere aliingizwa TANU na Schneider Plantan.

[2]Said Chamwenyewe ndiye liyeitafutia TANU wanachama wa mwanzo kutoka Rufiji alikotumwa
na Abdulwahid Sykes Julai 1954
. Alitoka TANU baada ya kuhitilafiana na Nyerere kuhusu Kura Tatu akamuunga
mkono Zuberi Mtemvu katikaAfrican National Congress.

[3]Sheikh Suleiman Takadir alifukuzwa TANU kwa kumshutumu Nyerere kuwa uhuru ukipatikana
hatawatendea haki Waislam walioupigania uhuru wa Tanganyika. Sheikh Takadir ndiye aliekuwa
Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa TANU Dar es Salaam.

 
Una uhakika alihutubia Bunge? au unarudia alichosema Mohammed Said? Kulikuwa na kikao gani cha Bunge kinaendelea Mei 15, 2003?


Nafikiri kiswahili tu hapo kina mapungufu lakin kuzungumza na wabunge katika semina ina nguvu sana kuliko kulihutubia Bunge. Kwani katika semina unapewa nafasi ya kuuliza masuala na hata kujadiliana kitu ambacho katika kuhutubia upati nafasi hiyo ya kuulizana maswali na mtoa mada.

All in all alisema na wawakilishi wa wananchi katika kufanya lobbing ili muswada wake wa Ugaidi upite kilainiiii.

Poleni sana.
 

Wewe unaifahamu dini yangu mimi? Nachangia kama Mtu mwenye usongo na nchi yake. Michango yangu humu haina uhusiano wowote ule na na isihusishwe na dini ya Kiislam au dini yoyote ile nyingine iwe ya Kikristo, kipagani, kienyeji, n.k. Hivyo si Mzee Mohamed au mtu wa dini nyingine yeyote yule atakayeweza kunisema kwa sababu michango yangu haihusu dini ya ya mtu yeyote yule.

Wewe ukikutana na chizi ambaye umri wake ni mkubwa kuliko babu yako utamwita nani? Anabakia kuwa chizi tu.
 
Wakati mwingine uwe unaandika kama mtu wa hadhi ya PhD. na wala sio mtu wa kawaida tu!unakuja na chuki zako badala ya uchambuzi wa kisomi! hebu basi tuletee hao wasiomi wakujiamini ambao Nyerere aliwatupa!
Wapo

Wapo wengi sana lakin ngoja nitakutajia wachache ambao umepata kuwasikia.
1. Mzee Edwin Mtei ( nimefanya nae kazi kwa ukaribu sana nikiwa wizara ya Fedha JMTz)
2. Dr (Engineer) Abdullah Salem Al-Harthy) huyu ni aucle wangu ni first Tz Engineer aliyegraduate Barmigham University 1960(Electrical) alikimbilia Oman
3. Mzee Kazibure (huyu aliwekwa kizuizini pale Kibaha Sec kama Mwalimu wakti alikuwa Mtaalamu wa masuala ya mawasiliano angani.


Na wengine wengi tu akina Osca kambona na wengine

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…