Cha kudebate tena hakuna kwani uovu wa Nyerere hata Mungu muumba wa mbingu na ardhi ametuonesha.Zali;Umejitahidi. Ni article nzuri. Sasa kwa vile katika posting yako ya #13365 umeonyesha tayari huyu Nyerere kapigwa laana hadi kufa kwa ukosefu wa kinga mwilini na tena polepole akipumulia mashine kama adhabu toka Mola wake, sasa tuna cha ku-debate tena hapa?
Hivi mlitaka kumwambia Nyerere nini? Mzee Bomani aliwahi kuniambia kwamba wote wale wanaomwita Nyerere haambiliki ni watu ambao walikuwa na uwoga wa kujenga hoja. Inaonekana na wewe ni mmoja wao. Nyerere alikuwa haburuzwi.\
WC,
Kwa tuliowahi kufanya kazi na Mwalimu , napenda kukwambia alikuwa HAAMBILIKI kwa lugha nyepesi alikuwa MUCH KNOW na ndio nchi yenu ameifikisha hapo ilipo. Hakuhishimu professionals na hakupenda wasomi wenye misimamo katika taaluma zao na ndio akawaingiza mkenge katika siasa ni kilimo na negine mengi.
Lakin nilitaka nikwambie rejea historia yote ya Tanganyika haijawahi kutokea ulanguzi wala rushwa hata wakti wa mkoloni hayo hayakuwepo. Lakin alipoingia yeye madarakani ndipo alipo aliasisi RUSHWA NA ULANGUZI na hivyo ndivyo wanatesa na kuwasibu mpaka leo. Kwani ulanguzi uliokomaa ndio tunaita UFISADI.
kifupi yeye ndie muasisi wa UFISADI nchini mwenu.
lakin je unakumbuka baada ya kwisha vita ya Uganda aliwaambia wananchi wote mfunge mikanda ya kiuchumi kwa miezi 18. Je ipo siku mpaka anakufa aliwaambia muifungue?
Wazee wa gerezani si umeona mwenyewe akina Nguruvi na Mwanakijiji walivyobwagwa chini baada ya kushindwa kuonesha uchochezi.Sasa wacha tuje kwa hayo mapinduzi naona mnakasha utanoga upya.Watazamaji watafika 300,000 InshaAllah.Labda wanamgambo wa Invisible wachoke.Naona mnakasha umeshageuka kutoka wazee wa Gerezani hadi mapinduzi ya Zanzibar.
Barubaru,
Nimeshakupa tuisheni kuhusu makabila ya Kenya na Uganda, siyo machache sana kama unavyodai. Anyway, kuhusu ukoloni nakubali walitumia devide and rule, siyo Kenya tu hata Tanzania. Wewe unadhani ni kwa nini Nyerere alipiga marufuku utawala wa uchifu? Kwa sababu machifu walikuwa na ushawishi mkubwa sana katika makabila yao. Usingeweza kujenga taifa lenye umoja kwa kuendeleza utawala wa machifu. Hilo moja. Pili, katika harakati za uhuru wa Kenya, TANU kilishirikisha viongozi wa makabila mbalimbali, akiwemo Jaramogi Odinga, ambaye alimpisha kiti Kenyatta kwa heshima tu, Paul Ngei, Tom Mboya na wengine wengi. Kenyatta alikuwa na nafasi ya kipekee kujenga umoja wa Wakenya lakini yeye alipoingia mamlakani akaanza kuwapendelea Wakikuyu. Mikopo yote ya kibiashara walipewa Wakikuyu peke yao. Ardhi katika Rift Valley, Mombasa hadi Taveta, walipewa Wakikuyu. Kuna wakati mwaka 1973 ukifika Nairobi ukipiga simu kwenye ofisi za serikali ama unajibiwa Kiingereza au Kikikuyu. Hiyo ndiyo Kenya ya Kenyatta. Nyerere alimwita "tribal chief." Matokeo yake tuliyaona sote 2007. Ukitaka somo kuhusu udogo au wingi wa makabila ya Uganda na Kenya nijulishe tena.
Zenj at last. Let me smell the karafuu. Ila posts zakeeeee, wenyewe so hot. Wanahitaji a deep breath. Lets move on. MS are you there?
Hivi mlitaka kumwambia Nyerere nini? Mzee Bomani aliwahi kuniambia kwamba wote wale wanaomwita Nyerere haambiliki ni watu ambao walikuwa na uwoga wa kujenga hoja. Inaonekana na wewe ni mmoja wao. Nyerere alikuwa haburuzwi.
Na kama kutosikiliza kwa Nyerere ndio kumetuletea matatizo mbona miaka karibu 30 tangu aondoke mamlakani mambo Tanzania yamezidi kuwa mabaya? Jiulizeni ninyi mnaoambilika what has gone wrong?
Naona unazidi kujikoroga mwenyewe.
Mimi nimekupambanulia vizuri kabisa katika utawala wa mkoloni na syile yake ya gawa na utawale kwa kenya na Uganda alitumia ukabila kwa sababu kenya na uganda hawakuwa na makabila mengi. (kenya hawakuwa na makabila zaidi 11 na uganda makabila 13 nchi nzima.
Upande wa tanganyika ambao kwa wakti huo kulikuwa na makabila zaidi ya 85 alitumia UDINI yaani dini moja kuwa superior kuliko nyingine na hata kutumia resource za taifa kunufaisha dini moja kwa kujenga maskuli na mahospital ili aweze kutawala.
hebu nikuulize je uliwahi kusikia imeitishwa harambee kujenga hospital kama KCMC au Bugando au skuli kama Ilboru au Umbwe au P
Kama ulimfahamu mzee Bomani hivi sasa ni marhemu.Jasusi.
Waarabu tuna usemi mmoja IN ORDER TO BUILD SOMETHING STRONG, IT HELPS TO START WITH BEST AND POSSIBLE MATERIALS. Na waswahli wanasema kila kitu ni msingi. kama umeweka msingi mbovu hata ufanyeje huwezii jenga kitu imara.
Sasa wa TZ ndio mupo hapo msingi mboovu mliojengewa na JKN ndio huo unaowasibu mpaka leo.
Kuhusu mzee Bomani naona tusiongee mengi kwani namfahamu vizuri sana sana sitaongea mengi bali mpe salam zangu atakwambia mengi kuhusu Mimi. Muulize tu Hamza Yousuf (alizoea kuniita Mwarabu au Mznz) kisha utanieleza.
Pole ndugu yangu
Naona mnakasha umeshageuka kutoka wazee wa Gerezani hadi mapinduzi ya Zanzibar.
Asante, Mohamed.Jasusi,
Haujageuka uko sawia.
Soma kichwa cha mnakasha "...na wapigania uhuru wa...Zanzibar."
Udini alitaka kuupandikiza Takadir. Huu tunaoshuhudia sasa umepandikizwa na CCM ya Kikwete hasa katika uchaguzi wa 2010.
Nimetoa hoja za kuthibitisha kwamba ama Nyerere ni MNAFIKI au ni CHIZI. Sasa wewe chagua moja kati ya sifa anayostahili ama MNAFIKI au CHIZI. Kama una hoja ya kumnusuru kutoka kwenye sifa mojawapo kati ya hizo alizojijengea mwenyewe kutokana na hotuba yake kama ilivyowewekwa na muanzisha thread hii, basi mnusuru kwa hoja.
Zali la Mentali ukitaka kuwa muongo mzuri jitahidi kutunza kumbukumbu. Naona kanuni hii wewe imekupita kisogoni. Kudhihilisha haya jaribu kurudia kusoma upumbavu wako hapo juu na huu uliopo hapa chini;
Asante mkuu kwa taarifa, basi namuachia mpuuzi mwenzie aendelee kumshukuru.Gwalihenzi
kubishana na huyu mtu i sawa kumpigia mbuzi gitaa! Ukingalia kwa makini join date yake (April 2013) itakupa majibu yote, huyu ni Member aliyeshindwa hoja ila kwa aibu nha kwa kuogopa kuwa tutamshangaa kwa hoja zake dhaifu kupitia ID inayofahamika, ameamua kutafuta ID nyingine ili kuficha ujinga wake.
Heshima yako mzee MS; Usijali ndugu yangu. Jitahidi na wewe ubane mtu. Nikuachie muda utafute. Nikizidisha hapa sote wawili twaweza kuwa "zombies au brain dead" Jioni njema
Sijajikoroga vyovyote vile. Ni kweli Waingereza walitumia mtindo wa divide and rule kote East Afrika, Tanganyika included.
Kwa Tanganyika walitumia machifu na ndiyo sababu Nyerere alipiga marufuku uchifu kwa sababu alitaka kuwepo direct rule. Pia kuhusu makabila check facts zako. Uganda ina makabila 64 na Kenya makabila 52. Huwezi kusema hayo ni makabila machache hata kidogo, hata siku moja. Unasema Tanganyika tulikuwa na makabila 85? Mwaka gani? Yaani makabila yetu yaliongezeka baada ya uhuru? Tanzania imekuwa daima na makabila 127 or thereabouts na siyo 85 kama unavyodai. Udini walitaka kuuanzisha akina Takadir, Nyerere akawazima. Udini umerudishwa tena Tanzania katika uchaguzi wa 2010 pale Kikwete alipoona Chadema inazidi kupamba moto. Ilibidi wapite msikiti hadi msikiti wahimize waislamu wamchague muislamu mwenzao, Kikwete, na hli katuthibitishia hapa Mohamed. KCMC na Bugando zilijengwa na hela za wamishenari. Actually kuna wakati serikali ilitaifisha hospitali ya Bugando lakini kama kawaida yao wakashindwa kuiendesha. Ilibidi wawarudishie. Una swali jengine?
Mohamed,Jasusi,
Huijui histori ya TANU na mchango wa Sheikh Suleiman Takadir.
Gwalihenzi
kubishana na huyu mtu i sawa kumpigia mbuzi gitaa! Ukingalia kwa makini join date yake (April 2013) itakupa majibu yote, huyu ni Member aliyeshindwa hoja ila kwa aibu nha kwa kuogopa kuwa tutamshangaa kwa hoja zake dhaifu kupitia ID inayofahamika, ameamua kutafuta ID nyingine ili kuficha ujinga wake.
Zali la Mentali wameshamweka upande wetu kama kawaida yao,twende kazi zali la mentali...
Asante mkuu kwa taarifa, basi namuachia mpuuzi mwenzie aendelee kumshukuru.