Yericko Nyerere
JF-Expert Member
- Dec 22, 2010
- 17,005
- 20,425
- Thread starter
-
- #13,921
Naona umeamua kurukia maeneo mengine na kukimbia masuali yangu haya hapa:
Mimi sijakuuliza kama Abdul alikuwa anafanya siasa gerezani au kitaifa. Ninachotaka kujua ni kwamba wakati Nyerere akiwa Makerere, katibu wa TAA alikuwa nani?
Na kama unakubali kwamba Nyerere alikuwa na haki ya kutomfahamu Abdul, kwa nini unampinga Mzee Said kwa kusema kwamba Nyerere alidai kutomfahamu Abdul?
Umeshindwa kujibu haya masuali? Mbona unarukia kwenye mada zingine na haya masuali unayakimbia kama kituo cha polisi?
Maswali yako kimsingi nilitakiwa kuyajibu mimi,
Na nilikuwa tayari kuyajibu, lakini kwabahati mbaya nilipitiwa na usingizi jana na leo nilitingwa na majukumu mengine!
Lakini kwa sasa sitajibu kwakuwa mkuu Nguruvi3 ameshajibu kwa weledi uleule na nimefurahi sana majibu yake kwakuwa ametembea kwenye medula zangu!
Alichouliza Mag3 mara tatu kina maana sana ingawa inahitaji akili za ziada na uhuru wa fikra kuona kilicho ndani yake.
Mag3 anasema wakati Nyerere akiwa ndani ya siasa na kiongozi Abdul Sykes alikuwa mtoto wa familia ya Sykes. Kwamba aliishi kwa sifa za familia yake
Maana yake ni kumwambia Mohamed kuwa Abdul Sykes(As much as we respect him) hakumuingiza Nyerere katika siasa na wala si yeye aliyemfundisha Nyerere siasa kama madai ya Mohamed yasemavyo
Julius Nyerere, lifelong learning and education. One of Africas most respected figures, Julius Nyerere (1922 1999) was a politician of principle and intelligence. Known as Mwalimu or teacher he had a vision of education and social action that was rich with possibility
Mkuu Nguruvi3, ni hapo ndipo kwa mbali tunapata fursa ya kupima upeo wa baadhi ya watu tunaojadiliana nao humu...kuna hii picha inajaribu kujengwa ya kuwaweka kwenye mizani Mwalimu Nyerere na Abdulwahid Sykes! Inafika wakati hata kunatolewa hoja eti ya kuwapambanisha kwa vigezo vya akili, uwezo na sifa. Ziko hata porojo zinatolewa eti Abdulwahid Sykes alikuwa ana akili kiasi cha kupata pass ya juu ya "first class" katika mtihani wa darasa la kumi! Hii yote inafanyika katika harakati za kumjenga na kumweka kwenye kundi la wasomi wa wakati huo!
Nguruvi3. mtu kufika darasa la kumi miaka ya 1940s ilikuwa ni mafanikio ya kujivunia, siyo tu kwa mhusika bali kwa jamii yote iliyomzunguka hadi kwa shule na waalimu waliomwandaa toka awali. Mtihani wa darasa la kumi la wakati huo ulijulikana kama Territorial Exam ambao ulifanywa na nchi zote zilizokuwa chini ya himaya ya Waingereza...ulikuwa ni mtihani uliokuwa na heshima kuliko hata degree ya sasa inayopatikana nchini kwetu sasa hivi. Mtu aliyeweza kupata "first class" aligombewa kama kuku wanavyogombea mahindi na nafasi za kuendelea zilikuwa nje nje na hazikujali uraia, rangi, dini wala ukabila...ni akili ya mtu tu iliangaliwa.
Kumbukeni pia wakati huo, masomo ya sekondari hayakuwepo, ukishinda vizuri ni moja kwa moja Makerere na kwingineko...ndio maana akina Dr. Hamza Mwapachu, Chief Kidaha Makwaia, Dr. Vedasto Kyaruzi na wengine wengi waliweza kuendelea mbele kwa masomo ya juu bila ubaguzi wowote. Hakuna, narudia, hakuna namna mhitimu wa darasa la kumi aliyefuzu vizuri kama inavyodaiwa kwa Abdulwahid Sykes kupata "division one" angeweza kunyimwa hiyo nafasi na badala yake akapelekwa vitani, hakuna, wakoloni walijali sana elimu na hasa intelligence ya mtu. Hata wale ambao hawakupasi vizuri kama inavyodaiwa kwa Abdul, walipata ajira nzuri tu katika utumishi sekalini.
Wanajamvi, lengo langu si kumdhalilisha mzee wetu Abdulwahid Sykes, lakini inafika mahala ukweli lazima utamalaki na hapa ni JF. Hata hivyo nakiri kuwa huenda ziko sababu maalum zilizomzuia Abdulwahid Sykes kuweza kuendelea na masomo ya juu zaidi...kama yupo anayeijua sababu hiyo naomba ajitokeze na sote bila shaka tutapima na kujiridhisha kwamba hapo kweli kulikuwa hamna namna. Kwenye miaka ya 1940s, jumla ya Watanganyika walioweza kumaliza darasa la kumi ilikuwa ndogo sana na aliyefaulu vizuri hakuhitaji kufanya jitihada zozote za binafsi kupata nafasi katika vyuo mbalimbali ndani na nje ya nchi.
Mimi na Gombesugu tushamalizana, sijui kwanini unarudisha huu mjadala wa ''mkoba wa Ibadan'' tena.Gombesugu,
Hasid hana sababu.
Anazungumzia Chuo Kikuu Cha Ibadan...
Mbona karuka Chuo Kikuu cha Johannesburg,
Chuo Kikuu Cha Ohio, Chuo Kikuu Cha Northwestwern,
Vipi Chuo Kikuu Cha Kenyatta, namna gani Zentrum Moderner
Orient, Berlin...
Chuo Kikuu Cha Zanzibar...
Ana wasiwasi na "scholarship..."
Vipi vitabu viwili nilivyochapa na Oxford University Press...
Hakika wazee wetu wametufunza kutojinasib lakini kuna mahali
hawa watu lazima waelezwe.
Ndugu yangu Gombesugu nakushukuru kwa yote.
Kimsingi hakuna sababu zilizomzuia Abdul Sykes kutoendelea na masomo zaidi ya KUFELI,
Maana kama akina Dr. HAMZA Mwapachu muislamu aliweza kuendelea na masomo iweje Abdul Sykes atengwe huku amefaulu?,
Lakini Mohamed Said atakuja na sababu za kidini!
Kimsingi hakuna sababu zilizomzuia Abdul Sykes kutoendelea na masomo zaidi ya KUFELI,
Maana kama akina Dr. HAMZA Mwapachu muislamu aliweza kuendelea na masomo iweje Abdul Sykes atengwe huku amefaulu?,
Lakini Mohamed Said atakuja na sababu za kidini!
Yericko,
Kwani kuna ubaya gani katika dini kiasi cha kunitishia?
Nimekusoma na ikiwa mjadala hapo ndipo ulipofika napo
si haba.
Nimekuuliza kuhudu Shariff Attas.
Duh! Haya sasa ni matusi ya waziwazi. Sina hakika Kama tumeamua kuweka busara pembeni au...
Nguvumoja,
Hakika sikujua kabisa kama historia ile niloandika
miaka mingi nikiwa kijana sana kama iko siku na
kwa bahati mbaya itazua mazito ya kufedhehesha
kama hivi.
Historia ya TANU itatulia tu pale utakapoiacha kama
ilivyotakiwa iwe.
Historia ya TANU inapata mtikisiko mkali ajabu pale
unapomleta marehemu Abdu Sykes na nyaraka zake
kuhusu African Association.
Hapo ndipo penye matatizo.
Mjadala umekosa heshima.
Sijui wanajamvi wenzangu mnasemaje.
Kweli ipo haja ya kuendelea na mnakasha?
Nguvumoja,
Hakika sikujua kabisa kama historia ile niloandika
miaka mingi nikiwa kijana sana kama iko siku na
kwa bahati mbaya itazua mazito ya kufedhehesha
kama hivi.
Historia ya TANU itatulia tu pale utakapoiacha kama
ilivyotakiwa iwe.
Historia ya TANU inapata mtikisiko mkali ajabu pale
unapomleta marehemu Abdu Sykes na nyaraka zake
kuhusu African Association.
Hapo ndipo penye matatizo.
Mjadala umekosa heshima.
Sijui wanajamvi wenzangu mnasemaje.
Kweli ipo haja ya kuendelea na mnakasha?
Julius Nyerere, lifelong learning and education. One of Africas most respected figures, Julius Nyerere (1922 1999) was a politician of principle and intelligence. Known as Mwalimu or teacher he had a vision of education and social action that was rich with possibility
Mkuu Nguruvi3, ni hapo ndipo kwa mbali tunapata fursa ya kupima upeo wa baadhi ya watu tunaojadiliana nao humu...kuna hii picha inajaribu kujengwa ya kuwaweka kwenye mizani Mwalimu Nyerere na Abdulwahid Sykes! Inafika wakati hata kunatolewa hoja eti ya kuwapambanisha kwa vigezo vya akili, uwezo na sifa. Ziko hata porojo zinatolewa eti Abdulwahid Sykes alikuwa ana akili kiasi cha kupata pass ya juu ya "first class" katika mtihani wa darasa la kumi! Hii yote inafanyika katika harakati za kumjenga na kumweka kwenye kundi la wasomi wa wakati huo!
Nguruvi3. mtu kufika darasa la kumi miaka ya 1940s ilikuwa ni mafanikio ya kujivunia, siyo tu kwa mhusika bali kwa jamii yote iliyomzunguka hadi kwa shule na waalimu waliomwandaa toka awali. Mtihani wa darasa la kumi la wakati huo ulijulikana kama Territorial Exam ambao ulifanywa na nchi zote zilizokuwa chini ya himaya ya Waingereza...ulikuwa ni mtihani uliokuwa na heshima kuliko hata degree ya sasa inayopatikana nchini kwetu sasa hivi. Mtu aliyeweza kupata "first class" aligombewa kama kuku wanavyogombea mahindi na nafasi za kuendelea zilikuwa nje nje na hazikujali uraia, rangi, dini wala ukabila...ni akili ya mtu tu iliangaliwa.
Kumbukeni pia wakati huo, masomo ya sekondari hayakuwepo, ukishinda vizuri ni moja kwa moja Makerere na kwingineko...ndio maana akina Dr. Hamza Mwapachu, Chief Kidaha Makwaia, Dr. Vedasto Kyaruzi na wengine wengi waliweza kuendelea mbele kwa masomo ya juu bila ubaguzi wowote. Hakuna, narudia, hakuna namna mhitimu wa darasa la kumi aliyefuzu vizuri kama inavyodaiwa kwa Abdulwahid Sykes kupata "division one" angeweza kunyimwa hiyo nafasi na badala yake akapelekwa vitani, hakuna, wakoloni walijali sana elimu na hasa intelligence ya mtu. Hata wale ambao hawakupasi vizuri kama inavyodaiwa kwa Abdul, walipata ajira nzuri tu katika utumishi sekalini.
Wanajamvi, lengo langu si kumdhalilisha mzee wetu Abdulwahid Sykes, lakini inafika mahala ukweli lazima utamalaki na hapa ni JF. Hata hivyo nakiri kuwa huenda ziko sababu maalum zilizomzuia Abdulwahid Sykes kuweza kuendelea na masomo ya juu zaidi...kama yupo anayeijua sababu hiyo naomba ajitokeze na sote bila shaka tutapima na kujiridhisha kwamba hapo kweli kulikuwa hamna namna. Kwenye miaka ya 1940s, jumla ya Watanganyika walioweza kumaliza darasa la kumi ilikuwa ndogo sana na aliyefaulu vizuri hakuhitaji kufanya jitihada zozote za binafsi kupata nafasi katika vyuo mbalimbali ndani na nje ya nchi.
Hii nayo ni hoja au topic mpya unaanzisha?
Mkuu kunauwezekano mkubwa kuwa mjadala huu hujauelewa ama hujausoma kabisa.
Naomba nikuulize,
Kitabu cha Mohamed Said kiitwacho Maisha na nyakati za Abdul Sykes umekisoma?
Kitabu cha historia ya TANU kilichoandikwa na chuo cha kivukoni umekisoma?
Je hoja yangu ya kupinga kitabu cha Mohamed Said umeisoma thread yote au umepitia nusu tu?
Nimelazimika kujua hayo baada ya wewe kuuliza swali hilo hapo juu!
Mimi nilidhani utajibu maswali yangu uliyoyawacha kiporo kwanza kabla hujaanza kuniuliza maswali mengine!!!
Kuendelea ama kutoendelea ni uamuzi wako tu mkuu,
Lakini kwakuwa unautetea uongo wako na uchochezi sitegemei kama utabanduka kwenye mjadala huu kirahisi!
Masuala yote ya AA na TANU tumeshayaeleza kwa ufasaha na tumefafanua kuwa ukoo wa akina Sykes haujawahi kuchaguliwa kuongoza chama chochote katika Tanganyika ama Tanzania!
Suali unalotakiwa kukaa nalo Mzee Mohamed Said ni kuwa, iweje wewe useme wao ndio waasisi wa AA,TAA, na TANU halafu hawakupata kuchaguliwa kuviongoza zaidi ya kukaimu tu?
Suala la Shariff Attas na Mwalimu Nyerere kama unavyotaka kunisimulia,
Kwanza mimi naona ni ngano isiyo na mafaa kwenye historia ya Tanganyika.
Tujadili ya maana kwanza kisha hadithi za nani alimpa chumvi ama kiberiti zitafuata!
Yericko,
Ikiwa yale umeona ni ngano basi hapana ugomvi.
Mwenyewe shariff angependa angeliweza "kumkumbusha" Nyerere
kuwa walikuwa wakifahamiana vyema lakini aliamua wabakie "hawajuani."
Ni haya tu ndiyo nilitaka kukueleza ingawa umenijibu kwa kibri.
Nikirudi katika historia...
Sishangai.
Nilikueleza hapo awali kuwa maswali yale sitayajibu,
Majibu ya mkuu Nguruvi3 yanatosha, sipunguzi wala kuongeza neno!
Yale uliyoyauliza kama maswali ya nyongeza kutokana na majibu ya Nguvuri3 sitayajibu kwakuwa hayana logic ya majibu ya hoja!
Bado majibu ya Nguruvi3 yanabeba maswali yako yote,
Mambo mengine jitafutie mwenyewe nyaraka na machapisho mbalimbali yahusuyo historia ya Tanganyika na ujisomee kwa mafaa yako na kizazi chako!
Sio kila kitu utafuniwe shekhe wangu!