Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Ndugu

Katika michango yako ya mwanzo kwenye uzi huu nilikutazama na kukutafasiri kama mmoja wa wanazuoni na mbobevu wa fikra za nera!

Lakini kwa aina ya ujumbe unaochangia kadiri mjadala huu unavyosonga ndivyo unavyonipa picha ya watu wa aina ya "ndio mzee"

Sitaraji na siamini kamwe kwa msomi na anaesimamia elimu yake ataunga mkono hadithi ya Atass kuwa ni sehemu ya historia ya uhuru wa nchi hii!

Kwanza nikujuze kinyume na Mohame kuwa huyo aitwae Sharif Atass hakuwa na "URAFIKI" na Mwalimu Nyerere kiasi cha eti mwalimu aishi miaka yote akimuweka akilini!

Hivi haikuingii akilini kuwa Mwalimu angemuweka akilini Sharif kwa lipi?

Kwakupiga ngano wote pale Kariakoo?

Jiulize Sharif Atass ni nani kwa Nyerere mpaka kiwe kisa chakusimuliwa na kiwe sehemu ya historia ya uhuru?

Ndugu yangu jisimamie kama ulivyoingia mwanzoni usibebwe na hisia!

Mjadala huu ni mzito kwakuwa ili uuelewe inakubidi hisia zako za kidini uziweke kando jambo ambalo wachangiaji wengi limewashinda na wewe ukiwemo!

Yericko,
Najua unasema hivyo kwa kuwa kuna mengi hujasikia kuhusu siasa
iliyokuwapo pale sokoni na nguvu iliyojikita TANU kutokana na watu
hawa.

Nyerere alikuwa haruhusiwi kula ovyo na ndiyo maana Shariff Attas
alikuwa kivuli chake wakenda kula pamoja.

Wakati ule Special Branch waliweka kambi nje ya ofisi ya Abdu...

Yericko wajukuu wa Shariff Attas wako Dar watafute wana mengi ambayo
iko siku utakapotaka kuandika historia ya baba yako yatakufaa.
 
Ndugu yangu Yericko sidhani kama ni busara sana kufurahia kwamba maandishi yako yamekuwa lulu kwa Wamarekani.
Hawa ndugu zetu ni mabeburu hawaoni tabu kutumia hila zozote kufikia malengo yao.Hawana rafiki wa kudumu wala adui wa kudumu.Tukikumbuka si zamani sana walimweka Mzee wetu Nelson Mandela katika list ya magaidi hatari,na wao wakashirikiana na makaburu kufanya madhila mengi kwa waafrika wenzetu.Mara tu baada ya makaburu kusalimu amri na Afrika kusini kuwa huru walibadilika na kurudi kumsifia sana Mzee wetu Madiba mpaka kumtaja kama kiongozi wa mfano duniani.

Usivutiwe sana na sifa zao ndugu yangu huenda wameona unafaa sana kwa sasa kueneza propoganda zao za ugaidi.

Yericko,
Hebu tufahamishe publisher wa kitabu chetu.
 
Yericko,
Najua unasema hivyo kwa kuwa kuna mengi hujasikia kuhusu siasa
iliyokuwapo pale sokoni na nguvu iliyojikita TANU kutokana na watu
hawa.

Nyerere alikuwa haruhusiwi kula ovyo na ndiyo maana Shariff Attas
alikuwa kivuli chake wakenda kula pamoja.

Wakati ule Special Branch waliweka kambi nje ya ofisi ya Abdu...

Yericko wajukuu wa Shariff Attas wako Dar watafute wana mengi ambayo
iko siku utakapotaka kuandika historia ya baba yako yatakufaa.
Hehee heeehee dah!

Mkuu Mohamed Said unanilazimisha sasa nizame kukijadili kisa hicho kwakutumia facts za kisomi na sio vingine,

Hebu twende taratibu,

Kwa kusema

"Nyerere alikuwa haruhusiwi kula ovyo na ndiyo maana Shariff Attas alikuwa kivuli chake wakenda kula pamoja".

Unamaana yakuwa Sharif Atass alikuwa mlinzi wa Mwalimu Nyerere??

Kama jibu ni ndio,

Kisa hicho hapo awali ulikitaja kuwa ni miaka ya 1950 na amini kuwa kipindi hicho Nyerere hakuwapo Dar na hakuwa kiongozi wa TAA hapa Dar je alimlindaje?

Kama ulinzi wa Sharif Atass kwa Nyerere ulianza baada ya Nyerere kuacha kazi ama kuchaguliwa kuwa rais wa TAA 1953, Je ulikoma baada ya Nyerere kuwa Rais wa Tanganyika?


Ngano za kutunga huwa ngumu sana kama unaowatungia ni mabingwa wa ngano pia!
 
Hapo ndipo mnapokosea sana. Kisa cha Shariff Attas kimewekwa ili tupate mazingatio, kuwa Nyerere alikuwa na tabia ya kuwasahau wahisani wake. Wewe upo kwenye kupeana vitu. Kuwa makini kuelewa maudhui Sio kusoma Kama hadithi simulizi.

Huyo dogo Yericko uwezo wake wa kuelewa mambo ni mdogo sana
 
Kuendelea ama kutoendelea ni uamuzi wako tu mkuu,

Lakini kwakuwa unautetea uongo wako na uchochezi sitegemei kama utabanduka kwenye mjadala huu kirahisi!

Masuala yote ya AA na TANU tumeshayaeleza kwa ufasaha na tumefafanua kuwa ukoo wa akina Sykes haujawahi kuchaguliwa kuongoza chama chochote katika Tanganyika ama Tanzania!

Suali unalotakiwa kukaa nalo Mzee Mohamed Said ni kuwa, iweje wewe useme wao ndio waasisi wa AA,TAA, na TANU halafu hawakupata kuchaguliwa kuviongoza zaidi ya kukaimu tu?

Yericko;
usiturudishe nyuma! historia ya Tanganyika sasa iko wazi na kila mwenye akili na ustaarabu hawezi kukubali kudanganywa tena na hisohistoria bandia za kumtukuza na kumsifia Nyerere tu ati katuletea uhuru! nikiwa shuleni msingi waalimu wa siasa na propaganda walituimbisha oo Nyerere,,,ameleta!!!! Kawawa,,,ameleta!!! na Jumbe,,, ameleta!!! uhuru wa Tanzania!!! angalia uongo huo!!! lini Nyerere, Kawawa na Jumbe wameleta uhuru wa TZ? la kuchekesha Jumbe alipochafua hali ya hewa mwaka 1984 na kulazimishwa kujiuzulu, wimbo huo wa kudai alileta uhuru wa TZ nao ukasimama!

Yericko;
Huu si wakati tena wa kuimbishwa zidumu fikra sahihi za Mwalimu! Wazee waliopigania uhuru wote wanajulikana! siasa za majitaka hazina nafasi karne hii ya 21! unaweza kudanganya umma kipindi fulani, lakini kuendelea kudanganya umma huo daima ni muhali!

Mohamed Said;

Nakuomba uendelee kutupa darsa kwani haki imesha dhihiri na wasiotaka haki wendezao! bado tunahitaji darsa lako adhimu la historia ya kweli ya Tanganyika na Zanzibar! nahakika una mengi ya kutujuza mbali na Tanganyika pia tuna hamu ya kujua mengi kuhusu Zanzibar na harakati zao za kupigania uhuru! Yericko na washirika wake wameshindwa kuthibitisha madai yao ya kukuhusisha wewe na uchochezi sasa wamebaki kurudia rudia na kuimba wimbo na ngonjera zisizokuwa na mwanzo wala mwisho! yaani hata ngonjera na mashairi yao hayakidhi masharti muhimu ya mizani na kimo!

Matusi na kejeli za baadhi ya wadau wachache yasikutishe! mpuuze yoyote anaekuja na kejeli au matusi kama unavyompuuza kubwa lao! hapa kuna umma unahamu na ghamu ya kuchota ilmu ili wende na kurudi tena! mahali tulipofika si haba tunamshukuru Mola! kaza kamba isikatike Mzee Mohamed!
 
Yericko;
usiturudishe nyuma! historia ya Tanganyika sasa iko wazi na kila mwenye akili na ustaarabu hawezi kukubali kudanganywa tena na hisohistoria bandia za kumtukuza na kumsifia Nyerere tu ati katuletea uhuru! nikiwa shuleni msingi waalimu wa siasa na propaganda walituimbisha oo Nyerere,,,ameleta!!!! Kawawa,,,ameleta!!! na Jumbe,,, ameleta!!! uhuru wa Tanzania!!! angalia uongo huo!!! lini Nyerere, Kawawa na Jumbe wameleta uhuru wa TZ? la kuchekesha Jumbe alipochafua hali ya hewa mwaka 1984 na kulazimishwa kujiuzulu, wimbo huo wa kudai alileta uhuru wa TZ nao ukasimama!

Yericko;
Huu si wakati tena wa kuimbishwa zidumu fikra sahihi za Mwalimu! Wazee waliopigania uhuru wote wanajulikana! siasa za majitaka hazina nafasi karne hii ya 21! unaweza kudanganya umma kipindi fulani, lakini kuendelea kudanganya umma huo daima ni muhali!

Mohamed Said;

Nakuomba uendelee kutupa darsa kwani haki imesha dhihiri na wasiotaka haki wendezao! bado tunahitaji darsa lako adhimu la historia ya kweli ya Tanganyika na Zanzibar! nahakika una mengi ya kutujuza mbali na Tanganyika pia tuna hamu ya kujua mengi kuhusu Zanzibar na harakati zao za kupigania uhuru! Yericko na washirika wake wameshindwa kuthibitisha madai yao ya kukuhusisha wewe na uchochezi sasa wamebaki kurudia rudia na kuimba wimbo na ngonjera zisizokuwa na mwanzo wala mwisho! yaani hata ngonjera na mashairi yao hayakidhi masharti muhimu ya mizani na kimo!

Matusi na kejeli za baadhi ya wadau wachache yasikutishe! mpuuze yoyote anaekuja na kejeli au matusi kama unavyompuuza kubwa lao! hapa kuna umma unahamu na ghamu ya kuchota ilmu ili wende na kurudi tena! mahali tulipofika si haba tunamshukuru Mola! kaza kamba isikatike Mzee Mohamed!

Kadogoo,
Nakushukuru kwa dua zako na maneno ya kunitia moyo.

In Sha Allah darsa itaendelea.
 
Umesema vema sana Mohamed, na hakika ndicho watu wanachokitaka kuwa hiistoria iachwe kama ilivyo.

Abdul alikuwa na wakati na mambo yake kama ilivyokuwa kwa Nyerere. Kuanza kuwaweak watu hawa katika mizani ni kuleta ulinganifu wa chungwa na embe kitu kisichowezekana. Tena chungwa na embe ni karibu sana labda niseme ni kiazi na nanasi.

Abdul alikwenda vitani hadi Burma alikoanzisha ''TANU'' na wala hakuwahi kuwa msomi wa kiwango cha chuo kikuu.
Nyerere hakwenda vitani wala Burma, hakuwa mtoto wa mjini 'townmen'', alikuwa mwanasiasa msomi na mwenye maono.
Alikuwa na kipaji chake na kwa namna inayoacha alama ya yeye kutajwa kila siku miaka 14 baada ya kifo chake.

Umejaribu sana kufanya hivyo, eti Abdul ana akili na Nyerere ni debater mzuri. Ukaleta ulinganifu wa mambo kadha wa kadha huku ukijitahidi sana kumdunisha, kumdhalilisha na kumfarakanisha Nyerere ili nyota ya Abdul ing'ae.
Narudia hawa ni watu wenye viwango visivyofanana.

Endapo ungemjibu Mag3 maswali yake ya jana na juzi ungeweza kuona wapi unajikanganya. Hilo ukaona litaharibu kila kitu na umeamua kurukia hoja za spelling.

Historia ipo wewe ndiye unataka kuipindua. Ukweli ni kuwa Abdul Sykes alikuwepo, alikuwa katibu wa TAA na mambo mengi tu alishiriki. Nyerere alikuwepo ndiye alikuwa Rais wa kwanza wa TANU na Tanganyika huru.Ndiye alifanya transformation ya chama
Jaribio la kutaka kumfanya Abdul awe Rais wa Tanganyika linapingana sana na hoja yako ya leo.
Hakuwa na hatakuwa, tunamshukuru sana kwa machango wake.

Kuhusu mnakasha kuwa na matusi, aaah Mohamed ! Matusi umeyaona leo. Wewe ulimshangilia sana Zali la Mentali alipoanza kuporomosha mitusi. Wengine tukakaa pembeni maana ilm hiyo hatuna.

Iache nyuzi ijifunge yenyewe kwasababu matusi umeshangalia yalipoletwa hata sisi wengine tukahoji utu uzima ni dawa kumbe wakati mwingine inaweza kuwa utu uzima ni mghafala.

Hivi huyu Nyerere aliyeuza uhuru wetu kwa kugeuzwa kibaraka wa Wamarekani, Waingereza na Kanisa Katoliki ndiye mnayemsifia kiasi hiki bila haya? Huyu ambaye aliendeleza ukoloni wa Watanganyika na baadaye Wazanzibari kwa kuruhusu wakoloni waendelee kutunyonya baada ya wao kushindwa kuendelea kufanya hivyo kutokana na mapambano ya Watanganyika na Wazanzibari dhidi ya wakoloni?

Upande wa Kanisa Katoliki nan chi za magharibi kumtumia Nyerere kuendeleza Mfumo Kristo nimeshauelezea. Sasa angalieni jinsi Nyerere alivyokuwa anatumiwa kama Condom na mataifa ya magharibi kwa ajili ya kutunyang'anya uhuru wetu uliopatikana kwa jasho kwa kufuatilia makala hii Justifying the role of imperialism in Africa - World Socialist Web Site

Huyu Nyerere HAFAI hata kupewa kumbukumbu kwa kuupa jina mtaa ulioko Manzese kwa Mfuga Mbwa.
 
Suala la historia ya Zanzibar ni mtambuka sana unahitaji kuisoma historia kwa utulivu sana,

Ukikurupuka utaibuka na histohisia za akina Mohamed Said ambao wanadai Mapinduzi yale Matukufu yalikuwa ni dhidi ya uislamu na sio dhidi ya ukoloni wa sultan!
 
Sioni sababu yakuganda hapa,

Kuhadhiri katika vyuo vyao si jambo laajabu,

Lakini nakueleza kuwa nimefika Pentagon kwaajili ya hiyo ngano yangu,

Nimeonana uso kwa uso na Bob Bequen, Mayers na waambata wengine ndani ya pentagon!

Maandishi yangu yamekuwa lulu kwao kiasi cha wao kuniomba haki shiriki kwa kukidurufu kwa lugha sita duniani kutoka lugha mama ya Kiswahili!

Haya sio mafanikio yangu bali ni waswahili wote ukiwemo wewe!

Yericko;

we kiboko! mwenzetu ulialikwa Pentagon! Jee, ulipiga picha na wenyeji wako? naomba tubandikie picha ulizopiga huko kama unazo tafadhali!
 
Isalia,
Shariff Attas hakuwa na wadhifa wowote katika TAA wala TANU ukitoa kuwa alikuwa mwanachama
na mmoja wa wanachama wa mwanzo katika TANU.

Yeye alikuwa dalali wa Soko la Kariakoo ambako Abdu Sykes ndiye alikuwa Market Master.
Hii ilikuwa 1950s kipindi cha mapinduzi katika TAA na wakati Abdu yuko katika pilika ya kuasisi TANU.

Lakini umuhimu wa Shariff Attas kwanza ni kuwa alikuwa mmoja wa wanamji na kubwa zaidi soko zima
lile likiendeshwa na watu maalum katika kila biashara.

Kwa ajili hii palikuwa na fedha za kutosha kuingizwa katika harakati.
Sasa hapa ndipo unapomkuta Mshume Kiyate dalali wa samaki.

Mshume alihodhi biashara hii na alitajirika kiasi kuwa aliweza peke yake kujitolea kumuhudumia Nyerere kila
kitu hadi uhuru ulipopatikana.

Hata Nyerere alipomwambia Mzee Mshume kuwa sasa apumzike yeye atahudumiwa na serikali Mzee Mshume
alimgomea Nyerere akamwambia, "Mimi nataka wewe na wanao mle chakula changu na hicho cha serikali wape
wageni wako."

Yapo mengi ya hawa wapigania uhuru waliosahaulika.
In Sha Allah tutaambizana kila nafasi ikipatikana.

Unajua ile dua ya akina Jumbe Tambaza walomfanyia Nyerere yeye hakuwa wa kwanza katika viongozi wa TANU
kufanyiwa.

Ile dua wa kwanza kufanyiwa alikuwa Abdu Sykes.
Sijui kama wanajamvi wangependa kusikia mkasa huu
.

MS;

Hapo umewashika pabaya! patamu hapo! endelea Mzee!
 

Shukran kwa kuiweka hiyo link,mimi nilishawahi kuiona.

Kama nilivyowahi kueleza katika mojawapo ya bayana zangu za awali hapa jamvini,yakuwa hili suala la Palestine,Non Alignment Movement na masuala ya Polisario ni baadhi ya vitu vichache mno nilivyokua nakubaliana na Nyerere. Japo sina hakika na motives zake,khususan kutokana na historia yake na vitimbi vyake kwa yale mengine alokua akifanza.

Kwa mfano kushiriki kwake kikamilifu katika mauaji ya kinyama/massacre ya Matabeleland. Sio WaTanzania wengi wanaofahamu yakuwa Nyerere alishiriki kikamilifu katika mauaji yale ya kikatili na kumuunga mkono kupita kiasi Robert Mugabe dhidi ya Joshua Nkomo na Wanachi wengine wa Zimbabwe. Nyerere/Tanzania ilipeleka Wanajeshi 350 kushiriki katika mauaji yale machafu dhidi ya raia wengi wasio na hatia wakiwemo wanawake,vikongwe na watoto.

Tukirejea katika suala la Palestine;ni aghalab kumkuta well learned Christian/Catholic hasa anaejua kwa kina masuala ya Medieval History,Anthrolopolgy,Contemporary History,Current Affairs,halafu awe anawakubali au kushirikiana na Israel kwa karibu mno. Nyerere alikua ni mahiri katika hayo majambo na pia alikua ni Mkristo/Mkatoliki mtiifu mno.

Mayahudi na Vatican,hawa ni maadui wa asili. Lakini uadui wao ulikithiri khasa katika ile Slave Trade. Vatican inafahamu fika yakuwa Mayahudi ndo watu pekee wanaojua siri zao za ndani. Na ndo hao hao Mayahudi wanaowachafua kila siku kwa kutumia kupitia mainstream media wanazohodhi.

Ndo maana katika ule mkutano wa JFK na Nyerere,hao Wakatoliki wawili walikumbushana pia "wajibu wao" wa kupambana na Jewish Lobby kwa kila njia.

Tunajua kabisa yakuwa JFK hakuwa mtu mwenye historia ya sympathy,empathy au hata mawasiliano mazuri na Civil Right Movements. Tafauti kabisa na Bobby Kennedy. Mara nyingi akina Tom Mboya walikua close na Senator Richard Nixon kuliko JFK. Lakini utaona ghafla baada ya Tanganyika kupata uhuru,na maagizo maalum kutoka Vatican kwenda kwa JFK ndipo utakuta ile connection ya Nyerere pale ilipokolea mno.

Kwa wale wajuba msotaka kusikia,jaribuni kupitia Barack Obama - The Story,JFK Biography by Prof. Michael O'Brien na nyaraka/sources nyingine mbalimbali na mtabainisha mengi.

Nilipitia baadhi ya Threads hapa JF,nikakuta malumbano fulani ya kidini na jinsi "jamaa fulani" anavyojaribu kuonyesha "mantiki" na kupambanua "hoja" zake ili kuhalalalisha yakuwa Tanzania ni bora iwe na mahusiano na Israel ati ili Wakristo waokoke na kupata misaada toka kwa "ndugu zao"! Ilinilazim kucheka.

Kwa kifupi,Rais ali Hassan Mwinyi alifanza mengi mno mazuri lakini nae katika yale machache ambayo sikubalianai nae ni hili suala la kurejesha uhusiano wetu kwa karibu mno na Israel. Niliwahi kumuuliza Bwana Jabir(alikua Private Secretary/Special Advisor wa Mwinyi) kuhusu habari hii ,akanijibu ati "ililazim" kufanza hivyo maana walishinikizwa!? Sina hakika maana hakunambia nami sikuona haja ya kumuuliza na nani au kwanini!?

Niliwahi kukutana na baadhi ya jamaa "Waandamizi" walioongozana na ujumbe wa Baloz Ali Idd pale Tel Aviv wakti fulani. Jinsi nilivyowasikia mazungumzo yao nilipatwa na butwaa...ni watu ambao hata nilianza kushuku viwango vyao vya elimu na uelewa wao wa mambo ya kimataifa. Wifey wangu ni Austrian Jew na tulikua pamoja. Aliwahi kuniuliza hivi kwanini hawa watu wanafuatana na Viongozi wakubwa kama hivi,tena kwenye misafara ya kimataifa kama hii lakini inaelekea kuna vitu hawavijui kabisa!? Wallahi nilitahayari pasi kiasi!

Kwa kifupi walichachafywa mno na "vijana waduchu waduchu" kutoka Israel Ministry of Foreign Affairs,mpaka ikaonekana kuwa hao jamaa ni kuwa walifanza tu ile trip bila hata ya maandalizi ya kutosha au kujua walifata nini pale!? Japo sipo hapo nyumbani kitambo,lakini nahisi Tanzania tunaeleka pabaya!!?

Ahsanta.
 
Mkuu Jasusi, kuna mambo mengi sana yameongelewa na yanayoonyesha jinsi gani imani zinavyowagawa Watanzania.

Lakini pia tumeona msimamo wa Nyerere anayetuhumiwa sana kuwa mkatoliki na kuhujumu imani nyingine, alivyofikia mahali pa kusema hatakwenda Jerusalem akipitia Israel! Kwa maana ya kuwa kwake utu ndio ulikuwa mbele zaidi ya watumia dini ambao waliingia kutaka kumlainisha kwa gia ya dini zao.

Inahitaji moyo mgumu sana kukataa hoja ambazo majibu yake hayahitaji hata darasa bali mantiki.

Kuna kitu kimenigusa sana, nacho ni ile shule ya Temeke.
Hakika wale wanafanya kazi ya jamii na dini na kama ningelikuwa katika position ya serikali ningewasaidia kwa namna yoyote.Wao wanaangalia mayatima halafu wanawapa silaha ya kupambana na uyatima siku za usoni ''ILM'

Tena wamesoma mazingira na kugundua kuwa wanatakiwa wawaingize vijana wao katika dunia ya ushindani.
Kwamba kila mtu apate fursa ili kuweza kuweka level ya ushindani.

Ukimwangalia yule binti mdogo aliyekuwa anaongea, yeye mawazo yake ni kusoma afanikiwe ili aweze kuweka mkate mchana na jioni mezani kwa ndugu zake.

Focus yake ni kufanikiwa na tayari ameshaji tune kwasababu ameona kuwa uwezekano wa kuondokana na hali hiyo ni kwa kupitia kusoma ''nitasoma nipate kazi ninunue chakula.....''
Huyu birnit anahitaji kulindwa tu kwasababu tayari yupo ''fire'' na future yake.

Ndiyo maana kila siku huwa nasema tunahitaji watu wa kuibadili society in positive way.
Kwamba mtu anaweza ku-instill confidence kwa desparate people kama hao watoto walioondokewa na wazazi wao.

Sasa inapotokea vijana kama hao wakaambiwa mafanikio yao yatafifishwa na NECTA kwasababu ya majina au hijabu zao, huo ni upotoshaji wa hali ya juu sana na ni kuwavuruga kimawazo na kuwajengea dhana chafu sana vichwani mwao.

Sakina Datoo ni role model wa vijana wengi na wa aina na itikadi mbali mbali.
Nasema kuwa amejaribu sana na kwakweli vizuri sana kuandaa documentary hiyo.
Ukiangalia mpangilio unapata picha ya mtu aliyefanya homework yake vizuri.
Kuna mapungufu pengine katika maswali lakini hayo ni ya kibinadamu.

Sakina ana hijabu yake na Mwalim Saddika anahijabu yake wote wanaongelea mambo mazito yanayoigusa jamii.
Kwa wale mabinti pale Temeke nadhani yupo aliyesema ''nataka niwe kama Sakina'' hiyo ni motivation kwamba anaweza kuwa Sakina bila kuathiri imani au itikadi yake na akafanya vema tu.

Sasa ukitaka kuwapotosha vijana wale, wakalishe chini uwaambie kuwa kwavile wanavaa hijabu basi chuo chao kikuu kilichokuwa kijengwe mwaka 1968 (hata wengine baba zao hawajazaliwa) ndicho kitakuwa kikwazo kwao.

Bilal comprehensive wameweza kufanya hilo tena katika mazingira magumu.
Wanatoa lishe na elimu hapo hapo kwa kutambua kuwa bila lishe nzuri hakuna elimu.

Kwanini basi Mohamed asifikirie kuwa huenda tatizo la Kilwa nalo linahitaji approach nyingine?
Kwanini watu wasikae chini na kuangalia kulia na kushoto, bali waishie kutengeneza vitabu, CD za matusi na mikoba ya Ibadan kana kwamba hilo ndilo suluhisho la tatizo.

Nadhani video hii imeonyesha japo kwa kiwango fulani kile ninachokisema hapa kuwa tatizo na suluhu ipo ndani ya waislam na wala si katika Uislam au nje ya waislam. Ndivyo wanvyofanya Shia, Ismailia, Bohora n.k.

Sijui kwanini wengine wanasugua vichwa kujenga chuki, farki, uongo hata kubeba mikoba hadi Ibadan Kupitia Murtala Mohamed Airport tena mchana ili hali wanajua wazi kuwa suluhisho lipo mikononi mwa wadau na wala si mtu mwingine.

Hebu msikilize mama Saddika halafu wasikilize akina nani hii.
Utajua kuwa elimu siyo certificate ni jinsi gani unaitumia kukabiliana na mazingira yako.

Kwamba kama kuna mtu anadhani elimu ni ghali basi ajaribu ujinga na kwamba ni wakati wa kutenda si projo, tamthilia, hadithi ngano na mikoba ya Ibadan.

''It can be done play your part''

Ni kweli elimu siyo certificate ndio maana tunasema ingawa Nyerere alisoma lakini certificate yake haikumsaidia pale alipoamua kuwapendelea Wakatoliki waziwazi dhidi ya dini na madhehebu mengine ya Kikristo na pale alipokubali kutumika kama Condom na wakoloni ili kuuza uhuru wa Watanganyika na baadaye Wazanzibari.

Kuhusu kusahau yaliyopita ili tugange yajayo, huo msemo ni sahihi tu kama utafahamu wapi tulipopita? Huwezi kujua njia unayotakiwa kupita kama hujui hapo ulipo ulitokea wapi. Ndio maana kazi za watu kama Mzee Said ni kazi za msingi sana sana kwa ajili ya maendeleo yetu ya mbeleni. Jua kwanza ulitokea wapi na wapi ulijikwaa. Ndipo utaweza kujua njia gani unatakiwa uende ili upate mafanikio yanayotarajiwa.
 
Yagawe utakavyo lakini moja ni kigano vingi ni vigano au ngano!

Sideeq,

Salaam

Huyu jamaa kila kukicha heshi kujinasib na Kiswahili na Uswahili,lakini anazidi kujinyambua na kujinanga kwa wale wenye kujua.

Tafadhali asikushughulishe.

Shukran.
 
Hehee heeehee dah!

Mkuu Mohamed Said unanilazimisha sasa nizame kukijadili kisa hicho kwakutumia facts za kisomi na sio vingine,

Hebu twende taratibu,

Kwa kusema

"Nyerere alikuwa haruhusiwi kula ovyo na ndiyo maana Shariff Attas alikuwa kivuli chake wakenda kula pamoja".

Unamaana yakuwa Sharif Atass alikuwa mlinzi wa Mwalimu Nyerere??

Kama jibu ni ndio,

Kisa hicho hapo awali ulikitaja kuwa ni miaka ya 1950 na amini kuwa kipindi hicho Nyerere hakuwapo Dar na hakuwa kiongozi wa TAA hapa Dar je alimlindaje?

Kama ulinzi wa Sharif Atass kwa Nyerere ulianza baada ya Nyerere kuacha kazi ama kuchaguliwa kuwa rais wa TAA 1953, Je ulikoma baada ya Nyerere kuwa Rais wa Tanganyika?



Ngano za kutunga huwa ngumu sana kama unaowatungia ni mabingwa wa ngano pia!

Yericko,
Kibri kimefunika hata hiyo elimu kiduchu ulokuwanayo.

Ndiyo maana umefikishwa mahali umetukanisha hadi wazazi wako.

Punguza ujuvi utajifunza mengi katika maisha ya awali ya baba yako
kutoka kwangu.
 
Nimekuja ukumbini kufyonza Ilm siyo kufyonza matusi, Mzee Mohamed Said tunakuomba chonde chonde usiondoke ukumbini endelea kutudarasisha kuhusu historia yetu tanganyika.
 
Back
Top Bottom