shukran MS nipo hapa tangu mwanzo wa mnakasha huu kuchota ilm ni vizuri na ni kheri kutuletea huo mkasa kujifunza popote tu
Isalia,
Katika vitu ambavyo vilinipa tabu katika kuandika kitabu cha Abdu Sykes ilikuwa lipi niliseme
lipi niliache.
Katika moja ambalo nililiacha kulisema ni hili la kafara walofanya wanaharakati wa TANU pale
Soko la Kariakoo kumhami Abdu Sykes dhidi ya Afisa wa Kiingereza aliyekuwa akimuamdama
kwa sababu ya uongozi wake katika TANU.
Shariff Attas anasema kuwa iko siku huyo afisa Mzungu alimvamia Abdu ofisini kwake na akakuta
Abdu ana kadi za TANU.
Abdu Sykes alikuwa akiuza kadi zile za TANU pale sokoni nyingene akiwapa jamaa kuzisambaza na
kuwaita wananchi kujiunga na chama.
Shariff Attas anasema siku ile kulikuwa na raha ya pekee kati ya Muingereza na Abdu.
Abdu alikuwa na ulimi mzuri wa kuzungumza Kiingereza na lile zogo kati ya Abdu na Mzungu lilifanyika
mbele ya watu wakiwasikiliza wakiparurana.
Yule Mzungu alihisi kafedheheka kwa hiyo alitunga uongo kuwa ofisi ile inatumiwa dhidi ya serikali na ikawa
Abdu sasa anatakiwa ajibu shtaka lile akishindwa afukuzwe kazi.
Soko liliwaka moto wanaharakati pale sokoni hawa akina Shariff Attas, Mshume Kiyate, Shariff Mbaya Mtu na
wengine wakawa sasa wanakwenda mbio kutafuta vipi wamsaidie Abdu dhidi ya njama za Waingereza.
Ndipo ikaamuliwa lifnywe kafara zito la kumzika kondoo mzima pwani huku kavishwa sanda na macho katobolewa.
Yalioyompata Mzungu yule naogopa hata kusema...
Abdu alibaki kazini.
Sasa Nyerere alipoanza kuandamwa na serikali ndipo ikaamuliwa ifanyike kafara kama ile ya Abdu Twining akomeshwe.
Isalia,
Historia ya uhuru ina mengi sana.
Sasa hawa wenyewe ukizungumza nao katika mambo haya kule kuamini kwao kwa ''silaha'' hizi na hisia zao zilikuwa juu
kiasi wewe msikizaji unaogopa kulichimba zaidi.
Ndiyo maana lile kafara na Nyerere ambalo mwenyewe alilieleza katika hotuba yake ya muago na hili kafara la Abdu Sykes sikutaja katika kitabu changu.