Muheshimiwa Mag3,
Tatizo ni yakuwa tuna mitazamo tafauti,ambalo pia ni jambo jema sana khasa kitaaluma.
Lakini tatizo jingine linipalo dhiki na madhila mengi,ni yakuwa nakuhisi wewe ndugu yangu Mag3 ni Mbaguzi wa rangi. Jambo ambalo ni hatari na khasara kwa Taifa letu changa.
Hayo majedwali yako hapo juu mimi binafsi na wewe ndugu yangu twajua yakuwa hizo informations/statistics ni fake na ni upotoshwaji wa Historia mkubwa mno!
Lakini napenda fursa kwa leo nirejee kiduchu kwenye huo ubaguzi wako wa rangi. Hivi Mag3 na wenzio woote hapa jamvini tangia lini mmeanza kuwa na Imani,huruma,majonzi,empathy,sympathy,sikitiko na labda pia kufikia kilio cha "ndugu zenu WaZanzibary Weusi"!? Halafu hizi definitions zenu za "Arabs","Africans","Bantu","Comorians" na mengineyo mengi,ndio mwanzo wa machochezi na kuhatarisha amani ya nchi.
Kuna baadhi ya Thread humu ndani nimeona ati huyo Mwanakijiji,amefikia hadi ya kujipa dhamana na authority ati ya kujua ni kiwango gani cha senti,hao WaZanzibary walipwe ili watolewe kwenye muungano!? Yaani imefikia huyo Mwanakijiji anajifanya yeye ni Fiscal Activist na kupangia Taifa/WaZanzibary kiasi gani cha senti wapewe ili waondoshe "gubu lao" kwa WaTanganyika!? Ama kweli hapa JF pana viroja vingi mno!
Ndo maana mimi binafsi,huwa nakuoneni yakuwa wengi wenu ni Wazandik tu. Yaani mnakuwa upande wa WaZanzibary pale tu inapo-suit matakwa na vigezo vyenu vya kibaguzi!? Sisi watu wa Madrassa hiyo tunaita Fitnatil Al Maaarifa.
Haya si ndo mambo mlokua mkimfanyia kebehi Sheikh Mohammed hapa jamvini,alipokua akitaja baadhi ya Makabila ya wenye mji/Wazee wetu hapo Mzizizma!?
Kama nilivywahi kunena hapo awali,haya majambo ya Race Issue ni very complex subject. Inalazim muwe waangalifu japo kiduchu,khasa mnapokua kwenye Public Forum kama hapa.
Mimi nina personal experience kutokana na family background yangu,kwa hiyo nazungumza kitu ninachokifahamu kwa undani na khatari zake kwenye Family au Taifa letu.
Kwa kumalizia napenda kama kipata fursa japo kiduchu,rejea baadhi ya bayana zangu za awali khasa ile niliyokua nikijadiliana na ndugu yangu Nyambala,na nilijaribu kuweka tahadhari kwa Taifa letu WaTanzania,kwa kutumia kigezo/mfano wa nchi ya Sudan.
Lazim leo ninene hapa barazani;yaani kuna wakti nafikira kama siku tukijaaliwa kukutana popote pale basi hata mimi pia waweza kuniona au kuniita yakuwa sio MTanzania/MTanganyika, khasa kutokana na hizo definitions zenu za urangi na Makabila. Jana nilikua nawasomea wanangu/wajukuu zako ambao ni viduchu mno khadith za kulalia/bed time reading. Basi ghafla nikakukumbuka wewe Babu yao Mag3,je utakubali kuwa wao nao pia ni WaAfrika/WaTanzania siku ukiwaona/wakija kukuamkua!?
Kaa chini kwa utuvu ufikirie haya majambo kwa kina...huna haja ya kujilazimisha kujibu kwa pupa na zogo. Tumia busara nyingi ulonazo kwa utaratibu na madhubuti.Insha Allah tuendelee na mnakasha,na nakutakia w'end njema.
Ahsnata.Cc;Ritz
Gombesugu nami nakuamkua huko ughaibuni ulipo. Je, kulikoni?
Naona umeguswa sana na suala la rangi. Nikufahamishe kuwa suala la rangi kwa ZNZ ni jambo ambalo huwezi kuliepuka katika siasa zake. Nadhani unajua kuwa hivi karibuni wapo viongozi waliotoa kauli za kuonyesha wazi urangi ulivyotamalaki visiwani.
Ni suala la historia na litabaki kama lilivyo kwasababu uwezo wa kupindua historia haupo isipokuwa kwa wachache waliojaaliwa. Ili kuipindua historia inabidi ujivike joho la uongo, fitna al maarifa kwa kutumia CD,paper au vitabu. Vyovyote iwavyo historia inabaki kama ilivyo na huko visiwani Urangi ni sehemu yake.
Kuna mahali umemgusa Mwanakijiji kuhusu masuala aliyoongelea ingawa umepindisha kidogo ili kutoa taswira unayoitaka na siyo iliyoongelewa.
Nalazimika kuingia hapa kwasababu katika nyuzi hiyo aliyochangia Mwanakijiji nami pia nilichangia.
Na hapa naweka rekodi sawa.
Aliyeleta hoja ya kugawana kila kitu pasu kwa pasu ni mzanzibar.
Mzanzibar huyo alidai kuwa muungano ukivunjika itabidi kugawana kila kitu kwa kuzingatia kuwa BoT ina mtaji wa 12.5%.
Katika majibu na langu likiwemo, tulisema kuwa hiyo haina taabu lakini basi kila kitu kiwekwe mezani.
Kwamba znz haijawahi kuwa na bajeti ya ulinzi na usalama, elimu ya juu, imekuwa inapata 7% zamani 4% ya pato la taifa, huduma za bure kama umeme, mishahara ya wastaafu, mishahara ya wafanyakazi wa SMZ hadi masheikh, kuziba nakisi ya bajeti ambayo ni pengo mara 3 kuliko pato la znz n.k.
Pesa zote hizo zinatoka Tanganyika na kwa Watanganyika kwasababu znz haina uwezo.
Haina uwezo kwa kuzingatia kuwa pato lake la mwaka ni bilioni 120 ambazo haziwezi kuendesha wizara ya mambo ya ndani ya muungano au basi hata vikosi viwili vya jeshi.
Kwa mantiki hiyo, 12.5 ya znz itawekwa mezani, lakini haitaishia hapo itabidi na makando kando mengine yawekwe mezani pia ili haki itamalaki. Kwa msingi huo znz itajikuta inalazimika kulipa na si kulipwa.
Hapo ndipo inaposemwa kuwa znz waondoke katika muungano salama salimini hawana kitu cha kudai, vinginevyo watakuwa wanakaribisha matatizo. Ili kuondoa Gubu wao waende zao taratibu.
Hapo hakuna suala la fiscal activist ni suala la ukweli na kama ni uongo, basi hebu tufahamiane wapi unapodhani kuna wahka ulioleta staftashi katika kiwango ulichoonyesha.
Kuhusu znz kutumika pale penye ''mafao''kwa Watanganyika, nadhani hilo halina ukweli.
ZNZ haina mafao na Mtanganyika ya aina yoyote.
Suala la muungano lipo wazi kuwa kama wamechoka na wanaona wanaonewa, basi wao kwa pamoja na viongozi wao waondoke Tanganyika warudi kwenye nchi yenye neema.
Ingawa wzn wengi wasingependa muungano uvunjike kwa manufaa wanayoyapa, hilo halizuii wao kuamua hatima yao wakitaka.
Lakini pia usisahau kuwa suala la Urangi linakuzwa sana na wzn wenyewe. Wanapomwita Karume Mnyasa, Mwinyi Mndengereko n.k. maana yake wanawagawa watu wao.
Kwamba ili uwe mznz halisi lazima uwe na nywele za ''katani'' midevu ya nguvu at least kuonyesha una unasaba mwingine na si wandengereko au Wanyasa.
Hapo ndipo ftina al maarufu ilipo kwahiyo kumlaumu Mag3 kwa kuweka anayoyafahamu kuhusu historia si kumtendea haki.Unapaswa uwasote vidole wzn ambao hutambuana kwa rangi kwanza.
Na mwisho, pengine uwaase wznz wenzako kuwa hizi habari za mkafir n.k. ndizo zinazozaa hisia za urangi.
Kwamba ukitoka bara ni chogo, na kama umezaliwa visiwani ni chogo mdogo.
Asiye chogo lazima awe na yale niliyoyasema hapo, ikiwa ni pamoja na karangi ka kiarabu japo kwa kuibia.
Khair Inshallah basi mjulie hali ahli wako na vijana.
cc. Al-akhyi wote,waungwana,wanajamvi na 'makafir'