Yericko Nyerere,
Kila siku siku zote napenda kukushauri pinda mgongo ufundishwe na wajuvi wa historia kama
Mohamed Said, hebu angalia unavyojichanganya hapa na hii historia yako kwa faida ya Wanaukumbi ngoja ni dadavue kiduchu bayana zako.
Wanaukumbi hapa tunaambia Sheikh Issa kazaliwa mwaka 1846 halafu amekutana na Askofu Maranda mwaka 1948 kwa hiyo tunaona Sheikh Issa alikuwa tayari na umri wa miaka 102. mtu mwenye umri huu anaweza kweli kufanya harakati za siasa mfano mdogo tu Nelson Mandela saizi ana umri wa miaka 94.
Wanaukumbi hapa tena Yericko anajichanganya tena, AA iliundwa mwaka 1929 tukiangalia mwaka huo Sheikh Issa atakuwa na umri wa miaka 83, kweli umri huu mtu anaweza kuwa na nguvu ya kuvua samaki.
Wanaukumbi hapa tena Yericko anajichanganya mwaka 1954 Sheikh Issa alikuwa na umri wa miaka 108, ha haa ha, hebu hapa chini tumsome Nyerere mwenyewe kwenye hotuba yake ya kuanga wewe unasema habari za mwaka 1954 Nyerere mwenywe anasema habari za mwaka 1952, ha haa haa, hizi bayana zina tashtit.
Julius Nyerere."Mimi nimeanza siasa na wazee wa Dar es Salaam; na wazee wa Tanzania. Nimeanza nao mapema sana; mapema kweli. Nilirudi kutoka masomoni, Uingereza Oktoba 1952 miaka 33 nyuma. Wakati huo nikiwa kijana mdogo wa miaka thelathini na kidogo hivi.
Julius Nyerere"
Ninasema yote haya kwa shukrani kwa wazee. Jamaa hawa walikuwa watu wazima wa Dar es Salaam, na mimi kijana mdogo Mzanaki, na Kiswahili changu si kizuri sana cha matatizo.
Nimekuja, natoka Ulaya, tena masomoni. Muda mfupi tu jamaa hawa wakaniamini haraka sana katika muda wa miezi mitatu. Wakanichagua Rais wa TAA. Hapo ndipo nilianza shughuli mpya ya kuandika katiba ya TAA na kuipa madhumuni hasa ya shabaha ya kuleta uhuru.
Siku moja, Dosa akanifuata Magomeni (Dar es Salaam). Akasema: Leo wazee wanakutaka. Wapi? Kwa Mzee Jumbe Tambaza. Wanakutaka usiku. Nikasema haya, nitakuja. Nikaenda. Nikakuta wazee wameshakaa; wameniita kijana wao kuniombea dua. Mimi Mkristo, wao Waislamu watupu. Wakaniombea dua za ubani. Tukamaliza.
Huyu Sheikh Issa ameishi vipi vyote kuanzia AA, TAA. TANU, CCM maana ujasema alifariki lini.