Yericko Nyerere
JF-Expert Member
- Dec 22, 2010
- 17,005
- 20,425
- Thread starter
-
- #16,561
Kulia lia haitakusaidia hapa watu hawabishani ni hoja juu ya hoja, naona umekurupuka utadhani umefumaniwa.
Umehamaki bure mpaka hautaki mimi niishi Tanzania umenitafutia mpaka sehemu unataka kunipeleka nikaiishi kisa nimemjibu Mkirsto mwenzako.
Njoo na hoja hao uliowataja ndiyo unawaogopa na ndiyo wanakushikia akili yako wewe kweli bat.
Kama ni hoja kwa hoja, nakujuza kuwa hoja hizi hapa chini zimekosa majibu kutoka kwenu!
Kwa wanajamvi wote;
Ni muhimu sana maswali yaliyoulizwajuu ya Zenj na Mapinduzi yakajibiwa kwa usahihi stahiki ili tuweze kupata hatua ya kutufikisha kuona kama kweli mzee MS anafanya uchochezi kama Yericko alivyodai. Maswali viporo ni kama ifuatavyo;
1. NANI ALITANGULIA NA AGENDA YA KUMPINDUA SULTAN NA KUMUOMBA MWENZIE MSAADA?, NI TANU AU ASP?/ JEE ASP WALILAZIMISHWA MSAADA NA TANU?
Jibu la swali hili litajenga msingi wa umiliki wa MAPINDUZI. Tunahitaji majibu
2. Mapinduzi haya ni halali au haram? Yaani sababu wanazotoa ASP kuhusu wao kumpindua Sultani ni za KWELI/UONGO?
Hapa lazima ieleweke kuwa tunaposema halali tunaangalia sababu za kupindua siyo idadi za walipoteza maisha au mali. Ili kuziba nafasi ya kupotosha hapa ni kuwa tunapounga mkono NATO katika kumpiga Hitler (WW2) tunaangalia sababu za kuingia vitani, siyo idadi ya waliopoteza maisha pande zote za uhasama. Principle hiyo ndiyo tunaitumia kuuliza.
Majibu yalenge sababu za ASP sio hisia
Maswali ya Nguruvi;
3. Tuhuma zinazojengwa ni kuwa Nyerere alitumiwa na Kanisa ili kuihujumu zenj. Kitabu cha Kwaheri Uhuru.... na CIA report (100 days.....Zanzibar) zote zinaonyesha ASP wakitafuta na kupokea silaha toka serikali ya TANU kwa agenda yao wanayoijua.
SWALI; Wao ASP walikuwa vibaraka wa Kanisa lipi wakati wanayashughulikia haya tunayoyasoma
4. Kumeonyeshwa katika Kitabu (kwaheri Uhuru...) waZenj wakienda Kipumbwi wanafundishwa uaskari kisha wanarudikwao kusubiri. Hivyo pia wenziwao wa Kipumbwi.
SWALI; Nani alikuwa na dhamana ya askari wote (aina mbili) juu ya nidhamu yao kama askari walipokuwa Zenj kwenye hilo jukumu lao? Yaani kamanda-in-chief wao alikuwa nani wakiwa Zenj wakati wa mapinduzi?
Maswali mengine yatafuata. Tunataka kwanza haya yajibiwe ili tujue shutuma dhidi ya Rais wa Tanganyika dhamana yake kwa maisha ya wazenj wakati wa Mapinduzi haya kama yana MASHIKO.
cc Painkiller, Nguruvi, Mohammed Said, Mag3, Nanren, BigShow, Jasusi, Jokakuu, Sheikh Farid,Nicholas, Prishaz, Son of Alaska, Cool runnings, Spike Lee,Ritz,Kadogoo, Yericko, Mr Iron.