Mkuu Nicholas,Mwanahistoria wetu Sheikh Mohamed ametutajia majina mengi ya wazee wetu na baadhi bado wako hai kwa nini hamuendi kuhakiki ukweli wa aliyoandika?Mzee Bilali Waikela,Tewa Saidi Tewa,Selemani Ngozi wote wapo hai mkuu nendeni mkahakiki mje mtujuze,msitokwe na mapovu tu bila ushahidi wowote.
Mwezi wa sita huu tupo tunafuatilia mtuonyeshe uchochezi uko wapi lakini hatuoni bali tunashuhudia mnavyodhihirisha chuki zenu dhidi ya uislamu na waislamu.
Uthman,
Ndugu yangu hawa jamaa hawana kitu.
Mie nimewashauri mara nyingi sana waandike kitabu cha historia hiyo
ambayo wao wataridhikanayo.
Wanakesha JF kupambana na kitabu abacho kipo sokoni huu sasa mwaka
wa 16 na tunaingia toleo la tatu.
Sisi tulikaa kimya miaka kadhaa wakati ikitamba historia ya TANU ile ya
Kivukoni College iliyowatoa wazee wetu wote.
Mimi sikutokwa povu hata siku moja.
Niko pale Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam mwanafunzi nasikiliza kebehi
za walimu wangu na nikizijibu kwa makini sana.
Wakati mwingine nauliza, ''Jamani mmepata kumsikia
Mshume Kiyate,
Sheikh Hassan bin Amir, Sheikh Suleiman Takadir nk. nk.''
Nawaeleza hadi kuwatajia namba zao za kadi za TANU hazizidi digit 2.
Kwanza walimu wakinipuuza lakini baada ya kuona yale niliyokuwa yote
nikyamwaga pale yalikuwa mageni kwao baadhi ya walimu zangu wakawa
sasa wananisikiliza kwa utuvu chembelecho
Gombesugu.
Ndipo nilipoamua kuandika historia hii iwe jibu kwa historia ya Chuo Cha
Kivukoni.
Kama wasemavyo Wazungu ''the rest is history.''
Sasa halazimishwi mtu kuamini haya nisemayo wala hii haiwezi kuwa sababu
ya sisi kutukanana.
Ikiwa unataka kuamini kuwa Nyerere kakutana na
Abdu Sykes na
Nyerere kaja
pale ana TANU yake sawa.
Mimi nani nimkatalie?
Lakini iwepo nafasi vilevile ya kuieleza TANU kwa mwelekeo usio huo.
Msiktukataze kuaianza TANU 1929 na
Kleist Sykes.
Ikiwa mtu anataka
Sheikh Hassan bin Amir na TAA Political Subcommittee asitajwe
katika historia ya TANU sawa hapana ugomvi lakini asizuiwe mtu mwingine kueleza
historia ya TANU Jimbo la Kusini akamtaja
Sheikh Mohamed Yusuf Badi na
Masoud
Mnonji na
Bi Shariffa biti Mzee.
Hii ni nchi huru alazimishwi mtu chochote kile uhuru wa mawazo unahakikishwa.
Ukitaka kuianza historia ya TANU kutoka Musoma ruksa, ukitaka kuanza historia ya
TANU Burma ruksa!
Mwasemaje wanajamvi wenzangu?
Wakati umefika wa kuanua jamvi au tuendelee na mieleka?