Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Ritz,
Baada ya Nyerere kupokea barua kutoka kwa waajiri wake
wamishionari kuwa achague moja kati ya mawili.
Achague kazi ya ualimu au siasa Nyerere alipeleka barua ile
kwa Clement Mtamila aliyekuwa Mwenyekiti wa Halmashauri
Kuu ya TANU.
Kikao kilifanyika nyumbani kwa Mzee Mtamila Mtaa wa Kipata
na Sikukuu.
Uamuzi ukapita kuwa Nyerere ajiuzulu kazi aajiriwe na TANU.
Nyerere alipojiuzulu kazi alikaa kwa muda nyumbani kwa Abdu.
Kisha Mzee Rupia ndipo akamtafutia nyumba Magomeni.
Ndiyo hiyo nyumba uliyoiona sasa Makumbusho.
Historia ya namna hii tuikubali tu yaishe. Wewe endelea kuwa "Authority" juu ya historia hii. Umesimuliwa peke yako hakuna namna ya kuzithibitisha simulizi hizi. Ulikosea sana kutotafuta KATIBA au miongozo ya AA, TAA, TANU na huenda hata katiba ya CCM haujapata kuiona!
Ulikosea Mzee Mohamed. Hivi swali kama hili utalijibu vipi: TAA ilianzishwa kwa madhumuni na malengo yapi? Utalijibu vipi swali hili bila kuiona katiba ya TAA? Simulizi za baadhi ya walioianzisha ni ushahidi tosha?WC,
Sijakosea chochote kuhusu kuitafuta katiba kwa kuwa sikuwa na shughulinayo.
Nimekaa Maktaba ya CCM Dodoma na katika orodha ya vitu nilivyokwenda kuvisaka
katiba haikuwapo katika orodha yangu.
Kama wewe unaona ina umuhimu itafute utujuvye.
Mimi sihitaji ithbati ya simulizi za baba yangu kutoka kwa yoyote.
Itakuwa kichekesho kuwa mimi nisimuamini baba yangu nije nimsikilize mpita njia.
Hivi kwa nini historia hii inakushughulisheni kiasi hiki?
Si inatosha nyie mkaipuuza?
Hili vipi linakushindeni?
Waliweza kuishi na vyama hivi bila KATIBA? Tunataka katiba ili tujue kwa uhakika vyama hivi vilianzishwa kwa madhumuni, imani na malengo gani.
Ni muhimu pia pale unapokataa kuwa AA na TAA havikuwa vyama vya starehe katiba zao ziwe ndio ushahidi sio kitabu chako cha mwaka 1998! Ambacho kimejaa simulizi tu za watu ambao karibu wote ni marehemu.
Ulikosea Mzee Mohamed. Hivi swali kama hili utalijibu vipi: TAA ilianzishwa kwa madhumuni na malengo yapi? Utalijibu vipi swali hili bila kuiona katiba ya TAA? Simulizi za baadhi ya walioianzisha ni ushahidi tosha?
Historia hii inatushughulisha kwa kuwa unadai ni ya NCHI na TANU yetu. Au TANU ni mali ya wazee wako tu!
TANU imeanzishwa na WATANGANYIKA wengi. Wale wazee 17 akiwemo Abdu na Mwalimu walitusaidia kuiasisi bila kutumwa na DINI zao.
Ninachokukatalia mimi ni kuwa AA haikuwa TAA; na TAA haikuwa TANU kama ambavyo CCM sio TANU wala ASP. Kila chama kiliundwa kwa madhumuni, imani na malengo tofauti. Wewe unataka AA iwe ndio TAA iwe ndio TANU. Katiba za vyama hivi zinavitenganisha sana. UONGOZI pia ulikuwa tofauti sana. Nyakati pia zilikuwa tofauti.WC,
Nashangaa vipi wewe katiba ya African Association unaidai kwangu.
Mie nakataa AA hakikuwa chama cha starehe.
Labda nikuulize swali dogo.
Hivi wewe ulitegemea waasisi wa African Association waseme kuwa
chama hiki ni cha siasa na madhumuni yake ni kuikomboa Tanganyika
kutoka kwa ukoloni wa Waingereza.
Hii ni mwaka 1929.
Hebu jitulize na fikiri kabla ya kuuliza maswali kama haya.
Haya na tujaalie kuwa African Association kilikuwa chama cha kupiga taarab
kwani hilo litaondoa zile kazi chama kilifanya hadi kuunda TANU mwaka 1954?
Narudia kukufahamisha tena.
Mimi sitaki ushahidi wa yoyote.
Nitake ushahidi kuthibitisha kitu gani?
Ikiwa unahisi mimi sijaandika kweli si na wewe uandike kitabu chenye kuonyesha
makosa ndani ya kitabu changu?
Unadhani kama mimi nisingejibu kitabu cha Kivukoni kwa kitabu leo tungekuwa hapa?
Andika.
Humtambulisi kama mwanamke wa Kiislamu... kwanini?
Huyu mama wa Kiislamu inaonekana alitoa mchango mkubwa kama wa Mshume Kiyeta lakini hata jina la mtaa halipo; maskini wa Mungu.
Duh; kumbe nilidhani wamesahauliwa Waislamu tu; kumbe wapo na wauza pombe waliotoa mchango mkubwa katika kuijenga TANU. Inabidi hawa nao wakumbukwe isije kuwa Nyerere alikuwa na jambo dhidi ya kinamama wauza pombe.
Nashukuru sana Mohamed Said nimejifunza kitu...Hakika una vitu vingi sana nazidi kuchota.
Ninachokukatalia mimi ni kuwa AA haikuwa TAA; na TAA haikuwa TANU kama ambavyo CCM sio TANU wala ASP. Kila chama kiliundwa kwa madhumuni, imani na malengo tofauti. Wewe unataka AA iwe ndio TAA iwe ndio TANU. Katiba za vyama hivi zinavitenganisha sana. UONGOZI pia ulikuwa tofauti sana. Nyakati pia zilikuwa tofauti.
Ninachokukatalia mimi ni kuwa AA haikuwa TAA; na TAA haikuwa TANU kama ambavyo CCM sio TANU wala ASP. Kila chama kiliundwa kwa madhumuni, imani na malengo tofauti. Wewe unataka AA iwe ndio TAA iwe ndio TANU. Katiba za vyama hivi zinavitenganisha sana. UONGOZI pia ulikuwa tofauti sana. Nyakati pia zilikuwa tofauti.
Mzee Said, kuna wakati ambapo Dossa Aziz na Mtevu walikuwa wanagombea wakiwa pande mbili tofauti? Naomba utusimilie kidogo kisa chao.
MM,
Usihangaishwe na Dossa na Mtemvu.
Mohamed Said atakuletea ngano tu.
Mzee Said, kuna wakati ambapo Dossa Aziz na Mtevu walikuwa wanagombea wakiwa pande mbili tofauti? Naomba utusimilie kidogo kisa chao.
Nashukuru sana Mohamed Said nimejifunza kitu...Hakika una vitu vingi sana nazidi kuchota.
Kuna elimu kubwa sana kwenye huu mjadala.