Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 21,967
- 32,074
MS kama kawaida yako mzee wangu nimeorodhesha hapo vitabu vitano na waandishi wake na vyote si riwaya. Dinesh D'souza au Glen Beck hawaandiki riwaya. Wewe ulipoona tu majina ya kina Musiba, Hammie Rajab na Shigongo tayari unataka kupindisha hoja. Hawa mm niliwataja kwa sababu ndiyo wanafahamika na watanzania wengi.
Na hao vijana wanaotaka kuandamana mimi niko pamoja nao, lakini tu wasisite kuleta ushahidi yakinifu wa namna gani NECTA inabagua kwa mgongo wa dini.
N,
Tusibishane kuhusu riwaya ni mtazamo tu pale ulipokichanganya
kitabu changu na hivyo vya riwaya.
Para yako ya mwisho ndiyo nzito.
Nitakumegea kuhusu NECTA.
Vimefanyika vikao kadhaa na yaliyokutikana yanafanyika NECTA
yanatisha.
Kikao cha mwisho hawakuruhusu mtu kutoka na karatasi yoyote
nje ya chumba cha mkutano.
Yote tunayosema Waislam ni kweli tupu.
Kinachofanyika sasa ni kujaribu kuwasihi Waislam wasizianike zile
hujma ati kwa maslahi ya umoja wetu.