MM,
Wewe ni mtu mmoja.
Nashukuru nazungumza na wewe.
Lakini mimi fikra na mawazo yangu
nimeelekeza kwa hawa 60,000+
wanaotusikiliza.
Wengi hawakupata kusikia haya
ninayoeleza humu JF.
Hawa ndiyo walengwa wangu na
wala nia yangu si kuwa waniamini.
Lengo langu wasikie Waislam tunasemaje.
Hapa ndipo huwa sikuelewi kabisa, hivi kwanini unalazimisha mawazo yako yawe mawazo ya waislam? Mohamed akisema ni waislam, Ponda akisema ni waislam, Ilunga akisema ni Waislam, UAMSHO wakisema nao ni waislam wanasema. Kwa mwenendo huu hivi mnaitendea dini haki kweli! Na kwa mwendo huo mnaupa uislam nafasi gani katika jamii na dunia!
Maufunzo ya dini kweli yanasema hivyo kuwa kila mtu atoe kauli kwa niaba ya waislam.
Uislam ni dini yenye muongozo wake hata ukifuatilia hadithi au sunna utaona wanazuoni maarufu walikuwa wakisema kama wao na si Uislam kwasababu Uislam unasimama bila fikra za mtu.
Hatari ya kuchukua maoni na maono ya watu kama ndio dini ya uislam imeufikisha Uislam katika kuonekana tofauti na ulivyo. Leo kuna watu wamefanya Ijumaa kama siku ya maandamano. Hakuna mahali popote penye aya, hadithi au sunna inayosema hivyo, kama ipo basi naomba waislam waiweke hapa tufaidike sote.
Sidhani kama waislam wote wanaosoma vitabu vyako wanakubaliana na hoja zako, na kama si hivyo, je , hao unawaweka kundi gani?
Hii dhana ya kutanguliza jina la dini ili kukidhi haja za kibinadamu na si za kidini ni hatari na mbaya sana. Ni dhana ile ile inayofanya watu wajifunge mabomu na kulipua abiria kwa mwanvuli wa Uislam. Ni dhana hiyo ndiyo inapelekea watu kwa mitazamo yao wafarikiane kwasababu tu kila mmoja ni mwislam zaidi ya mwingine.
Ni kwanini Shia wawalipue Sunni kwasababu tu wametofuatiana tafsiri za dini, hadithi na hata mahalifa au maimam!
Huko nyuma umesema waislam walisimama kupinga dhulma ya wakoloni. Leo tunafaham kuwa miongoni mwao walifasadi asset za AA na nyumba aliyotoa mkoloni D.Cameron. Sasa unapoutanguliza Uislam kama kinga ujue wakati huo huo unauweka katika wakati mgumu.
Uislam haukueleza watu wapinge dhulma ya mkoloni halafu wafanye dhulma ya asset za AA!
Mohamed, jaribu kutofautisha dini, uumini na Uislam na mambo mengine ya mwanadamu.