Mag3,
Nakushukuru kwa taarifa hizi.
Niachotaka uzingatie ni hili.
Hayo yote yaloandikwa hapo ndiyo yakijulikana siku zote.
Sasa mimi nilipokuja na kitabu changu ndipo ikajulikana kuwa
kumbe ile haikuwa historia yote.
Yapo mengine ambayo hayakuwa yamewekwa wazi na khasa
nafasi ya Waislam katika kupigania uhuru wa Tanganyika.
Wasomi siku zote hupenda kupata tafiti mpya.
Kitabu changu kilikidhi haja ya utafiti mpya na hapo ndipo ikawa
sasa Abdulwahid anaingia na ukimuingiza yeye inabidi umtie na
baba yake na historia ihame 1954 ianze 1929 Kleist alipoasisi AA.
Historia irudi nyuma 1933 pale Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika
ilipoasisiwa na viongozi walewale waliosisi African Association.
Kwa mwanafunzi yoyte wa historia hapa atajiuliza maswali mengi tu.
Kwa ufupi ndiyo unaona sasa kitabu kikapata umaarufu na ''reviews''
hadi katika Cambridge Journal of African History.
TANU haukuasisiwa St. Francis College.
Huo ni muhali.
Ikiwa unataka kuamini kuwa Nyerere kaja Dar es Salaam mgeni mno
kawa na fedha na ofisi na watu wa kuwasemeza na akaunda TANU
mimi sina uwezo wa kubadili fikra zako.
Lakini kaa ukijua kuwa hata kama Nyerere angetaka kuanzisha TANU
nyumbani kwao Musoma au Butiama asingeweza.
Dossa na Abdu walifilisika kwa ajili ya TANU na harakati za kudai uhuru.
Chama hakiasisiwa kwa siku mbili.
Kuasisi chama ni mchakato mrefu.
Ilichukua robo karne kuitoa African Association hadi kufikia TANU.
Soma hapa chini umsikie Kleist anasema nini kuhusu harakati zile:
[TABLE="class: MsoNormalTable"]
[TR]
[TD="colspan: 2"]
Abdulwahid now 30 years old, had accomplished the ambition of his lifetime, an ambition which had originated from his late father, who 25 years before had predicted a continuous struggle between the Africans of Tanganyika and the colonial state.
Kleist Sykes had foretold the role of the next generation.
In a letter he wrote in 1933 to Mzee bin Sudi, then president of the African Association, Kleist at the tender age of twenty-nine years had this to write:
[/TD]
[TD="width: 59"][/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 59"][/TD]
[TD="width: 601, colspan: 2"][/TD]
[/TR]
[/TABLE]
[TABLE="class: MsoNormalTable"]
[TR]
[TD][/TD]
[TD="width: 601, colspan: 2"]
''Let us struggle with all our hearts towards
the path of civilization just like other tribes
are doing.
It does not matter if we do not accomplish
everything.
Those who will come after us will finish the rest.'' [1]
[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
[1] See Buruku, op. cit. p. 105.
[TABLE="class: MsoNormalTable"]
[TR]
[TD]
Msome: Duverger, Maurice, Political Parties: Their Organisation
and Activity in the Modern State, John Wiley and Sons, New York,
1963 [/TD]
[/TR]
[/TABLE]
Hizo taarifa ulizobandika hebu fananisha na haya nilokuwekea kutoka kwe ''wenyewe''
walioasisi TAA na TANU kisha jisikize wewe mwenyewe.
Wajuzi wa historia ya Afrika waliposoma haya hawakustahamili...
Nilikuwa nimekuja na mambo mapya kabisa.
Walinitafuta.