Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Mgashi,

Ni vizuri wewe umejua msimamo wetu Waislam na sisi tumesikia jinsi unavyoziona
shida zetu.

Haya yote yatakujatufaa huko mbeleni itakapofika mahali kuwa ni lazima tuzungumze.

"itakapofika ni lazima tuzungmze"-----YOU WISH!!!!!---- hii tone yako ni kama umeipa ultimatum serikali-yaani unajiongopea mpaka inakua reality in your head
 
Mtafiti tunaomba udhibitisho wa hapo kwenye red.. Ili tuweze kuwakata ulimi wale wasemao maandishi yako ni Histohisia na Ngano.

Remote,

Kutoa uthibitisho si kwa sababu ya ''kuwakata ulimi'' uthibitisho kama upo
ni bora kuutoa kwani unaongeza ithibati ya kauli.

Katika jambo kama hilo ni uthibitisho gani unaoutaka?

Mimi sijaingia hapa kutaka ushindi la hasha.
Nia yangu ni kueleza yale ambayo wengi hawakuwa wanayajua.

Remote je wewe binafsi umefaidika au hujafaidika na darsa zangu?
 
Nisamehe kwa kukukwaza Sheikh, na ndio maana nikasihi; USINIELEWE VIBAYA.

Winama,

Hayo yamepita.
Najua hapa zinaongea key board hunioni.

Laiti ungeniona na ukajua umri wangu...
nina hakika ungeanisemeza kwa adabu.

Uliza tena swali lako Insha Allah nitakujibu.
 
Remote,

Kutoa uthibitisho si kwa sababu ya ''kuwakata ulimi'' uthibitisho kama upo
ni bora kuutoa kwani unaongeza ithibati ya kauli.

Katika jambo kama hilo ni uthibitisho gani unaoutaka?

Mimi sijaingia hapa kutaka ushindi la hasha.
Nia yangu ni kueleza yale ambayo wengi hawakuwa wanayajua.

Remote je wewe binafsi uefaidika au hujafaidika na darsa zangu?

watu wengi humu wanatoa darsa tunafaidika,tatizo ni wakikubana mbavu unasema "tusifuatanefuatane" matokeo yake unatuacha wanafunzi katika "limbo"
 
"itakapofika ni lazima tuzungmze"-----YOU WISH!!!!!---- hii tone yako ni kama umeipa ultimatum serikali-yaani unajiongopea mpaka inakua reality in your head

Son...

Hapana.
Tupo jirani sana na mazungumzo.

Nadhani unasikia hizo kamati za masheikh na maaskofu kujadili amani.

Ikifika wakati kuwa masheikh wanasema hawana cha kuzungumza na
maaskofu bali serikali...

Hapo tutakuwa tumevuka kizingiti kikubwa sana.

Mimi sina uwezo wa kuipa ''ultimatum'' serikali.

Lakini nina uwezo wa kufanya ''prediction'' na hiki ni kitu ambacho mtu
yeyote anaweza kukifanya kwa kuangalia mambo yanavyokwenda.

Baada ya Sheikh Hassan bin Amir kufukuzwa palipita kipindi kirefu mambo
yakifanywa chinichini hadi leo mkutano wa mfumokristo umefanywa Diamond
Jubilee Hall na ukarushwa mubashara (live) na Radio Imaan na Waislam nchi
nzima wakajua kuwa mambo yamewiva.
 
Haya ndio majibu ya kihuni mnayoyatoa mkibanwa wewe na mzee wako Mohamed Saidi. Kwakweli sijawahi kuwaona watu wanafiki na waongo kama ninyi!

Hebu kunywa maji kwanza munkari ushuke kisha tuendelee na munakasha.
 
watu wengi humu wanatoa darsa tunafaidika,tatizo ni wakikubana mbavu unasema "tusifuatanefuatane" matokeo yake unatuacha wanafunzi katika "limbo"

Son...

Mimi siogopi kubanwa mbavu.
Unacheza miereka vipi utaogopa kuangushwa chini?

Yule jamaa nimemwambia maneno yale kwa kuwa si
muungwana.

Mbona wewe hunipi muda wa kupumua na tunajadili?
 
Mgashi,

Hatutanii haya mambo ni kweli.
Itatufaa kitu gani sie kuzua uongo mzito kama huu.

Ndugu zanguni tunakusihini hebu nanyi fanyeni uchunguzi.
Mkiujua ukweli tutasaidiana kuondoa fitna hii.

Tukijaamka mambo yeshavurugika tutakuwa tumechelewa.
Mgashi ansema hivi hebu tuambie nani ni Dr, Lawyer, Mwalimu, Mhandisi ambaye amenyimwa kazi kwa dini yake. Kwamba kazi ipo lakini kwasababu ni mwislam kanyimwa tu!

Hivi Ramadhani Dau yupo pale kwasababu ya utaalam au kwasababu ya dini yake? Hivi Gharib Bilal ambaye ni mtaalam wa Nyuklia alipewa umakamu kwasababu ya dini yake au maarifa yake ya uongozi.

Hivi Dr Bushir Ally ni mhadhiri kwasababu ya utaalam au kwasababu ya dini yake.
Othman Chande ni Jaji kwasababu ya dini au utaalam wake.

Prof Haroub alikuwa pro kwasababu ya dini au maarifa yake.
Lipumba anakubalika hata katika mfumokristo wa dunia , hivi maarifa yake ni ya dini au utaalam wake.
Kupewa uenyekiti wa tume ya uchumi ya dunia kulitegemea chapuo la Mohamed Said au ni kukaa chini na kutumia akili yeke vema kwa busara na adabu kwa faida yake na taifa lake.

Mohamed dunia ya leo ni ya ushindani, unachotakiwa ni kuwaambia watu wawe washindani si kuwadanganya! dhambi kubwa sana! Unajua kuwa unachokisema ni uongo lakini bado unarudia kwakujua kuwa uongo ukirudiwa rudiwa unakuwa ukweli. Hata kama una mhalifu mwenyezi, hiyo ni jihad ! Real

Kesho utalalamika kwanini Standard charter, Uniliver n.k hakuna waislam. Mwaka unaofuata utalalamika kwanini Tumaini University na KCMC hawajiri waislam wengi. Mwaka unaofuata utahoji kwanini idadi ya waislam world vision ni 1:6

Kwamba wewe ni mtu wa kutafuta sababu na si suluhu, wewe ni mtu wa kuangalia mkristo kafanya nini si mwislam kafanya nini. Wewe kila kukicha unafikiri kipi kipya ili utunge hadithi na farki.

Mwangosi kauawa, Saroga kawekewa Tindikali, Kibanda yupo south, Ulimboka kang'olewa meno, maalbino wanauawa, padri kauawa hayo yote hayashughulishi fikra zako kuwa kuna ukiukaji sheria wa hali ya juu, jicho lako lipo kwa vijana wawili walioko magereza waliokamatwa kwa kuvaa kanzu!

Who said kanzu ni Uislam! come on!
Come up with evidence tupo hapa kujadili hilo.
 
Kuwa na adabu kijana na kauli zako unaweza kuwa unamjibu mtu ambaye amesoma na mzazi wako wa kike au wa kiume na wamesaidiana vitu vingi shuleni na kwenye mabweni.

it doesn't matter.. Nawe unaona ulichojbu ni sahihi hapo juu!
 
Haya ndio majibu ya kihuni mnayoyatoa mkibanwa wewe na mzee wako Mohamed Saidi. Kwakweli sijawahi kuwaona watu wanafiki na waongo kama ninyi!

Gwalihenzi,

Yawezekana hujui.
Lakini ni hivi.

Mnapokuwa katika majadiliano kuna lugha huwezi kutumia kwa kuwa ni matusi.
Mathalan kumwita mtu ''mnafiki,'' ''muongo'' nk.

Hiyo kwa mtu muungwana anakuwa hakujibu na ndiyo mwisho wenu.
Mimi naamini si kila mtu anaweza kuwa kapitia adab kama hizi.

Lakini amini usiamini mimi hizi ''etiquetes'' nimejifunza madras nikiwa na umri mdogo.
 
Mgashi ansema hivi hebu tuambie nani ni Dr, Lawyer, Mwalimu, Mhandisi ambaye amenyimwa kazi kwa dini yake. Kwamba kazi ipo lakini kwasababu ni mwislam kanyimwa tu!

Hivi Ramadhani Dau yupo pale kwasababu ya utaalam au kwasababu ya dini yake? Hivi Gharib Bilal ambaye ni mtaalam wa Nyuklia alipewa umakamu kwasababu ya dini yake au maarifa yake ya uongozi.

Hivi Dr Bushir Ally ni mhadhiri kwasababu ya utaalam au kwasababu ya dini yake.
Othman Chande ni Jaji kwasababu ya dini au utaalam wake.

Prof Haroub alikuwa pro kwasababu ya dini au maarifa yake.
Lipumba anakubalika hata katika mfumokristo wa dunia , hivi maarifa yake ni ya dini au utaalam wake.
Kupewa uenyekiti wa tume ya uchumi ya dunia kulitegemea chapuo la Mohamed Said au ni kukaa chini na kutumia akili yeke vema kwa busara na adabu kwa faida yake na taifa lake.

Mohamed dunia ya leo ni ya ushindani, unachotakiwa ni kuwaambia watu wawe washindani si kuwadanganya! dhambi kubwa sana! Unajua kuwa unachokisema ni uongo lakini bado unarudia kwakujua kuwa uongo ukirudiwa rudiwa unakuwa ukweli. Hata kama una mhalifu mwenyezi, hiyo ni jihad ! Real

Kesho utalalamika kwanini Standard charter, Uniliver n.k hakuna waislam. Mwaka unaofuata utalalamika kwanini Tumaini University na KCMC hawajiri waislam wengi. Mwaka unaofuata utahoji kwanini idadi ya waislam world vision ni 1:6

Kwamba wewe ni mtu wa kutafuta sababu na si suluhu, wewe ni mtu wa kuangalia mkristo kafanya nini si mwislam kafanya nini. Wewe kila kukicha unafikiri kipi kipya ili utunge hadithi na farki.

Mwangosi kauawa, Saroga kawekewa Tindikali, Kibanda yupo south, Ulimboka kang'olewa meno, maalbino wanauawa, padri kauawa hayo yote hayashughulishi fikra zako kuwa kuna ukiukaji sheria wa hali ya juu, jicho lako lipo kwa vijana wawili walioko magereza waliokamatwa kwa kuvaa kanzu!

Who said kanzu ni Uislam! come on!
Come up with evidence tupo hapa kujadili hilo.

Nguruvi,
Nimekusoma.
 
Mgashi ansema hivi hebu tuambie nani ni Dr, Lawyer, Mwalimu, Mhandisi ambaye amenyimwa kazi kwa dini yake. Kwamba kazi ipo lakini kwasababu ni mwislam kanyimwa tu!

Hivi Ramadhani Dau yupo pale kwasababu ya utaalam au kwasababu ya dini yake? Hivi Gharib Bilal ambaye ni mtaalam wa Nyuklia alipewa umakamu kwasababu ya dini yake au maarifa yake ya uongozi.

Hivi Dr Bushir Ally ni mhadhiri kwasababu ya utaalam au kwasababu ya dini yake.
Othman Chande ni Jaji kwasababu ya dini au utaalam wake.

Prof Haroub alikuwa pro kwasababu ya dini au maarifa yake.
Lipumba anakubalika hata katika mfumokristo wa dunia , hivi maarifa yake ni ya dini au utaalam wake.
Kupewa uenyekiti wa tume ya uchumi ya dunia kulitegemea chapuo la Mohamed Said au ni kukaa chini na kutumia akili yeke vema kwa busara na adabu kwa faida yake na taifa lake.

Mohamed dunia ya leo ni ya ushindani, unachotakiwa ni kuwaambia watu wawe washindani si kuwadanganya! dhambi kubwa sana! Unajua kuwa unachokisema ni uongo lakini bado unarudia kwakujua kuwa uongo ukirudiwa rudiwa unakuwa ukweli. Hata kama una mhalifu mwenyezi, hiyo ni jihad ! Real

Kesho utalalamika kwanini Standard charter, Uniliver n.k hakuna waislam. Mwaka unaofuata utalalamika kwanini Tumaini University na KCMC hawajiri waislam wengi. Mwaka unaofuata utahoji kwanini idadi ya waislam world vision ni 1:6

Kwamba wewe ni mtu wa kutafuta sababu na si suluhu, wewe ni mtu wa kuangalia mkristo kafanya nini si mwislam kafanya nini. Wewe kila kukicha unafikiri kipi kipya ili utunge hadithi na farki.

Mwangosi kauawa, Saroga kawekewa Tindikali, Kibanda yupo south, Ulimboka kang'olewa meno, maalbino wanauawa, padri kauawa hayo yote hayashughulishi fikra zako kuwa kuna ukiukaji sheria wa hali ya juu, jicho lako lipo kwa vijana wawili walioko magereza waliokamatwa kwa kuvaa kanzu!

Who said kanzu ni Uislam! come on!
Come up with evidence tupo hapa kujadili hilo.

Nguruvi3,

Nimependa uchambuzi wako muruwa.

Naomba utupe "Ratio" ya Waislam na Wakirsto tukianza na Wizara ya Mambo ya Ndani, Wizara ya Ujenzi, Wizara ya Fedha, Wizara ya Afya, na Wizara zingine.

Halafu tupe "Ratio" ya Waislam na Wakisto Mawaziri na Manaibu wake.

Halafu tupe "Ratio" ya Waislam na Wakirsto Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya.

Halafu tupe "Ratio" ya Waislam na Wakirsto Makatibu Wakuu wa Wizara.
 
Gwalihenzi,

Yawezekana hujui.
Lakini ni hivi.

Mnapokuwa katika majadiliano kuna lugha huwezi kutumia kwa kuwa ni matusi.
Mathalan kumwita mtu ''mnafiki,'' ''muongo'' nk.

Hiyo kwa mtu muungwana anakuwa hakujibu na ndiyo mwisho wenu.
Mimi naamini si kila mtu anaweza kuwa kapitia adab kama hizi.

Lakini amini usiamini mimi hizi ''etiquetes'' nimejifunza madras nikiwa na umri mdogo.
Mohamed Said, unalalamika bila kujali madhara makubwa yatakayoletwa na mahubiri yako ya chuki kwa watanzania! Madai unayoyatoa yamechambuliwa kwa undani na ufasaha na huyu mtanzania mwenzetu, lakini wewe ukatoa majibu ya kihuni! na bado unadai tukuheshimu kwa lipi hasa? ebu jaribu kusoma tena busara hii;
Na lipo sio moja, kuna mengi. Lakini duara ni kubwa sana ukitaka tu-breakdown matatizo ya nchi hii kulingana
na Rangi, Dini, Kabila na eneo hutakosa la kukuunga mkono.

Tuseme hivi:
Hakika Wahindi na Waarabu katika nchi wana afueni sana, lakini Wamatumbi kama sisi wengi wetu dhoofu hali.
Walioko jela wengi weusi, wanaokula mlo mmoja tu kwa siku wengi weusi n.k n.k.

Waislam wengi tu (Ismailia, Bohora) wana afueni na mambo yao Alhamdulillah yamewanyookea kwenye Elimu na hali. Lakini Waislam wa Kilwa, Rufiji, Kisarawe hali si hali. Halafu rudi kwa Waislam wa Machame mambo yao si mabaya kulinganisha na hao wengine ingawa si mazuri sana kama Ismailia/Bohora!

Njoo kwenye kanda, Kusini si bora sana Kielimu na Kiuchumi kuliko Kaskazini na Nyanda za juu kusini. Lakini hapohapo Kaskazini Manyara wako nyuma kuliko Arusha na Kilimanjaro. Hata mkoa wa Kilimanjaro, Moshi iko mbele kuliko Same.

Unataka na makabila?
Wanyakyusa wako vizuri kielimu kuliko Wagogo. Lakini Wanyakyusa wa Rungwe wako vizuri zaidi ya wale wa Chunya!

Sasa Humo kwa Weusi utakuta Wakristo, Waislam, Wachaga, Wanyakyusa, Wasukuma n.k.
Kwa Kanda utakuta Weusi, Weupe, Wakristo ,Waislam, Wasukuma, Wadengereko n.k
Kwenye dini utakuta kuna Weupe, Weusi, Wasukuma, Wachaga , Wadengereko nk n.k
Na kwenye kabila Hao woote juu pia wamo.

Ndio maana nakushauri toka kwenye hiyo level nenda level ya juu zaidi. Hata miongoni mwa watoto wa familia moja kuna tofauti itakuwa Taifa?
Yatazame matatizo ya Nchi hii kwa upana wake utagundua mengi na hapana shaka tutatoka hapa tulipo kama Taifa.
 
Nguruvi3,

Nimependa uchambuzi wako muruwa.

Naomba utupe "Ratio" ya Waislam na Wakirsto tukianza na Wizara ya Mambo ya Ndani, Wizara ya Ujenzi, Wizara ya Fedha, Wizara ya Afya, na Wizara zingine.

Halafu tupe "Ratio" ya Waislam na Wakisto Mawaziri na Manaibu wake.

Halafu tupe "Ratio" ya Waislam na Wakirsto Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya.

Halafu tupe "Ratio" ya Waislam na Wakirsto Makatibu Wakuu wa Wizara.

Rudi kinyumenyume:
Kwamba ratio vyuoni ikoje kati ya Waislam na Wakristo
Sekondari ratio ikoje na shule ya Msingi ration ikoje

Halafu unakuja huku uraiani kwenye maeneo yenye Waislam wengi (Pwani, Lindi, mtwara, Tanga, Kigoma)
mwamko ukoje kuhusu Elimu, vipi kuhusu shule za Seminari za Kiislam zipo kwenye hali gani.
Tena nenda hatua moja zaidi linganisha Maua Seminary, Marian girls, St Anthony nk nk ziko kwenye hali
gani na kina nani wana watoto huko.

Unaweza kuchepuka kidogo ukaangalia pia Wachaga, Wahaya, Wanyakyusa kule wanapotoka na mwamko wao
kwenye Elimu halafu piga hesabu mumo ratio ikoje kwa Waislam na Wakristo.

Halafu mbona umechagua nafasi za appointment. Hujafikiria pia madaktari. Nenda Muhimbili utafute akina Kimario
Edward, Swai John, Mwakingwe nk uone wako wangapi halafu linganisha idadi yao na akina Pazi nk.
Au na kwenye udaktari kuna Waislam wananyimwa fursa ya kutibu watu na uhaba woote wa madaktari nchi hii?

Tuambie nani huyo anawanyima watanzania fursa ya kupata matibabu tumlaani.
 
Back
Top Bottom