Ritz
Mimi naamini sina upande. Inawezekana ninao lakini sijajua bado.
Nikweli nimesema sioni dhulma, lakini haimanishi siamini kuwa kunauwezekanao ipo ila mimi sijaiona bado, ndo mana mnakasha huu nimeupenda na nimeamua kuwa neautral ili nijaribu kuangalia kwa jicho la pili ushahidi yakinifu wa madai haya.
Mimi nipo hapa natafuta kwelj na ushahidi wa madai haya ya muda mrefu. Ndo mana nimepinga ushahidi wa Research ya Warsha kwasababu makosa yake yameokena na nikasema si vyema kutumia takwimu zile kama kielezo cha dhulma dhidi ya waislamu kwasababu haikuchukuliwa kitaalamu.
As so for historia, kama Mzee Said alivyoiandika, nivigumu kwangu kujua ukweli kwasababu
Kwanza ni Historia na mimi sina utaalamu
Pili any events za historia lazima zisapotiwe na wana historia wengine kuipa uhalali wake. Lasivyo mtu yoyote anaweza akaweka event yake kwenye historia hata kama haikuwepo na kung'ang'ania ni kweli.
Lakini ushahidi huu wa hisrtoria nikasema nimeanza kuwa na wasiwasi nao kwasababu Mzee Saidi ameshaanza kuonesha makosa madogo madogo lakini yenye uzito mkubwa kwenye kitabu chake (na mwenyewe amekiri kama ni makosa ya kibinadamu) kiasi mtu unajiuliza how can believe the rest of the story....????
So mimi bado naheshimu madai ya watu wanaosema waislamu wanadhulumiwa na mfumo kristo, lakini bado natafuta ushahidi nijiridhishe.
Ila pia kuna kitu nimeona labda ningepata ufafanuzi,
Kipindi cha uhuru mnasema Kanisa na Nyerere walikandamiza waislamu,
Wakati Yule sheikh msouth africa alivyorudishwa mkasema kanisa lika mshinikiza Mwinyi kumfukuza (manake mmemtoa Mwinyi kwenye makosa, kwamba kosa sio lake bali alishinikizwa)
Kipindi hiko hiko mnamlaumu waziri wa mambo ya ndani Mrema aliwakandamiza na kuwauwa Waislamu lakini Raisi Mwinyi hausishwi.
Kipindi cha Mwembe chai wakati wa Mkapa mkasema laana ya damu ya waislamu ipo mikononi mwake,
Kipindi hiki cha kikwete ambapo kuna viongozi waandamizi wengi sana waislamu, kuanzia Raisi, makamo wa Raisi, mkuu wa Polisi na kamanda Kova nae, mnasema kanisa ndo linashinikiza na kupiga vita, wamekamatwa wakina Ponda lawama hazijaenda kwa Kwikwete wala IGP wala kova bali kanisa.
Sasa je hamuoni mko selective jinsi mnavyo laumu?
Mnachagua nani wakumlaumu na wakumluka?
Lasivyo basi tuite dhulma zidi ya waislamu kutoka mfumo kristo, kanisa na waislamu wenyewe...
Ambapo tutarudi kwenye swali la msingi, Je hao waislamu wanaodhulumiwa mpaka na waislamu wenzao ni waislamu gani???