Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Si kweli! Hapa ndipo hoja ya Mag3 inapokuwa na nguvu sana.
Mag3 ameweka wazi jinsi Nyerere alivyokuja mwaka 1946 (kama mwaka ni sawa) na akauliza wakati huo Abdul alikuwa na sifa gani katika siasa?

Nyerere alikutana na Dosa Aziz kabla ya kukutana na Abdul. Kwa uchache alikuwa ameshaanza kufahamiana na wanamji

Ama kuendesha Benz kama hilo lilitokea basi kwa nyakati hizo ilikuwa ni heshima kwasababu Watanganyika wengi hawakumudu kiatu sembuse Benz. Sasa kuheshimiwa ikiwa ni pamoja na Nyerere hayo ni maneno yako kwasababu hakuna mahali pamenukuliwa akisema hayo. Tunaheshimu sana mawazo yako binafsi na si ya kihistoria.

Wazee wote waliopigania uhuru wa nchi hii wanapaswa kupewa heshima.
Hakuna mwenye heshima kubwa au ndogo, heshima ni heshima.

Jitihada za kumpandisha Abdul awe Rais wa TAA na TANU kisha Tanganyika haziwezi kuzaa matunda kwa werevu.
Abdul atabaki kuwa na mchango wake na kuheshimiwa kwa hilo.

Jitihada za kumdhalilisha Nyerere ili kusafisha nyota ya Abdul hazitazaa matunda asilani.
Nyerere atabaki kuwa kiongozi wa TAA,TANU, Rais wa kwanza wa Tanganyika huru, mwenyekiti wa kwanza wa CCM.

Na hapa umetusadia sana kutambua kuwa kumbe hata Abdul alifahamu kuwa ipo haja ya kuwa na mtu mwenye uwezo wa kuwaunganisha Watanganyika. Kidaha alikataa, Nyerere akakubali. Swali ni kuwa je, lengo la Abdul kuwaunganisha Watanganyika kwa kumtumia Nyerere lilifanikiwa au la?

Nguruvi,
Lengo la Abdu lilifanikiwa pakubwa sana.
Kama wasemavyo Waingereza "The rest is history."

Kwa kweli mie sina tatizo la mtu atakuwa na tafsiri
gani ya historia ya wazee wangu.

Lengo langu ni kuisomesha hii historia ambayo kwa
muda mrefu ilikuwa haijulikani.

Hufarijika sana pale mnapopiga "critique" haikuwa
hivi ilikuwa vile nk.

Huko tulikotoka haya hayakuwapo.

Ndiyo sishi kusema mtu yuko huru kuamini historia
aionayo ndiyo kweli.
 
Kwa bahati mbaya sana, historia unaisimulia kwa hisia kinyume na historia hiyo inavyotakiwa kusimuliwa!

Historia hutembea na huishi kwa fact na sio hisia!

Hata uwezo wakutafsiri hiyo hotuba mpaka leo tangu ilipowekwa hapa januari umeshindwa kijana?

Narudia tena kukusihi, itendee haki jf,

Elimu yote liyoipata katika uzi huu ninakushangaa isipokuwa na mafaa kwako!

Huu mbini mie sijauelekeza kwako ni mahusisi kwa wanaukumbi ambao wanaofuatilia huu mnakasha.

Wewe endelea na porojo zako za mafaa.

Yericko umekwisha...ha haa ha.
 
Mimi nakesha hapa 24/7 na ikibid hata 365 kunyonya elimu kutoka kwa Moh Said na wengineo,na kuwabeza wengine wote wanaozuia na kukejeli elimu hii inayomwaga hapa bila tozo bila mashartii...
Naamini kubeza kwa msomi huendana na hoja na sio makelele! sote tunapenda kunyonya elimu inayotolewa na Mohamed, lakini Mohamed si mtume, anapokosea na watu wakamkosoa basi tusiwaone hao wanaomkosoa ni wabaya kiasi cha wewe kuwashambulia wao binafsi badala ya hoja zao!
 
Huu mbini mie sijauelekeza kwako ni mahusisi kwa wanaukumbi ambao wanaofuatilia huu mnakasha.

Wewe endelea na porojo zako za mafaa.

Umekwisha...ha haa ha.

mkuu Ritz, Ms, na wengineo poleni kwakazi nzito ya kuwaelimisha hawa ndugu zetu manake naona kazi ya kuelewa inakuwa nzito sana. Poleni sana mungu atakulipeni kwa kazi yenu nzito.
 
Kuna habari za kusikitisha ukumbini nadhani Mohamed Said, atatuelezea Inshaalah.

Wanajamvi,
Innalilah Wainnailaihy Rajuun.

Kwa Allah tumetoka na kwake ni marejeo yetu.

Bwana Ally Kleist Sykes amefariki dunia Nairobi.
 
Yericko Nyerere,

Kila siku nakuanbia wewe ni mtupu sana sana kwenye historia ya Tanganyika huna unachokijua kwenye AA, TAA, TANU, unachotakiwa upinde mgongo usomeshwe historia unajipunja mengi sana kutoka kwa Mohamed Said.


Hebu msome Nyerere mwenyewe hapa chini sijui wewe na Nyerere nani anasema kweli na nani muongo wapi Nyerere kasema walianzisha chama cha harakati za mwafrika...
Julius Nyerere

'"Mimi nimeanza siasa na wazee wa Dar es Salaam; na wazee wa Tanzania. Nimeanza nao mapema sana; mapema kweli. Nilirudi kutoka masomoni, Uingereza Oktoba 1952 – miaka 33 nyuma. Wakati huo nikiwa kijana mdogo wa miaka thelathini na kidogo hivi.
Niliporejea nchini hapo Oktoba, nikaenda Butiama. Januari nikarudi Dar es Salaam. Nikaanza kazi. Nikataka kujua habari za African Association. Mzee Mwangosi anakumbuka. Yeye ndiye aliniambia habari za African Association. Aliisha niambia habari hizo tangu nikiwa Makerere – Chuo Kikuu – nikiwa mwanafunzi.

Pale, mimi na wanafunzi wenzangu tulikuwa tumeanzisha chama kinachoitwa Tanganyika African Welfare Association (TAWA) cha wanafunzi wa Tanganyika; mimi nikiwa katibu wao. Hapa tukaona mambo yanakwenda vizuri kidogo.

Tukaona kwanini TAWA iwe ya wanafunzi peke yao na siyo Tanganyika nzima. Kwa hiyo nikawaandikia baadhi ya watu Tanganyika. Nikasema, jamani ee, tumeanzisha chama, kwanini msianzishe huko matawi ya chama hicho?

Ndugu Mwangosi akapata barua hiyo. Alikuwa miongoni mwa waliopata barua hiyo. Akaniandikia – nikiwa Makerere – akasema: wewe kwanini unataka kuanzisha chama kipya? Kipo chama. Kipo chama cha TAA (Tanganyika African Association).


Nadhani wewe ndiyo unatakiwa ufanye utafiti kabla ya kuandika hebu tuendelee kumsoma Nyerere mwenyewe hapa chini...

Julius Nyerere.
Hivyo ndivyo tulivyofanya. Kwa hiyo mimi nikawa katibu wa katawi ka TAA hapo Makerere. Niliporudi Tabora na kuanza kufundisha pale St. Marys (sasa inaitwa Sekondari ya Milambo), nikachaguliwa katibu wa TAA wa jimbo ambalo makao yake makuu yalikuwa Tabora. Ulipofanyika mkutano wa TAA mjini Dar es Salaam, nilihudhuria nikiwa mjumbe kutoka Tabora.

Kwa hiyo nilikuwa naijua Tanganyika African Association. Nilipokuwa ninaondoka kwenda Ulaya kusoma, nilikuwa nimeishaonja shughuli za TAA. Sasa niliporudi, baada ya kukaa Pugu siku chache, nikaja mjini Dar es Salaam. Nikauliza nani wanaongoza TAA? Nikaambiwa kuna jamaa mmoja anaitwa Abdul Sykes. Sasa ni marehemu. Abdul ndiye alikuwa katibu wakati huo.

Nilipelekwa na Kasela Bantu - ambaye naye aliteleza-teleza na hatunaye hapa (kwenye mkutano). Kasela Bantu alikuwa mwalimu mwenzangu. Tulifundisha pamoja Milambo. Nilipokuja Dar es Salaam, nikakuta anafanya kazi Redio (Tanganyika Broadcasting Corporation). Ni Kasela Bantu aliyenipeleka kwa Sykes.



Hebu msome tena Nyerere hapa chini anavyoelezea harakati zake za kisiasa pamoja na wazee wetu ambao walikuwa na mahaba makubwa na Nyerere ingawa wewe unawaletea kejeli na dhihaka na kuwaita wazee wa vibarazani tu....

Julius Nyerere.
Ninasema yote haya kwa shukrani kwa wazee. Jamaa hawa walikuwa watu wazima wa Dar es Salaam, na mimi kijana mdogo Mzanaki, na Kiswahili changu si kizuri sana – cha matatizo.

Nimekuja, natoka Ulaya, tena masomoni. Muda mfupi tu jamaa hawa wakaniamini haraka sana – katika muda wa miezi mitatu. Wakanichagua Rais wa TAA. Hapo ndipo nilianza shughuli mpya ya kuandika katiba ya TAA na kuipa madhumuni hasa ya shabaha ya kuleta uhuru.

Baada ya miezi 13, hapo 1954, tukaanzisha TANU. Jina hili lilipendekezwa na akina Abdul Sykes. Walikuwa wamelifikiria tangu zamani, walipokuwa askari vitani huko Burma (Vita vya Pili).


Mohamed Said, wala alazimishi umma wamuamini hata Nyerere mwenyewe anasema hebu msome hapa chini. hapa wanaukumbi tulizaneni mumsome vizuri Nyerere.

Julius Nyerere.

Siku moja, Dosa akanifuata Magomeni (Dar es Salaam). Akasema: Leo wazee wanakutaka. Wapi? Kwa Mzee Jumbe Tambaza. Wanakutaka usiku. Nikasema haya, nitakuja. Nikaenda. Nikakuta wazee wameshakaa; wameniita kijana wao kuniombea dua. Mimi Mkristo, wao Waislamu watupu. Wakaniombea dua za ubani. Tukamaliza.

Tulipomaliza wakasema kuna dua pia za wazee wao. Basi wakanitoa nje. Tukatoka. Zilipomalizika zilikuwa za Korani; sasa zikaja dua za wazee – za jadi.

Walikuwa na beberu la mbuzi. Wamechimba shimo. Wakaniambia simama. Nikasimama. Beberu akachinjwa, huku anaambiwa, "Twining (Twainingi) umekwisha!" (Edward Twining alikuwa Gavana wakati huo). Ndipo nikaambiwa: Tambuka! Nikavuka lile shimo. Hapo nikaambiwa na wazee: Basi nenda zako; tangu leo Twainingi amekwisha!

Sasa mimi Mkristo; hao Waislamu. Na mimi mkorofi-korofi katika mambo haya (ya kutambika). Lakini tulikuwa tunaelewana na wazee wangu hao. Kwa hiyo nilitambuka pale na kuambiwa: Nenda nyumbani salama. Twaining hawezi tena!

Wazee wangu wengine wanakumbuka tulikuwa tunakwenda Bagamoyo. Kwenye makaburi kule! Tunapiga dua huko kwenye makaburi na wazee wangu.

Baadhi yetu mtakumbuka safari moja jamaa wa Kenya, hawa akina Tom Mboya (marehemu) walishitakiwa. Tukasema tuwasaidie. Tuwasaidie vipi? Tukasema tufunge. Tukaomba nchi nzima kufunga siku hiyo. Tufunge! Tukafunga. Hakuna kula. Na siku ya kufunga tulikuwa na mkutano Bagamoyo. Tukaenda huko. Tukafanya mkutano hadi saa 12 jioni.

Baada ya mkutano tukaenda nyumbani kwa Mzee Mohamed Ramia (marehemu). Hapa ndipo tulikuwa tumefikia. Mimi nikamuuliza mzee: Sheikh, una Aspro? Akajibu: Kwa nini unataka Aspro? Nikajibu kuwa kichwa kinaniuma kwelikweli. Akasema subiri.

Tulisubiri hadi saa ya kufuturu. Tukafuturu vizuri. Mzee Ramia akaniuliza: bado unataka Aspro? Nikajibu kichwa sasa hakiumi. Kumbe ilikuwa njaa.

Nawaelezeni haya kwa sababu huko tulikotoka, tulishikamana sana. Tulishirikiana sana na wazee."'

Hizi picha za wazee wetu wakionyesha sura za bashasha pamoja na Nyerere, Sheikh Takadir kushoto kwa Nyerere kavaa kanzu na kofia kashika fimbo yake...
11.jpg


Hapa Wazee wapo uwanja wa ndege wakumuaga Nyerere akielekea UNO.
nyerere_departing_for_UNO.jpg

Mkuu Ritz, hebu msome mzee Mohamed Said hapa chini kuhusu hadhi ya TAA;QUOTE=Mohamed Said;6386015].

Haya yote yalisababisha wakoloni kutoa Government Circular No. 5 na 6 mwaka
1953 kuionya TAA kuwa inaingilia siasa za Tanganyika.

Hii si dalili ya chama kudorora.
Yako mengi.

Chama kilidorora 1953 mara tu Nyerere alipochukua uongozi
Alonambia haya ni Dossa Aziz.

.[/QUOTE]
 
Last edited by a moderator:
Jokakuu,
Chadema kupokea Takrima toka kwa kada wa CCM tafsiri yake nini? ni kichekesho kwa Chama kinachodai ni Wapinzani huku wanapokea Takrima toka kwa kada wa Chama tawala! Sabodo ni kada wa CCM au CDM? haingii akilini kada 1 kupenda vyama 2 tofauti! hapa kuna usiri fulani tunaomba akina Jokakuu watufichulie!
Kadogoo,

..kwa kweli hili ni gumu.

..si tumeambiwa hata Dr.Slaa ana kadi ya CCM na anailipia.

..mimi naipenda CDM siyo kwasababu ni nzuri sana, but kwasababu CCM ni mbaya zaidi.

NB:

..nadhani masuala ya CDM yana thread nyingi sana. tujaribu kutowajadili ktk thread hii.

cc: Ritz, Nguruvi3
 
Last edited by a moderator:
Nashukuru kwa jibu lako murua.

Na Nyerere je asili yake ilikuwa wapi?

Hata mbunge wenu wa Chadema Mwanza Nyamagani Wenje ni Mtanzania mwenye asili ya Kenya.

Sabodo ni mwafrika au siyo mwafrika hapa ndiyo nataka kujua.
Ritz,

..Sabodo siyo Mwafrika ni Muasia.

..sasa kwasababu ni raia wa nchi hii, basi ana haki zote sawa na sisi Waafrika.
 
Last edited by a moderator:
i

Hao wanajeshi je unajua wote walifukuzwa. Huyo wa Air force ngerengere alifukuzwa na wa china japo alikuwa mahiri sana kuongea kichina.Uliza utaelezwa.

Na hao wengine wote kama walipata degree basi wamepata degree zao baada ya baba yao kuondoka madarakani.Lakin jiulize je walisoma skuli gani za Sc na kama yupo aliyewahi kwenda High sch skuli gani?

Naomba uchunguze hilo kisha nikosoe kama nitakuwa nimenena uwongo

usitake niseme meng

Barubaru,

..nimesikia Makongoro Nyerere alitoka JKT akaenda mstari wa mbele vita vya Kagera.

..mimi sidhani kama Mwinyi,Mkapa,au Kikwete, wanaweza kuruhusu jambo kama hilo kwa watoto wao.

..kumbuka kati ya hao kuna waliowatorosha watoto wao kwenda JKT.

..sasa hivi kwenye shule za kata, na hata zile kongwe za sekondari, it is very rare kukuta watoto wa viongozi.

NB:

..lile shairi lako la Watwana wakiamka...linazungumzia Znz??

cc: Jasusi, Ritz, nguruvi, Mohamed Said, Wickama
 
Last edited by a moderator:
Ritz,

..Sabodo siyo Mwafrika ni Muasia.

..sasa kwasababu ni raia wa nchi hii, basi ana haki zote sawa na sisi Waafrika.

Sudan, Misri, Chad, Morocco, Niger, hawa vipi ni waafrika?
 
Last edited by a moderator:
Huu ni msiba wa kitaifa, kila mtanzania unamuhusu,

Hakika tumepoteza hazina kuu ya tunu ya uhuru wetu,

Alisimama kidete kupigania uhuru kwa jasho na damu!

Mungu amlaze pema peponi mpigania uhuru wa Tanganyika Mzee wetu Ally Klest Sykes!
 
Wanajamvi,
Innalilah Wainnailaihy Rajuun.

Kwa Allah tumetoka na kwake ni marejeo yetu.

Bwana Ally Kleist Sykes amefariki dunia Nairobi.

Wanajamvi,
Nakuwekeeni hapa chini maneno ya Ally Sykes akijieleza mwenyewe kuhusu
nasaba yake na historia ya wazee wake.

Tulikuwa tumekaa ofisini kwake kiasi cha miaka 16 iliyopita yeye anazungumza
na mimi nimeshika kinasa sauti changu namsikiliza.

NImgependa ku ''share'' kumbukumbu hizi za mzee wangu Bwana Ally Sykes na
nyinyi ndugu zangu wana ukumbi katika siku hii ambayo ni ya majonzi makubwa
sana kwangu:

''My name is Ally Kleist Sykes. I was born in Dar es Salaam on 10 th September 1926 from Kleist Sykes Mbuwane, the son of a Zulu mercenary, Sykes Mbuwane and Bibi Mruguru bint Mussa who my father married in February 1923.

My father's other name is Abdallah but he never identified himself by this name. This is the name written on his tombstone, which today identifies his grave at the Kisutu Muslim graveyard in Dar es Salaam.

I was named Ally after my father's elder brother Ally Sykes, or Kattini Mbuwane, as he was known back home in Mozambique. My grandfather is from the Shangaan a Zulu clan, which originated from South Africa but settled in Mozambique.

The reason which caused the Zulu migration to Mozambique, was to run away from civil upheavals caused by the reign of Shaka, the Zulu King. My father was the second child; the first one was Ally Kattini who was born from Mbuwane's first wife back home.

My uncle Kattini was blind. When Mbuwane came to Tanganyika he came with him but he was later sent back home. The village, which my people settled, is known as Kwa Likunyi. I had the occasion to visit the village of our origins in 1952 and I was able to trace some members of our family.

At that time the country was under the harsh rule of the Portuguese. I will narrate the story of my travel to trace my people later on.


The history of my family begins at a village called Kwa Likunyi in the then Portuguese Mozambique about a hundred years ago. I learned most of the history of my forefathers from my father, Kleist Sykes. Kleist Sykes was born in Pangani in 1894.

His mother, my grandmother, was a Nyaturu from Central Tanganyika. My father always considered himself an aristocrat of sorts and had his own exceptional way of carrying himself.

He behaved and even dressed differently in comparison to other Africans. He was always immaculately dressed and all his existing photographs show him in suit and tie. He considered himself a modern man, a man of the times.

He was however very conscious of his Zulu origins and loved and longed for the country which he never set foot on. My father sentimental and melancholy used to talk about his father, Sykes Mbuwane, who he never even knew because Mbuwane my grandfather, died soon after my father was born.

My grandfather, Sykes Mbuwane, the Zulu mercenary and warrior from Inhambane died in Uhehe. Mbuwane died crossing River Ruaha returning from the campaign against Chief Mkwawa. He had seen cows crossing and he thought the water was shallow. Measuring himself up the Zulu warrior and others attempted to cross the river and were swept away and drowned.

My father's narration about his people was stories of wars and power of the white men over Africans. He used to narrate to us this history when we were young. I now can understand why that part of history was important to him.

That history was the only thing he could hold on about his people and tribe. Kleist was sentimental and melancholy because apart from us, his children he never had a living relative in Tanganyika.

Whatever relatives he had were left behind in Inhambane, Mozambique at the turn of the century even before he was born. Part of that history and indeed the history of our family has also been recorded together with the history of Tanganyika itself.

Kleist preserved this history through his own pen. And it was from Kleist's pen that many years after he had passed away that we now have an accurate account of those days long passed.

Before he died on 23 May 1949 my father left behind his memoirs in his long flowing Germany handwriting picked from a Germany school he attended in Dar es Salaam, as a child in early 1900s. These memoirs were later revisited by Abdulwahid my elder brother with his daughter Aisha Daisy Sykes, then an undergraduate student at Dar es Salaam University under the tutelage of Illife the renowned historian from Cambridge University.

A month before he died on 12 October 1968 Abdulwahid had had already assisted Daisy to complete her research assignment of prominent Africans in Tanganyika for a history seminar on the life of her grandfather. The aim of this project was to document the life history of our father, Kleist Sykes and his achievement in politics, education and business.


It was from his diaries, personal papers as primary sources and with the assistance of Daisy that Iliffe was able to research and write accurately on African Association and early colonial politics. This work was submitted to the History Department of University of Dar es Salaam in September 1968.

It was later published in 1973 in a book edited by Illife. It is a pity that Abdulwahid who was the main informant on the biography did not leave to see the fruits of his work.

Prior to publishing of my father's biography, little was known about the founding fathers of the African Association.
..''
 
Huu ni msiba wa kitaifa, kila mtanzania unamuhusu,

Hakika tumepoteza hazina kuu ya tunu ya uhuru wetu,

Alisimama kidete kupigania uhuru kwa jasho na damu!

Mungu amlaze pema peponi mpigania uhuru wa Tanganyika Mzee wetu Ally Klest Sykes!

Yericko,

Amin.

Msome mzee wetu Ally Sykes hapa akinieleza yaliyomtokea baada ya wao kuunda TANU:

''My transfer saddened Nyerere.

We all knew that the transfer was politically motivated as a way to weaken the new political party.

I also knew that so long as the British were in control of our country people like me who cherish aspirations for freedom will always be haunted and intimidated.

The government could have dismissed me from government service but that would have made me a martyr.

The best decision was to take me out of the political limelight in Dar es Salaam.

This feeling rather than dampen my enthusiasm for TANU increased my zeal to struggle and fight back against the British until independence was achieved.

Zuberi Mtemvu had warned me of the consequence in challenging the government.

In a letter which Zuberi Mtemvu wrote to me he had this to say, "You will never be transferred back to Dar es Salaam or earmarked not to have any responsible post for ever while in Government."
 
Back
Top Bottom